< Yeremia 7 >

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
The word that came to Jeremiah from the Lord, saying:
2 “Simama kwenye lango la nyumba ya Bwana, na huko upige mbiu ya ujumbe huu: “‘Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mliokuja kupitia malango haya ili kumwabudu Bwana.
“Stand at the gate to the house of the Lord, and preach this word there, and say: Listen to the word of the Lord, all you of Judah who enter through these gates to adore the Lord.
3 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Tengenezeni njia zenu na matendo yenu, nami nitawaacha mkae mahali hapa.
Thus says the Lord of hosts, the God of Israel: Make your ways and your intentions good, and I will live with you in this place.
4 Msitumainie maneno ya udanganyifu na kusema, “Hili ni Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana!”
Do not choose to trust in lying words, saying: ‘This is the temple of the Lord! The temple of the Lord! The temple of the Lord!’
5 Kama kweli mkibadili njia zenu na matendo yenu, mkatendeana haki kila mmoja na mwenzake,
For if you direct your ways and your intentions well, if you exercise judgment between a man and his neighbor,
6 kama msipomwonea mgeni, yatima wala mjane, na kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa, nanyi kama msipofuata miungu mingine kwa madhara yenu wenyewe,
if you do not act with deceit toward the new arrival, the orphan, and the widow, and if you do not pour out innocent blood in this place, and if you do not walk after strange gods, which is to your own harm,
7 ndipo nitawaacha mkae mahali hapa, katika nchi niliyowapa baba zenu milele na milele.
then I will live with you in this place, in the land that I gave to your fathers from the beginning and even forever.
8 Lakini tazama, mnatumainia maneno ya udanganyifu yasiyo na maana.
Behold, you trust in false words, which will not benefit you,
9 “‘Je, mtaiba na kuua, mtazini na kuapa kwa uongo, na kufukiza uvumba kwa Baali, na kufuata miungu mingine ambayo hamkuijua,
so as to steal, to murder, to commit adultery, to swear falsely, to offer libations to Baal, and to go after strange gods, which you do not know.
10 kisha mje na kusimama mbele yangu katika nyumba hii inayoitwa kwa Jina langu, mkisema, “Tuko salama.” Salama kwa kufanya mambo haya yote ya kuchukiza?
And you arrived and stood before me in this house, where my name is invoked, and you said: ‘We have been freed because we carried out all these abominations.’
11 Je, nyumba hii, iitwayo kwa Jina langu, imekuwa pango la wanyangʼanyi kwenu? Lakini nimekuwa nikiona yanayotendeka! asema Bwana.
So then, has this house, where my name has been invoked, become a den of robbers in your eyes? It is I, I am, I have seen, says the Lord.
12 “‘Nendeni sasa mahali pangu palipokuwa huko Shilo, mahali ambapo nilipafanya pa kwanza kuwa makao ya Jina langu, nanyi mwone lile nililopafanyia kwa ajili ya uovu wa watu wangu Israeli.
Go to my place in Shiloh, where my name has lived from the beginning, and see what I did to it because of the wickedness of my people Israel.
13 Mlipokuwa mnafanya yote haya, asema Bwana, nilisema nanyi tena na tena, lakini hamkusikiliza; niliwaita, lakini hamkujibu.
And now, because you have done all these works, says the Lord, and because I have spoken to you from your morning rising, and because I was speaking, but you were not listening, and because I have called you, but you have not responded:
14 Kwa hiyo, nililolifanyia Shilo, nitalifanya sasa kwa nyumba hii iitwayo kwa Jina langu, Hekalu mnalolitumainia, mahali nilipowapa ninyi na baba zenu.
I will do to this house, in which my name is invoked, and in which you have confidence, even to this place which I gave to you and to your fathers, just as I have done to Shiloh.
15 Nitawafukuza mbele yangu, kama nilivyowafanyia ndugu zenu, watu wa Efraimu.’
And I will cast you away from my face, just as I have cast away all your brothers, the entire offspring of Ephraim.
16 “Kwa hiyo usiombe kwa ajili ya watu hawa, wala usinililie, na usifanye maombi kwa ajili yao; usinisihi, kwa sababu sitakusikiliza.
Therefore, you should not pray for this people, nor take up praise and supplication on their behalf. And you should not stand in opposition to me. For then I will not heed you.
17 Je, huyaoni hayo wanayoyatenda katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu?
Have you not seen what they are doing in the cities of Judah and in the streets of Jerusalem?
18 Watoto wanakusanya kuni, baba zao wanawasha moto, na wanawake wanakanda unga na kuoka mikate kwa ajili ya Malkia wa Mbinguni. Wanamimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine ili kunikasirisha.
The sons gather the wood, and the fathers kindle the fire, and the wives spread the grease, so as to make cakes to the queen of heaven and to offer libations to strange gods, and so as to provoke me to anger.
19 Lakini je, mimi ndiye wanayenikasirisha? asema Bwana. Je, hawajiumizi wenyewe na kujiaibisha?
But are they provoking me to anger, says the Lord? Are they not provoking themselves, to the confusion of their own faces?”
20 “‘Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenyezi: Hasira yangu na ghadhabu yangu itamwagwa mahali hapa, juu ya mwanadamu na mnyama, juu ya miti ya shambani na juu ya matunda ya ardhini, nayo itaungua pasipo kuzimwa.
Therefore, thus says the Lord God: “Behold, my fury and my indignation is kindled against this place, over men and over beasts, and over the trees of the countryside and over the fruits of the land, and it will burn and not be extinguished.”
21 “‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Endeleeni, ongezeni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya dhabihu zenu nyingine, mle nyama hiyo wenyewe!
Thus says the Lord of hosts, the God of Israel: “Add your holocausts to your sacrifices, and eat the flesh.
22 Kwa kuwa nilipowaleta baba zenu kutoka Misri na kusema nao, sikuwapa amri kuhusu sadaka za kuteketezwa na dhabihu tu,
For concerning the matter of holocausts and sacrifices, I did not speak with your fathers, and I did not instruct them, in the day when I led them away from the land of Egypt.
23 lakini niliwapa amri hii nikisema: Nitiini mimi, nami nitakuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu. Enendeni katika njia zote ninazowaamuru ili mpate kufanikiwa.
But on this matter I did instruct them, saying: Listen to my voice, and I will be your God, and you will be my people. And walk in the entire way that I have commanded you, so that it may be well with you.
24 Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Walirudi nyuma badala ya kusonga mbele.
But they did not listen, nor did they incline their ear. Instead, they walked by their own will and in the depravity of their own wicked heart. And so, they went backward, and not forward,
25 Tangu wakati ule baba zenu walipotoka Misri hadi sasa, siku baada ya siku, tena na tena nimewatumia watumishi wangu manabii.
from the day when their fathers went forth from the land of Egypt, even to this day. And I have sent all my servants, the prophets, to you, throughout the day, rising at first light and sending them.
26 Lakini hawakunisikiliza wala hawakujali. Walikuwa na shingo ngumu na kufanya maovu kuliko baba zao.’
But they have not listened to me, nor have they inclined their ear. Instead, they have stiffened their neck, and they have behaved worse than their fathers did.
27 “Utakapowaambia haya yote, hawatakusikiliza; utakapowaita, hawatajibu.
And so, you will speak to them all these words, but they will not listen to you. And you will call to them, but they will not respond to you.
28 Kwa hiyo waambie, ‘Hili ni taifa ambalo halimtii Bwana, Mungu wao, wala kukubali maonyo. Kweli imekufa, imetoweka midomoni mwao.
And you will say to them: This is the nation that has not listened to the voice of the Lord their God, nor accepted discipline. Faith has perished and been taken away from their mouth.
29 Nyoeni nywele zenu na kuzitupa, ombolezeni katika miinuko iliyo kame, kwa kuwa Bwana amekikataa na kukiacha kizazi hiki kilichomkasirisha.
Cut off your hair, and cast it away. And take up a lamentation on high. For the Lord has cast aside and abandoned this generation of his fury.
30 “‘Watu wa Yuda wamefanya maovu machoni pangu, asema Bwana. Wameziweka sanamu zao za machukizo ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu, na wameitia unajisi.
For the sons of Judah have done evil in my eyes, says the Lord. They have stationed their abominations in the house where my name is invoked, so that they may defile it.
31 Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia sanamu pa Tofethi kwenye Bonde la Ben-Hinomu ili kuwateketeza wana wao na binti zao kwenye moto, kitu ambacho sikuamuru, wala hakikuingia akilini mwangu.
And they have built the exalted places of Topheth, which is in the Valley of the son of Hinnom, so that they may burn their sons and their daughters with fire, something I neither instructed, nor thought in my heart.
32 Kwa hiyo mjihadhari, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu watakapokuwa hawapaiti Tofethi au Bonde la Ben-Hinomu, lakini watapaita Bonde la Machinjo, kwa sababu watawazika wafu huko Tofethi mpaka pasiwe tena nafasi.
For this reason, behold, the days will arrive, says the Lord, when it will no longer be called Topheth, nor the Valley of the son of Hinnom, but instead the Valley of Slaughter. Yet they will bury in Topheth, because there will be no other place.
33 Ndipo mizoga ya watu hawa itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwafukuza.
And the corpses of this people will be food for the birds of the air and for the wild beasts of the land, and there will be no one to drive them away.
34 Nitazikomesha sauti za shangwe na furaha, na sauti za bwana arusi na bibi arusi katikati ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, kwa sababu nchi itakuwa ukiwa.
And from the cities of Judah and the streets of Jerusalem, I will cause the cessation of the voice of gladness and the voice of rejoicing, the voice of the groom and the voice of the bride. For the land will be in utter desolation.”

< Yeremia 7 >