< Yeremia 6 >
1 “Kimbieni kwa usalama wenu, enyi watu wa Benyamini! Kimbieni kutoka Yerusalemu! Pigeni tarumbeta katika Tekoa! Inueni ishara juu ya Beth-Hakeremu! Kwa kuwa maafa yanaonekana yakitoka kaskazini, na uharibifu wa kutisha.
“Güvenliğiniz için kaçın, ey Benyamin halkı! Yeruşalim'den kaçın! Tekoa'da boru çalın! Beythakkerem'e bir işaret koyun. Çünkü kuzeyden bir felaket, Büyük bir yıkım gelecek gibi görünüyor.
2 Nitamwangamiza Binti Sayuni, aliye mzuri sana na mwororo.
Siyon kızını, o güzel, narin kızı yok edeceğim.
3 Wachungaji pamoja na makundi yao watakuja dhidi yake; watapiga mahema yao kumzunguka, kila mmoja akichunga kundi lake mwenyewe.”
Çobanlar sürüleriyle ona geliyor, Çevresinde çadırlarını kuracaklar. Herkes kendi sürüsünü otlatacak.”
4 “Jiandaeni kwa vita dhidi yake! Inukeni tumshambulie mchana! Lakini, ole wetu, mchana unaisha, na vivuli vya jioni vinazidi kuwa virefu.
“Yeruşalim'e karşı savaş hazırlığı yapın! Kalkın, öğleyin saldırıya geçelim! Vay halimize, gün kararıyor! Akşamın gölgeleri gitgide uzuyor.
5 Kwa hiyo inukeni, tufanye mashambulizi usiku, na kuharibu ngome zake!”
Haydi, gece saldırıya geçelim, Kentin kalelerini yerle bir edelim.”
6 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Kateni miti mjenge boma kuzunguka Yerusalemu. Mji huu ni lazima uadhibiwe, umejazwa na uonevu.
Her Şeye Egemen RAB diyor ki, “Ağaçları kesin, Yeruşalim'e karşı kuşatma rampaları yapın. Bu kent cezalandırılmalı, İçinde zorbalıktan başka bir şey yok.
7 Kama vile kisima kinavyomwaga maji yake, ndivyo anavyomwaga uovu wake. Ukatili na maangamizi yasikika ndani yake, ugonjwa wake na majeraha yake viko mbele yangu daima.
Kuyu suyunu nasıl taze tutuyorsa, Yeruşalim de kötülüğünü öyle taze tutuyor. Şiddet ve yıkım yankılanıyor orada, Karşımda hep hastalık ve yaralar var.
8 Pokea onyo, ee Yerusalemu, la sivyo nitageukia mbali nawe na kuifanya nchi yako kuwa ukiwa, asiweze mtu kuishi ndani yake.”
Uyarılara kulak ver, ey Yeruşalim! Yoksa seni bırakacağım, Seni bir viraneye, Oturulmaz bir ülkeye çevireceğim.”
9 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Wao na wayakusanye mabaki ya Israeli kwa uangalifu kama kwenye mzabibu; pitisha mkono wako kwenye matawi tena, kama yeye avunaye zabibu.”
Her Şeye Egemen RAB diyor ki, “Asmadan nasıl üzüm toplanırsa, İsrail halkından geride kalanları da öyle toplayacaklar. Üzüm toplayan biri gibi Elini yine asma dallarına uzat.”
10 Niseme na nani na kumpa onyo? Ni nani atakayenisikiliza mimi? Masikio yao yameziba, kwa hiyo hawawezi kusikia. Neno la Bwana ni chukizo kwao, hawalifurahii.
İşitsinler diye kiminle konuşayım, Kimi uyarayım? Kulakları tıkalı, işitemiyorlar. RAB'bin sözünü aşağılıyor, Ondan hoşlanmıyorlar.
11 Lakini nimejaa ghadhabu ya Bwana, nami siwezi kuizuia. “Wamwagie watoto walioko barabarani, na juu ya vijana waume waliokusanyika; mume na mke watakumbwa pamoja ndani yake, hata nao wazee waliolemewa na miaka.
Bu yüzden RAB'bin öfkesiyle doluyum, Kendimi tutmaktan yoruldum. “Sokaktaki çocukların, Toplanan gençlerin üzerine boşalt öfkeni. Nasıl olsa karı da koca da, Yaşlı da yıllarca yaşamış olan da kurtulamayacak.
12 Nyumba zao zitapewa watu wengine, pamoja na mashamba yao na wake zao, nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya wale waishio katika nchi,” asema Bwana.
Evleri, tarlaları, karıları Başkalarına verilecek, Çünkü ülkede yaşayanlara karşı Elimi kaldıracağım” diyor RAB.
13 “Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa, wote wana tamaa ya kupata faida zaidi; manabii na makuhani wanafanana, wote wanafanya udanganyifu.
“Küçük büyük herkes kazanç peşinde, Peygamberler, kâhinler, hepsi halkı aldatıyor.
14 Wanafunga majeraha ya watu wangu bila uangalifu. Wanasema, ‘Amani, amani,’ wakati hakuna amani.
Esenlik yokken, ‘Esenlik, esenlik’ diyerek Halkımın yarasını sözde iyileştirdiler.
15 Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yao inayochukiza mno? Hapana, hawana aibu hata kidogo; hawajui hata kuona haya. Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka, watashushwa chini nitakapowaadhibu,” asema Bwana.
Yaptıkları iğrençliklerden utandılar mı? Hayır, ne utanması? Kızarıp bozarmanın ne olduğunu bile bilmiyorlar. Bu yüzden onlar da düşenlerin arasında yer alacak, Onları cezalandırdığımda sendeleyip düşecekler” diyor RAB.
16 Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Simama kwenye njia panda utazame, ulizia mapito ya zamani, ulizia wapi ilipo njia nzuri, uifuate hiyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu. Lakini ninyi mlisema, ‘Hatutaipita hiyo.’
RAB diyor ki, “Yol kavşaklarında durup bakın, Eski yolları sorun, İyi yol nerede, öğrenin, O yolda yürüyün, Canlarınız rahata kavuşur. Ama onlar, ‘O yolda yürümeyiz’ dediler.
17 Niliweka walinzi juu yenu na kusema, ‘Sikieni sauti ya tarumbeta!’ Lakini mkasema, ‘Hatutasikiliza.’
Size bekçiler atayıp, ‘Boru sesini dinleyin’ dedim, Ama onlar, ‘Dinlemeyiz’ dediler.
18 Kwa hiyo sikilizeni, enyi mataifa, angalieni, enyi mashahidi, lile litakalowatokea.
Bundan ötürü, ey uluslar, Başlarına neler geleceğini işitin! Sen de anla, ey topluluk!
19 Sikia, ee nchi: Ninaleta maafa juu ya watu hawa, matunda ya mipango yao, kwa sababu hawakusikiliza maneno yangu na wameikataa sheria yangu.
Dinle, ey yeryüzü! Bu halkın üzerine felaket, Kendi kurduğu düzenin sonucunu getirmek üzereyim. Çünkü sözlerime kulak asmadılar, Kutsal Yasam'ı reddettiler.
20 Unanifaa nini uvumba kutoka Sheba, au udi wa harufu nzuri kutoka nchi ya mbali? Sadaka zako za kuteketezwa hazikubaliki, dhabihu zako hazinifurahishi mimi.”
Neden bana Saba'dan günnük, Uzak bir ülkeden güzel kokulu kamış getiriliyor? Yakmalık sunularınızı kabul etmiyorum, Kurbanlarınızdan hoşnut değilim.”
21 Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Nitaweka vikwazo mbele ya watu hawa. Baba na wana wao watajikwaa juu yake, majirani na marafiki wataangamia.”
Bu yüzden RAB diyor ki, “Bu halkın önüne tökezler koyacağım, Babalar da oğullar da Tökezleyip birlikte düşecek, Komşu dostuyla birlikte yok olacak.”
22 Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Tazama, jeshi linakuja kutoka nchi ya kaskazini, taifa kubwa linaamshwa kutoka miisho ya dunia.
RAB diyor ki, “İşte kuzeyden bir ordu geliyor. Dünyanın uçlarından Büyük bir ulus harekete geçiyor.
23 Wamejifunga pinde na mkuki, ni wakatili na hawana huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao. Wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Sayuni.”
Yay, pala kuşanmışlar, Gaddar ve acımasızlar. Atlara binmiş gelirken, Kükreyen denizi andırıyor sesleri. Savaşa hazır savaşçılar Karşına dizilecekler, ey Siyon kızı!”
24 Tumesikia taarifa zao, nayo mikono yetu imelegea. Uchungu umetushika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Haberlerini aldık, Ellerimizde derman kalmadı. Doğuran kadın gibi Üzüntü, sancı sardı bizi.
25 Usitoke kwenda mashambani au kutembea barabarani, kwa kuwa adui ana upanga, na kuna vitisho kila upande.
Kırlara çıkmayın, Yolda yürümeyin! Düşmanın kılıcı orada, Her yer dehşet içinde.
26 Enyi watu wangu, vaeni magunia mjivingirishe kwenye majivu, ombolezeni kwa kilio cha uchungu kama amliliaye mwana pekee, kwa maana ghafula mharabu atatujia.
Ey halkım, çula sarın, Kül içinde yuvarlan. Biricik oğul için yas tutar gibi Acı acı dövün. Çünkü yok edici ansızın gelecek üzerimize.
27 “Nimekufanya wewe kuwa kitu cha kujaribu chuma, nao watu wangu kama mawe yenye madini, ili upate kuzijua na kuzijaribu njia zao.
“Seni halkımı deneyesin diye atadım, Öyle ki, onları tanıyıp yollarını sınayasın.
28 Wote ni waasi sugu, wakienda huku na huko kusengenya. Wao ni shaba na chuma, wote wanatenda upotovu.
Hepsi de çok dikbaşlı, Onu bunu çekiştirerek dolaşan insanlardır, Tunç kadar, demir kadar katıdırlar. Hepsi baştan çıkmıştır.
29 Mivuo inavuma kwa nguvu, kinachoungua kwa huo moto ni risasi, lakini pamoja na kusafisha kote huku ni bure; waovu hawaondolewi.
Körük üfürdükçe üfürüyor, Kurşunu ateşte eritiyor, Ama boşunadır yapılan işlem, Çünkü kötüler arınmıyor.
30 Wanaitwa fedha iliyokataliwa, kwa sababu Bwana amewakataa.”
Onlara gümüş artığı denecek, Çünkü RAB onları reddetti.”