< Yeremia 51 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama nitaamsha roho ya mwangamizi dhidi ya Babeli na watu wakaao Leb-Kamai.
Ainsi a dit l'Éternel: Je fais lever un vent de destruction contre Babylone, et contre les habitants de ce pays, qui est le cœur de mes adversaires.
2 Nitawatuma wageni Babeli kumpepeta na kuiharibu nchi yake; watampinga kila upande katika siku ya maafa yake.
Et j'envoie contre Babylone des vanneurs qui la vanneront, et qui videront son pays; car ils viendront sur elle de tous côtés, au jour du malheur.
3 Usimwache mpiga upinde afunge kamba upinde wake, wala usimwache avae silaha zake. Usiwaonee huruma vijana wake; angamiza jeshi lake kabisa.
Qu'on bande l'arc contre celui qui bande son arc, et contre celui qui est fier dans sa cuirasse! Et n'épargnez pas ses gens d'élite; vouez à l'interdit toute son armée;
4 Wataanguka waliouawa katika Babeli, wakiwa na majeraha ya kutisha barabarani zake.
Qu'ils tombent blessés à mort au pays des Caldéens, et transpercés dans ses rues!
5 Kwa maana Israeli na Yuda hawajaachwa na Mungu wao, Bwana Mwenye Nguvu Zote, ingawa nchi yao imejaa uovu mbele zake yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Car Israël et Juda ne sont pas abandonnés de leur Dieu, de l'Éternel des armées, et le pays des Caldéens est rempli de crimes devant le Saint d'Israël.
6 “Kimbieni kutoka Babeli! Okoeni maisha yenu! Msiangamizwe kwa sababu ya dhambi zake. Ni wakati wa kisasi cha Bwana, atamlipa kile anachostahili.
Fuyez loin de Babylone, et que chacun sauve sa vie, de peur que vous ne périssiez dans son iniquité! Car c'est le temps de la vengeance de l'Éternel; il lui rend ce qu'elle a mérité.
7 Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu katika mkono wa Bwana; aliufanya ulimwengu wote ulewe. Mataifa walikunywa mvinyo wake; kwa hiyo sasa wameingiwa na wazimu.
Babylone était dans la main de l'Éternel une coupe d'or, qui enivrait toute la terre; les nations ont bu de son vin, c'est pourquoi les nations sont devenues folles.
8 Babeli ataanguka ghafula na kuvunjika. Mwombolezeni! Tafuteni zeri ya kutuliza maumivu yake, labda anaweza kupona.
En un instant Babylone est tombée; elle s'est brisée; gémissez sur elle! Prenez du baume pour sa douleur; peut-être guérira-t-elle.
9 “‘Tungemponya Babeli, lakini hawezi kuponyeka; tumwacheni, na kila mmoja wetu aende nchi yake mwenyewe, kwa kuwa hukumu yake inafika angani, inapanda juu hadi mawinguni.’
Nous avons traité Babylone, et elle n'est pas guérie. Laissez-la; et allons-nous-en, chacun dans son pays; car son jugement atteint aux cieux, et s'élève jusqu'aux nues.
10 “‘Bwana amethibitisha haki yetu; njooni, tutangaze katika Sayuni kitu ambacho Bwana Mungu wetu amefanya.’
L'Éternel a manifesté notre justice. Venez, et racontons dans Sion l'œuvre de l'Éternel, notre Dieu.
11 “Noeni mishale, chukueni ngao! Bwana amewaamsha wafalme wa Wamedi, kwa sababu nia yake ni kuangamiza Babeli. Bwana atalipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
Aiguisez les flèches, saisissez les boucliers! L'Éternel a réveillé l'esprit des rois de Médie, parce qu'il a résolu de détruire Babylone. Car c'est ici la vengeance de l'Éternel, la vengeance de son temple.
12 Twekeni bendera juu ya kuta za Babeli! Imarisheni ulinzi, wekeni walinzi, andaeni waviziao! Bwana atatimiza kusudi lake, amri yake juu ya watu wa Babeli.
Élevez un étendard contre les murailles de Babylone! Renforcez la garnison, posez les gardes; préparez les embuscades! Car c'est l'Éternel qui a projeté, c'est l'Éternel qui exécute ce qu'il a dit contre les habitants de Babylone.
13 Wewe uishiye kando ya maji mengi na uliye na wingi wa hazina, mwisho wako umekuja, wakati wako wa kukatiliwa mbali.
Toi qui es assise sur plusieurs eaux, toi qui abondes en trésors, ta fin est venue, la mesure de ton avarice est comble!
14 Bwana Mwenye Nguvu Zote ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: ‘Hakika nitakujaza na watu, kama kundi la nzige, nao watapiga kelele za ushindi juu yako.’
L'Éternel des armées l'a juré par lui-même: Certainement je te remplirai d'hommes comme de sauterelles, et ils pousseront contre toi le cri de guerre!
15 “Aliiumba dunia kwa uweza wake; akaweka misingi ya ulimwengu kwa hekima yake na akazitandaza mbingu kwa ufahamu wake.
C'est lui qui a fait la terre par sa puissance, qui a fondé le monde par sa sagesse, qui a étendu les cieux par son intelligence.
16 Atoapo sauti yake, maji yaliyo katika mbingu hunguruma, huyafanya mawingu yainuke kutoka miisho ya dunia. Hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua, naye huuleta upepo kutoka ghala zake.
Au son de sa voix, les eaux s'amassent dans les cieux; il fait monter les vapeurs du bout de la terre, il produit les éclairs et la pluie; il tire le vent de ses trésors.
17 “Kila mtu ni mjinga na hana maarifa; kila sonara ameaibishwa na sanamu zake. Vinyago vyake ni vya udanganyifu, havina pumzi ndani yavyo.
Tout homme est abruti dans sa science; tout orfèvre est honteux de son image taillée; car ses idoles ne sont que mensonge, il n'y a point de respiration en elles;
18 Havifai kitu, ni vitu vya kufanyia mzaha, hukumu yavyo itakapowadia, vitaangamia.
Elles ne sont que vanité, une œuvre de tromperie. Elles périront, au temps où Dieu les visitera.
19 Yeye Aliye Fungu la Yakobo sivyo alivyo, kwani ndiye Muumba wa vitu vyote, pamoja na kabila la urithi wake: Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.
Celui qui est la part de Jacob n'est pas comme elles; car c'est lui qui a tout formé, et Israël est la tribu de son héritage. Son nom est l'Éternel des armées.
20 “Wewe ndiwe rungu langu la vita, silaha yangu ya vita: kwa wewe navunjavunja mataifa, kwa wewe naangamiza falme,
Tu m'as été un marteau, un instrument de guerre: par toi j'ai mis en pièces des nations, par toi j'ai détruit des royaumes.
21 kwa wewe navunjavunja farasi na mpanda farasi, kwa wewe navunjavunja gari la vita na mwendeshaji wake,
Par toi j'ai mis en pièces le cheval et son cavalier; par toi j'ai mis en pièces le char et celui qui le monte.
22 kwa wewe napondaponda mwanaume na mwanamke, kwa wewe napondaponda mzee na kijana, kwa wewe napondaponda kijana wa kiume na mwanamwali,
Par toi j'ai mis en pièces l'homme et la femme; par toi j'ai mis en pièces le vieillard et le jeune garçon; par toi j'ai mis en pièces le jeune homme et la vierge.
23 kwa wewe nampondaponda mchungaji na kundi, kwa wewe nampondaponda mkulima na maksai, kwa wewe nawapondaponda watawala na maafisa.
Par toi j'ai mis en pièces le berger et son troupeau; par toi j'ai mis en pièces le laboureur et son attelage; par toi j'ai mis en pièces le gouverneur et les magistrats.
24 “Mbele ya macho yako nitamlipiza Babeli na wote waishio Ukaldayo kwa ajili ya makosa yote waliyofanya katika Sayuni,” asema Bwana.
Mais je rendrai à Babylone et à tous les habitants de la Caldée, sous vos yeux, tous les maux qu'ils ont faits dans Sion, dit l'Éternel.
25 “Mimi niko kinyume nawe, ee mlima unaoharibu, wewe uangamizaye dunia yote,” asema Bwana. “Nitanyoosha mkono wangu dhidi yako, nikuvingirishe kutoka kwenye kilele cha mwamba, na kukufanya mlima ulioteketezwa kwa moto.
Voici, je viens à toi, dit l'Éternel, montagne de destruction, qui détruisais toute la terre! J'étendrai aussi ma main sur toi, et je te roulerai du haut des rochers, et je ferai de toi une montagne embrasée.
26 Hakuna jiwe litakalochukuliwa kutoka kwako kwa ajili ya kufanywa jiwe la pembeni, wala jiwe lolote kwa ajili ya msingi, kwa maana utakuwa ukiwa milele,” asema Bwana.
Et on ne pourra prendre de toi ni pierres angulaires, ni pierre de fondements, car tu seras réduite en désolations perpétuelles dit l'Éternel.
27 “Twekeni bendera katika nchi! Pigeni tarumbeta katikati ya mataifa! Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake, iteni falme hizi dhidi yake: Ararati, Mini na Ashkenazi. Wekeni jemadari dhidi yake, pelekeni farasi wengi kama kundi la nzige.
Élevez l'étendard sur la terre; sonnez de la trompette parmi les nations; préparez les nations contre elle! Appelez contre elle les royaumes d'Ararat, de Minni et d'Ashkénaz! Établissez contre elle des capitaines! Faites monter les chevaux comme des sauterelles effrayantes!
28 Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake, wafalme wa Wamedi, watawala wao na maafisa wao wote, pamoja na nchi zote wanazotawala.
Préparez contre elle des nations, les rois de Médie, ses gouverneurs, et tous ses magistrats, et tout le pays de sa domination!
29 Nchi inatetemeka na kugaagaa, kwa kuwa makusudi ya Bwana dhidi ya Babeli yanasimama: yaani, kuangamiza nchi ya Babeli ili pasiwe na yeyote atakayeishi humo.
La terre s'ébranle, et elle est en travail; car les desseins de l'Éternel contre Babylone s'exécutent, pour faire du pays de Babylone un désert sans habitants.
30 Mashujaa wa Babeli wameacha kupigana, wamebaki katika ngome zao. Nguvu zao zimekwisha, wamekuwa kama wanawake. Makazi yake yameteketezwa kwa moto, makomeo ya malango yake yamevunjika.
Les hommes vaillants de Babylone cessent de combattre, ils se tiennent dans les forteresses; leur force est épuisée; ils sont devenus comme des femmes. On a incendié ses demeures; les barres de ses portes sont brisées.
31 Tarishi mmoja humfuata mwingine, na mjumbe humfuata mjumbe, kumtangazia mfalme wa Babeli kwamba mji wake wote umetekwa,
Les courriers, les messagers se croisent, pour annoncer au roi de Babylone que sa ville est prise de tous côtés,
32 Vivuko vya mito vimekamatwa, mabwawa yenye mafunjo yametiwa moto, nao askari wameingiwa na hofu kuu.”
Que les passages sont saisis, les marais embrasés par le feu, et que les hommes de guerre sont éperdus.
33 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria wakati inapokanyagwa; wakati wa kumvuna utakuja upesi.”
Car ainsi a dit l'Éternel des armées, le Dieu d'Israël: La fille de Babylone est comme l'aire au temps où on la foule; encore un peu, et le temps de la moisson sera venu.
34 “Nebukadneza mfalme wa Babeli ametula, ametufanya tuchangayikiwe, ametufanya tuwe gudulia tupu. Kama nyoka ametumeza na kujaza tumbo lake kwa vyakula vyetu vizuri, kisha akatutapika.
Nébucadnetsar, roi de Babylone, m'a dévorée, il m'a brisée; il nous a laissés comme un vase vide; il nous a engloutis comme le dragon; il a rempli son ventre de ce que j'avais de plus excellent; il nous a chassés au loin.
35 Jeuri iliyofanyiwa miili yetu na iwe juu ya Babeli,” ndivyo wasemavyo wakaao Sayuni. “Damu yetu na iwe juu ya wale waishio Babeli,” asema Yerusalemu.
Que la violence faite à moi et à ma chair, retombe sur Babylone! dira l'habitante de Sion. Que mon sang soit sur les habitants de la Caldée! dira Jérusalem.
36 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo: “Tazama, nitatetea shauri lako na kulipiza kisasi kwa ajili yako; nitaikausha bahari yake na kuzikausha chemchemi zake.
C'est pourquoi, ainsi a dit l'Éternel: Voici, je défendrai ta cause, et je ferai la vengeance pour toi; je dessécherai sa mer, et je ferai tarir sa source.
37 Babeli utakuwa lundo la magofu na makao ya mbweha, kitu cha kutisha na kudharauliwa, mahali asipoishi mtu.
Et Babylone deviendra des monceaux de ruines, un gîte de chacals, un objet d'étonnement et de moquerie, et personne n'y habitera.
38 Watu wake wote wananguruma kama simba wadogo, wanakoroma kama wana simba.
Ils rugiront ensemble comme des lions, ils crieront comme des lionceaux.
39 Lakini wakati wakiwa wameamshwa, nitawaandalia karamu na kuwafanya walewe, ili wapige kelele kwa kicheko, kisha walale milele na wasiamke,” asema Bwana.
Quand ils seront échauffés, je leur présenterai à boire; je les enivrerai, pour qu'ils se réjouissent, et s'endorment d'un sommeil éternel, et ne se réveillent plus, dit l'Éternel.
40 “Nitawateremsha kama wana-kondoo waendao machinjoni, kama kondoo dume na mbuzi.
Je les ferai descendre comme des agneaux à la tuerie, et comme des béliers avec des boucs.
41 “Tazama jinsi Sheshaki atakamatwa, majivuno ya dunia yote yatakavyonyakuliwa. Babeli atakuwa mwenye hofu kiasi gani kati ya mataifa!
Comment Shéshac a-t-elle été prise? Comment a-t-elle été saisie, celle que louait toute la terre? Comment Babylone est-elle réduite en désolation parmi les peuples?
42 Bahari itainuka juu ya Babeli; mawimbi yake yenye kunguruma yatamfunika.
La mer est montée sur Babylone; elle est couverte par la multitude de ses flots.
43 Miji yake itakuwa ukiwa, kame na jangwa, nchi ambayo hakuna yeyote anayeishi ndani yake, ambayo hakuna mtu anayepita humo.
Ses villes sont devenues un désert, une terre d'aridité et de landes, une terre où personne n'habite et où ne passe aucun fils d'homme.
44 Nitamwadhibu Beli katika Babeli, na kumfanya atapike kile alichokimeza. Mataifa hayatamiminika tena kwake. Nao ukuta wa Babeli utaanguka.
Et je punirai Bel dans Babylone, et je ferai sortir de sa bouche ce qu'il a englouti, et les nations n'afflueront plus vers lui. La muraille même de Babylone est tombée!
45 “Tokeni ndani yake, enyi watu wangu! Okoeni maisha yenu! Ikimbieni hasira kali ya Bwana.
Sortez du milieu d'elle, mon peuple, et que chacun sauve sa vie devant l'ardeur de la colère de l'Éternel!
46 Msikate tamaa wala msiogope tetesi zitakaposikika katika nchi; tetesi moja inasikika mwaka huu, nyingine mwaka unaofuata; tetesi juu ya jeuri katika nchi, na ya mtawala dhidi ya mtawala.
Que votre cœur ne faiblisse pas, et ne soyez pas effrayés des bruits que l'on entendra dans le pays. Car cette année viendra ce bruit, puis une autre année un autre bruit; et il y aura violence dans le pays, et dominateur contre dominateur.
47 Kwa kuwa hakika wakati utawadia nitakapoziadhibu sanamu za Babeli; nchi yake yote itatiwa aibu, na watu wake wote waliouawa wataangukia ndani yake.
C'est pourquoi, voici, les jours viennent où je visiterai les images taillées de Babylone; et tout son pays sera rendu honteux, et tous ses blessés à mort tomberont au milieu d'elle.
48 Ndipo mbingu na dunia na vyote vilivyomo ndani yake vitapiga kelele za shangwe juu ya Babeli, kwa kuwa kutoka kaskazini waharabu watamshambulia,” asema Bwana.
Et les cieux, et la terre, et tout ce qui est en eux, se réjouiront avec un chant de triomphe sur Babylone, parce que du nord les dévastateurs viendront contre elle, dit l'Éternel.
49 “Babeli ni lazima aanguke kwa sababu ya kuwaua Waisraeli, kama vile waliouawa duniani kote walivyoanguka kwa sababu ya Babeli.
Comme Babylone a fait tomber les blessés à mort d'Israël, ainsi tomberont à Babylone les blessés à mort de tout le pays.
50 Wewe uliyepona upanga, ondoka wala usikawie! Mkumbuke Bwana ukiwa katika nchi ya mbali, na utafakari juu ya Yerusalemu.”
Vous qui avez échappé à l'épée, partez, ne vous arrêtez point! Dans la terre lointaine souvenez-vous de l'Éternel, et que Jérusalem se présente à vos cœurs!
51 “Tumetahayari, kwa maana tumetukanwa na aibu imefunika nyuso zetu, kwa sababu wageni wameingia mahali patakatifu pa nyumba ya Bwana.”
Nous sommes honteux, direz-vous, des opprobres que nous avons entendus; la confusion a couvert nos faces, quand des étrangers sont venus contre les sanctuaires de la maison de l'Éternel.
52 “Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapoadhibu sanamu zake, na katika nchi yake yote waliojeruhiwa watalia kwa maumivu makali.
C'est pourquoi, voici les jours viennent, dit l'Éternel, où je visiterai ses images taillées, et les blessés à mort gémiront par tout son pays.
53 Hata kama Babeli ikifika angani na kuziimarisha ngome zake ndefu, nitatuma waharabu dhidi yake,” asema Bwana.
Quand Babylone s'élèverait jusqu'aux cieux, et quand elle rendrait inaccessible sa forteresse, les dévastateurs y entreront de par moi, dit l'Éternel.
54 “Sauti ya kilio inasikika kutoka Babeli, sauti ya uharibifu mkuu kutoka nchi ya Wakaldayo.
De Babylone un cri se fait entendre, un grand fracas, du pays des Caldéens.
55 Bwana ataiangamiza Babeli, atanyamazisha makelele ya kishindo chake. Mawimbi ya adui yatanguruma kama maji makuu, ngurumo ya sauti zao itavuma.
Car l'Éternel va ravager Babylone, il va faire cesser au milieu d'elle la grande voix. Leurs flots grondent comme les grosses eaux; leur voix retentit avec éclat.
56 Mharabu atakuja dhidi ya Babeli, mashujaa wake watakamatwa, nazo pinde zao zitavunjwa. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa kisasi, yeye atalipiza kikamilifu.
Car le dévastateur est venu sur elle, sur Babylone. Ses hommes forts sont pris, et leurs arcs sont brisés; car l'Éternel est le Dieu des rétributions; il rend à chacun ce qui lui est dû.
57 Nitawafanya maafisa wake na wenye busara walewe, watawala wao, maafisa, pamoja na wapiganaji wao; watalala milele na hawataamka,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote.
J'enivrerai ses princes et ses sages, ses gouverneurs, ses magistrats et ses hommes de guerre; ils s'endormiront d'un sommeil éternel et ne se réveilleront plus, dit le Roi, dont le nom est l'Éternel des armées.
58 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Ukuta mnene wa Babeli utasawazishwa, na malango yaliyoinuka yatateketezwa kwa moto; mataifa yanajichosha bure, taabu ya mataifa ni nishati tu ya miali ya moto.”
Ainsi a dit l'Éternel des armées: Ces murailles de Babylone, si larges, seront entièrement rasées, et ses portes, si hautes, seront brûlées par le feu; ainsi les peuples auront travaillé pour le néant, et les nations se seront lassées pour le feu.
59 Huu ndio ujumbe Yeremia aliompa afisa Seraya mwana wa Neria mwana wa Maaseya, alipokwenda Babeli pamoja na Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wake.
C'est ici l'ordre que Jérémie, le prophète, donna à Séraja, fils de Nérija, fils de Machséja, quand il alla à Babylone avec Sédécias, roi de Juda, la quatrième année de son règne. Or Séraja était premier chambellan.
60 Yeremia alikuwa ameandika ndani ya kitabu kuhusu maafa yote yatakayoipata Babeli, yaani yote yaliyokuwa yameandikwa kuhusu Babeli.
Jérémie écrivit, dans un livre, tout le mal qui devait venir sur Babylone, toutes ces paroles qui sont écrites sur Babylone.
61 Yeremia akamwambia Seraya, “Utakapofika Babeli, hakikisha kwamba umesoma maneno haya yote kwa sauti kubwa.
Jérémie dit à Séraja: Sitôt que tu seras arrivé à Babylone, tu regarderas et tu liras toutes ces paroles,
62 Kisha sema, ‘Ee Bwana, umesema utaangamiza mahali hapa ili mtu wala mnyama asiishi ndani yake, napo patakuwa ukiwa milele.’
Et tu diras: “Éternel! tu as dit de ce lieu que tu le détruirais, en sorte qu'il n'y ait plus d'habitant, ni homme ni bête, mais qu'il soit réduit en des désolations perpétuelles. “
63 Utakapomaliza kusoma hiki kitabu, kifungie jiwe kisha ukitupe ndani ya Mto Frati.
Et dès que tu auras achevé de lire ce livre, tu y attacheras une pierre et tu le jetteras dans l'Euphrate;
64 Kisha sema, ‘Hivi ndivyo Babeli utakavyozama na usiinuke tena, kwa sababu ya maafa nitakayoleta juu yake. Nao watu wake wataanguka.’” Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.
Et tu diras: Ainsi s'abîmera Babylone! et elle ne se relèvera point du mal que je vais faire venir sur elle; ils seront accablés! Jusqu'ici sont les paroles de Jérémie.

< Yeremia 51 >