< Yeremia 51 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama nitaamsha roho ya mwangamizi dhidi ya Babeli na watu wakaao Leb-Kamai.
The Lord seith these thingis, Lo! Y schal reise on Babiloyne, and on the dwelleris therof, that reisiden her herte ayens me, as a wynd of pestilence.
2 Nitawatuma wageni Babeli kumpepeta na kuiharibu nchi yake; watampinga kila upande katika siku ya maafa yake.
And Y schal sende in to Babiloyne wyndeweris, and thei schulen wyndewe it, and thei schulen destrie the lond of it; for thei camen on it on ech side, in the dai of the turment therof.
3 Usimwache mpiga upinde afunge kamba upinde wake, wala usimwache avae silaha zake. Usiwaonee huruma vijana wake; angamiza jeshi lake kabisa.
He that beendith his bowe, beende not, and a man clothid in haburioun, stie not; nyle ye spare the yonge men therof, sle ye al the chyualrie therof.
4 Wataanguka waliouawa katika Babeli, wakiwa na majeraha ya kutisha barabarani zake.
And slayn men schulen falle in the lond of Caldeis, and woundid men in the cuntreis therof.
5 Kwa maana Israeli na Yuda hawajaachwa na Mungu wao, Bwana Mwenye Nguvu Zote, ingawa nchi yao imejaa uovu mbele zake yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
For whi Israel and Juda was not maad widewe fro her God, the Lord of oostis; but the lond of hem was fillid with trespas of the hooli of Israel.
6 “Kimbieni kutoka Babeli! Okoeni maisha yenu! Msiangamizwe kwa sababu ya dhambi zake. Ni wakati wa kisasi cha Bwana, atamlipa kile anachostahili.
Fle ye fro the myddis of Babiloyne, that ech man saue his soule; nyle ye be stille on the wickidnesse therof, for whi tyme of veniaunce therof is to the Lord; he schal yelde while to it.
7 Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu katika mkono wa Bwana; aliufanya ulimwengu wote ulewe. Mataifa walikunywa mvinyo wake; kwa hiyo sasa wameingiwa na wazimu.
Babiloyne is a goldun cuppe in the hond of the Lord, and fillith al erthe; hethene men drunken of the wyn therof, and therfor thei ben mouyd.
8 Babeli ataanguka ghafula na kuvunjika. Mwombolezeni! Tafuteni zeri ya kutuliza maumivu yake, labda anaweza kupona.
Babiloyne felle doun sudenli, and is al to-brokun; yelle ye on it, take ye recyn to the sorewe therof, if perauenture it be heelid.
9 “‘Tungemponya Babeli, lakini hawezi kuponyeka; tumwacheni, na kila mmoja wetu aende nchi yake mwenyewe, kwa kuwa hukumu yake inafika angani, inapanda juu hadi mawinguni.’
We heeliden Babiloyne, and it is not maad hool; forsake we it and go we ech in to his lond; for the doom therof cam `til to heuenes, and is reisid `til to cloudis.
10 “‘Bwana amethibitisha haki yetu; njooni, tutangaze katika Sayuni kitu ambacho Bwana Mungu wetu amefanya.’
The Lord hath brouyt forth oure riytfulnessis; come ye, and telle we in Sion the werk of oure Lord God.
11 “Noeni mishale, chukueni ngao! Bwana amewaamsha wafalme wa Wamedi, kwa sababu nia yake ni kuangamiza Babeli. Bwana atalipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
Scharpe ye arowis, fille ye arowe caasis; the Lord reiside the spirit of the kyngis of Medeis, and his mynde is ayen Babiloyne, that he leese it, for it is the veniaunce of the Lord, the veniaunce of his temple. The kyng of Medeis is reisid of the Lord ayens Babiloyne.
12 Twekeni bendera juu ya kuta za Babeli! Imarisheni ulinzi, wekeni walinzi, andaeni waviziao! Bwana atatimiza kusudi lake, amri yake juu ya watu wa Babeli.
Reise ye a signe on the wallis of Babiloyne, encreesse ye kepyng, reise ye keperis, make ye redi buyschementis; for the Lord thouyte, and dide, what euer thing he spak ayens the dwelleris of Babiloyne.
13 Wewe uishiye kando ya maji mengi na uliye na wingi wa hazina, mwisho wako umekuja, wakati wako wa kukatiliwa mbali.
A! thou Babiloyne, that dwellist on many watris, riche in thi tresours, thin ende cometh, the foote mesure of thi kittyng doun.
14 Bwana Mwenye Nguvu Zote ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: ‘Hakika nitakujaza na watu, kama kundi la nzige, nao watapiga kelele za ushindi juu yako.’
The Lord of oostis swoor bi his soule, that Y schal fille thee with men, as with bruke, and a myry song schal be sungun on thee.
15 “Aliiumba dunia kwa uweza wake; akaweka misingi ya ulimwengu kwa hekima yake na akazitandaza mbingu kwa ufahamu wake.
The Lord swoor, which made erthe bi his strengthe, made redy the world bi his wisdom, and stretchide forth heuenes bi his prudence.
16 Atoapo sauti yake, maji yaliyo katika mbingu hunguruma, huyafanya mawingu yainuke kutoka miisho ya dunia. Hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua, naye huuleta upepo kutoka ghala zake.
Whanne he yyueth vois, watris ben multiplied in heuene; which Lord reisith cloudis fro the laste of erthe, made leitis in to reyn, and brouyt forth wynd of hise tresouris.
17 “Kila mtu ni mjinga na hana maarifa; kila sonara ameaibishwa na sanamu zake. Vinyago vyake ni vya udanganyifu, havina pumzi ndani yavyo.
Ech man is maad a fool of kunnyng, ech wellere togidere is schent in a grauun ymage; for his wellyng togidere is fals, and a spirit is not in tho.
18 Havifai kitu, ni vitu vya kufanyia mzaha, hukumu yavyo itakapowadia, vitaangamia.
The werkis ben veyn, and worthi of scorn; tho schulen perische in the tyme of her visityng.
19 Yeye Aliye Fungu la Yakobo sivyo alivyo, kwani ndiye Muumba wa vitu vyote, pamoja na kabila la urithi wake: Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.
The part of Jacob is not as these thingis; for he that made alle thingis is the part of Jacob, and Israel is the septre of his eritage; the Lord of oostis is his name.
20 “Wewe ndiwe rungu langu la vita, silaha yangu ya vita: kwa wewe navunjavunja mataifa, kwa wewe naangamiza falme,
Thou hurtlist doun to me the instrumentis of batel, and Y schal hurtle doun folkis in thee, and Y schal leese rewmes in thee;
21 kwa wewe navunjavunja farasi na mpanda farasi, kwa wewe navunjavunja gari la vita na mwendeshaji wake,
and Y schal hurtle doun in thee an hors, and the ridere therof; and Y schal hurtle doun in thee a chare, and the stiere therof;
22 kwa wewe napondaponda mwanaume na mwanamke, kwa wewe napondaponda mzee na kijana, kwa wewe napondaponda kijana wa kiume na mwanamwali,
and Y schal hurtle doun in thee a man and womman; and Y schal hurtle doun in thee an elde man and a child; and Y schal hurtle doun in thee a yong man and a virgyn;
23 kwa wewe nampondaponda mchungaji na kundi, kwa wewe nampondaponda mkulima na maksai, kwa wewe nawapondaponda watawala na maafisa.
and Y schal hurtle doun in thee a scheepherde and his floc; and Y schal hurtle doun in thee an erthetiliere and his yok beestis; and Y schal hurtle doun in thee duykis and magistratis.
24 “Mbele ya macho yako nitamlipiza Babeli na wote waishio Ukaldayo kwa ajili ya makosa yote waliyofanya katika Sayuni,” asema Bwana.
And Y schal yelde, seith the Lord, to Babiloyne, and to alle the dwelleris of Caldee, al her yuel, which thei diden in Sion, bifore youre iyen.
25 “Mimi niko kinyume nawe, ee mlima unaoharibu, wewe uangamizaye dunia yote,” asema Bwana. “Nitanyoosha mkono wangu dhidi yako, nikuvingirishe kutoka kwenye kilele cha mwamba, na kukufanya mlima ulioteketezwa kwa moto.
Lo! Y, seith the Lord, to thee, thou hil berynge pestilence, which corrumpist al erthe. Y schal stretche forth myn hond on thee, and Y schal vnwlappe thee fro stoonys, and Y schal yyue thee in to an hil of brennyng.
26 Hakuna jiwe litakalochukuliwa kutoka kwako kwa ajili ya kufanywa jiwe la pembeni, wala jiwe lolote kwa ajili ya msingi, kwa maana utakuwa ukiwa milele,” asema Bwana.
And Y schal not take of thee a stoon in to a corner, and a stoon in to foundementis; but thou schalt be lost with outen ende, seith the Lord.
27 “Twekeni bendera katika nchi! Pigeni tarumbeta katikati ya mataifa! Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake, iteni falme hizi dhidi yake: Ararati, Mini na Ashkenazi. Wekeni jemadari dhidi yake, pelekeni farasi wengi kama kundi la nzige.
Reise ye a signe in the lond, sowne ye with a clarioun in hillis; halewe ye folkis on it, telle ye to the kyngis of Ararath, of Menny, and of Ascheneth ayens it; noumbre ye Tapser ayens it, and bringe ye an hors, as a bruke hauynge a pricke.
28 Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake, wafalme wa Wamedi, watawala wao na maafisa wao wote, pamoja na nchi zote wanazotawala.
Halowe ye folkis ayens it, the kyngis of Medey, the duykis therof, and alle magistratis therof, and al the lond of his power.
29 Nchi inatetemeka na kugaagaa, kwa kuwa makusudi ya Bwana dhidi ya Babeli yanasimama: yaani, kuangamiza nchi ya Babeli ili pasiwe na yeyote atakayeishi humo.
And the erthe schal be mouyd, and schal be disturblid; for the thouyt of the Lord schal fulli wake ayens Babiloyne, that he sette the lond of Babiloyne desert, and vnhabitable.
30 Mashujaa wa Babeli wameacha kupigana, wamebaki katika ngome zao. Nguvu zao zimekwisha, wamekuwa kama wanawake. Makazi yake yameteketezwa kwa moto, makomeo ya malango yake yamevunjika.
The stronge men of Babiloyne ceessiden of batel, thei dwelliden in stronge holdis; the strengthe of hem is deuourid, and thei ben maad as wymmen; the tabernaclis therof ben brent, the barris therof ben al to-brokun.
31 Tarishi mmoja humfuata mwingine, na mjumbe humfuata mjumbe, kumtangazia mfalme wa Babeli kwamba mji wake wote umetekwa,
A rennere schal come ayens a rennere, and a messanger ayens a messanger, to telle to the kyng of Babiloyne, that his citee is takun fro the toon ende `til to the tother ende;
32 Vivuko vya mito vimekamatwa, mabwawa yenye mafunjo yametiwa moto, nao askari wameingiwa na hofu kuu.”
and the forthis ben bifore ocupied, and the mareisis ben brent with fier, and the men werryours ben disturblid.
33 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria wakati inapokanyagwa; wakati wa kumvuna utakuja upesi.”
For the Lord of oostis, God of Israel, seith these thingis, The douyter of Babiloyne is as a corn floor, the tyme of threischyng therof; yit a litil, and the tyme of repyng therof schal come.
34 “Nebukadneza mfalme wa Babeli ametula, ametufanya tuchangayikiwe, ametufanya tuwe gudulia tupu. Kama nyoka ametumeza na kujaza tumbo lake kwa vyakula vyetu vizuri, kisha akatutapika.
Nabugodonosor, the kyng of Babiloyne, eet me, and deuouride me; he made me as a voide vessel, he as a dragoun swolewide me; he fillide his wombe with my tendirnesse, and he castide me out.
35 Jeuri iliyofanyiwa miili yetu na iwe juu ya Babeli,” ndivyo wasemavyo wakaao Sayuni. “Damu yetu na iwe juu ya wale waishio Babeli,” asema Yerusalemu.
Wickidnesse ayens me, and my fleisch on Babiloyne, seith the dwellyng of Sion; and my blood on the dwelleris of Caldee, seith Jerusalem.
36 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo: “Tazama, nitatetea shauri lako na kulipiza kisasi kwa ajili yako; nitaikausha bahari yake na kuzikausha chemchemi zake.
Therfor the Lord seith these thingis, Lo! Y schal deme thi cause, and Y schal venge thi veniaunce; and Y schal make the see therof forsakun, and Y schal make drie the veyne therof.
37 Babeli utakuwa lundo la magofu na makao ya mbweha, kitu cha kutisha na kudharauliwa, mahali asipoishi mtu.
And Babiloyne schal be in to biriels, it schal be the dwellyng of dragouns, wondryng and hissyng, for that no dwellere is.
38 Watu wake wote wananguruma kama simba wadogo, wanakoroma kama wana simba.
Thei schulen rore togidere as liouns, and thei schulen schake lockis, as the whelpis of liouns.
39 Lakini wakati wakiwa wameamshwa, nitawaandalia karamu na kuwafanya walewe, ili wapige kelele kwa kicheko, kisha walale milele na wasiamke,” asema Bwana.
In the heete of hem Y schal sette the drynkis of hem; and Y schal make hem drunkun, that thei be brouyt asleepe, and that thei slepe euerlastynge sleep, and rise not, seith the Lord.
40 “Nitawateremsha kama wana-kondoo waendao machinjoni, kama kondoo dume na mbuzi.
Y schal lede forth hem, as lambren to slayn sacrifice, and as wetheris with kidis. Hou is Sesac takun, and the noble citee of al erthe is takun?
41 “Tazama jinsi Sheshaki atakamatwa, majivuno ya dunia yote yatakavyonyakuliwa. Babeli atakuwa mwenye hofu kiasi gani kati ya mataifa!
Hou is Babiloyne made in to wondre among hethene men?
42 Bahari itainuka juu ya Babeli; mawimbi yake yenye kunguruma yatamfunika.
And the see stiede on Babiloyne, it was hilid with the multitude of hise wawis.
43 Miji yake itakuwa ukiwa, kame na jangwa, nchi ambayo hakuna yeyote anayeishi ndani yake, ambayo hakuna mtu anayepita humo.
The citees therof ben maad in to wondryng, the lond is maad vnhabitable and forsakun; the lond wherynne no man dwellith, and the sone of man schal not passe bi it.
44 Nitamwadhibu Beli katika Babeli, na kumfanya atapike kile alichokimeza. Mataifa hayatamiminika tena kwake. Nao ukuta wa Babeli utaanguka.
And Y schal visite on Bel in to Babiloyne, and Y schal caste out of hise mouth that, that he hadde swolewid, and folkis schulen no more flowe to it; for also the wal of Babiloyne schal falle doun.
45 “Tokeni ndani yake, enyi watu wangu! Okoeni maisha yenu! Ikimbieni hasira kali ya Bwana.
Mi puple, go ye out fro the myddis therof, that ech man saue his soule fro the wraththe of the strong veniaunce of the Lord;
46 Msikate tamaa wala msiogope tetesi zitakaposikika katika nchi; tetesi moja inasikika mwaka huu, nyingine mwaka unaofuata; tetesi juu ya jeuri katika nchi, na ya mtawala dhidi ya mtawala.
and lest perauenture youre herte wexe neische, and lest ye dreden the heryng, that schal be herd in the lond; and heryng schal come in a yeer, and aftir this yeer schal come heryng and wickidnesse in the lond, and a lord on a lord.
47 Kwa kuwa hakika wakati utawadia nitakapoziadhibu sanamu za Babeli; nchi yake yote itatiwa aibu, na watu wake wote waliouawa wataangukia ndani yake.
Therfor lo! daies comen, seith the Lord, and Y schal visite on the grauun ymagis of Babiloyne; and al the lond therof schal be schent, and alle slayn men therof schulen falle doun in the myddis therof.
48 Ndipo mbingu na dunia na vyote vilivyomo ndani yake vitapiga kelele za shangwe juu ya Babeli, kwa kuwa kutoka kaskazini waharabu watamshambulia,” asema Bwana.
And heuenes, and erthis, and alle thingis that ben in tho, schulen herie on Babiloyne; for rauynours schulen come fro the north to it, seith the Lord.
49 “Babeli ni lazima aanguke kwa sababu ya kuwaua Waisraeli, kama vile waliouawa duniani kote walivyoanguka kwa sababu ya Babeli.
And as Babiloyne dide, that slayn men felle doun in Israel, so of Babiloyne slayn men schulen falle doun and in al the lond.
50 Wewe uliyepona upanga, ondoka wala usikawie! Mkumbuke Bwana ukiwa katika nchi ya mbali, na utafakari juu ya Yerusalemu.”
Come ye, that fledden the swerd, nyle ye stonde; haue ye mynde afer on the Lord, and Jerusalem stie on youre herte.
51 “Tumetahayari, kwa maana tumetukanwa na aibu imefunika nyuso zetu, kwa sababu wageni wameingia mahali patakatifu pa nyumba ya Bwana.”
We ben schent, for we herden schenschipe; schame hilide oure faces, for aliens comen on the halewyng of the hous of the Lord.
52 “Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapoadhibu sanamu zake, na katika nchi yake yote waliojeruhiwa watalia kwa maumivu makali.
Therfor lo! daies comen, seith the Lord, and Y schal visite on the grauun ymagis of Babiloyne, and in al the lond therof a woundid man schal loowe.
53 Hata kama Babeli ikifika angani na kuziimarisha ngome zake ndefu, nitatuma waharabu dhidi yake,” asema Bwana.
If Babiloyne stieth in to heuene, and makith stidfast his strengthe an hiy, distrieris therof schulen come on me, seith the Lord.
54 “Sauti ya kilio inasikika kutoka Babeli, sauti ya uharibifu mkuu kutoka nchi ya Wakaldayo.
The vois of a criere of Babiloyne, and greet sorewe of the lond of Caldeis,
55 Bwana ataiangamiza Babeli, atanyamazisha makelele ya kishindo chake. Mawimbi ya adui yatanguruma kama maji makuu, ngurumo ya sauti zao itavuma.
for the Lord distriede Babiloyne, and lost of it a greet vois; and the wawis of hem schulen sowne as many watris. The vois of hem yaf sown,
56 Mharabu atakuja dhidi ya Babeli, mashujaa wake watakamatwa, nazo pinde zao zitavunjwa. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa kisasi, yeye atalipiza kikamilifu.
for a rauenour cam on it, that is, on Babiloyne; and the stronge men therof ben takun, and the bouwe of hem welewide, for the stronge vengere the Lord yeldynge schal yelde.
57 Nitawafanya maafisa wake na wenye busara walewe, watawala wao, maafisa, pamoja na wapiganaji wao; watalala milele na hawataamka,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And Y schal make drunkun the princis therof, and the wise men therof, the duykis therof, and the magistratis therof, and the stronge men therof; and thei schulen slepe euerlastynge sleep, and thei schulen not be awakid, seith the kyng, the Lord of oostis is name of hym.
58 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Ukuta mnene wa Babeli utasawazishwa, na malango yaliyoinuka yatateketezwa kwa moto; mataifa yanajichosha bure, taabu ya mataifa ni nishati tu ya miali ya moto.”
The Lord God of oostis seith these thingis, Thilke brodeste wal of Babiloyne schal be mynyd with mynyng, and the hiye yatis therof schulen be brent with fier; and the trauels of puples schulen be to nouyt, and the trauels of hethene men schulen be in to fier, and schulen perische.
59 Huu ndio ujumbe Yeremia aliompa afisa Seraya mwana wa Neria mwana wa Maaseya, alipokwenda Babeli pamoja na Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wake.
The word which Jeremye, the profete, comaundide to Saraie, sone of Nerie, sone of Maasie, whanne he yede with Sedechie, the kyng, in to Babiloyne, in the fourthe yeer of his rewme; forsothe Saraie was prynce of profesie.
60 Yeremia alikuwa ameandika ndani ya kitabu kuhusu maafa yote yatakayoipata Babeli, yaani yote yaliyokuwa yameandikwa kuhusu Babeli.
And Jeremye wroot al the yuel, that was to comynge on Babiloyne, in a book, alle these wordis that weren writun ayens Babiloyne.
61 Yeremia akamwambia Seraya, “Utakapofika Babeli, hakikisha kwamba umesoma maneno haya yote kwa sauti kubwa.
And Jeremye seide to Saraie, Whanne thou comest in to Babiloyne, and seest, and redist alle these wordis,
62 Kisha sema, ‘Ee Bwana, umesema utaangamiza mahali hapa ili mtu wala mnyama asiishi ndani yake, napo patakuwa ukiwa milele.’
thou schalt seie, Lord, thou spakist ayens this place, that thou schuldist leese it, that noon be that dwelle therynne, fro man `til to beeste, and that it be an euerlastynge wildirnesse.
63 Utakapomaliza kusoma hiki kitabu, kifungie jiwe kisha ukitupe ndani ya Mto Frati.
And whanne thou hast fillid to rede this book, thou schalt bynde to it a stoon, and thou schalt caste it forth in to the myddis of Eufrates; and thou schalt seie,
64 Kisha sema, ‘Hivi ndivyo Babeli utakavyozama na usiinuke tena, kwa sababu ya maafa nitakayoleta juu yake. Nao watu wake wataanguka.’” Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.
So Babiloyne schal be drenchid, and it schal not rise fro the face of turment, which Y brynge on it, and it schal be distried. Hidurto ben the wordis of Jeremye.

< Yeremia 51 >