< Yeremia 7 >

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
The word that came to Jeremiah from Yahweh, saying,
2 “Simama kwenye lango la nyumba ya Bwana, na huko upige mbiu ya ujumbe huu: “‘Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mliokuja kupitia malango haya ili kumwabudu Bwana.
“Stand at the gate of Yahweh's house and proclaim this word! Say, 'Hear the word of Yahweh, all you of Judah, you who enter these gates to worship Yahweh.
3 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Tengenezeni njia zenu na matendo yenu, nami nitawaacha mkae mahali hapa.
Yahweh of hosts, God of Israel, says this: Make your ways and practices good, and I will let you continue to live in this place.
4 Msitumainie maneno ya udanganyifu na kusema, “Hili ni Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana!”
Do not entrust yourself to deceitful words and say, “Temple of Yahweh! Temple of Yahweh! Temple of Yahweh!”
5 Kama kweli mkibadili njia zenu na matendo yenu, mkatendeana haki kila mmoja na mwenzake,
For if you actually make your ways and practices good; if you completely execute justice between a man and his neighbor—
6 kama msipomwonea mgeni, yatima wala mjane, na kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa, nanyi kama msipofuata miungu mingine kwa madhara yenu wenyewe,
if you do not exploit the one staying in the land, the orphan, or the widow and do not pour out innocent blood in this place, and do not walk after other gods to your own harm—
7 ndipo nitawaacha mkae mahali hapa, katika nchi niliyowapa baba zenu milele na milele.
then I will let you stay in this place, in the land that I gave to your ancestors from ancient times and forever.
8 Lakini tazama, mnatumainia maneno ya udanganyifu yasiyo na maana.
Behold! You are trusting in deceitful words that do not help you.
9 “‘Je, mtaiba na kuua, mtazini na kuapa kwa uongo, na kufukiza uvumba kwa Baali, na kufuata miungu mingine ambayo hamkuijua,
Do you steal, kill, and commit adultery? Do you swear deceitfully and offer incense to Baal and walk after other gods whom you have not known?
10 kisha mje na kusimama mbele yangu katika nyumba hii inayoitwa kwa Jina langu, mkisema, “Tuko salama.” Salama kwa kufanya mambo haya yote ya kuchukiza?
Then do you come and stand before me in this house that is called by my name and say, “We are saved,” so you can do all of these abominations?
11 Je, nyumba hii, iitwayo kwa Jina langu, imekuwa pango la wanyangʼanyi kwenu? Lakini nimekuwa nikiona yanayotendeka! asema Bwana.
Is this house, which carries my name, a den of bandits in your eyes? But behold, I have seen it—this is Yahweh's declaration.'
12 “‘Nendeni sasa mahali pangu palipokuwa huko Shilo, mahali ambapo nilipafanya pa kwanza kuwa makao ya Jina langu, nanyi mwone lile nililopafanyia kwa ajili ya uovu wa watu wangu Israeli.
'So go to my place that was in Shiloh, where I allowed my name to stay there in the beginning, and look at what I did to it because of the wickedness of my people Israel.
13 Mlipokuwa mnafanya yote haya, asema Bwana, nilisema nanyi tena na tena, lakini hamkusikiliza; niliwaita, lakini hamkujibu.
So now, on account of your doing all of these practices—this is Yahweh's declaration—I spoke to you time and time again, but you did not listen. I summoned you, but you did not answer.
14 Kwa hiyo, nililolifanyia Shilo, nitalifanya sasa kwa nyumba hii iitwayo kwa Jina langu, Hekalu mnalolitumainia, mahali nilipowapa ninyi na baba zenu.
Therefore, what I did to Shiloh, I will also do to this house that is called by my name, the house in which you have trusted, this place that I gave to you and your ancestors.
15 Nitawafukuza mbele yangu, kama nilivyowafanyia ndugu zenu, watu wa Efraimu.’
For I will send you out from before me just as I had sent out all your brothers, all the descendants of Ephraim.'
16 “Kwa hiyo usiombe kwa ajili ya watu hawa, wala usinililie, na usifanye maombi kwa ajili yao; usinisihi, kwa sababu sitakusikiliza.
As for you, Jeremiah, do not pray for this people, and do not lift up a lamenting wail or say a prayer on their behalf, and do not petition me, for I will not listen to you.
17 Je, huyaoni hayo wanayoyatenda katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu?
Do you not see what they are doing in the cities of Judah and in the streets of Jerusalem?
18 Watoto wanakusanya kuni, baba zao wanawasha moto, na wanawake wanakanda unga na kuoka mikate kwa ajili ya Malkia wa Mbinguni. Wanamimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine ili kunikasirisha.
The children are gathering wood and the fathers kindling the fire! The women are kneading dough to make cakes for the queen of the heavens and pour out drink offerings for other gods so that they will provoke me.
19 Lakini je, mimi ndiye wanayenikasirisha? asema Bwana. Je, hawajiumizi wenyewe na kujiaibisha?
Are they truly provoking me?—this is Yahweh's declaration—is it not themselves whom they are provoking, so that shame is on them?
20 “‘Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenyezi: Hasira yangu na ghadhabu yangu itamwagwa mahali hapa, juu ya mwanadamu na mnyama, juu ya miti ya shambani na juu ya matunda ya ardhini, nayo itaungua pasipo kuzimwa.
Therefore the Lord Yahweh says this, 'See, my anger and wrath will gush out onto this place, on both man and beast, on the tree in the fields and the fruit on the ground. It will burn and never be extinguished.'
21 “‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Endeleeni, ongezeni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya dhabihu zenu nyingine, mle nyama hiyo wenyewe!
Yahweh of hosts, God of Israel says this, 'Add your burnt offerings to your sacrifices and the meat from them.
22 Kwa kuwa nilipowaleta baba zenu kutoka Misri na kusema nao, sikuwapa amri kuhusu sadaka za kuteketezwa na dhabihu tu,
For when I brought your ancestors out from the land of Egypt, I did not require anything from them. I gave them no command about matters of burnt offerings and sacrifices.
23 lakini niliwapa amri hii nikisema: Nitiini mimi, nami nitakuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu. Enendeni katika njia zote ninazowaamuru ili mpate kufanikiwa.
I only gave them this command, “Listen to my voice, and I will be your God and you will be my people. So walk in all the ways that I am commanding you, so that it may go well with you.”
24 Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Walirudi nyuma badala ya kusonga mbele.
But they did not listen or pay attention. They lived by their own stubborn plans of their wicked hearts, so they went backwards, not forward.
25 Tangu wakati ule baba zenu walipotoka Misri hadi sasa, siku baada ya siku, tena na tena nimewatumia watumishi wangu manabii.
Ever since the day when your ancestors went out from the land of Egypt until this day, I have sent every one of my servants, my prophets, to you. I persisted in sending them.
26 Lakini hawakunisikiliza wala hawakujali. Walikuwa na shingo ngumu na kufanya maovu kuliko baba zao.’
But they did not listen to me. They paid no attention. Instead, they hardened their necks. They were more wicked than their ancestors.'
27 “Utakapowaambia haya yote, hawatakusikiliza; utakapowaita, hawatajibu.
So proclaim all these words to them, but they will not listen to you. Proclaim these things to them, but they will not answer you.
28 Kwa hiyo waambie, ‘Hili ni taifa ambalo halimtii Bwana, Mungu wao, wala kukubali maonyo. Kweli imekufa, imetoweka midomoni mwao.
Say to them: This is a nation that does not listen to the voice of Yahweh its God and does not receive discipline. Truth is destroyed and cut off from their mouths.
29 Nyoeni nywele zenu na kuzitupa, ombolezeni katika miinuko iliyo kame, kwa kuwa Bwana amekikataa na kukiacha kizazi hiki kilichomkasirisha.
Cut off your hair and shave yourself, and throw away your hair. Sing a funeral song over the open places. For Yahweh has rejected and abandoned this generation in his rage.
30 “‘Watu wa Yuda wamefanya maovu machoni pangu, asema Bwana. Wameziweka sanamu zao za machukizo ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu, na wameitia unajisi.
For the sons of Judah have done evil in my eye—this is Yahweh's declaration—they have set their detestable things in the house that is called by my name, in order to defile it.
31 Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia sanamu pa Tofethi kwenye Bonde la Ben-Hinomu ili kuwateketeza wana wao na binti zao kwenye moto, kitu ambacho sikuamuru, wala hakikuingia akilini mwangu.
Then they built the high place of Topheth that is in the Valley of Ben Hinnom. They did this to burn their sons and daughters in fire—something that I did not command, nor did it enter my mind.
32 Kwa hiyo mjihadhari, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu watakapokuwa hawapaiti Tofethi au Bonde la Ben-Hinomu, lakini watapaita Bonde la Machinjo, kwa sababu watawazika wafu huko Tofethi mpaka pasiwe tena nafasi.
So see, days are coming—this is Yahweh's declaration—when it will no longer be called Topheth or Valley of Ben Hinnom. It will be the Valley of Slaughter; they will bury bodies in Topheth until there is no room left.
33 Ndipo mizoga ya watu hawa itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwafukuza.
The corpses of this people will be food for the birds of the skies and the beasts of the earth, and there will be no one to frighten them away.
34 Nitazikomesha sauti za shangwe na furaha, na sauti za bwana arusi na bibi arusi katikati ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, kwa sababu nchi itakuwa ukiwa.
I will put an end to the cities of Judah and the streets of Jerusalem, the sound of joy and the sound of gladness, the sound of the groom and the sound of the bride, for the land will become a desolation.”

< Yeremia 7 >