< Yeremia 8 >
1 “‘Wakati huo, asema Bwana, mifupa ya wafalme na maafisa wa Yuda, mifupa ya makuhani na manabii, na mifupa ya watu wa Yerusalemu itaondolewa kutoka makaburi yao.
"En ce temps-là, dit l’Eternel, on tirera de leurs tombeaux les ossements des rois de Juda, et les ossements de ses princes, et les ossements des prêtres, et les ossements des prophètes et les ossements des habitants de Jérusalem,
2 Itawekwa wazi kwa jua, na mwezi, na nyota zote za mbingu, ambazo walizipenda na kuzitumikia, na ambazo wamezifuata kutafuta ushauri na kuziabudu. Hawatakusanywa pamoja au kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyotapakaa juu ya ardhi.
et on les étalera à la face du soleil, de la lune et de tous les astres du ciel, qu’ils avaient aimés et adorés, qu’ils avaient suivis et recherchés, et devant lesquels ils s’étaient prosternés; ils ne seront ni recueillis ni rendus à la tombe: ils serviront d’engrais à la surface du sol.
3 Popote nitakapowafukuzia, mabaki wote wa kizazi hiki kiovu watatamani kufa kuliko kuishi, asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.’
Alors la mort paraîtra plus désirable que la vie à tous les survivants qui resteront de cette race perverse, qui resteront dans les lieux où je les reléguerai", dit l’Eternel-Cebaot.
4 “Waambie, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “‘Je, watu wanapoanguka hawainuki? Je, mtu anapopotea harudi?
Tu leur diras: "Si l’on tombe, ne doit-on pas se relever? Si l’on se détourne, ne doit-on pas revenir?
5 Kwa nini basi watu hawa walipotea? Kwa nini Yerusalemu inapotea kila mara? Wanangʼangʼania udanganyifu na wanakataa kurudi.
Pourquoi ce peuple, à Jérusalem, se rend-il coupable d’une défection obstinée? Pourquoi persévèrent-ils dans la fraude, refusent-ils de s’amender?
6 Nimewasikiliza kwa makini, lakini hawataki kusema lililo sawa. Hakuna anayetubia makosa yake akisema, “Nimefanya nini?” Kila mmoja hufuata njia yake mwenyewe kama farasi anayekwenda vitani.
J’Ai prêté attention et j’ai écouté: ils profèrent des mensonges, personne parmi eux ne regrette ses mauvaises actions et ne dit: "Qu’ai-je fait?" Tous ils reprennent leur course, tels qu’un cheval qui se précipite au combat.
7 Hata korongo aliyeko angani anayajua majira yake yaliyoamriwa, nao njiwa, mbayuwayu na koikoi hufuata majira yao ya kurudi. Lakini watu wangu hawajui Bwana anachotaka kwao.
Même la cigogne dans les airs connaît les saisons qui lui sont propres; la tourterelle, l’hirondelle et la grue observent l’époque de leurs migrations, mais mon peuple ne connaît point la loi de l’Eternel!
8 “‘Mwawezaje kusema, “Sisi tuna busara kwa sababu tunayo sheria ya Bwana,” wakati ambapo kwa hakika kalamu ya uongo ya waandishi imeandika kwa udanganyifu?
Comment pouvez-vous dire: "Nous sommes des sages! Nous sommes en possession de la doctrine de l’Eternel!" Oui, mais le stylet mensonger des scribes en a fait un mensonge!
9 Wenye hekima wataaibika, watafadhaika na kunaswa. Kwa kuwa wamelikataa neno la Bwana, hiyo hekima waliyo nayo ni ya namna gani?
Ils seront couverts de confusion, ces sages. Ils seront pris de terreur, ils seront capturés; aussi bien, ils ont traité avec dédain la parole de l’Eternel: en quoi consiste donc leur sagesse?
10 Kwa hiyo nitawapa watu wengine wake zao, na mashamba yao kwa wamiliki wengine. Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa, wote wana tamaa ya kupata zaidi; manabii na makuhani wanafanana, wote wanafanya udanganyifu.
C’Est pourquoi je livrerai leurs femmes à d’autres, leurs champs à des conquérants; car, du plus petit au plus grand, tous sont âpres au gain; du prophète jusqu’au prêtre, tous pratiquent le mensonge.
11 Wanafunga majeraha ya watu wangu bila uangalifu. Wanasema, “Amani, amani,” wakati hakuna amani.
Ils ont bien vite fait de remédier à la ruina de mon peuple en disant: "Paix! Paix!" et il n’y a point de paix.
12 Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yao inayochukiza mno? Hapana, hawana aibu hata kidogo, hawajui hata kuona haya. Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka, watashushwa chini watakapoadhibiwa, asema Bwana.
Ils devraient avoir honte de commettre des abominations; mais ils n’ont aucune pudeur ni ne savent rougir; aussi succomberont-ils avec ceux qui succombent; à l’heure où j’aurai à les châtier, ils trébucheront", dit l’Eternel.
13 “‘Nitayaondoa mavuno yao, asema Bwana. Hapatakuwepo zabibu kwenye mzabibu. Hapatakuwepo na tini kwenye mtini, majani yake yatanyauka. Kile nilichowapa watanyangʼanywa.’”
"Je suis décidé à en finir avec eux", dit l’Eternel. Il n’y a plus de raisins au vignoble, ni de figues au figuier, les feuilles sont flétries: ce que je leur avais donné passera en d’autres mains.
14 “Kwa nini tunaketi hapa? Kusanyikeni pamoja! Tukimbilie kwenye miji yenye maboma, tukaangamie huko! Kwa kuwa Bwana, Mungu wetu ametuhukumu kuangamia, na kutupa maji yenye sumu tunywe, kwa sababu tumemtenda dhambi.
Pourquoi demeurons-nous sur place? Rassemblez-vous! Retirons-nous dans les villes fortes et demeurons-y immobiles, car l’Eternel, notre Dieu, nous a condamnés à périr et abreuvés d’eaux empoisonnées, parce que nous avons péché contre l’Eternel.
15 Tulitegemea amani, lakini hakuna jema lililokuja, tulitegemea wakati wa kupona, lakini kulikuwa hofu tu.
On espérait la paix, et rien d’heureux n’arrive; une ère de réparation, et voici l’épouvante!
16 Mkoromo wa farasi za adui umesikika kuanzia Dani, kwa mlio wa madume yao ya farasi, nchi yote inatetemeka. Wamekuja kuangamiza nchi na vyote vilivyomo, mji na wote waishio ndani yake.”
Depuis Dan on entend le souffle de ses chevaux, le bruyant hennissement de ses puissants coursiers fait trembler la terre: ils viennent et dévorent le pays avec ce qu’il renferme, la ville et ses habitants.
17 “Tazama, nitatuma nyoka wenye sumu kali katikati yenu, fira ambao hawawezi kulogwa, nao watawauma,” asema Bwana.
Car je vais lâcher contre vous des serpents, des basilics qui défient toute incantation; ils vous déchireront de leurs morsures, dit l’Eternel.
18 Ee Mfariji wangu katika huzuni, moyo wangu umezimia ndani yangu.
Comme je voudrais dominer ma douleur! Mon coeur souffre au dedans de moi.
19 Sikia kilio cha watu wangu kutoka nchi ya mbali: “Je, Bwana hayuko Sayuni? Je, Mfalme wake hayuko tena huko?” “Kwa nini wamenikasirisha kwa vinyago vyao, kwa sanamu zao za kigeni zisizofaa?”
Voici, j’entends la voix suppliante de la fille de mon peuple venant d’un pays lointain: "L’Eternel n’est-il plus à Sion? Son roi n’y est-il plus? Pourquoi aussi m’ont-ils contrarié par leurs idoles, les vaines divinités de l’étranger?"
20 “Mavuno yamepita, kiangazi kimekwisha, nasi hatujaokolewa.”
La moisson est achevée, la récolte touche à sa fin et nous n’avons pas reçu de secours!
21 Kwa kuwa watu wangu wamepondwa, nami nimepondeka pia; ninaomboleza, nayo hofu kuu imenishika.
A cause de la catastrophe qui a brisé la fille de mon peuple, je suis brisé; je suis voilé de deuil, en proie au désespoir.
22 Je, hakuna zeri ya kuponya katika Gileadi? Je, hakuna tabibu huko? Kwa nini basi hakuna uponyaji wa majeraha ya watu wangu?
N’Y a-t-il plus de baume à Galaad? Ne s’y trouve-t-il plus de médecin? Pourquoi ne s’offre-t-il aucun remède pour la fille de mon peuple?