< Yeremia 9 >

1 Laiti kichwa changu kingekuwa chemchemi ya maji na macho yangu yangekuwa kisima cha machozi! Ningelia usiku na mchana kwa kuuawa kwa watu wangu.
Who will give water to my head, and a fountain of tears to my eyes? and I will weep day and night for the slain of the daughter of my people.
2 Laiti ningekuwa na nyumba ya kukaa wasafiri jangwani, ningewaacha watu wangu na kwenda mbali nao, kwa kuwa wote ni wazinzi, kundi la watu wadanganyifu.
Who will give me in the wilderness a lodging place of wayfaring men, and I will leave my people, and depart from them? because they are all adulterers, an assembly of transgressors.
3 “Huweka tayari ndimi zao kama upinde, ili kurusha uongo; wamekuwa na nguvu katika nchi lakini si katika ukweli. Wanatoka dhambi moja hadi nyingine, hawanitambui mimi,” asema Bwana.
And they have bent their tongue, as a bow, for lies, and not for truth: they have strengthened themselves upon the earth, for they have proceeded from evil to evil, and me they have not known, saith the Lord.
4 “Jihadhari na rafiki zako; usiwaamini ndugu zako. Kwa kuwa kila ndugu ni mdanganyifu, na kila rafiki ni msingiziaji.
Let every man take heed of his neighbor, and let his not trust in any brother of his: for every brother will utterly supplant, and every friend will walk deceitfully.
5 Rafiki humdanganya rafiki, hakuna yeyote asemaye kweli. Wamefundisha ndimi zao kudanganya, wanajichosha wenyewe katika kutenda dhambi.
And a man shall mock his brother, and they will not speak the truth: for they have taught their tongue to speak lies: they have laboured to commit iniquity.
6 Unakaa katikati ya udanganyifu; katika udanganyifu wao wanakataa kunitambua mimi,” asema Bwana.
Thy habitation is in the midst of deceit: Through deceit they have refused to know me, saith the Lord.
7 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Tazama, nitawasafisha na kuwajaribu, kwani ni nini kingine niwezacho kufanya kwa sababu ya dhambi ya watu wangu?
Therefore thus saith the Lord of hosts: Behold I will melt, and try them: for what else shall I do before the daughter of my people?
8 Ndimi zao ni mshale wenye sumu, hunena kwa udanganyifu. Kwa kinywa chake kila mmoja huzungumza maneno mazuri na jirani yake, lakini moyoni mwake humtegea mtego.
Their tongue is a piercing arrow, it hath spoken deceit: with his mouth one speaketh peace with his friend, and secretly he lieth in wait for him.
9 Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya jambo hili?” asema Bwana. “Je, nisijilipizie kisasi kwa taifa kama hili?”
Shall I not visit them for these things, saith the Lord? or shall not my soul be revenged on such a nation?
10 Nitalia na kuomboleza kwa ajili ya milima na kuomboleza kuhusu malisho ya jangwani. Yamekuwa ukiwa, wala hakuna apitaye humo, milio ya ngʼombe haisikiki. Ndege wa angani wametoroka na wanyama wamekimbia.
For the mountains I will take up weeping and lamentation, and for the beautiful places of the desert, mourning: because they are burnt up, for that there is not a man that passeth through them: and they have not heard the voice of the owner: from the fowl of the air to the beasts they are gone away and departed.
11 “Nitaifanya Yerusalemu lundo la magofu, makao ya mbweha; nami nitaifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa ili asiwepo atakayeishi humo.”
And I will make Jerusalem to be heaps of sand, and dens of dragons: and I will make the cities of Juda desolate, for want of an inhabitant.
12 Ni mtu yupi aliye na hekima ya kutosha ayaelewe haya? Ni nani aliyefundishwa na Bwana awezaye kuyaeleza haya? Kwa nini nchi imeharibiwa na kufanywa ukiwa kama jangwa ambapo hakuna awezaye kupita?
Who is the wise man, that may understand this, and to whom the word of the mouth of the Lord may come that he may declare this, why the land hath perished, and is burnt up like a wilderness, which none passeth through?
13 Bwana akasema, “Ni kwa sababu wameiacha sheria yangu, niliyoiweka mbele yao: hawajaniheshimu mimi wala kufuata sheria yangu.
And the Lord said: Because they have forsaken my law, which I gave them, and have not heard my voice, and have not walked in it.
14 Badala yake wamefuata ukaidi wa mioyo yao, wamefuata Mabaali, kama vile baba zao walivyowafundisha.”
But they have gone after the perverseness of their own heart, and after Baalim, which their fathers taught them.
15 Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: “Tazama, nitawafanya watu hawa wale chakula kichungu na kunywa maji yenye sumu.
Therefore thus saith the Lord of hosts the God of Israel: Behold I will feed this people with wormwood, and give them water of gall to drink.
16 Nitawatawanya katika mataifa ambayo wao wala baba zao hawakuwajua, nikiwafuata kwa upanga mpaka niwe nimewaangamiza kabisa.”
And I will scatter them among the nations, which they and their fathers have not known: and I will send the sword after them till they be consumed.
17 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Fikiri sasa! Waite wanawake waombolezao waje, waite wale walio na ustadi kuliko wote.
Thus saith the Lord of hosts the God of Israel: Consider ye, and call for the mourning women, and let them come: and send to them that are wise women, and let them make haste:
18 Nao waje upesi na kutuombolezea, mpaka macho yetu yafurike machozi na vijito vya maji vitoke kwenye kope zetu.
Let them hasten and take up a lamentation for us: let our eyes shed tears, and our eyelids run down with waters.
19 Sauti ya kuomboleza imesikika kutoka Sayuni: ‘Tazama jinsi tulivyoangamizwa! Tazama jinsi aibu yetu ilivyo kubwa! Ni lazima tuihame nchi yetu kwa sababu nyumba zetu zimekuwa magofu.’”
For a voice of wailing is heard out of Sion: How are we wasted and greatly confounded? because we have left the land, because our dwellings are cast down.
20 Basi, enyi wanawake, sikieni neno la Bwana; fungueni masikio yenu msikie maneno ya kinywa chake. Wafundisheni binti zenu kuomboleza; fundishaneni kila mmoja na mwenzake maombolezo.
Hear therefore, ye women, the word of the Lord: and let your ears receive the word of his mouth: and teach your daughters wailing: and every one her neighbor mourning.
21 Mauti imeingia ndani kupitia madirishani, imeingia kwenye majumba yetu ya fahari; imewakatilia mbali watoto katika barabara na vijana waume kutoka viwanja vya miji.
For death is come up through our windows, it is entered into our houses to destroy the children from without, the young men from the streets.
22 Sema, “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Maiti za wanaume zitalala kama mavi katika mashamba, kama malundo ya nafaka nyuma ya mvunaji, wala hakuna anayekusanya.’”
Speak: Thus saith the Lord: Even the carcass of man shall fall as dung upon the face of the country, and as grass behind the back of the mower, and there is none to gather it.
23 Hili ndilo asemalo Bwana: “Mwenye hekima asijisifu katika hekima yake, au mwenye nguvu ajisifu katika nguvu zake, wala tajiri ajisifu katika utajiri wake,
Thus saith the Lord: Let not the wise man glory in his wisdom, and let not the strong man glory in his strength, and let not the rich man glory in his riches:
24 lakini yeye ajisifuye, na ajisifu kwa sababu hili: kwamba ananifahamu na kunijua mimi, kwamba mimi ndimi Bwana, nitendaye wema, hukumu na haki duniani, kwa kuwa napendezwa na haya,” asema Bwana.
But let him that glorieth glory in this, that he understandeth and knoweth me, for I am the Lord that exercise mercy, and judgment, and justice in the earth: for these things please me, saith the Lord.
25 “Siku zinakuja, nitakapowaadhibu wale wote ambao wametahiriwa kimwili tu, asema Bwana,
Behold, the days come, saith the Lord, and I will visit upon every one that hath the foreskin circumcised.
26 yaani Misri, Yuda, Edomu, Amoni, Moabu na wote wanaoishi jangwani sehemu za mbali. Kwa maana mataifa haya yote hayakutahiriwa mioyo yao, nayo nyumba yote ya Israeli haikutahiriwa.”
Upon Egypt, and upon Juda, and upon Edom, and upon the children of Ammon, and upon Moab, and upon all that have their hair polled round, that dwell in the desert: for all the nations are uncircumcised in the flesh, but all the house of Israel are uncircumcised in the heart.

< Yeremia 9 >