< Yeremia 7 >

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
Parole qui a été adressée à Jérémie par le Seigneur, disant:
2 “Simama kwenye lango la nyumba ya Bwana, na huko upige mbiu ya ujumbe huu: “‘Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mliokuja kupitia malango haya ili kumwabudu Bwana.
Tiens-toi à la porte de la maison du Seigneur, et publie là cette parole, et dis: Ecoutez la parole du Seigneur, vous tous, habitants de Juda, qui entrez par ces portes afin d’adorer le Seigneur.
3 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Tengenezeni njia zenu na matendo yenu, nami nitawaacha mkae mahali hapa.
Voici ce que dit le Seigneur des armées, Dieu d’Israël: Rendez bonnes vos voies et vos œuvres; et j’habiterai avec vous dans ce lieu.
4 Msitumainie maneno ya udanganyifu na kusema, “Hili ni Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana!”
Ne vous confiez pas en des paroles de mensonge, disant: Le temple du Seigneur, le temple du Seigneur, c’est le temple du Seigneur.
5 Kama kweli mkibadili njia zenu na matendo yenu, mkatendeana haki kila mmoja na mwenzake,
Parce que si vous dirigez bien vos voies et vos œuvres; si vous faites la Justice entre un homme et son prochain;
6 kama msipomwonea mgeni, yatima wala mjane, na kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa, nanyi kama msipofuata miungu mingine kwa madhara yenu wenyewe,
Si vous ne faites point de violence à l’étranger, au pupille et à la veuve; si vous ne répandez pas un sang innocent en ce lieu, et si vous ne marchez pas à la suite des dieux étrangers pour votre propre malheur:
7 ndipo nitawaacha mkae mahali hapa, katika nchi niliyowapa baba zenu milele na milele.
J’habiterai avec vous d’un siècle à un autre siècle dans ce lieu, dans cette terre que j’ai donnée à vos pères.
8 Lakini tazama, mnatumainia maneno ya udanganyifu yasiyo na maana.
Mais voilà que vous vous confiez en des paroles de mensonge, qui ne vous seront pas utiles:
9 “‘Je, mtaiba na kuua, mtazini na kuapa kwa uongo, na kufukiza uvumba kwa Baali, na kufuata miungu mingine ambayo hamkuijua,
Dérober, tuer, commettre l’adultère, jurer en mentant, faire des libations aux Baalim, aller à la suite de dieux étrangers que vous ne connaissez pas.
10 kisha mje na kusimama mbele yangu katika nyumba hii inayoitwa kwa Jina langu, mkisema, “Tuko salama.” Salama kwa kufanya mambo haya yote ya kuchukiza?
Et vous êtes venus vous présenter devant moi dans cette maison, dans laquelle a été invoqué mon nom, et vous avez dit. Nous sommes délivrés, parce que nous avons fait toutes ces abominations.
11 Je, nyumba hii, iitwayo kwa Jina langu, imekuwa pango la wanyangʼanyi kwenu? Lakini nimekuwa nikiona yanayotendeka! asema Bwana.
Est-ce donc qu’elle est devenue une caverne de voleurs, cette maison dans laquelle a été invoqué mon nom devant vos yeux? C’est moi, moi qui suis; moi qui ai vu, dit le Seigneur.
12 “‘Nendeni sasa mahali pangu palipokuwa huko Shilo, mahali ambapo nilipafanya pa kwanza kuwa makao ya Jina langu, nanyi mwone lile nililopafanyia kwa ajili ya uovu wa watu wangu Israeli.
Allez à mon lieu, à Silo, où a habité mon nom dès le commencement, et voyez ce que je lui ai fait, à cause de la méchanceté d’Israël, mon peuple;
13 Mlipokuwa mnafanya yote haya, asema Bwana, nilisema nanyi tena na tena, lakini hamkusikiliza; niliwaita, lakini hamkujibu.
Et maintenant, parce que vous avez fait toutes ces choses, dit le Seigneur, et que je vous ai parlé, me levant dès le matin, et parlant, que vous n’avez pas entendu; que je vous ai appelés et que vous n’avez pas répondu:
14 Kwa hiyo, nililolifanyia Shilo, nitalifanya sasa kwa nyumba hii iitwayo kwa Jina langu, Hekalu mnalolitumainia, mahali nilipowapa ninyi na baba zenu.
Je ferai à cette maison, dans laquelle a été invoqué mon nom, et en laquelle vous avez confiance, et à ce lieu que je vous ai donné à vous et à vos pères, comme j’ai fait à Silo.
15 Nitawafukuza mbele yangu, kama nilivyowafanyia ndugu zenu, watu wa Efraimu.’
Et je vous rejetterai de ma face, comme j’ai rejeté tous vos frères, toute la race d’Ephraïm.
16 “Kwa hiyo usiombe kwa ajili ya watu hawa, wala usinililie, na usifanye maombi kwa ajili yao; usinisihi, kwa sababu sitakusikiliza.
Toi donc, ne prie pas pour ce peuple, ne m’adresse pour eux ni louange ni prière, et ne t’oppose pas à moi, parce que je ne t’exaucerai point.
17 Je, huyaoni hayo wanayoyatenda katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu?
Ne vois-tu pas ce que font ceux-ci dans les villes de Juda, et dans les places publiques de Jérusalem?
18 Watoto wanakusanya kuni, baba zao wanawasha moto, na wanawake wanakanda unga na kuoka mikate kwa ajili ya Malkia wa Mbinguni. Wanamimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine ili kunikasirisha.
Les fils amassent le bois, les pères allument le feu, et les femmes arrosent de farine la graisse, afin de faire des gâteaux à la reine du ciel, des libations à des dieux étrangers, et me provoquer au courroux.
19 Lakini je, mimi ndiye wanayenikasirisha? asema Bwana. Je, hawajiumizi wenyewe na kujiaibisha?
Est-ce moi qu’ils provoquent au courroux, dit le Seigneur? N’est-ce pas eux-mêmes qu’il provoquent à la confusion de leur visage?
20 “‘Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenyezi: Hasira yangu na ghadhabu yangu itamwagwa mahali hapa, juu ya mwanadamu na mnyama, juu ya miti ya shambani na juu ya matunda ya ardhini, nayo itaungua pasipo kuzimwa.
C’est pourquoi voici ce que dit le Seigneur Dieu: Voilà que ma fureur et mon indignation se sont embrasées sur ce lieu, sur les hommes et sur les animaux; sur les arbres de la contrée, et sur les fruits de la terre; et un feu brûlera, et il ne s’éteindra pas.
21 “‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Endeleeni, ongezeni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya dhabihu zenu nyingine, mle nyama hiyo wenyewe!
Voici ce que dit le Seigneur des armées. Dieu d’Israël: Ajoutez vos holocaustes à vos victimes, et mangez-en les chairs;
22 Kwa kuwa nilipowaleta baba zenu kutoka Misri na kusema nao, sikuwapa amri kuhusu sadaka za kuteketezwa na dhabihu tu,
Parce que je n’ai point parlé à vos pères, je ne leur ai rien commandé au jour que je les ai tirés de la terre d’Egypte, au sujet des holocaustes et des victimes.
23 lakini niliwapa amri hii nikisema: Nitiini mimi, nami nitakuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu. Enendeni katika njia zote ninazowaamuru ili mpate kufanikiwa.
Mais voici la chose que je leur ai commandée: Ecoutez ma voix, et je serai votre Dieu, et vous serez mon peuple; et marchez dans toute la voie que je vous ai prescrite, afin que bien vous soit.
24 Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Walirudi nyuma badala ya kusonga mbele.
Et ils n’ont pas écouté, et ils n’ont pas incliné leur oreille; mais ils se sont abandonnés à leurs volontés et à la dépravation de leur cœur mauvais; ils sont allés en arrière, et non en avant,
25 Tangu wakati ule baba zenu walipotoka Misri hadi sasa, siku baada ya siku, tena na tena nimewatumia watumishi wangu manabii.
Depuis le jour que leurs pères sont sortis de l’Egypte jusqu’à ce jour. Et je vous ai envoyé tous mes serviteurs les prophètes, me levant au point du jour, et les envoyant.
26 Lakini hawakunisikiliza wala hawakujali. Walikuwa na shingo ngumu na kufanya maovu kuliko baba zao.’
Et ils ne m’ont pas écouté, et ils n’ont pas incliné leur oreille; mais ils ont rendu leur cou inflexible, et ils ont fait pis que leurs pères.
27 “Utakapowaambia haya yote, hawatakusikiliza; utakapowaita, hawatajibu.
Et tu leur diras toutes ces choses, et ils ne t’écouteront point; tu les appelleras, et ils ne te répondront point.
28 Kwa hiyo waambie, ‘Hili ni taifa ambalo halimtii Bwana, Mungu wao, wala kukubali maonyo. Kweli imekufa, imetoweka midomoni mwao.
Et tu leur diras: Voici la nation qui n’a pas écouté la voix du Seigneur son Dieu, et qui n’a pas reçu sa correction; la bonne foi a péri, et elle a été enlevée de leur bouche.
29 Nyoeni nywele zenu na kuzitupa, ombolezeni katika miinuko iliyo kame, kwa kuwa Bwana amekikataa na kukiacha kizazi hiki kilichomkasirisha.
Tonds ta chevelure, et jette-la; pousse en haut des plaintes, parce que le Seigneur a rejeté et abandonné la génération de sa fureur.
30 “‘Watu wa Yuda wamefanya maovu machoni pangu, asema Bwana. Wameziweka sanamu zao za machukizo ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu, na wameitia unajisi.
Parce que les fils de Juda ont fait le mal devant mes yeux, dit le Seigneur. Ils ont mis leurs pierres d’achoppement dans la maison dans laquelle a été invoqué mon nom, afin de la souiller;
31 Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia sanamu pa Tofethi kwenye Bonde la Ben-Hinomu ili kuwateketeza wana wao na binti zao kwenye moto, kitu ambacho sikuamuru, wala hakikuingia akilini mwangu.
Et ils ont bâti des hauts lieux à Topheth, qui est dans la Vallée du fils d’Ennom, afin d’y brûler leurs fils et leurs filles au feu; choses que je n’ai pas ordonnées, ni pensées dans mon cœur.
32 Kwa hiyo mjihadhari, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu watakapokuwa hawapaiti Tofethi au Bonde la Ben-Hinomu, lakini watapaita Bonde la Machinjo, kwa sababu watawazika wafu huko Tofethi mpaka pasiwe tena nafasi.
C’est pourquoi voilà que des jours viendront, dit le Seigneur, et l’on ne dira plus Topheth, et la Vallée du fils d’Ennom; mais la Vallée du carnage; et l’on ensevelira à Topheth, parce qu’il n’y aura pas d’autre lieu pour ensevelir.
33 Ndipo mizoga ya watu hawa itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwafukuza.
Et les cadavres de ce peuple seront en pâture aux oiseaux du ciel et aux bêtes de la terre, et il n’y aura personne qui les chasse.
34 Nitazikomesha sauti za shangwe na furaha, na sauti za bwana arusi na bibi arusi katikati ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, kwa sababu nchi itakuwa ukiwa.
Et je ferai cesser, dans les villes de Juda et dans les places publiques de Jérusalem, la voix de la joie et la voix de l’allégresse, la voix de l’époux et la voix de l’épouse; car la terre sera désolée.

< Yeremia 7 >