< Yeremia 6 >

1 “Kimbieni kwa usalama wenu, enyi watu wa Benyamini! Kimbieni kutoka Yerusalemu! Pigeni tarumbeta katika Tekoa! Inueni ishara juu ya Beth-Hakeremu! Kwa kuwa maafa yanaonekana yakitoka kaskazini, na uharibifu wa kutisha.
Fortifiez-vous, fils de Benjamin, au milieu de Jérusalem, et dans Thécua sonnez de la trompette, et sur Bethacarem levez l’étendard; parce qu’un mal a été vu du côté de l’aquilon, ainsi qu’une grande destruction.
2 Nitamwangamiza Binti Sayuni, aliye mzuri sana na mwororo.
À une femme belle et délicate j’ai comparé la fille de Sion.
3 Wachungaji pamoja na makundi yao watakuja dhidi yake; watapiga mahema yao kumzunguka, kila mmoja akichunga kundi lake mwenyewe.”
Vers elle viendront les pasteurs et leurs troupeaux; ils ont dressé leurs tentes à l’entour; chacun d’eux fera paître ceux qui sont sous sa main.
4 “Jiandaeni kwa vita dhidi yake! Inukeni tumshambulie mchana! Lakini, ole wetu, mchana unaisha, na vivuli vya jioni vinazidi kuwa virefu.
Consacrez contre elle une guerre; levez-vous, et montons au milieu du jour; malheur à nous, parce que le jour décline, parce que les ombres du soir sont allongées.
5 Kwa hiyo inukeni, tufanye mashambulizi usiku, na kuharibu ngome zake!”
Levez-vous et montons pendant la nuit, et renversons ses maisons.
6 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Kateni miti mjenge boma kuzunguka Yerusalemu. Mji huu ni lazima uadhibiwe, umejazwa na uonevu.
Parce que voici ce que dit le Seigneur des armées: Coupez ses arbres, et faites autour de Jérusalem un rempart; c’est la cité de la Visitation; toute sorte de violence est au milieu d’elle.
7 Kama vile kisima kinavyomwaga maji yake, ndivyo anavyomwaga uovu wake. Ukatili na maangamizi yasikika ndani yake, ugonjwa wake na majeraha yake viko mbele yangu daima.
Comme la citerne rend froide son eau, ainsi cette cité a commis froidement ses méchancetés; iniquité et ravage, c’est ce qui sera ouï en elle; devant moi elle est toujours infirmité et plaie.
8 Pokea onyo, ee Yerusalemu, la sivyo nitageukia mbali nawe na kuifanya nchi yako kuwa ukiwa, asiweze mtu kuishi ndani yake.”
Instruis-toi, Jérusalem, de peur que mon âme ne se retire de toi, et que je ne fasse de toi un désert, une terre inhabitable.
9 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Wao na wayakusanye mabaki ya Israeli kwa uangalifu kama kwenye mzabibu; pitisha mkono wako kwenye matawi tena, kama yeye avunaye zabibu.”
Voici ce que dit le Seigneur des armées: On rassemblera les restes d’Israël comme dans une vigne jusqu’à la dernière grappe; reporte ta main comme le vendangeur dans la corbeille.
10 Niseme na nani na kumpa onyo? Ni nani atakayenisikiliza mimi? Masikio yao yameziba, kwa hiyo hawawezi kusikia. Neno la Bwana ni chukizo kwao, hawalifurahii.
À qui parlerai-je? et qui prendrai-je à témoin pour qu’il entende? voici que leurs oreilles sont incirconcises, et qu’ils ne peuvent entendre. Voici que la parole du Seigneur leur est devenue un opprobre; et ils ne la recevront pas.
11 Lakini nimejaa ghadhabu ya Bwana, nami siwezi kuizuia. “Wamwagie watoto walioko barabarani, na juu ya vijana waume waliokusanyika; mume na mke watakumbwa pamoja ndani yake, hata nao wazee waliolemewa na miaka.
C’est pour cela que je suis plein de la fureur du Seigneur et que j’ai peine à la supporter; répandez-la sur le petit enfant au dehors, et sur le conseil des jeunes gens assemblés; car l’homme sera pris avec la femme, le vieillard avec celui qui est plein de jours.
12 Nyumba zao zitapewa watu wengine, pamoja na mashamba yao na wake zao, nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya wale waishio katika nchi,” asema Bwana.
Et leurs maisons passeront à des étrangers, leurs champs, et leurs femmes également, parce que j’étendrai ma main sur ceux qui habitent la terre, dit le Seigneur.
13 “Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa, wote wana tamaa ya kupata faida zaidi; manabii na makuhani wanafanana, wote wanafanya udanganyifu.
Depuis le plus petit jusqu’au plus grand, tous se livrent à l’avarice; et depuis le prophète jusqu’au prêtre, tous agissent avec tromperie.
14 Wanafunga majeraha ya watu wangu bila uangalifu. Wanasema, ‘Amani, amani,’ wakati hakuna amani.
Et ils guérissaient la plaie de la fille de mon peuple avec ignominie, disant: Paix, paix; et il n’y avait point de paix.
15 Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yao inayochukiza mno? Hapana, hawana aibu hata kidogo; hawajui hata kuona haya. Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka, watashushwa chini nitakapowaadhibu,” asema Bwana.
Ils ont été confus, parce qu’ils ont fait des abominations; et encore ne l’ont-ils pas été entièrement, et n’ont-ils pas su rougir; à cause de cela ils tomberont parmi ceux qui sont renversés; au temps de leur Visitation, ils seront renversés tous ensemble, dit le Seigneur.
16 Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Simama kwenye njia panda utazame, ulizia mapito ya zamani, ulizia wapi ilipo njia nzuri, uifuate hiyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu. Lakini ninyi mlisema, ‘Hatutaipita hiyo.’
Voici ce que dit le Seigneur: Tenez-vous sur les voies et voyez; demandez, touchant les sentiers anciens, quelle est la bonne voie, et marchez-y; et vous trouverez un rafraîchissement pour vos âmes. Et ils ont dit: Nous n’y marcherons pas.
17 Niliweka walinzi juu yenu na kusema, ‘Sikieni sauti ya tarumbeta!’ Lakini mkasema, ‘Hatutasikiliza.’
Et j’ai établi sur vous des sentinelles. Ecoutez la voix de la trompette. Et ils ont dit: Nous ne l’écouterons pas.
18 Kwa hiyo sikilizeni, enyi mataifa, angalieni, enyi mashahidi, lile litakalowatokea.
C’est pourquoi, écoutez, nations, et apprenez, assemblée des peuples, les grandes choses que je ferai contre eux.
19 Sikia, ee nchi: Ninaleta maafa juu ya watu hawa, matunda ya mipango yao, kwa sababu hawakusikiliza maneno yangu na wameikataa sheria yangu.
Ecoute, terre: Voilà que moi j’amènerai sur ce peuple des maux, fruit de ses pensées, parce qu’ils n’ont point écouté mes paroles et qu’ils ont rejeté ma loi.
20 Unanifaa nini uvumba kutoka Sheba, au udi wa harufu nzuri kutoka nchi ya mbali? Sadaka zako za kuteketezwa hazikubaliki, dhabihu zako hazinifurahishi mimi.”
Pourquoi m’apportez-vous de l’encens de Saba, et la canne à l’odeur suave d’une terre éloignée? Vos holocaustes ne me sont pas agréables, et vos victimes ne m’ont pas plu.
21 Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Nitaweka vikwazo mbele ya watu hawa. Baba na wana wao watajikwaa juu yake, majirani na marafiki wataangamia.”
À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur: Voilà que je ferai fondre sur ce peuple des ruines; les pères y tomberont et les fils en même temps; les voisins et les proches y périront.
22 Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Tazama, jeshi linakuja kutoka nchi ya kaskazini, taifa kubwa linaamshwa kutoka miisho ya dunia.
Voici ce que dit le Seigneur: Voilà qu’un peuple vient de la terre de l’aquilon, et une grande nation s’élèvera des confins de la terre.
23 Wamejifunga pinde na mkuki, ni wakatili na hawana huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao. Wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Sayuni.”
Elle saisira la flèche et le bouclier; elle est cruelle et elle n’aura pas de pitié; sa voix comme la mer retentira; et ils monteront sur leurs chevaux, et préparés comme un homme qui va au combat, ils marcheront contre toi, fille de Sion.
24 Tumesikia taarifa zao, nayo mikono yetu imelegea. Uchungu umetushika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Nous avons ouï la nouvelle de son dessein, nos mains ont défailli; la tribulation nous a saisis, et les douleurs comme la femme en travail.
25 Usitoke kwenda mashambani au kutembea barabarani, kwa kuwa adui ana upanga, na kuna vitisho kila upande.
Ne sortez point dans les champs, et dans la voie ne marchez point, parce que le glaive de l’ennemi et l’épouvante sont à l’entour.
26 Enyi watu wangu, vaeni magunia mjivingirishe kwenye majivu, ombolezeni kwa kilio cha uchungu kama amliliaye mwana pekee, kwa maana ghafula mharabu atatujia.
Fille de mon peuple, ceins-toi d’un cilice, couvre-toi de cendre; sois en deuil comme d’un fils unique, pousse des plaintes amères, parce que tout d’un coup viendra le dévastateur sur nous.
27 “Nimekufanya wewe kuwa kitu cha kujaribu chuma, nao watu wangu kama mawe yenye madini, ili upate kuzijua na kuzijaribu njia zao.
Je t’ai établi au milieu de mon peuple comme un fondeur robuste; tu sauras, et tu éprouveras leur voie.
28 Wote ni waasi sugu, wakienda huku na huko kusengenya. Wao ni shaba na chuma, wote wanatenda upotovu.
Tous ses princes ont dévié, marchant frauduleusement; c’est de l’airain et du fer; tous se sont corrompus.
29 Mivuo inavuma kwa nguvu, kinachoungua kwa huo moto ni risasi, lakini pamoja na kusafisha kote huku ni bure; waovu hawaondolewi.
Le soufflet a manqué, dans le feu s’est consumé le plomb; en vain le fondeur les a mis dans le fourneau; car leurs méchancetés n’ont pas été consumées.
30 Wanaitwa fedha iliyokataliwa, kwa sababu Bwana amewakataa.”
Appelez-les un argent réprouvé, parce que le Seigneur les a rejetés.

< Yeremia 6 >