< Yeremia 52 >

1 Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.
Sedechie was a sone of oon and twenti yeer, whanne he bigan to regne, and he regnede enleuene yeer in Jerusalem; and the name of his modir was Amychal, the douyter of Jeremye of Lobna.
2 Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.
And he dide yuels bifore the iyen of the Lord, bi alle thingis whiche Joachym hadde do.
3 Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake. Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.
For the stronge veniaunce of the Lord was in Jerusalem, and in Juda, til he castide hem awey fro his face. And Sedechie yede awei fro the kyng of Babiloyne.
4 Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Wakapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote.
Forsothe it was don in the nynthe yeer of his rewme, in the tenthe monethe, in the tenthe dai of the monethe, Nabugodonosor, the kyng of Babiloyne, cam, he and al his oost, ayens Jerusalem; and thei bisegiden it, and bildiden ayens it strengthis in cumpas.
5 Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.
And the citee was bisegid, til to the enleuenthe yeer of the rewme of Sedechie.
6 Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu.
Forsothe in the fourthe monethe, in the nynthe dai of the monethe, hungur helde the citee; and foodis weren not to the puple of the lond.
7 Kisha ukuta wa mji ukavunjwa na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba.
And the citee was brokun, and alle men werriouris therof fledden; and thei yeden out of the citee in the niyt, bi the weie of the yate, which is bitwixe twei wallis, and ledith to the gardyn of the kyng, while Caldeis bisegiden the citee in cumpas; and thei yeden forth bi the weie that ledith in to desert.
8 Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia Mfalme Sedekia na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika,
Sotheli the oost of Caldeis pursuede the kyng; and thei token Sedechie in desert, which is bisidis Jerico, and al his felouschipe fledde awei fro hym.
9 naye akakamatwa. Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.
And whanne thei hadden take the kyng, thei brouyten hym to the kyng of Babiloyne in Reblatha, which is in the lond of Emath; and the kyng of Babiloyne spak domes to hym.
10 Huko Ribla mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Pia akawaua maafisa wote wa Yuda.
And the kyng of Babiloyne stranglide the sones of Sedechie bifore hise iyen; but also he killide alle the princes of Juda in Rablatha.
11 Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia, akamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli, alipomweka gerezani mpaka siku ya kifo chake.
And he puttide out the iyen of Sedechie, and boond hym in stockis; and the kyng of Babiloyne brouyte hym in to Babiloyne, and puttide hym in the hous of prisoun, til to the dai of his deth.
12 Mnamo siku ya kumi ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, aliyemtumikia mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu.
Forsothe in the nynthe monethe, in the tenthe dai of the monethe, thilke is the nyntenthe yeer of the kyng of Babiloyne, Nabusardan, the prince of chyualrie, that stood bifore the kyng of Babiloyne, cam in to Jerusalem.
13 Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu.
And he brente the hous of the Lord, and the hous of the kyng, and alle the housis of Jerusalem; and he brente with fier ech greet hous.
14 Jeshi lote la Wakaldayo chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme walivunja kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu.
And al the ost of Caldeis, that was with the maistir of chyualrie, distriede al the wal of Jerusalem bi cumpas.
15 Nebuzaradani, jemadari wa askari walinzi, akawapeleka uhamishoni baadhi ya watu maskini sana na wale waliobaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli.
Sotheli Nabusardan, the prince of chyualrie, translatide of the pore men of the puple, and of the residue comyn puple, that was left in the citee, and of the fleeris ouer, that fledden ouer to the kyng of Babiloyne; and he translatide other men of the multitude.
16 Lakini Nebuzaradani akawaacha mabaki ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
But Nabusardan, the prince of chyualrie, lefte of the pore men of the lond vyne tilers, and erthe tilers.
17 Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba yote na kuipeleka Babeli.
Also Caldeis brakun the brasun pilers, that weren in the hous of the Lord, and the foundementis, and the brasun waischyng vessel, that was in the hous of the Lord; and thei token al the metal of tho in to Babiloyne.
18 Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu.
And thei tokun cawdruns, and fleischokis, and sautrees, and violis, and morteris, and alle brasun vessels, that weren in seruyce;
19 Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua yale masinia, vile vyetezo, yale mabakuli ya kunyunyizia, zile sufuria, vile vinara vya taa, zile sahani na yale mabakuli yaliyotumika kwa sadaka za vinywaji, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.
thei token also `watir pottis, and vessels of encense, and pottis, and basyns, and candilstikis, and morters, and litle cuppis; hou manye euere goldun, goldun, and hou manye euere siluerne, siluerne.
20 Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na wale mafahali kumi na mawili wa shaba waliokuwa chini yake, pamoja na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Mfalme Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika.
The maister of chyualrie took twei pilers, and o waischyng vessel, and twelue brasun caluys, that weren vndur the foundementis, whiche kyng Salomon hadde maad in the hous of the Lord. No weiyte was of the metal of alle these vessels.
21 Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane, kimo chake na mzunguko dhiraa kumi na mbili, na unene wa nyanda nne, na zote zilikuwa wazi ndani.
Forsothe of the pilers, eiytene cubitis of heiythe weren in o piler, and a roop of twelue cubitis cumpasside it; certis the thickenesse therof was of foure fyngris, and was holowe withynne.
22 Sehemu ya shaba juu ya ile nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tano, na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na makomamanga yake ilifanana na hiyo ya kwanza.
And brasun pomels weren on euer either; and the heiythe of a pomel was of fyue cubitis; and werkis lijk nettis and pumgranatis weren on the coroun `in cumpas.
23 Kulikuwa na makomamanga tisini na sita pembeni; jumla ya makomamanga juu ya wavu uliokuwa umezunguka yalikuwa mia moja.
And the pumgranatis weren nynti and sixe hangynge doun, and alle pumgranatis weren cumpassid with an hundred werkis lijk nettis.
24 Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu.
And the maister of the chyualrie took Saraie, the firste preest, and Sophonye, the secounde preest, and three keperis of the vestiarie.
25 Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri saba wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji.
And of the citee he took o chast seruaunt and onest, that was souereyn on the men werriours; and seuene men of hem that sien the face of the kyng, whiche weren foundun in the citees; and a scryuen, prince of knyytis, that preuyde yonge knyytis; and sixti men of the puple of the lond, that weren foundun in the myddis of the citee.
26 Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.
Forsothe Nabusardan, the maistir of chyualrie, took hem, and brouyte hem to the kyng of Babiloyne in Reblatha.
27 Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe. Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao.
And the kyng of Babiloyne smoot hem, and killide hem in Reblatha, in the lond of Emath; and Juda was translatid fro his lond.
28 Hii ndiyo hesabu ya watu ambao Nebukadneza aliwachukua kwenda uhamishoni: katika mwaka wa saba, Wayahudi 3,023;
This is the puple, whom Nabugodonosor translatide in the seuenthe yeer; Jewis, thre thousynde and thre and twenti.
29 katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Nebukadneza, watu 832 kutoka Yerusalemu;
In the eiytenthe yeer, Nabugodonosor translatide fro Jerusalem eiyte hundrid and two and thritti persoones.
30 katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake, Wayahudi 745 walichukuliwa kwenda uhamishoni na Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme. Jumla ya watu wote walikuwa 4,600.
In the thre and twentithe yeer of Nabugodonosor, Nabusardan, the maister of chyualrie, translatide seuene hundrid and fyue and fourti persoones of Jewis. Therfor alle the persoones weren foure thousynde and sixe hundrid.
31 Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini mfalme wa Yuda, na kumfungua kutoka gerezani siku ya ishirini na tano ya mwezi wa kumi na mbili.
And it was doon, in the seuene and threttithe yeer of the passyng ouer of Joachym, kyng of Juda, in the tweluethe monethe, in the fyue and twentithe dai of the monethe, Euylmerodach, kyng of Babiloyne, reiside in that yeer of his rewme the heed of Joachym, kyng of Juda; and ledde hym out of the hous of the prisoun,
32 Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli.
and spak good thingis with hym. And he settide the trone of him aboue the trones of kyngis, that weren after hym in Babiloyne,
33 Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme.
and chaungide the clothis of his prisoun. And Joachym eet breed bifore hym euere, in alle the daies of his lijf;
34 Siku kwa siku mfalme wa Babeli alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake, hadi siku ya kifo chake.
and hise metis, euerlastynge metis weren youun to hym of the kyng of Babiloyne, ordeyned bi ech dai, til to the dai of his deth, in alle the daies of his lijf. And it was don, aftir that Israel was led in to caitiftee, and Jerusalem was distried, Jeremye, the profete, sat wepinge, and biweilide Jerusalem with this lamentacioun; and he siyyide, and weilide with bitter soule, and seide.

< Yeremia 52 >