< Yeremia 7 >

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
The word which it came to Jeremiah from with Yahweh saying.
2 “Simama kwenye lango la nyumba ya Bwana, na huko upige mbiu ya ujumbe huu: “‘Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mliokuja kupitia malango haya ili kumwabudu Bwana.
Stand in [the] gate of [the] house of Yahweh and you will proclaim there the word this and you will say hear [the] word of Yahweh O all Judah who come in the gates these to bow down to Yahweh.
3 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Tengenezeni njia zenu na matendo yenu, nami nitawaacha mkae mahali hapa.
Thus he says Yahweh of hosts [the] God of Israel make good ways your and deeds your so let me cause to dwell you in the place this.
4 Msitumainie maneno ya udanganyifu na kusema, “Hili ni Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana!”
May not you trust for yourselves to words of deception saying [the] temple of Yahweh [the] temple of Yahweh [are] [the] temple of Yahweh they.
5 Kama kweli mkibadili njia zenu na matendo yenu, mkatendeana haki kila mmoja na mwenzake,
That except certainly you will make good ways your and deeds your certainly [if] you will do justice between everyone and between neighbor his.
6 kama msipomwonea mgeni, yatima wala mjane, na kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa, nanyi kama msipofuata miungu mingine kwa madhara yenu wenyewe,
[the] sojourner [the] fatherless And [the] widow not you must oppress and blood innocent may not you shed in the place this and after gods other not you must walk for harm of you.
7 ndipo nitawaacha mkae mahali hapa, katika nchi niliyowapa baba zenu milele na milele.
And I will cause to dwell you in the place this in the land which I gave to ancestors your from antiquity and until perpetuity.
8 Lakini tazama, mnatumainia maneno ya udanganyifu yasiyo na maana.
Here! you [are] relying for yourselves on words of deception to not to profit.
9 “‘Je, mtaiba na kuua, mtazini na kuapa kwa uongo, na kufukiza uvumba kwa Baali, na kufuata miungu mingine ambayo hamkuijua,
¿ Will you steal - will you murder? and will you commit adultery? and will you swear? to falsehood and will you make smoke? to Baal and will you walk? after gods other which not you have known.
10 kisha mje na kusimama mbele yangu katika nyumba hii inayoitwa kwa Jina langu, mkisema, “Tuko salama.” Salama kwa kufanya mambo haya yote ya kuchukiza?
And you will come and you will stand before me in the house this which it is called name my on it and you will say we are delivered so as to do all the abominations these.
11 Je, nyumba hii, iitwayo kwa Jina langu, imekuwa pango la wanyangʼanyi kwenu? Lakini nimekuwa nikiona yanayotendeka! asema Bwana.
¿ A den of robbers has it become the house this which it is called name my on it in view your also I here! I have seen [the] utterance of Yahweh.
12 “‘Nendeni sasa mahali pangu palipokuwa huko Shilo, mahali ambapo nilipafanya pa kwanza kuwa makao ya Jina langu, nanyi mwone lile nililopafanyia kwa ajili ya uovu wa watu wangu Israeli.
That go please to place my which [was] in Shiloh where I caused to dwell name my there at the former [time] and see [that] which I did to it because of [the] wickedness of people my Israel.
13 Mlipokuwa mnafanya yote haya, asema Bwana, nilisema nanyi tena na tena, lakini hamkusikiliza; niliwaita, lakini hamkujibu.
And therefore because did you all the deeds these [the] utterance of Yahweh and I spoke to you rising early and speaking and not you listened and I called you and not you answered.
14 Kwa hiyo, nililolifanyia Shilo, nitalifanya sasa kwa nyumba hii iitwayo kwa Jina langu, Hekalu mnalolitumainia, mahali nilipowapa ninyi na baba zenu.
And I will do to the house - which it is called name my on it which you [are] trusting in it and to the place which I gave to you and to ancestors your just as I did to Shiloh.
15 Nitawafukuza mbele yangu, kama nilivyowafanyia ndugu zenu, watu wa Efraimu.’
And I will cast out you from on face my just as I cast out all relatives your all [the] offspring of Ephraim.
16 “Kwa hiyo usiombe kwa ajili ya watu hawa, wala usinililie, na usifanye maombi kwa ajili yao; usinisihi, kwa sababu sitakusikiliza.
And you may not you pray - for the people this and may not you lift up for them a cry of entreaty and a prayer and may not you entreat me for not I [will be] hearing you.
17 Je, huyaoni hayo wanayoyatenda katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu?
¿ [are] not You seeing what? [are] they doing in [the] cities of Judah and in [the] streets of Jerusalem.
18 Watoto wanakusanya kuni, baba zao wanawasha moto, na wanawake wanakanda unga na kuoka mikate kwa ajili ya Malkia wa Mbinguni. Wanamimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine ili kunikasirisha.
The children [are] gathering wood and the fathers [are] kindling the fire and the women [are] kneading dough to make cakes for [the] queen of the heavens and they are pouring out drink offerings to gods other so as to provoke to anger me.
19 Lakini je, mimi ndiye wanayenikasirisha? asema Bwana. Je, hawajiumizi wenyewe na kujiaibisha?
¿ Me [are] they provoking [the] utterance of Yahweh ¿ not themselves for [the] sake of [the] shame of faces their.
20 “‘Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenyezi: Hasira yangu na ghadhabu yangu itamwagwa mahali hapa, juu ya mwanadamu na mnyama, juu ya miti ya shambani na juu ya matunda ya ardhini, nayo itaungua pasipo kuzimwa.
Therefore thus he says - [the] Lord Yahweh here! anger my and rage my [are] about to be poured out against the place this on humankind and on the animal[s] and on [the] tree[s] of the field and on [the] fruit of the ground and it will burn and not it will be quenched.
21 “‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Endeleeni, ongezeni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya dhabihu zenu nyingine, mle nyama hiyo wenyewe!
Thus he says Yahweh of hosts [the] God of Israel burnt offerings your add to sacrifices your and eat meat.
22 Kwa kuwa nilipowaleta baba zenu kutoka Misri na kusema nao, sikuwapa amri kuhusu sadaka za kuteketezwa na dhabihu tu,
For not I spoke with ancestors your and not I commanded them on [the] day (brought out I *Q(K)*) them from [the] land of Egypt on matters of burnt offering and sacrifice.
23 lakini niliwapa amri hii nikisema: Nitiini mimi, nami nitakuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu. Enendeni katika njia zote ninazowaamuru ili mpate kufanikiwa.
That except the matter this I commanded them saying listen to voice my and I will become for you God and you you will become for me a people and you will walk in every way which I will command you so that it may go well for you.
24 Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Walirudi nyuma badala ya kusonga mbele.
And not they listened and not they inclined ear their and they walked in counsels in [the] stubbornness of heart their evil and they were backwards and not forwards.
25 Tangu wakati ule baba zenu walipotoka Misri hadi sasa, siku baada ya siku, tena na tena nimewatumia watumishi wangu manabii.
From the day when they came out ancestors your from [the] land of Egypt until the day this and I sent to you all servants my the prophets day rising early and sending.
26 Lakini hawakunisikiliza wala hawakujali. Walikuwa na shingo ngumu na kufanya maovu kuliko baba zao.’
And not they listened to me and not they inclined ear their and they stiffened neck their they did evil more than ancestors their.
27 “Utakapowaambia haya yote, hawatakusikiliza; utakapowaita, hawatajibu.
And you will say to them all the words these and not they will listen to you and you will call to them and not they will answer you.
28 Kwa hiyo waambie, ‘Hili ni taifa ambalo halimtii Bwana, Mungu wao, wala kukubali maonyo. Kweli imekufa, imetoweka midomoni mwao.
And you will say to them this [is] the nation which not they listened to [the] voice of Yahweh God its and not they accepted correction it has perished faithfulness and it has been cut off from mouth their.
29 Nyoeni nywele zenu na kuzitupa, ombolezeni katika miinuko iliyo kame, kwa kuwa Bwana amekikataa na kukiacha kizazi hiki kilichomkasirisha.
Cut off hair your and throw [it] away and take up on bare heights a lamentation for he has rejected Yahweh and he has abandoned [the] generation of fury his.
30 “‘Watu wa Yuda wamefanya maovu machoni pangu, asema Bwana. Wameziweka sanamu zao za machukizo ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu, na wameitia unajisi.
For they have done [the] people of Judah the evil in view my [the] utterance of Yahweh they have put detestable things their in the house which it is called name my on it to make unclean it.
31 Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia sanamu pa Tofethi kwenye Bonde la Ben-Hinomu ili kuwateketeza wana wao na binti zao kwenye moto, kitu ambacho sikuamuru, wala hakikuingia akilini mwangu.
And they have built [the] high places of Topheth which [is] in [the] valley of Ben Hinnom to burn sons their and daughters their in the fire which not I commanded and not it came up on heart my.
32 Kwa hiyo mjihadhari, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu watakapokuwa hawapaiti Tofethi au Bonde la Ben-Hinomu, lakini watapaita Bonde la Machinjo, kwa sababu watawazika wafu huko Tofethi mpaka pasiwe tena nafasi.
Therefore here! days [are] coming [the] utterance of Yahweh and not it will be said again Topheth and [the] valley of Ben Hinnom that except [the] valley of slaughter and people will bury in Topheth from not room.
33 Ndipo mizoga ya watu hawa itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwafukuza.
And it will become [the] corpse[s] of the people this food for [the] bird[s] of the heavens and for [the] animal[s] of the earth and there not [will be one who] terrifies.
34 Nitazikomesha sauti za shangwe na furaha, na sauti za bwana arusi na bibi arusi katikati ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, kwa sababu nchi itakuwa ukiwa.
And I will cause to cease - from [the] cities of Judah and from [the] streets of Jerusalem [the] sound of joy and [the] sound of gladness [the] sound of a bridegroom and [the] sound of a bride for a desolation it will become the land.

< Yeremia 7 >