< Yeremia 52 >

1 Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.
Sédécias avait vingt et un ans lorsqu'il commença à régner. Il régna onze ans à Jérusalem. Sa mère s'appelait Hamutal, fille de Jérémie, de Libna.
2 Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.
Il fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel, selon tout ce qu'avait fait Jojakim.
3 Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake. Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.
Car c'est par la colère de Yahvé que cela arriva à Jérusalem et en Juda, jusqu'à ce qu'il les eût chassés de sa présence. Sédécias se révolta contre le roi de Babylone.
4 Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Wakapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote.
La neuvième année de son règne, le dixième jour du mois, Nabuchodonosor, roi de Babylone, vint, lui et toute son armée, contre Jérusalem, et campa devant elle; ils construisirent des forts tout autour.
5 Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.
La ville fut ainsi assiégée jusqu'à la onzième année du roi Sédécias.
6 Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu.
Au quatrième mois, le neuvième jour du mois, la famine sévit dans la ville, de sorte qu'il n'y eut pas de pain pour le peuple du pays.
7 Kisha ukuta wa mji ukavunjwa na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba.
Alors il y eut une brèche dans la ville, et tous les hommes de guerre s'enfuirent et sortirent de nuit de la ville par le chemin de la porte entre les deux murs, qui était près du jardin du roi. Or les Chaldéens étaient contre la ville tout autour. Les hommes de guerre se dirigèrent vers la plaine.
8 Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia Mfalme Sedekia na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika,
Mais l'armée des Chaldéens poursuivit le roi et atteignit Sédécias dans les plaines de Jéricho, et toute son armée fut dispersée devant lui.
9 naye akakamatwa. Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.
Ils prirent le roi, et le firent monter vers le roi de Babylone, à Ribla, dans le pays de Hamath, qui prononça un jugement contre lui.
10 Huko Ribla mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Pia akawaua maafisa wote wa Yuda.
Le roi de Babylone fit mourir sous ses yeux les fils de Sédécias. Il tua aussi tous les princes de Juda à Ribla.
11 Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia, akamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli, alipomweka gerezani mpaka siku ya kifo chake.
Il fit crever les yeux à Sédécias, et le roi de Babylone le lia avec des chaînes, le transporta à Babylone et le mit en prison jusqu'au jour de sa mort.
12 Mnamo siku ya kumi ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, aliyemtumikia mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu.
Le cinquième mois, le dixième jour du mois, qui était la dix-neuvième année du roi Nebucadnetsar, roi de Babylone, Nebuzaradan, chef des gardes, qui se tenait devant le roi de Babylone, entra dans Jérusalem.
13 Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu.
Il brûla la maison de Yahvé et la maison du roi, et il brûla au feu toutes les maisons de Jérusalem, toutes les grandes maisons.
14 Jeshi lote la Wakaldayo chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme walivunja kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu.
Toute l'armée des Chaldéens, qui était avec le chef des gardes, abattit toutes les murailles de Jérusalem, tout autour.
15 Nebuzaradani, jemadari wa askari walinzi, akawapeleka uhamishoni baadhi ya watu maskini sana na wale waliobaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli.
Puis Nebuzaradan, chef des gardes, emmena en captivité les plus pauvres du peuple, le reste du peuple qui était resté dans la ville, les réfractaires qui s'étaient ralliés au roi de Babylone, et le reste de la multitude.
16 Lakini Nebuzaradani akawaacha mabaki ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
Mais Nebuzaradan, chef des gardes, laissa les plus pauvres du pays comme vignerons et cultivateurs.
17 Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba yote na kuipeleka Babeli.
Les Chaldéens brisèrent les colonnes d'airain qui étaient dans la maison de l'Éternel, les socles et la mer d'airain qui étaient dans la maison de l'Éternel, et ils emportèrent tout l'airain à Babylone.
18 Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu.
Ils emportèrent aussi les marmites, les pelles, les éteignoirs, les bassins, les cuillères et tous les ustensiles d'airain avec lesquels on faisait le service.
19 Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua yale masinia, vile vyetezo, yale mabakuli ya kunyunyizia, zile sufuria, vile vinara vya taa, zile sahani na yale mabakuli yaliyotumika kwa sadaka za vinywaji, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.
Le chef des gardes emporta les coupes, les poêles à feu, les bassins, les marmites, les chandeliers, les cuillères et les coupes, ce qui était d'or comme de l'or, et ce qui était d'argent comme de l'argent.
20 Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na wale mafahali kumi na mawili wa shaba waliokuwa chini yake, pamoja na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Mfalme Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika.
Ils prirent les deux colonnes, la mer unique et les douze taureaux d'airain qui étaient sous les socles, que le roi Salomon avait faits pour la maison de Yahvé. Le bronze de tous ces objets était sans poids.
21 Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane, kimo chake na mzunguko dhiraa kumi na mbili, na unene wa nyanda nne, na zote zilikuwa wazi ndani.
Quant aux colonnes, la hauteur de l'une d'elles était de dix-huit coudées; une ligne de douze coudées l'entourait; son épaisseur était de quatre doigts. Elle était creuse.
22 Sehemu ya shaba juu ya ile nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tano, na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na makomamanga yake ilifanana na hiyo ya kwanza.
Il était surmonté d'un chapiteau d'airain; la hauteur de ce chapiteau était de cinq coudées, avec un réseau et des grenades sur le chapiteau tout autour, le tout d'airain. Le second pilier avait aussi la même chose, avec des grenades.
23 Kulikuwa na makomamanga tisini na sita pembeni; jumla ya makomamanga juu ya wavu uliokuwa umezunguka yalikuwa mia moja.
Il y avait quatre-vingt-seize grenades sur les côtés, et cent grenades sur le réseau, tout autour.
24 Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu.
Le chef des gardes prit Seraja, le souverain sacrificateur, Sophonie, le second sacrificateur, et les trois gardiens du seuil;
25 Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri saba wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji.
il prit dans la ville un officier préposé aux hommes de guerre, sept hommes de ceux qui avaient vu le visage du roi et qui se trouvaient dans la ville, le secrétaire du chef de l'armée, qui rassemblait le peuple du pays, et soixante hommes du peuple du pays, qui se trouvaient au milieu de la ville.
26 Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.
Nebuzaradan, chef des gardes, les prit et les amena au roi de Babylone, à Ribla.
27 Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe. Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao.
Le roi de Babylone les frappa et les fit mourir à Ribla, dans le pays de Hamath. Et Juda fut emmené captif hors de son pays.
28 Hii ndiyo hesabu ya watu ambao Nebukadneza aliwachukua kwenda uhamishoni: katika mwaka wa saba, Wayahudi 3,023;
Voici le nombre de personnes que Nebucadnetsar emmena en captivité: la septième année, trois mille vingt-trois Juifs;
29 katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Nebukadneza, watu 832 kutoka Yerusalemu;
La dix-huitième année de Nabuchodonosor, il emmena en captivité de Jérusalem huit cent trente-deux personnes;
30 katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake, Wayahudi 745 walichukuliwa kwenda uhamishoni na Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme. Jumla ya watu wote walikuwa 4,600.
La vingt-troisième année de Nebucadnetsar, Nebuzaradan, chef des gardes, emmena captifs des Juifs sept cent quarante-cinq personnes. Tout le peuple était au nombre de quatre mille six cents.
31 Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini mfalme wa Yuda, na kumfungua kutoka gerezani siku ya ishirini na tano ya mwezi wa kumi na mbili.
La trente-septième année de la captivité de Jojakin, roi de Juda, le douzième mois, le vingt-cinquième jour du mois, Evilmérodac, roi de Babylone, la première année de son règne, releva la tête de Jojakin, roi de Juda, et le fit sortir de prison.
32 Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli.
Il lui parla avec bonté, plaça son trône au-dessus du trône des rois qui étaient avec lui à Babylone,
33 Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme.
et changea ses vêtements de prison. Jehoïachin mangea du pain devant lui continuellement tous les jours de sa vie.
34 Siku kwa siku mfalme wa Babeli alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake, hadi siku ya kifo chake.
Pour son argent de poche, le roi de Babylone lui donna une allocation continuelle, chaque jour une portion jusqu'au jour de sa mort, tous les jours de sa vie.

< Yeremia 52 >