< Yeremia 52 >

1 Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.
Sédécias était âgé de vingt et un ans lorsqu'il devint roi, et il régna onze ans à Jérusalem. Sa mère s'appelait Amital, fille de Jérémie, de Lobna.
2 Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.
Il fit ce qui est mal aux yeux de Yahweh, imitant tout ce qu'avait fait Joakim.
3 Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake. Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.
Cela arriva à Jérusalem et en Juda, à cause de la colère de Yahweh, jusqu'à ce qu'il les rejette de devant sa face. Et Sédécias se révolta contre le roi de Babylone.
4 Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Wakapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote.
La neuvième année du règne de Sédécias, le dixième mois, le dixième jour du mois, Nabuchodonosor, roi de Babylone, vint avec toute son armée contre Jérusalem; ils campèrent devant elle et construisirent tout autour des murs d'approche.
5 Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.
La ville fut assiégée jusqu'à la onzième année du roi Sédécias.
6 Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu.
Au quatrième mois, le neuvième jour du mois, comme la famine était grande dans la ville, et qu'il n'y avait plus de pain pour le peuple du pays,
7 Kisha ukuta wa mji ukavunjwa na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba.
une brèche fut faite à la ville, et tous les gens de guerre s'enfuirent et sortirent de la ville pendant la nuit, par la porte entre les deux murs, près du jardin du roi, pendant que les Chaldéens environnaient la ville; et ils prirent le chemin de la plaine.
8 Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia Mfalme Sedekia na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika,
Mais l'armée des chaldéens poursuivit le roi; ils atteignirent Sédécias dans les plaines de Jéricho, et toute son armée se dispersa loin de lui.
9 naye akakamatwa. Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.
Ayant saisi roi, ils le firent monter vers le roi de Babylone, à Rébla, dans le pays de d'Émath, et il prononça sur lui des sentences.
10 Huko Ribla mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Pia akawaua maafisa wote wa Yuda.
Le roi de Babylone égorgea les fils de Sédécias sous les yeux de leur père; il égorgea aussi tous les chefs de Juda à Rébla.
11 Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia, akamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli, alipomweka gerezani mpaka siku ya kifo chake.
Puis il creva les yeux à Sédécias et le lia avec deux chaînes d'airain; et le roi de Babylone le mena à Babylone, et le tint en prison jusqu'au jour de sa mort.
12 Mnamo siku ya kumi ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, aliyemtumikia mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu.
Le cinquième mois, le dixième jour du mois, — c'était la dix-neuvième année du règne de Nabuchodonosor, roi de Babylone, — Nabuzardan, capitaine des gardes, qui était ministre du roi de Babylone, vint à Jérusalem.
13 Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu.
Il brûla la maison de Yahweh, la maison du roi, et toutes les maisons de Jérusalem; il livra au feu toutes les grandes maisons.
14 Jeshi lote la Wakaldayo chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme walivunja kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu.
Toute l'armée des chaldéens qui était avec le capitaine des gardes démolit les murailles formant l'enceinte de Jérusalem.
15 Nebuzaradani, jemadari wa askari walinzi, akawapeleka uhamishoni baadhi ya watu maskini sana na wale waliobaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli.
Nabuzardan, capitaine des gardes, emmena captifs une partie des plus pauvres du peuple, avec le reste du peuple qui était demeuré dans la ville, les transfuges qui s'étaient rendus au roi de Babylone, et le reste des artisans.
16 Lakini Nebuzaradani akawaacha mabaki ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
Mais Nabuzardan, capitaine des gardes, laissa comme vignerons et comme laboureurs quelques-uns des pauvres du pays.
17 Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba yote na kuipeleka Babeli.
Les Chaldéens brisèrent les colonnes d'airain qui appartenaient à la maison de Yahweh, ainsi que les bases et la mer d'airain qui étaient dans la maison de Yahweh, et ils en emportèrent l'airain à Babylone.
18 Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu.
Ils prirent les pots, les pelles, les couteaux, les tasses, les coupes et tous les ustensiles d'airain avec lesquels on faisait le service.
19 Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua yale masinia, vile vyetezo, yale mabakuli ya kunyunyizia, zile sufuria, vile vinara vya taa, zile sahani na yale mabakuli yaliyotumika kwa sadaka za vinywaji, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.
Le capitaine des gardes prit encore les bassins, les encensoirs, les tasses, les pots, les chandeliers, les cuillers et les urnes, ce qui était d'or et ce qui était d'argent.
20 Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na wale mafahali kumi na mawili wa shaba waliokuwa chini yake, pamoja na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Mfalme Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika.
Quant aux deux colonnes, à la mer et aux douze bœufs d'airain qui étaient dessous, et aux bases que le roi Salomon avait faites dans la maison de Yahweh, il n'y avait pas à peser l'airain de tous ces ustensiles.
21 Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane, kimo chake na mzunguko dhiraa kumi na mbili, na unene wa nyanda nne, na zote zilikuwa wazi ndani.
Quant aux colonnes, la hauteur d'une colonne était de dix-huit coudées, et un cordon de douze coudées en mesurait le tour; son épaisseur était de quatre doigts, et elle était creuse.
22 Sehemu ya shaba juu ya ile nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tano, na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na makomamanga yake ilifanana na hiyo ya kwanza.
Il y avait au-dessus un chapiteau d'airain, et la hauteur d'un chapiteau était de cinq coudées; et il y avait tout autour du chapiteaux un treillis et des grenades, le tout d'airain. Il en était de même de la seconde colonne; avec les grenades.
23 Kulikuwa na makomamanga tisini na sita pembeni; jumla ya makomamanga juu ya wavu uliokuwa umezunguka yalikuwa mia moja.
Il y avait quatre-vingt-seize grenades sur les faces, et toutes les grenades étaient au nombre de cent sur le treillis, tout autour.
24 Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu.
Le capitaine des gardes prit Saraïas, le grand-prêtre, Sophonie, prêtre de second ordre, et les trois gardiens de la porte.
25 Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri saba wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji.
De la ville il prit un officier qui commandait aux gens de guerre, sept hommes faisant partie du conseil privé du roi et qui furent trouvés dans la ville, le secrétaire du chef de l'armée chargé d'enrôler le peuple du pays, et soixante hommes du peuple du pays qui se trouvaient dans la ville.
26 Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.
Les ayant pris, Nabuzardan, capitaine des gardes, les conduisit vers le roi de Babylone à Rébla.
27 Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe. Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao.
Et le roi de Babylone les frappa et les fit mourir à Rébla, dans le pays de d'Emath. Ainsi Juda fut emmené captif loin de sa patrie.
28 Hii ndiyo hesabu ya watu ambao Nebukadneza aliwachukua kwenda uhamishoni: katika mwaka wa saba, Wayahudi 3,023;
Voici le nombre des hommes que Nabuchodonosor emmena captifs: la septième année, trois mille vingt-trois hommes de Juda;
29 katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Nebukadneza, watu 832 kutoka Yerusalemu;
la dix-huitième année de Nabuchodonosor, huit cent trente-deux personnes de la population de Jérusalem;
30 katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake, Wayahudi 745 walichukuliwa kwenda uhamishoni na Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme. Jumla ya watu wote walikuwa 4,600.
la vingt-troisième année de Nabuchodonosor, Nabuzardan, capitaine des gardes, emmena encore captifs sept cent quarante-cinq hommes de Juda; en tout quatre mille six cents personnes.
31 Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini mfalme wa Yuda, na kumfungua kutoka gerezani siku ya ishirini na tano ya mwezi wa kumi na mbili.
La trente-septième année de la captivité de Joachin, roi de Juda, le douzième mois, le vingt-cinquième jour du mois, Evil-Mérodach, roi de Babylone, en l'année de son avènement, releva la tête de Joachin, roi de Juda, et le fit sortir de prison.
32 Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli.
Il lui parla avec bonté et mit son trône au-dessus du trône des rois qui étaient avec lui à Babylone.
33 Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme.
Il lui fit changer ses vêtements de prison, et Joachin mangea en sa présence, toujours, tous les jours de sa vie.
34 Siku kwa siku mfalme wa Babeli alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake, hadi siku ya kifo chake.
Quant à son entretien, son entretien perpétuel, le roi de Babylone y pourvut chaque jour, jusqu'au jour de sa mort, tous les jours de sa vie.

< Yeremia 52 >