< Yeremia 8 >
1 “‘Wakati huo, asema Bwana, mifupa ya wafalme na maafisa wa Yuda, mifupa ya makuhani na manabii, na mifupa ya watu wa Yerusalemu itaondolewa kutoka makaburi yao.
En ce temps-là, dit l’Éternel, on sortira de leurs sépulcres les os des rois de Juda, et les os de ses princes, et les os des sacrificateurs, et les os des prophètes, et les os des habitants de Jérusalem,
2 Itawekwa wazi kwa jua, na mwezi, na nyota zote za mbingu, ambazo walizipenda na kuzitumikia, na ambazo wamezifuata kutafuta ushauri na kuziabudu. Hawatakusanywa pamoja au kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyotapakaa juu ya ardhi.
et on les étendra devant le soleil, et devant la lune, et devant toute l’armée des cieux, qu’ils ont aimés, et qu’ils ont servis, et après lesquels ils ont marché, et qu’ils ont recherchés, et devant lesquels ils se sont prosternés: ils ne seront pas recueillis, et ne seront pas enterrés; ils seront du fumier sur la face du sol.
3 Popote nitakapowafukuzia, mabaki wote wa kizazi hiki kiovu watatamani kufa kuliko kuishi, asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.’
Et tout le résidu choisira la mort plutôt que la vie, ceux qui restent de cette méchante famille dans tous les lieux où j’aurai chassé ceux qui sont de reste, dit l’Éternel des armées.
4 “Waambie, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “‘Je, watu wanapoanguka hawainuki? Je, mtu anapopotea harudi?
Et tu leur diras: Ainsi dit l’Éternel: Est-ce qu’on tombe, et qu’on ne se relève pas? Est-ce qu’on se détourne, et qu’on ne revient pas?
5 Kwa nini basi watu hawa walipotea? Kwa nini Yerusalemu inapotea kila mara? Wanangʼangʼania udanganyifu na wanakataa kurudi.
Pourquoi ce peuple de Jérusalem s’est-il détourné par un égarement continuel? Ils tiennent ferme à la tromperie, ils refusent de revenir.
6 Nimewasikiliza kwa makini, lakini hawataki kusema lililo sawa. Hakuna anayetubia makosa yake akisema, “Nimefanya nini?” Kila mmoja hufuata njia yake mwenyewe kama farasi anayekwenda vitani.
J’ai fait attention, et j’ai écouté: ils ne parlent pas droitement, il n’y a personne qui se repente de son iniquité, disant: Qu’ai-je fait? Tous ils retournent à leur course, comme le cheval qui se précipite dans la bataille.
7 Hata korongo aliyeko angani anayajua majira yake yaliyoamriwa, nao njiwa, mbayuwayu na koikoi hufuata majira yao ya kurudi. Lakini watu wangu hawajui Bwana anachotaka kwao.
Même la cigogne dans les cieux connaît sa saison; et la tourterelle, et l’hirondelle, et la grue, prennent garde au temps où elles doivent venir, mais mon peuple ne connaît pas le jugement de l’Éternel.
8 “‘Mwawezaje kusema, “Sisi tuna busara kwa sababu tunayo sheria ya Bwana,” wakati ambapo kwa hakika kalamu ya uongo ya waandishi imeandika kwa udanganyifu?
Comment dites-vous: Nous sommes sages, et la loi de l’Éternel est avec nous? – Mais voici, la plume menteuse des scribes [en] a fait une fausseté.
9 Wenye hekima wataaibika, watafadhaika na kunaswa. Kwa kuwa wamelikataa neno la Bwana, hiyo hekima waliyo nayo ni ya namna gani?
Les sages sont couverts de honte, ils ont peur, et sont pris; voici, ils ont méprisé la parole de l’Éternel, et quelle sagesse ont-ils?
10 Kwa hiyo nitawapa watu wengine wake zao, na mashamba yao kwa wamiliki wengine. Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa, wote wana tamaa ya kupata zaidi; manabii na makuhani wanafanana, wote wanafanya udanganyifu.
C’est pourquoi je donnerai leurs femmes à d’autres, leurs champs à ceux qui les posséderont; car depuis le petit jusqu’au grand, ils sont tous adonnés au gain déshonnête; depuis le prophète jusqu’au sacrificateur, tous usent de fausseté.
11 Wanafunga majeraha ya watu wangu bila uangalifu. Wanasema, “Amani, amani,” wakati hakuna amani.
Et ils ont pansé la plaie de la fille de mon peuple légèrement, disant: Paix, paix! et il n’y avait point de paix.
12 Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yao inayochukiza mno? Hapana, hawana aibu hata kidogo, hawajui hata kuona haya. Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka, watashushwa chini watakapoadhibiwa, asema Bwana.
Avaient-ils honte, parce qu’ils avaient commis l’abomination? Ils n’ont eu même aucune honte, et ils ne savent pas ce que c’est que d’être confus; c’est pourquoi ils tomberont parmi ceux qui tombent; au temps de leur visitation ils trébucheront, dit l’Éternel.
13 “‘Nitayaondoa mavuno yao, asema Bwana. Hapatakuwepo zabibu kwenye mzabibu. Hapatakuwepo na tini kwenye mtini, majani yake yatanyauka. Kile nilichowapa watanyangʼanywa.’”
Je les ôterai entièrement, dit l’Éternel. Il n’y a pas de raisins sur la vigne, et pas de figues sur le figuier, et la feuille est flétrie; et je les livrerai à ceux qui passeront sur eux.
14 “Kwa nini tunaketi hapa? Kusanyikeni pamoja! Tukimbilie kwenye miji yenye maboma, tukaangamie huko! Kwa kuwa Bwana, Mungu wetu ametuhukumu kuangamia, na kutupa maji yenye sumu tunywe, kwa sababu tumemtenda dhambi.
Pourquoi sommes-nous là assis? Assemblez-vous, et entrons dans les villes fortes, et là nous garderons le silence; car l’Éternel, notre Dieu, nous a réduits au silence et nous a fait boire de l’eau de fiel, car nous avons péché contre l’Éternel.
15 Tulitegemea amani, lakini hakuna jema lililokuja, tulitegemea wakati wa kupona, lakini kulikuwa hofu tu.
On attend la paix, et il n’y a rien de bon, – le temps de la guérison, et voici l’épouvante.
16 Mkoromo wa farasi za adui umesikika kuanzia Dani, kwa mlio wa madume yao ya farasi, nchi yote inatetemeka. Wamekuja kuangamiza nchi na vyote vilivyomo, mji na wote waishio ndani yake.”
De Dan nous avons entendu le ronflement de ses chevaux; au bruit des hennissements de ses puissants [coursiers] tout le pays a tremblé; ils sont venus, et ont dévoré le pays et ce qu’il contient, la ville et ceux qui y habitent.
17 “Tazama, nitatuma nyoka wenye sumu kali katikati yenu, fira ambao hawawezi kulogwa, nao watawauma,” asema Bwana.
Car voici, j’envoie au milieu de vous des serpents, des vipères, contre lesquels il n’y a point de charmes, et ils vous mordront, dit l’Éternel.
18 Ee Mfariji wangu katika huzuni, moyo wangu umezimia ndani yangu.
Ô ma consolation dans ma douleur! Mon cœur est languissant au-dedans de moi.
19 Sikia kilio cha watu wangu kutoka nchi ya mbali: “Je, Bwana hayuko Sayuni? Je, Mfalme wake hayuko tena huko?” “Kwa nini wamenikasirisha kwa vinyago vyao, kwa sanamu zao za kigeni zisizofaa?”
Voici, la voix du cri de la fille de mon peuple [vient] d’un pays lointain: L’Éternel n’est-il pas dans Sion? Son Roi n’est-il pas au milieu d’elle? Pourquoi m’ont-ils provoqué par leurs images taillées, par les vanités de l’étranger?
20 “Mavuno yamepita, kiangazi kimekwisha, nasi hatujaokolewa.”
La moisson est passée, l’été est fini, et nous ne sommes pas sauvés.
21 Kwa kuwa watu wangu wamepondwa, nami nimepondeka pia; ninaomboleza, nayo hofu kuu imenishika.
Je suis brisé de la ruine de la fille de mon peuple; je mène deuil, l’épouvante m’a saisi.
22 Je, hakuna zeri ya kuponya katika Gileadi? Je, hakuna tabibu huko? Kwa nini basi hakuna uponyaji wa majeraha ya watu wangu?
N’y a-t-il point de baume en Galaad? N’y a-t-il point là de médecin? Car pourquoi n’a-t-on pas appliqué un appareil de pansement à la fille de mon peuple?