< Yeremia 7 >
1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
The word that was maad of the Lord to Jeremye,
2 “Simama kwenye lango la nyumba ya Bwana, na huko upige mbiu ya ujumbe huu: “‘Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mliokuja kupitia malango haya ili kumwabudu Bwana.
and seide, Stonde thou in the yate of the hous of the Lord, and preche there this word, and seie, Al Juda, that entren bi these yatis for to worschipe the Lord, here ye the word of the Lord.
3 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Tengenezeni njia zenu na matendo yenu, nami nitawaacha mkae mahali hapa.
The Lord of oostis, God of Israel, seith these thingis, Make ye good youre weies, and youre studies, and Y schal dwelle with you in this place.
4 Msitumainie maneno ya udanganyifu na kusema, “Hili ni Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana!”
Nyle ye triste in the wordis of leesyng, and seie, The temple of the Lord, the temple of the Lord, the temple of the Lord is.
5 Kama kweli mkibadili njia zenu na matendo yenu, mkatendeana haki kila mmoja na mwenzake,
For if ye blessen youre weies, and your studies; if ye doon doom bitwixe a man and his neiybore;
6 kama msipomwonea mgeni, yatima wala mjane, na kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa, nanyi kama msipofuata miungu mingine kwa madhara yenu wenyewe,
if ye maken not fals caleng to a comelyng, and to a fadirles child, and to a widewe; nether scheden out innocent blood in this place, and goen not after alien goddis, in to yuel to you silf,
7 ndipo nitawaacha mkae mahali hapa, katika nchi niliyowapa baba zenu milele na milele.
Y schal dwelle with you in this place, in the lond which Y yaf to youre fadris, fro the world and til in to the world.
8 Lakini tazama, mnatumainia maneno ya udanganyifu yasiyo na maana.
Lo! ye trusten to you in the wordis of leesyng, that shulen not profite to you;
9 “‘Je, mtaiba na kuua, mtazini na kuapa kwa uongo, na kufukiza uvumba kwa Baali, na kufuata miungu mingine ambayo hamkuijua,
to stele, to sle, to do auowtrie, to swere falsli, to make sacrifice to Baalym, and to go aftir alien goddys, whiche ye knowen not.
10 kisha mje na kusimama mbele yangu katika nyumba hii inayoitwa kwa Jina langu, mkisema, “Tuko salama.” Salama kwa kufanya mambo haya yote ya kuchukiza?
And ye camen, and stoden bifor me in this hous, in which my name is clepid to help; and ye seiden, We ben delyuered, for we han do alle these abhomynaciouns.
11 Je, nyumba hii, iitwayo kwa Jina langu, imekuwa pango la wanyangʼanyi kwenu? Lakini nimekuwa nikiona yanayotendeka! asema Bwana.
Whether therfor this hous, wherynne my name is clepid to help bifore youre iyen, is maad a denne of theues? I, Y am, Y siy, seith the Lord.
12 “‘Nendeni sasa mahali pangu palipokuwa huko Shilo, mahali ambapo nilipafanya pa kwanza kuwa makao ya Jina langu, nanyi mwone lile nililopafanyia kwa ajili ya uovu wa watu wangu Israeli.
Go ye to my place in Silo, where my name dwellide at the bigynnyng, and se ye what thingis Y dide to it, for the malice of my puple Israel.
13 Mlipokuwa mnafanya yote haya, asema Bwana, nilisema nanyi tena na tena, lakini hamkusikiliza; niliwaita, lakini hamkujibu.
And now, for ye han do alle these werkis, seith the Lord, and Y spak to you, and roos eerli, and Y spak, and ye herden not, and Y clepide you, and ye answeriden not;
14 Kwa hiyo, nililolifanyia Shilo, nitalifanya sasa kwa nyumba hii iitwayo kwa Jina langu, Hekalu mnalolitumainia, mahali nilipowapa ninyi na baba zenu.
Y schal do to this hous, wherynne my name is clepid to help, and in which hous ye han trist, and to the place which Y yaf to you and to youre fadris, as Y dide to Silo.
15 Nitawafukuza mbele yangu, kama nilivyowafanyia ndugu zenu, watu wa Efraimu.’
And Y schal caste you forth fro my face, as Y castide forth alle youre britheren, al the seed of Effraym.
16 “Kwa hiyo usiombe kwa ajili ya watu hawa, wala usinililie, na usifanye maombi kwa ajili yao; usinisihi, kwa sababu sitakusikiliza.
Therfor nyl thou preie for this puple, nether take thou heriyng and preier for hem; and ayenstonde thou not me, for Y schal not here thee.
17 Je, huyaoni hayo wanayoyatenda katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu?
Whether thou seest not, what these men don in the citees of Juda, and in the stretis of Jerusalem?
18 Watoto wanakusanya kuni, baba zao wanawasha moto, na wanawake wanakanda unga na kuoka mikate kwa ajili ya Malkia wa Mbinguni. Wanamimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine ili kunikasirisha.
The sones gaderen stickis, and the fadris kyndlen a fier; and wymmen sprengen togidere ynnere fatnesse, to make kakis to the queen of heuene, to make sacrifice to alien goddis, and to terre me to wrathfulnesse.
19 Lakini je, mimi ndiye wanayenikasirisha? asema Bwana. Je, hawajiumizi wenyewe na kujiaibisha?
Whether thei stiren me to wrathfulnesse? seith the Lord; whether thei stiren not hem silf in to schenschip of her cheer?
20 “‘Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenyezi: Hasira yangu na ghadhabu yangu itamwagwa mahali hapa, juu ya mwanadamu na mnyama, juu ya miti ya shambani na juu ya matunda ya ardhini, nayo itaungua pasipo kuzimwa.
Therfor the Lord God seith these thingis, Lo! my strong veniaunce and myn indignacioun is wellid togidere on this place, on men, and on beestis, and on the tree of the cuntrei, and on the fruitis of erthe; and it schal be kyndlid, and it schal not be quenchid.
21 “‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Endeleeni, ongezeni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya dhabihu zenu nyingine, mle nyama hiyo wenyewe!
The Lord of oostis, God of Israel, seith these thingis, Heepe ye youre brent sacrifices to youre slayn sacrifices, and ete ye fleischis.
22 Kwa kuwa nilipowaleta baba zenu kutoka Misri na kusema nao, sikuwapa amri kuhusu sadaka za kuteketezwa na dhabihu tu,
For Y spak not with youre fadris, and Y comaundide not to hem of the word of brent sacrifices, and of slayn sacrifices, in the dai in which Y ledde hem out of the lond of Egipt.
23 lakini niliwapa amri hii nikisema: Nitiini mimi, nami nitakuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu. Enendeni katika njia zote ninazowaamuru ili mpate kufanikiwa.
But Y comaundide this word to hem, and Y seide, Here ye my vois, and Y schal be God to you, and ye schulen be a puple to me; and go ye in al the weie which Y comaundide to you, that it be wel to you.
24 Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Walirudi nyuma badala ya kusonga mbele.
And thei herden not, nether bowiden doun her eere, but thei yeden in her lustis, and in the schrewidnesse of her yuel herte; and thei ben put bihynde, and not bifore,
25 Tangu wakati ule baba zenu walipotoka Misri hadi sasa, siku baada ya siku, tena na tena nimewatumia watumishi wangu manabii.
fro the dai in which her fadris yeden out of the lond of Egipt til to this dai. And Y sente to you alle my seruauntis profetis, and Y roos eerli bi the dai, and Y sente.
26 Lakini hawakunisikiliza wala hawakujali. Walikuwa na shingo ngumu na kufanya maovu kuliko baba zao.’
And thei herden not me, nether bowiden doun her eere; but thei maden hard her nol, and wrouyten worse than the fadris of hem.
27 “Utakapowaambia haya yote, hawatakusikiliza; utakapowaita, hawatajibu.
And thou schalt speke to hem alle these wordis, and thei schulen not heere thee; and thou schalt clepe hem, and thei schul not answere to thee.
28 Kwa hiyo waambie, ‘Hili ni taifa ambalo halimtii Bwana, Mungu wao, wala kukubali maonyo. Kweli imekufa, imetoweka midomoni mwao.
And thou schalt seie to hem, This is the folc, that herde not the vois of her Lord God, nether resseyuede chastysyng; feith perischide, and is takun awei fro the mouth of hem.
29 Nyoeni nywele zenu na kuzitupa, ombolezeni katika miinuko iliyo kame, kwa kuwa Bwana amekikataa na kukiacha kizazi hiki kilichomkasirisha.
Clippe thin heer, and cast awei, and take thou weilyng streiytli; for the Lord hath cast awei, and hath forsake the generacioun of his strong veniaunce.
30 “‘Watu wa Yuda wamefanya maovu machoni pangu, asema Bwana. Wameziweka sanamu zao za machukizo ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu, na wameitia unajisi.
For the sones of Juda han do yuel bifor myn iyen, seith the Lord; thei han set her offendyngis in the hous, in which my name is clepid to help, that thei schulden defoule that hous;
31 Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia sanamu pa Tofethi kwenye Bonde la Ben-Hinomu ili kuwateketeza wana wao na binti zao kwenye moto, kitu ambacho sikuamuru, wala hakikuingia akilini mwangu.
and thei bildiden hiye thingis in Tophet, which is in the valei of the sone of Ennon, that thei schulden brenne her sones and her douytris bi fier, whiche thingis Y comaundide not, nether thouyte in myn herte.
32 Kwa hiyo mjihadhari, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu watakapokuwa hawapaiti Tofethi au Bonde la Ben-Hinomu, lakini watapaita Bonde la Machinjo, kwa sababu watawazika wafu huko Tofethi mpaka pasiwe tena nafasi.
Therfor lo! daies comen, seith the Lord, and it schal no more be seid Tophet, and the valei of the sone of Ennon, but the valey of sleyng; and thei schulen birie in Tophet, for ther is no place.
33 Ndipo mizoga ya watu hawa itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwafukuza.
And the deed careyn of this puple schal be in to mete to the briddis of heuene, and to the beestis of erthe; and noon schal be that schal dryue awei.
34 Nitazikomesha sauti za shangwe na furaha, na sauti za bwana arusi na bibi arusi katikati ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, kwa sababu nchi itakuwa ukiwa.
And Y schal make to ceesse the vois of ioye, and the vois of gladnesse, and the vois of spouse, and the vois of spousesse fro the citees of Juda, and fro the stretis of Jerusalem; for the lond schal be in desolacioun.