< Yeremia 9 >
1 Laiti kichwa changu kingekuwa chemchemi ya maji na macho yangu yangekuwa kisima cha machozi! Ningelia usiku na mchana kwa kuuawa kwa watu wangu.
Who makes my head waters, And my eye a fountain of tears? And I weep by day and by night, For the wounded of the daughter of my people.
2 Laiti ningekuwa na nyumba ya kukaa wasafiri jangwani, ningewaacha watu wangu na kwenda mbali nao, kwa kuwa wote ni wazinzi, kundi la watu wadanganyifu.
Who gives me in a wilderness A lodging-place for travelers? And I leave my people, and go from them, For all of them [are] adulterers, An assembly of treacherous ones.
3 “Huweka tayari ndimi zao kama upinde, ili kurusha uongo; wamekuwa na nguvu katika nchi lakini si katika ukweli. Wanatoka dhambi moja hadi nyingine, hawanitambui mimi,” asema Bwana.
“And they bend their tongue, Their bow [is] a lie, And they have not been mighty for steadfastness in the land, For they have gone forth from evil to evil, And they have not known Me,” A declaration of YHWH!
4 “Jihadhari na rafiki zako; usiwaamini ndugu zako. Kwa kuwa kila ndugu ni mdanganyifu, na kila rafiki ni msingiziaji.
“You each beware of his friend, And do not trust any brother, For every brother utterly supplants, For every friend slanderously walks,
5 Rafiki humdanganya rafiki, hakuna yeyote asemaye kweli. Wamefundisha ndimi zao kudanganya, wanajichosha wenyewe katika kutenda dhambi.
And they each mock at his friend, And they do not speak truth, They taught their tongue to speak falsehood, They have labored to commit iniquity.
6 Unakaa katikati ya udanganyifu; katika udanganyifu wao wanakataa kunitambua mimi,” asema Bwana.
Your dwelling [is] in the midst of deceit, Through deceit they refused to know Me,” A declaration of YHWH.
7 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Tazama, nitawasafisha na kuwajaribu, kwani ni nini kingine niwezacho kufanya kwa sababu ya dhambi ya watu wangu?
Therefore, thus said YHWH of Hosts: “Behold, I am refining them, and have tried them, For how do I deal with the daughter of My people?
8 Ndimi zao ni mshale wenye sumu, hunena kwa udanganyifu. Kwa kinywa chake kila mmoja huzungumza maneno mazuri na jirani yake, lakini moyoni mwake humtegea mtego.
Their tongue [is] a slaughtering arrow, It has spoken deceit in its mouth, It speaks peace with its neighbor, And in its heart it lays its ambush,
9 Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya jambo hili?” asema Bwana. “Je, nisijilipizie kisasi kwa taifa kama hili?”
Do I not see after them for these things?” A declaration of YHWH, “Does My soul not avenge itself against a nation such as this?”
10 Nitalia na kuomboleza kwa ajili ya milima na kuomboleza kuhusu malisho ya jangwani. Yamekuwa ukiwa, wala hakuna apitaye humo, milio ya ngʼombe haisikiki. Ndege wa angani wametoroka na wanyama wamekimbia.
I lift up weeping and wailing for the mountains, And a lamentation for the habitations of the wilderness, For they have been burned up without any passing over, Nor have they heard the voice of livestock, From the bird of the heavens and to the beast—they have fled, They have gone.
11 “Nitaifanya Yerusalemu lundo la magofu, makao ya mbweha; nami nitaifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa ili asiwepo atakayeishi humo.”
“And I make Jerusalem become heaps, A habitation of dragons, And I make the cities of Judah a desolation, Without inhabitant.”
12 Ni mtu yupi aliye na hekima ya kutosha ayaelewe haya? Ni nani aliyefundishwa na Bwana awezaye kuyaeleza haya? Kwa nini nchi imeharibiwa na kufanywa ukiwa kama jangwa ambapo hakuna awezaye kupita?
Who [is] the wise man? And he understands this, And he to whom the mouth of YHWH spoke? And he declares it, For why has the land perished? It has been burned up as a wilderness, Without any passing through.
13 Bwana akasema, “Ni kwa sababu wameiacha sheria yangu, niliyoiweka mbele yao: hawajaniheshimu mimi wala kufuata sheria yangu.
And YHWH says: “Because of their forsaking My law that I set before them, And they have not listened to My voice nor walked in it,
14 Badala yake wamefuata ukaidi wa mioyo yao, wamefuata Mabaali, kama vile baba zao walivyowafundisha.”
And they walk after the stubbornness of their heart, And after the Ba‘alim, That their fathers taught them,”
15 Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: “Tazama, nitawafanya watu hawa wale chakula kichungu na kunywa maji yenye sumu.
Therefore, thus said YHWH of Hosts, God of Israel: “Behold, I am causing them—this people—to eat wormwood, And I have caused them to drink water of gall,
16 Nitawatawanya katika mataifa ambayo wao wala baba zao hawakuwajua, nikiwafuata kwa upanga mpaka niwe nimewaangamiza kabisa.”
And I have scattered them among nations Which they did not know, they and their fathers, And have sent the sword after them, Until I have consumed them.”
17 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Fikiri sasa! Waite wanawake waombolezao waje, waite wale walio na ustadi kuliko wote.
Thus said YHWH of Hosts: “Consider, and call for mourning women, And they come, And send to the wise women, And they come,
18 Nao waje upesi na kutuombolezea, mpaka macho yetu yafurike machozi na vijito vya maji vitoke kwenye kope zetu.
And they hurry, and lift up a wailing for us. And tears run down our eyes, And waters flow from our eyelids.
19 Sauti ya kuomboleza imesikika kutoka Sayuni: ‘Tazama jinsi tulivyoangamizwa! Tazama jinsi aibu yetu ilivyo kubwa! Ni lazima tuihame nchi yetu kwa sababu nyumba zetu zimekuwa magofu.’”
For a voice of wailing is heard from Zion: How we have been spoiled! We have been greatly ashamed, Because we have forsaken the land, Because they have cast down our dwelling places.”
20 Basi, enyi wanawake, sikieni neno la Bwana; fungueni masikio yenu msikie maneno ya kinywa chake. Wafundisheni binti zenu kuomboleza; fundishaneni kila mmoja na mwenzake maombolezo.
But hear, you women, a word of YHWH, And your ear receives a word of His mouth, And teach your daughters wailing, And each her neighbor lamentation.
21 Mauti imeingia ndani kupitia madirishani, imeingia kwenye majumba yetu ya fahari; imewakatilia mbali watoto katika barabara na vijana waume kutoka viwanja vya miji.
For death has come up into our windows, It has come into our palaces, To cut off the suckling from outside, Young men from the broad places.
22 Sema, “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Maiti za wanaume zitalala kama mavi katika mashamba, kama malundo ya nafaka nyuma ya mvunaji, wala hakuna anayekusanya.’”
Speak thus, “A declaration of YHWH, And the carcass of man has fallen, As dung on the face of the field, And as a handful after the reaper, And there is none gathering.”
23 Hili ndilo asemalo Bwana: “Mwenye hekima asijisifu katika hekima yake, au mwenye nguvu ajisifu katika nguvu zake, wala tajiri ajisifu katika utajiri wake,
Thus said YHWH: “Do not let the wise boast himself in his wisdom, Nor let the mighty boast himself in his might, Do not let the rich boast himself in his riches,
24 lakini yeye ajisifuye, na ajisifu kwa sababu hili: kwamba ananifahamu na kunijua mimi, kwamba mimi ndimi Bwana, nitendaye wema, hukumu na haki duniani, kwa kuwa napendezwa na haya,” asema Bwana.
But let the boaster boast himself in this, In understanding and knowing Me, For I [am] YHWH, doing kindness, Judgment, and righteousness, in the earth, For I have delighted in these,” A declaration of YHWH.
25 “Siku zinakuja, nitakapowaadhibu wale wote ambao wametahiriwa kimwili tu, asema Bwana,
“Behold, days are coming,” A declaration of YHWH, “And I have laid a charge on all circumcised in the foreskin,
26 yaani Misri, Yuda, Edomu, Amoni, Moabu na wote wanaoishi jangwani sehemu za mbali. Kwa maana mataifa haya yote hayakutahiriwa mioyo yao, nayo nyumba yote ya Israeli haikutahiriwa.”
On Egypt, and on Judah, and on Edom, And on the sons of Ammon, and on Moab, And on all cutting the corner [of the beard], Who are dwelling in the wilderness, For all the nations [are] uncircumcised, And all the house of Israel [are] uncircumcised in heart!”