< Yeremia 9 >
1 Laiti kichwa changu kingekuwa chemchemi ya maji na macho yangu yangekuwa kisima cha machozi! Ningelia usiku na mchana kwa kuuawa kwa watu wangu.
Who schal yyue watir to myn heed, and a welle of teeris to myn iyen? And Y schal biwepe dai and niyt the slayn men of the douyter of my puple.
2 Laiti ningekuwa na nyumba ya kukaa wasafiri jangwani, ningewaacha watu wangu na kwenda mbali nao, kwa kuwa wote ni wazinzi, kundi la watu wadanganyifu.
Who schal yyue me in to a wildirnesse of dyuerse weigoeris? And I schal forsake my puple, and Y schal go awei fro hem. For whi alle ben auowteris, and the cumpenyes of trespassouris ayens the lawe;
3 “Huweka tayari ndimi zao kama upinde, ili kurusha uongo; wamekuwa na nguvu katika nchi lakini si katika ukweli. Wanatoka dhambi moja hadi nyingine, hawanitambui mimi,” asema Bwana.
and thei helden forth her tunge as a bouwe of leesyng, and not of treuthe Thei ben coumfortid in erthe, for thei yeden out fro yuel to yuel, and thei knewen not me, seith the Lord.
4 “Jihadhari na rafiki zako; usiwaamini ndugu zako. Kwa kuwa kila ndugu ni mdanganyifu, na kila rafiki ni msingiziaji.
Ech man kepe hym fro his neiybore, and haue no trist in ony brother of hym; for whi ech brother disseyuyng schal disseyue, and ech frend schal go gilefuli.
5 Rafiki humdanganya rafiki, hakuna yeyote asemaye kweli. Wamefundisha ndimi zao kudanganya, wanajichosha wenyewe katika kutenda dhambi.
And a man schal scorne his brother, and schal not speke treuthe; for thei tauyten her tunge to speke leesyng; thei traueliden to do wickidli.
6 Unakaa katikati ya udanganyifu; katika udanganyifu wao wanakataa kunitambua mimi,” asema Bwana.
Thi dwellyng is in the myddis of gile; in gile thei forsoken to knowe me, seith the Lord.
7 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Tazama, nitawasafisha na kuwajaribu, kwani ni nini kingine niwezacho kufanya kwa sababu ya dhambi ya watu wangu?
Therfor the Lord of oostis seith these thingis, Lo! Y schal welle togidere, and Y schal preue hem; for whi what other thing schal Y do fro the face of the douyter of my puple?
8 Ndimi zao ni mshale wenye sumu, hunena kwa udanganyifu. Kwa kinywa chake kila mmoja huzungumza maneno mazuri na jirani yake, lakini moyoni mwake humtegea mtego.
The tunge of hem is an arowe woundynge, and spak gile; in his mouth he spekith pees with his frend, and priueli he settith tresouns to hym.
9 Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya jambo hili?” asema Bwana. “Je, nisijilipizie kisasi kwa taifa kama hili?”
Whether Y schal not visite on these thingis, seith the Lord, ether schal not my soule take veniaunce on siche a folc?
10 Nitalia na kuomboleza kwa ajili ya milima na kuomboleza kuhusu malisho ya jangwani. Yamekuwa ukiwa, wala hakuna apitaye humo, milio ya ngʼombe haisikiki. Ndege wa angani wametoroka na wanyama wamekimbia.
On hillis Y schal take wepyng and mournyng, and weilyng on the faire thingis of desert, for tho ben brent; for no man is passynge forth, and thei herden not the vois of hym that weldith; fro a brid of the eir `til to scheep, tho passiden ouer, and yeden awei.
11 “Nitaifanya Yerusalemu lundo la magofu, makao ya mbweha; nami nitaifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa ili asiwepo atakayeishi humo.”
And Y schal yyue Jerusalem in to heepis of grauel, and in to dennes of dragouns; and Y schal yyue the citees of Juda in to desolacioun, for ther is no dwellere.
12 Ni mtu yupi aliye na hekima ya kutosha ayaelewe haya? Ni nani aliyefundishwa na Bwana awezaye kuyaeleza haya? Kwa nini nchi imeharibiwa na kufanywa ukiwa kama jangwa ambapo hakuna awezaye kupita?
Who is a wise man that schal vndurstonde these thingis, and to whom the word of the mouth of the Lord schal be maad, that he telle this? Whi the erthe perischide, it is brent as desert, for noon is that passith?
13 Bwana akasema, “Ni kwa sababu wameiacha sheria yangu, niliyoiweka mbele yao: hawajaniheshimu mimi wala kufuata sheria yangu.
And the Lord seide, For thei forsoken my lawe, which Y yaf to hem, and thei herden not my vois, and thei yeden not therynne;
14 Badala yake wamefuata ukaidi wa mioyo yao, wamefuata Mabaali, kama vile baba zao walivyowafundisha.”
and thei yeden aftir the schrewidnesse of her herte, and aftir Baalym, which thei lerneden of her fadris;
15 Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: “Tazama, nitawafanya watu hawa wale chakula kichungu na kunywa maji yenye sumu.
therfor the Lord of oostis, God of Israel, seith these thingis, Lo! Y schal fede this puple with wermod, and Y schal yyue to hem drynke the watir of galle.
16 Nitawatawanya katika mataifa ambayo wao wala baba zao hawakuwajua, nikiwafuata kwa upanga mpaka niwe nimewaangamiza kabisa.”
And Y schal scatere hem among hethene men, whiche thei and her fadris knewen not; and Y schal sende swerd aftir hem, til thei ben wastid.
17 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Fikiri sasa! Waite wanawake waombolezao waje, waite wale walio na ustadi kuliko wote.
The Lord of oostis, God of Israel, seith these thingis, Biholde ye, and clepe ye wymmen `that weilen, and come thei; and sende ye to tho wymmen that ben wise, and haste thei.
18 Nao waje upesi na kutuombolezea, mpaka macho yetu yafurike machozi na vijito vya maji vitoke kwenye kope zetu.
Haste thei, and take thei weilynge on you; youre iyen brynge doun teeris, and youre iyelidis flowe with watris;
19 Sauti ya kuomboleza imesikika kutoka Sayuni: ‘Tazama jinsi tulivyoangamizwa! Tazama jinsi aibu yetu ilivyo kubwa! Ni lazima tuihame nchi yetu kwa sababu nyumba zetu zimekuwa magofu.’”
for the vois of weilyng is herd fro Sion. Hou ben we distried, and schent greetli? for we han forsake the lond, for oure tabernaclis ben forsakun.
20 Basi, enyi wanawake, sikieni neno la Bwana; fungueni masikio yenu msikie maneno ya kinywa chake. Wafundisheni binti zenu kuomboleza; fundishaneni kila mmoja na mwenzake maombolezo.
Therfor, wymmen, here ye the word of the Lord, and youre eeris take the word of his mouth; and teche ye youre douytris weilyng, and ech womman teche hir neiybore mournyng.
21 Mauti imeingia ndani kupitia madirishani, imeingia kwenye majumba yetu ya fahari; imewakatilia mbali watoto katika barabara na vijana waume kutoka viwanja vya miji.
For whi deth stiede bi youre wyndows, it entride in to youre housis, to leese litle children with outforth, and yonge men fro the stretis.
22 Sema, “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Maiti za wanaume zitalala kama mavi katika mashamba, kama malundo ya nafaka nyuma ya mvunaji, wala hakuna anayekusanya.’”
Speke thou, the Lord seith, these thingis, And the deed bodi of a man schal fal doun as a toord on the face of the cuntrei, and as hei bihynde the bak of the mowere, and noon is that gaderith.
23 Hili ndilo asemalo Bwana: “Mwenye hekima asijisifu katika hekima yake, au mwenye nguvu ajisifu katika nguvu zake, wala tajiri ajisifu katika utajiri wake,
The Lord seith these thingis, A wise man haue not glorie in his wisdom, and a strong man haue not glorie in his strengthe, and a riche man haue not glorie in hise richessis; but he that hath glorie,
24 lakini yeye ajisifuye, na ajisifu kwa sababu hili: kwamba ananifahamu na kunijua mimi, kwamba mimi ndimi Bwana, nitendaye wema, hukumu na haki duniani, kwa kuwa napendezwa na haya,” asema Bwana.
haue glorie in this, to wite and knowe me, for Y am the Lord, that do merci and dom and riytfulnesse in erthe. For whi these thingis plesen me, seith the Lord.
25 “Siku zinakuja, nitakapowaadhibu wale wote ambao wametahiriwa kimwili tu, asema Bwana,
Lo! daies comen, seith the Lord, and Y schal visite on ech man that hath prepucie vncircumcidid; on Egipt,
26 yaani Misri, Yuda, Edomu, Amoni, Moabu na wote wanaoishi jangwani sehemu za mbali. Kwa maana mataifa haya yote hayakutahiriwa mioyo yao, nayo nyumba yote ya Israeli haikutahiriwa.”
and on Juda, and on Edom, and on the sones of Amon, and on Moab, and on alle men that ben clippid on long heer, and dwellen in desert; for whi alle hethene men han prepucie, forsothe al the hous of Israel ben vncircumcidid in herte.