< Yeremia 52 >
1 Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.
[was] a son of Twenty and one year[s] Zedekiah when became king he and one [plus] ten year[s] he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his ([was] Hamutal *Q(K)*) [the] daughter of Jeremiah from Libnah.
2 Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.
And he did the evil in [the] eyes of Yahweh according to all that he had done Jehoiakim.
3 Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake. Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.
For - on [the] anger of Yahweh it happened in Jerusalem and Judah until cast out he them from on face his and he rebelled Zedekiah against [the] king of Babylon.
4 Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Wakapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote.
And it was in the year ninth of reigning his in the month tenth on the ten of the month he came Nebuchadnezzar [the] king of Babylon he and all army his on Jerusalem and they encamped on it and they built on it a siege-wall all around.
5 Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.
And it came the city in state of siege until one [plus] ten year of the king Zedekiah.
6 Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu.
In the month fourth on [day] nine of the month and it was severe the famine in the city and not it belonged food to [the] people of the land.
7 Kisha ukuta wa mji ukavunjwa na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba.
And it was broken into the city and all [the] men of war they fled and they went out from the city night [the] way of [the] gate between the two walls which [was] at [the] garden of the king and [the] Chaldeans [were] on the city all around and they went [the] way of the Arabah.
8 Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia Mfalme Sedekia na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika,
And they pursued [the] army of [the] Chaldeans after the king and they overtook Zedekiah in [the] plains of Jericho and all army his they were scattered from with him.
9 naye akakamatwa. Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.
And they seized the king and they brought up him to [the] king of Babylon Riblah towards in [the] land of Hamath and he spoke with him judgments.
10 Huko Ribla mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Pia akawaua maafisa wote wa Yuda.
And he slaughtered [the] king of Babylon [the] sons of Zedekiah to eyes his and also all [the] officials of Judah he slaughtered at Riblah.
11 Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia, akamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli, alipomweka gerezani mpaka siku ya kifo chake.
And [the] eyes of Zedekiah he made blind and he bound him with bronze fetters and he brought him [the] king of Babylon Babylon towards and he put him ([the] house of *Q(K)*) punishment until [the] day of death his.
12 Mnamo siku ya kumi ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, aliyemtumikia mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu.
And in the month fifth on the ten of the month it [was] year nine-teen year of the king Nebuchadnezzar [the] king of Babylon he came Nebuzaradan [the] chief of [the] bodyguards he stood before [the] king of Babylon in Jerusalem.
13 Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu.
And he burned [the] house of Yahweh and [the] house of the king and all [the] houses of Jerusalem and every house of great [person] he burned with fire.
14 Jeshi lote la Wakaldayo chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme walivunja kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu.
And all [the] walls of Jerusalem all around they broke down all [the] army of [the] Chaldeans which [was] with [the] chief of [the] bodyguards.
15 Nebuzaradani, jemadari wa askari walinzi, akawapeleka uhamishoni baadhi ya watu maskini sana na wale waliobaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli.
And some of [the] poor people of the people and [the] rest of the people - who remained in the city and those [who] had fallen who they had fallen to [the] king of Babylon and [the] rest of the craftsman he took into exile Nebuzaradan [the] chief of [the] bodyguards.
16 Lakini Nebuzaradani akawaacha mabaki ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
And some of [the] poor people of the land he left behind Nebuzaradan [the] chief of [the] bodyguards to vinedressers and to ploughmen.
17 Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba yote na kuipeleka Babeli.
And [the] pillars of bronze which [belonged] to [the] house of Yahweh and the stands and [the] sea of bronze which [were] in [the] house of Yahweh they broke [the] Chaldeans and they carried off all bronze their Babylon towards.
18 Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu.
And the pots and the shovels and the snuffers and the bowls and the pans and all [the] articles of bronze which they served with them they took away.
19 Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua yale masinia, vile vyetezo, yale mabakuli ya kunyunyizia, zile sufuria, vile vinara vya taa, zile sahani na yale mabakuli yaliyotumika kwa sadaka za vinywaji, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.
And the basins and the fire-pans and the bowls and the pots and the lampstands and the pans and the bowls which [were] gold gold and which [were] silver silver he took away [the] chief of [the] bodyguards.
20 Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na wale mafahali kumi na mawili wa shaba waliokuwa chini yake, pamoja na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Mfalme Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika.
The pillars - two the sea one and the bull[s] two [plus] ten bronze which [were] under the stands which he had made the king Solomon for [the] house of Yahweh not it belonged weight to bronze their all the articles these.
21 Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane, kimo chake na mzunguko dhiraa kumi na mbili, na unene wa nyanda nne, na zote zilikuwa wazi ndani.
And the pillars [was] eight-teen cubit[s] ([the] height of *Q(K)*) the pillar one and a line of two [plus] ten cubit[s] it goes round it and thickness its [was] four fingers hollow.
22 Sehemu ya shaba juu ya ile nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tano, na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na makomamanga yake ilifanana na hiyo ya kwanza.
And a capital on it [was] bronze and [the] height of the capital one [was] five cubits and a network and pomegranates [was] on the capital all around everything [was] bronze and like these [belonged] to the pillar second and pomegranates.
23 Kulikuwa na makomamanga tisini na sita pembeni; jumla ya makomamanga juu ya wavu uliokuwa umezunguka yalikuwa mia moja.
And they were the pomegranates ninety and six [the] side towards all the pomegranates [were] one hundred on the network all around.
24 Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu.
And he took [the] chief of [the] bodyguards Seraiah [the] priest of the head and Zephaniah [the] priest of the second rank and [the] three [the] keepers of the threshold.
25 Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri saba wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji.
And from the city he took a court-official one who he was an officer - over [the] men of war and seven men from [those who] saw [the] face of the king who they were found in the city and [the] scribe of [the] commander of the army who mustered [the] people of the land and sixty person[s] from [the] people of the land who were found in [the] midst of the city.
26 Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.
And he took them Nebuzaradan [the] chief of [the] bodyguards and he brought them to [the] king of Babylon Riblah towards.
27 Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe. Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao.
And he struck down them [the] king of Babylon and he put to death them at Riblah in [the] land of Hamath and it went into exile Judah from on land its.
28 Hii ndiyo hesabu ya watu ambao Nebukadneza aliwachukua kwenda uhamishoni: katika mwaka wa saba, Wayahudi 3,023;
This [is] the people which he took into exile Nebuchadnezzar in year seven Jews three thousand and twenty and three.
29 katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Nebukadneza, watu 832 kutoka Yerusalemu;
In year eight-teen of Nebuchadnezzar from Jerusalem person[s] eight hundred thirty and two.
30 katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake, Wayahudi 745 walichukuliwa kwenda uhamishoni na Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme. Jumla ya watu wote walikuwa 4,600.
In year three and twenty of Nebuchadnezzar he took into exile Nebuzaradan [the] chief of [the] bodyguards Jews person[s] seven hundred forty and five every person [was] four thousand and six hundred.
31 Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini mfalme wa Yuda, na kumfungua kutoka gerezani siku ya ishirini na tano ya mwezi wa kumi na mbili.
And it was in thirty and seven year of [the] exile of Jehoiachin [the] king of Judah in two [plus] ten month on [day] twenty and five of the month he lifted Evil-Merodach [the] king of Babylon in [the] year of kingdom his [the] head of Jehoiachin [the] king of Judah and he brought out him from [the] house of (imprisonment. *Q(K)*)
32 Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli.
And he spoke with him good and he put seat his from above [the] seat of (the kings *Q(K)*) who [were] with him in Babylon.
33 Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme.
And he changed [the] clothes of imprisonment his and he ate food before him continually all [the] days of life his.
34 Siku kwa siku mfalme wa Babeli alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake, hadi siku ya kifo chake.
And allowance his an allowance of continuity it was given to him from with [the] king of Babylon a matter of a day in day its until [the] day of death his all [the] days of life his.