< Yeremia 51 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama nitaamsha roho ya mwangamizi dhidi ya Babeli na watu wakaao Leb-Kamai.
Yahvé dit: « Voici que je me lève contre Babylone, et contre les habitants de Lebkamai, un vent destructeur.
2 Nitawatuma wageni Babeli kumpepeta na kuiharibu nchi yake; watampinga kila upande katika siku ya maafa yake.
J'enverrai à Babylone des étrangers, qui la vanneront. Ils vont vider sa terre; car au jour de la détresse, ils seront tous contre elle.
3 Usimwache mpiga upinde afunge kamba upinde wake, wala usimwache avae silaha zake. Usiwaonee huruma vijana wake; angamiza jeshi lake kabisa.
Contre celui qui se courbe, que l'archer courbe son arc, également contre celui qui s'élève dans sa cotte de mailles. N'épargnez pas ses jeunes hommes! Détruisez complètement son armée!
4 Wataanguka waliouawa katika Babeli, wakiwa na majeraha ya kutisha barabarani zake.
Ils tomberont tués dans le pays des Chaldéens, et poussé dans ses rues.
5 Kwa maana Israeli na Yuda hawajaachwa na Mungu wao, Bwana Mwenye Nguvu Zote, ingawa nchi yao imejaa uovu mbele zake yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Car Israël n'est pas abandonné, ni Juda, par son Dieu, par Yahvé des Armées; bien que leur terre soit pleine de culpabilité envers le Saint d'Israël.
6 “Kimbieni kutoka Babeli! Okoeni maisha yenu! Msiangamizwe kwa sababu ya dhambi zake. Ni wakati wa kisasi cha Bwana, atamlipa kile anachostahili.
« Fuyez du milieu de Babylone! Tout le monde sauve sa vie! Ne sois pas coupé dans son iniquité, car c'est le temps de la vengeance de Yahvé. Il lui rendra la monnaie de sa pièce.
7 Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu katika mkono wa Bwana; aliufanya ulimwengu wote ulewe. Mataifa walikunywa mvinyo wake; kwa hiyo sasa wameingiwa na wazimu.
Babylone a été une coupe d'or dans la main de Yahvé, qui a rendu toute la terre ivre. Les nations ont bu de son vin; c'est pourquoi les nations sont devenues folles.
8 Babeli ataanguka ghafula na kuvunjika. Mwombolezeni! Tafuteni zeri ya kutuliza maumivu yake, labda anaweza kupona.
Babylone est soudainement tombée et a été détruite! Gémissez pour elle! Prenez du baume pour sa douleur. Peut-être qu'elle peut être guérie.
9 “‘Tungemponya Babeli, lakini hawezi kuponyeka; tumwacheni, na kila mmoja wetu aende nchi yake mwenyewe, kwa kuwa hukumu yake inafika angani, inapanda juu hadi mawinguni.’
« Nous aurions guéri Babylone, mais elle n'est pas guérie. Abandonnez-la, et que chacun aille dans son propre pays; car son jugement atteint le ciel, et s'élève jusqu'aux cieux.
10 “‘Bwana amethibitisha haki yetu; njooni, tutangaze katika Sayuni kitu ambacho Bwana Mungu wetu amefanya.’
« C'est Yahvé qui a produit notre justice. Venez, et annonçons dans Sion l'œuvre de Yahvé notre Dieu ».
11 “Noeni mishale, chukueni ngao! Bwana amewaamsha wafalme wa Wamedi, kwa sababu nia yake ni kuangamiza Babeli. Bwana atalipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
« Rendez les flèches acérées! Tenez fermement les boucliers! Yahvé a éveillé l'esprit des rois de Médie, car son but est contre Babylone, pour la détruire; car c'est la vengeance de Yahvé, la vengeance de son temple.
12 Twekeni bendera juu ya kuta za Babeli! Imarisheni ulinzi, wekeni walinzi, andaeni waviziao! Bwana atatimiza kusudi lake, amri yake juu ya watu wa Babeli.
Dressez un étendard contre les murs de Babylone! Rendez la montre forte! Mettez en place les gardiens, et préparer les embuscades; car Yahvé a voulu et fait ce qu'il a dit au sujet des habitants de Babylone.
13 Wewe uishiye kando ya maji mengi na uliye na wingi wa hazina, mwisho wako umekuja, wakati wako wa kukatiliwa mbali.
Toi qui habites sur de grandes eaux, abondantes en trésors, ta fin est arrivée, la mesure de ta convoitise.
14 Bwana Mwenye Nguvu Zote ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: ‘Hakika nitakujaza na watu, kama kundi la nzige, nao watapiga kelele za ushindi juu yako.’
L'Éternel des armées l'a juré par lui-même, en disant, Je vais te remplir d'hommes, comme pour les sauterelles, et ils pousseront des cris de joie contre toi ».
15 “Aliiumba dunia kwa uweza wake; akaweka misingi ya ulimwengu kwa hekima yake na akazitandaza mbingu kwa ufahamu wake.
« Il a fait la terre par sa puissance. Il a établi le monde par sa sagesse. Par son intelligence, il a étendu les cieux.
16 Atoapo sauti yake, maji yaliyo katika mbingu hunguruma, huyafanya mawingu yainuke kutoka miisho ya dunia. Hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua, naye huuleta upepo kutoka ghala zake.
Quand il fait entendre sa voix, il y a un rugissement des eaux dans les cieux, et il fait monter les vapeurs des extrémités de la terre. Il fait des éclairs pour la pluie, et fait sortir le vent de ses trésors.
17 “Kila mtu ni mjinga na hana maarifa; kila sonara ameaibishwa na sanamu zake. Vinyago vyake ni vya udanganyifu, havina pumzi ndani yavyo.
« Tout homme est devenu stupide et sans connaissance. Tout orfèvre est déçu par son image, car ses images en fusion sont des mensonges, et il n'y a pas de souffle en eux.
18 Havifai kitu, ni vitu vya kufanyia mzaha, hukumu yavyo itakapowadia, vitaangamia.
Ils ne sont que vanité, une œuvre d'illusion. Au moment de leur visite, ils périront.
19 Yeye Aliye Fungu la Yakobo sivyo alivyo, kwani ndiye Muumba wa vitu vyote, pamoja na kabila la urithi wake: Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.
La part de Jacob n'est pas comme celles-ci, car il a formé toutes choses, y compris la tribu de son héritage. Yahvé des Armées est son nom.
20 “Wewe ndiwe rungu langu la vita, silaha yangu ya vita: kwa wewe navunjavunja mataifa, kwa wewe naangamiza falme,
« Vous êtes ma hache de guerre et mes armes de guerre. Avec toi, je briserai les nations en morceaux. Avec toi, je détruirai des royaumes.
21 kwa wewe navunjavunja farasi na mpanda farasi, kwa wewe navunjavunja gari la vita na mwendeshaji wake,
Avec vous, je briserai en morceaux le cheval et son cavalier.
22 kwa wewe napondaponda mwanaume na mwanamke, kwa wewe napondaponda mzee na kijana, kwa wewe napondaponda kijana wa kiume na mwanamwali,
Avec vous, je briserai en morceaux le char et celui qui le conduit. Avec toi, je vais briser en morceaux homme et femme. Avec toi, je vais briser en morceaux le vieil homme et le jeune. Avec toi, je vais briser en morceaux le jeune homme et la vierge.
23 kwa wewe nampondaponda mchungaji na kundi, kwa wewe nampondaponda mkulima na maksai, kwa wewe nawapondaponda watawala na maafisa.
Avec vous, je briserai en morceaux le berger et son troupeau. Avec toi, je vais briser en morceaux le fermier et son joug. Avec toi, je vais briser en morceaux gouverneurs et adjoints.
24 “Mbele ya macho yako nitamlipiza Babeli na wote waishio Ukaldayo kwa ajili ya makosa yote waliyofanya katika Sayuni,” asema Bwana.
« Je rendrai à Babylone et à tous les habitants de la Chaldée tout le mal qu'ils ont fait à Sion sous tes yeux, dit Yahvé.
25 “Mimi niko kinyume nawe, ee mlima unaoharibu, wewe uangamizaye dunia yote,” asema Bwana. “Nitanyoosha mkono wangu dhidi yako, nikuvingirishe kutoka kwenye kilele cha mwamba, na kukufanya mlima ulioteketezwa kwa moto.
« Voici, je suis contre toi, montagne dévastatrice, dit Yahvé, « qui détruit toute la terre. J'étendrai ma main sur toi, te faire descendre des rochers, et fera de toi une montagne brûlée.
26 Hakuna jiwe litakalochukuliwa kutoka kwako kwa ajili ya kufanywa jiwe la pembeni, wala jiwe lolote kwa ajili ya msingi, kwa maana utakuwa ukiwa milele,” asema Bwana.
Ils ne te prendront pas une pierre angulaire, ni une pierre pour les fondations; mais tu seras désolée pour toujours », dit Yahvé.
27 “Twekeni bendera katika nchi! Pigeni tarumbeta katikati ya mataifa! Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake, iteni falme hizi dhidi yake: Ararati, Mini na Ashkenazi. Wekeni jemadari dhidi yake, pelekeni farasi wengi kama kundi la nzige.
« Établissez une norme dans le pays! Sonnez la trompette parmi les nations! Préparez les nations contre elle! Rassemblez contre elle les royaumes d'Ararat, de Minni et d'Ashkenaz! Nommez un marshal contre elle! Faites monter les chevaux comme des sauterelles!
28 Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake, wafalme wa Wamedi, watawala wao na maafisa wao wote, pamoja na nchi zote wanazotawala.
Préparez contre elle les nations, les rois des Mèdes, ses gouverneurs, et tous ses députés, et tout le pays de leur domination!
29 Nchi inatetemeka na kugaagaa, kwa kuwa makusudi ya Bwana dhidi ya Babeli yanasimama: yaani, kuangamiza nchi ya Babeli ili pasiwe na yeyote atakayeishi humo.
Le pays tremble et souffre; pour que les desseins de Yahvé contre Babylone tiennent, pour faire du pays de Babylone une désolation, sans habitant.
30 Mashujaa wa Babeli wameacha kupigana, wamebaki katika ngome zao. Nguvu zao zimekwisha, wamekuwa kama wanawake. Makazi yake yameteketezwa kwa moto, makomeo ya malango yake yamevunjika.
Les puissants de Babylone ont cessé de se battre, ils restent dans leurs forteresses. Leur puissance a échoué. Ils sont devenus des femmes. Ses habitations sont incendiées. Ses barreaux sont cassés.
31 Tarishi mmoja humfuata mwingine, na mjumbe humfuata mjumbe, kumtangazia mfalme wa Babeli kwamba mji wake wote umetekwa,
Un coureur courra à la rencontre d'un autre, et un messager pour en rencontrer un autre, pour montrer au roi de Babylone que sa ville est prise de toutes parts.
32 Vivuko vya mito vimekamatwa, mabwawa yenye mafunjo yametiwa moto, nao askari wameingiwa na hofu kuu.”
Les passages sont donc saisis. Ils ont brûlé les roseaux au feu. Les hommes de guerre sont effrayés. »
33 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria wakati inapokanyagwa; wakati wa kumvuna utakuja upesi.”
Car Yahvé des Armées, le Dieu d'Israël, dit: « La fille de Babylone est comme une aire de battage au moment où elle est foulée. Encore un peu de temps, et le temps de la moisson viendra pour elle. »
34 “Nebukadneza mfalme wa Babeli ametula, ametufanya tuchangayikiwe, ametufanya tuwe gudulia tupu. Kama nyoka ametumeza na kujaza tumbo lake kwa vyakula vyetu vizuri, kisha akatutapika.
« Nabuchodonosor, roi de Babylone, m'a dévoré. Il m'a écrasé. Il a fait de moi un récipient vide. Il m'a, comme un monstre, englouti. Il a rempli sa bouche de mes délices. Il m'a chassé.
35 Jeuri iliyofanyiwa miili yetu na iwe juu ya Babeli,” ndivyo wasemavyo wakaao Sayuni. “Damu yetu na iwe juu ya wale waishio Babeli,” asema Yerusalemu.
Que la violence faite à moi et à ma chair soit sur Babylone! » l'habitant de Sion dira: et, « Que mon sang soit sur les habitants de la Chaldée! » Jérusalem dira.
36 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo: “Tazama, nitatetea shauri lako na kulipiza kisasi kwa ajili yako; nitaikausha bahari yake na kuzikausha chemchemi zake.
C'est pourquoi Yahvé dit: « Voici, je vais plaider ta cause, et se venger pour vous. Je vais assécher sa mer, et rendre sa fontaine sèche.
37 Babeli utakuwa lundo la magofu na makao ya mbweha, kitu cha kutisha na kudharauliwa, mahali asipoishi mtu.
Babylone deviendra un monceau, un lieu de résidence pour les chacals, un étonnement, et un sifflement, sans habitant.
38 Watu wake wote wananguruma kama simba wadogo, wanakoroma kama wana simba.
Ils rugiront ensemble comme de jeunes lions. Ils grogneront comme des lionceaux.
39 Lakini wakati wakiwa wameamshwa, nitawaandalia karamu na kuwafanya walewe, ili wapige kelele kwa kicheko, kisha walale milele na wasiamke,” asema Bwana.
Quand ils seront enflammés, je ferai leur festin, et je les rendrai ivres, pour qu'ils puissent se réjouir, et dormir d'un sommeil perpétuel, et ne pas se réveiller », dit Yahvé.
40 “Nitawateremsha kama wana-kondoo waendao machinjoni, kama kondoo dume na mbuzi.
« Je les ferai descendre comme des agneaux à l'abattoir, comme des béliers avec des chèvres mâles.
41 “Tazama jinsi Sheshaki atakamatwa, majivuno ya dunia yote yatakavyonyakuliwa. Babeli atakuwa mwenye hofu kiasi gani kati ya mataifa!
« Comment Sheshach est pris! Comme la louange de la terre entière est saisie! Comme Babylone est devenue une désolation parmi les nations!
42 Bahari itainuka juu ya Babeli; mawimbi yake yenye kunguruma yatamfunika.
La mer est montée sur Babylone. Elle est couverte de la multitude de ses vagues.
43 Miji yake itakuwa ukiwa, kame na jangwa, nchi ambayo hakuna yeyote anayeishi ndani yake, ambayo hakuna mtu anayepita humo.
Ses villes sont devenues une désolation, une terre aride, et un désert, une terre dans laquelle aucun homme n'habite. Aucun fils de l'homme ne passe à côté.
44 Nitamwadhibu Beli katika Babeli, na kumfanya atapike kile alichokimeza. Mataifa hayatamiminika tena kwake. Nao ukuta wa Babeli utaanguka.
J'exécuterai le jugement sur Bel à Babylone, et je ferai sortir de sa bouche ce qu'il a englouti. Les nations ne couleront plus vers lui. Oui, le mur de Babylone va tomber.
45 “Tokeni ndani yake, enyi watu wangu! Okoeni maisha yenu! Ikimbieni hasira kali ya Bwana.
« Mon peuple, éloigne-toi du milieu d'elle, et que chacun d'entre vous se sauve de l'ardente colère de Yahvé.
46 Msikate tamaa wala msiogope tetesi zitakaposikika katika nchi; tetesi moja inasikika mwaka huu, nyingine mwaka unaofuata; tetesi juu ya jeuri katika nchi, na ya mtawala dhidi ya mtawala.
Ne laissez pas votre cœur s'évanouir. Ne craignez pas les nouvelles qui seront entendues dans le pays. Car les nouvelles viendront dans un an, et après cela, dans une autre année, des nouvelles viendront, et la violence dans le pays, dirigeant contre dirigeant.
47 Kwa kuwa hakika wakati utawadia nitakapoziadhibu sanamu za Babeli; nchi yake yote itatiwa aibu, na watu wake wote waliouawa wataangukia ndani yake.
C'est pourquoi voici que les jours viennent où j'exécuterai le jugement sur les images gravées de Babylone; et tout son pays sera confondu. Tous ses morts tomberont au milieu d'elle.
48 Ndipo mbingu na dunia na vyote vilivyomo ndani yake vitapiga kelele za shangwe juu ya Babeli, kwa kuwa kutoka kaskazini waharabu watamshambulia,” asema Bwana.
Puis les cieux et la terre, et tout ce qui s'y trouve, chanteront de joie sur Babylone; car les destructeurs lui viendront du nord, dit Yahvé.
49 “Babeli ni lazima aanguke kwa sababu ya kuwaua Waisraeli, kama vile waliouawa duniani kote walivyoanguka kwa sababu ya Babeli.
« Comme Babylone a fait tomber les morts d'Israël, et les morts de tout le pays tomberont à Babylone.
50 Wewe uliyepona upanga, ondoka wala usikawie! Mkumbuke Bwana ukiwa katika nchi ya mbali, na utafakari juu ya Yerusalemu.”
Vous qui avez échappé à l'épée, partez! Ne restez pas immobile! Souvenez-vous de Yahvé de loin, et laisse Jérusalem entrer dans ton esprit. »
51 “Tumetahayari, kwa maana tumetukanwa na aibu imefunika nyuso zetu, kwa sababu wageni wameingia mahali patakatifu pa nyumba ya Bwana.”
« Nous sommes confondus parce que nous avons entendu des reproches. La confusion a recouvert nos visages, car des étrangers sont entrés dans les sanctuaires de la maison de Yahvé. »
52 “Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapoadhibu sanamu zake, na katika nchi yake yote waliojeruhiwa watalia kwa maumivu makali.
« C'est pourquoi voici, les jours viennent, dit Yahvé, « que j'exécuterai le jugement sur ses images gravées; et dans tout son pays, les blessés gémiront.
53 Hata kama Babeli ikifika angani na kuziimarisha ngome zake ndefu, nitatuma waharabu dhidi yake,” asema Bwana.
Quand Babylone s'élèverait jusqu'au ciel, et bien qu'elle doive fortifier l'apogée de sa force, mais des destructeurs lui viendront de ma part, dit Yahvé.
54 “Sauti ya kilio inasikika kutoka Babeli, sauti ya uharibifu mkuu kutoka nchi ya Wakaldayo.
« Le son d'un cri vient de Babylone, et d'une grande destruction du pays des Chaldéens!
55 Bwana ataiangamiza Babeli, atanyamazisha makelele ya kishindo chake. Mawimbi ya adui yatanguruma kama maji makuu, ngurumo ya sauti zao itavuma.
Car Yahvé ravage Babylone, et détruit en elle la grande voix! Leurs vagues grondent comme de nombreuses eaux. Le bruit de leur voix se fait entendre.
56 Mharabu atakuja dhidi ya Babeli, mashujaa wake watakamatwa, nazo pinde zao zitavunjwa. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa kisasi, yeye atalipiza kikamilifu.
Car le destructeur est venu sur elle, même sur Babylone. Ses hommes puissants sont pris. Leurs arcs sont brisés en morceaux, car Yahvé est un Dieu de châtiment. Il vous remboursera sûrement.
57 Nitawafanya maafisa wake na wenye busara walewe, watawala wao, maafisa, pamoja na wapiganaji wao; watalala milele na hawataamka,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Je ferai d'elle des princes, des sages, ses gouverneurs, ses députés, et ses puissants hommes ivres. Ils dormiront d'un sommeil perpétuel, et ne pas se réveiller, » dit le Roi, dont le nom est Yahvé des Armées.
58 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Ukuta mnene wa Babeli utasawazishwa, na malango yaliyoinuka yatateketezwa kwa moto; mataifa yanajichosha bure, taabu ya mataifa ni nishati tu ya miali ya moto.”
Yahvé des Armées dit: « Les larges murs de Babylone seront complètement renversés. Ses hautes portes seront brûlées par le feu. Les peuples travailleront pour la vanité, et les nations pour le feu; et ils seront fatigués. »
59 Huu ndio ujumbe Yeremia aliompa afisa Seraya mwana wa Neria mwana wa Maaseya, alipokwenda Babeli pamoja na Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wake.
Parole de Jérémie, le prophète, à Seraja, fils de Neriah, fils de Mahséja, lorsqu'il partit avec Sédécias, roi de Juda, pour Babylone, la quatrième année de son règne. Or Seraiah était quartier-maître en chef.
60 Yeremia alikuwa ameandika ndani ya kitabu kuhusu maafa yote yatakayoipata Babeli, yaani yote yaliyokuwa yameandikwa kuhusu Babeli.
Jérémie écrivit dans un livre tous les malheurs qui devaient frapper Babylone, et toutes ces paroles qui sont écrites sur Babylone.
61 Yeremia akamwambia Seraya, “Utakapofika Babeli, hakikisha kwamba umesoma maneno haya yote kwa sauti kubwa.
Jérémie dit à Seraïa: « Quand tu arriveras à Babylone, tu liras toutes ces paroles,
62 Kisha sema, ‘Ee Bwana, umesema utaangamiza mahali hapa ili mtu wala mnyama asiishi ndani yake, napo patakuwa ukiwa milele.’
et tu diras: « Yahvé, tu as parlé au sujet de ce lieu, de l'exterminer, afin que personne n'y habite, ni homme ni bête, et qu'il soit à jamais désert.
63 Utakapomaliza kusoma hiki kitabu, kifungie jiwe kisha ukitupe ndani ya Mto Frati.
Lorsque tu auras fini de lire ce livre, tu lieras une pierre et tu la jetteras au milieu de l'Euphrate.
64 Kisha sema, ‘Hivi ndivyo Babeli utakavyozama na usiinuke tena, kwa sababu ya maafa nitakayoleta juu yake. Nao watu wake wataanguka.’” Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.
Et tu diras: « C'est ainsi que Babylone s'enfoncera et ne se relèvera pas, à cause des malheurs que je ferai venir sur elle, et ils seront fatigués. » Ainsi vont les paroles de Jérémie.

< Yeremia 51 >