< Yeremia 6 >
1 “Kimbieni kwa usalama wenu, enyi watu wa Benyamini! Kimbieni kutoka Yerusalemu! Pigeni tarumbeta katika Tekoa! Inueni ishara juu ya Beth-Hakeremu! Kwa kuwa maafa yanaonekana yakitoka kaskazini, na uharibifu wa kutisha.
Flee for refuge - O people of Benjamin from [the] midst of Jerusalem and in Tekoa blow a trumpet and at Beth Hakkerem raise a signal for calamity it has looked down from [the] north and destruction great.
2 Nitamwangamiza Binti Sayuni, aliye mzuri sana na mwororo.
The beautiful [one] and the dainty [one] I resemble [the] daughter of Zion.
3 Wachungaji pamoja na makundi yao watakuja dhidi yake; watapiga mahema yao kumzunguka, kila mmoja akichunga kundi lake mwenyewe.”
To it they will come shepherds and flocks their they will pitch at it tents all around they will graze everyone hand his.
4 “Jiandaeni kwa vita dhidi yake! Inukeni tumshambulie mchana! Lakini, ole wetu, mchana unaisha, na vivuli vya jioni vinazidi kuwa virefu.
Consecrate on it battle arise so we may go up at noon woe! to us for it has turned the day for they are stretched out [the] shadows of evening.
5 Kwa hiyo inukeni, tufanye mashambulizi usiku, na kuharibu ngome zake!”
Arise so we may go up in the night and let us destroy fortresses its.
6 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Kateni miti mjenge boma kuzunguka Yerusalemu. Mji huu ni lazima uadhibiwe, umejazwa na uonevu.
For thus he says Yahweh of hosts cut down wood and pour out on Jerusalem a mound that city it will be visited all of it [is] oppression in midst its.
7 Kama vile kisima kinavyomwaga maji yake, ndivyo anavyomwaga uovu wake. Ukatili na maangamizi yasikika ndani yake, ugonjwa wake na majeraha yake viko mbele yangu daima.
As keeps cool (a well *Q(K)*) water its so it has kept cool evil its violence and havoc it is heard in it [are] on face my continually sickness and wound[s].
8 Pokea onyo, ee Yerusalemu, la sivyo nitageukia mbali nawe na kuifanya nchi yako kuwa ukiwa, asiweze mtu kuishi ndani yake.”
Let yourself be instructed O Jerusalem lest it should be alienated self my from you lest I should make you a desolation a land [which] not it is inhabited.
9 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Wao na wayakusanye mabaki ya Israeli kwa uangalifu kama kwenye mzabibu; pitisha mkono wako kwenye matawi tena, kama yeye avunaye zabibu.”
Thus he says Yahweh of hosts thoroughly people will glean like vine [the] remnant of Israel return hand your like a grape gatherer over branches.
10 Niseme na nani na kumpa onyo? Ni nani atakayenisikiliza mimi? Masikio yao yameziba, kwa hiyo hawawezi kusikia. Neno la Bwana ni chukizo kwao, hawalifurahii.
To whom? will I speak and will I warn? and they may listen there! [is] uncircumcised ear their and not they are able to pay attention there! [the] word of Yahweh it has become for them a reproach not they delight in it.
11 Lakini nimejaa ghadhabu ya Bwana, nami siwezi kuizuia. “Wamwagie watoto walioko barabarani, na juu ya vijana waume waliokusanyika; mume na mke watakumbwa pamoja ndani yake, hata nao wazee waliolemewa na miaka.
And [the] rage of Yahweh - I am full I am weary to hold [it] in pour [it] out on child[ren] in the street and on [the] gathering of young men alike for also a husband with a wife they will be caught [the] old with [the] full of days.
12 Nyumba zao zitapewa watu wengine, pamoja na mashamba yao na wake zao, nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya wale waishio katika nchi,” asema Bwana.
And they will be turned over houses their to others fields and wives alike for I will stretch out hand my on [the] inhabitants of the land [the] utterance of Yahweh.
13 “Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa, wote wana tamaa ya kupata faida zaidi; manabii na makuhani wanafanana, wote wanafanya udanganyifu.
That from little their and unto great their all of it [is] gaining unjust gain and from prophet and unto priest all of him [is] doing falsehood.
14 Wanafunga majeraha ya watu wangu bila uangalifu. Wanasema, ‘Amani, amani,’ wakati hakuna amani.
And they have healed [the] fracture of people my on a trifling [thing] saying peace - peace and there not [is] peace.
15 Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yao inayochukiza mno? Hapana, hawana aibu hata kidogo; hawajui hata kuona haya. Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka, watashushwa chini nitakapowaadhibu,” asema Bwana.
Are they ashamed? that an abomination they have done neither at all not they are ashamed nor to exhibit shame not they know therefore they will fall among [those who] fall at [the] time [when] I have visited them they will stumble he says Yahweh.
16 Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Simama kwenye njia panda utazame, ulizia mapito ya zamani, ulizia wapi ilipo njia nzuri, uifuate hiyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu. Lakini ninyi mlisema, ‘Hatutaipita hiyo.’
Thus he says Yahweh stand at [the] roads and look and ask - of paths of ancient time where? this [is] [the] way of the good and walk in it and find rest for self your and they said not we will walk.
17 Niliweka walinzi juu yenu na kusema, ‘Sikieni sauti ya tarumbeta!’ Lakini mkasema, ‘Hatutasikiliza.’
And I raised up over you watchmen pay attention to [the] sound of a trumpet and they said not we will pay attention.
18 Kwa hiyo sikilizeni, enyi mataifa, angalieni, enyi mashahidi, lile litakalowatokea.
Therefore listen O nations and know O congregation [that] which [is] in them.
19 Sikia, ee nchi: Ninaleta maafa juu ya watu hawa, matunda ya mipango yao, kwa sababu hawakusikiliza maneno yangu na wameikataa sheria yangu.
Hear O earth here! I [am] about to bring calamity to the people this [the] fruit of own schemes their for on words my not they have paid attention and law my and they have rejected it.
20 Unanifaa nini uvumba kutoka Sheba, au udi wa harufu nzuri kutoka nchi ya mbali? Sadaka zako za kuteketezwa hazikubaliki, dhabihu zako hazinifurahishi mimi.”
Why? this to me frankincense [which] from Sheba it comes and [the] cane good from a land of distance burnt offerings your not [are] for acceptance and sacrifices your not they are pleasing to me.
21 Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Nitaweka vikwazo mbele ya watu hawa. Baba na wana wao watajikwaa juu yake, majirani na marafiki wataangamia.”
Therefore thus he says Yahweh here I [am] about to give to the people this stumbling blocks and they will stumble over them fathers and sons alike a neighbor and friend his (and they will perish. *Q(K)*)
22 Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Tazama, jeshi linakuja kutoka nchi ya kaskazini, taifa kubwa linaamshwa kutoka miisho ya dunia.
Thus he says Yahweh there! a people [is] about to come from a land of [the] north and a nation great it will be roused from [the] remotest parts of [the] earth.
23 Wamejifunga pinde na mkuki, ni wakatili na hawana huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao. Wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Sayuni.”
Bow and javelin they take hold of [is] cruel it and not they have mercy sound their [is] like the sea [which] it roars and on horses they ride arranged like a man for battle on you O daughter of Zion.
24 Tumesikia taarifa zao, nayo mikono yetu imelegea. Uchungu umetushika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
We heard [the] report of it they hung limp hands our distress it took hold of us anguish like [woman] giving birth.
25 Usitoke kwenda mashambani au kutembea barabarani, kwa kuwa adui ana upanga, na kuna vitisho kila upande.
May not (you go out *Q(K)*) the field and on the road mau not (you walk *Q(K)*) for a sword [belongs] to [the] enemy terror [is] from round about.
26 Enyi watu wangu, vaeni magunia mjivingirishe kwenye majivu, ombolezeni kwa kilio cha uchungu kama amliliaye mwana pekee, kwa maana ghafula mharabu atatujia.
O daughter of people my gird yourself sackcloth and roll in ash[es] [the] mourning of an only [child] observe for yourself wailing of bitterness for suddenly it will come the destroyer on us.
27 “Nimekufanya wewe kuwa kitu cha kujaribu chuma, nao watu wangu kama mawe yenye madini, ili upate kuzijua na kuzijaribu njia zao.
An assayer I have made you among people my fortification so you may observe and you will test conduct their.
28 Wote ni waasi sugu, wakienda huku na huko kusengenya. Wao ni shaba na chuma, wote wanatenda upotovu.
All of them [are those who] turn aside of rebels [those who] go about of slander bronze and iron all of them [are] destroyers they.
29 Mivuo inavuma kwa nguvu, kinachoungua kwa huo moto ni risasi, lakini pamoja na kusafisha kote huku ni bure; waovu hawaondolewi.
It puffs [the] bellow[s] (from a fire it is complete *Q(K)*) lead for vanity someone has refined steadfastly and evil [people] not they have been separated.
30 Wanaitwa fedha iliyokataliwa, kwa sababu Bwana amewakataa.”
Silver rejected people called them for he has rejected Yahweh them.