< Yeremia 51 >
1 Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama nitaamsha roho ya mwangamizi dhidi ya Babeli na watu wakaao Leb-Kamai.
thus to say LORD look! I to rouse upon Babylon and to(wards) to dwell Leb (Leb)-kamai spirit to ruin
2 Nitawatuma wageni Babeli kumpepeta na kuiharibu nchi yake; watampinga kila upande katika siku ya maafa yake.
and to send: depart to/for Babylon be a stranger and to scatter her and to empty [obj] land: country/planet her for to be upon her from around: side in/on/with day distress: harm
3 Usimwache mpiga upinde afunge kamba upinde wake, wala usimwache avae silaha zake. Usiwaonee huruma vijana wake; angamiza jeshi lake kabisa.
not to tread (to tread *Q(K)*) [the] to tread bow his and not to ascend: rise in/on/with armor his and not to spare to(wards) youth her to devote/destroy all army her
4 Wataanguka waliouawa katika Babeli, wakiwa na majeraha ya kutisha barabarani zake.
and to fall: fall slain: killed in/on/with land: country/planet Chaldea and to pierce in/on/with outside her
5 Kwa maana Israeli na Yuda hawajaachwa na Mungu wao, Bwana Mwenye Nguvu Zote, ingawa nchi yao imejaa uovu mbele zake yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
for not forsaken Israel and Judah from God his from LORD Hosts for land: country/planet their to fill guilt (offering) from holy Israel
6 “Kimbieni kutoka Babeli! Okoeni maisha yenu! Msiangamizwe kwa sababu ya dhambi zake. Ni wakati wa kisasi cha Bwana, atamlipa kile anachostahili.
to flee from midst Babylon and to escape man: anyone soul: life his not to silence: destroyed in/on/with iniquity: punishment her for time vengeance he/she/it to/for LORD recompense he/she/it to complete to/for her
7 Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu katika mkono wa Bwana; aliufanya ulimwengu wote ulewe. Mataifa walikunywa mvinyo wake; kwa hiyo sasa wameingiwa na wazimu.
cup gold Babylon in/on/with hand LORD be drunk all [the] land: country/planet from wine her to drink nation upon so to be foolish nation
8 Babeli ataanguka ghafula na kuvunjika. Mwombolezeni! Tafuteni zeri ya kutuliza maumivu yake, labda anaweza kupona.
suddenly to fall: fall Babylon and to break to wail upon her to take: take balsam to/for pain her perhaps to heal
9 “‘Tungemponya Babeli, lakini hawezi kuponyeka; tumwacheni, na kila mmoja wetu aende nchi yake mwenyewe, kwa kuwa hukumu yake inafika angani, inapanda juu hadi mawinguni.’
(to heal *Q(k)*) [obj] Babylon and not to heal to leave: forsake her and to go: went man: anyone to/for land: country/planet his for to touch to(wards) [the] heaven justice: judgement her and to lift: raise till cloud
10 “‘Bwana amethibitisha haki yetu; njooni, tutangaze katika Sayuni kitu ambacho Bwana Mungu wetu amefanya.’
to come out: send LORD [obj] righteousness our to come (in): come and to recount in/on/with Zion [obj] deed: work LORD God our
11 “Noeni mishale, chukueni ngao! Bwana amewaamsha wafalme wa Wamedi, kwa sababu nia yake ni kuangamiza Babeli. Bwana atalipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
to purify [the] arrow to fill [the] shield to rouse LORD [obj] spirit king Mede for upon Babylon plot his to/for to ruin her for vengeance LORD he/she/it vengeance temple his
12 Twekeni bendera juu ya kuta za Babeli! Imarisheni ulinzi, wekeni walinzi, andaeni waviziao! Bwana atatimiza kusudi lake, amri yake juu ya watu wa Babeli.
to(wards) wall Babylon to lift: raise ensign to strengthen: strengthen [the] custody to arise: establish to keep: guard to establish: prepare [the] to ambush for also to plan LORD also to make: do [obj] which to speak: speak to(wards) to dwell Babylon
13 Wewe uishiye kando ya maji mengi na uliye na wingi wa hazina, mwisho wako umekuja, wakati wako wa kukatiliwa mbali.
(to dwell *Q(k)*) upon water many many treasure to come (in): come end your cubit unjust-gain your
14 Bwana Mwenye Nguvu Zote ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: ‘Hakika nitakujaza na watu, kama kundi la nzige, nao watapiga kelele za ushindi juu yako.’
to swear LORD Hosts in/on/with soul: myself his that if: except if: except to fill you man like/as locust and to sing upon you shout
15 “Aliiumba dunia kwa uweza wake; akaweka misingi ya ulimwengu kwa hekima yake na akazitandaza mbingu kwa ufahamu wake.
to make land: country/planet in/on/with strength his to establish: make world in/on/with wisdom his and in/on/with understanding his to stretch heaven
16 Atoapo sauti yake, maji yaliyo katika mbingu hunguruma, huyafanya mawingu yainuke kutoka miisho ya dunia. Hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua, naye huuleta upepo kutoka ghala zake.
to/for voice to give: cry out he crowd water in/on/with heaven and to ascend: rise mist from end land: country/planet lightning to/for rain to make and to come out: send spirit: breath from treasure his
17 “Kila mtu ni mjinga na hana maarifa; kila sonara ameaibishwa na sanamu zake. Vinyago vyake ni vya udanganyifu, havina pumzi ndani yavyo.
be brutish all man from knowledge be ashamed all to refine from idol for deception drink offering his and not spirit: breath in/on/with them
18 Havifai kitu, ni vitu vya kufanyia mzaha, hukumu yavyo itakapowadia, vitaangamia.
vanity they(masc.) deed: work delusion in/on/with time punishment their to perish
19 Yeye Aliye Fungu la Yakobo sivyo alivyo, kwani ndiye Muumba wa vitu vyote, pamoja na kabila la urithi wake: Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.
not like/as these portion Jacob for to form: formed [the] all he/she/it and tribe inheritance his LORD Hosts name his
20 “Wewe ndiwe rungu langu la vita, silaha yangu ya vita: kwa wewe navunjavunja mataifa, kwa wewe naangamiza falme,
war-club you(m. s.) to/for me article/utensil battle and to shatter in/on/with you nation and to ruin in/on/with you kingdom
21 kwa wewe navunjavunja farasi na mpanda farasi, kwa wewe navunjavunja gari la vita na mwendeshaji wake,
and to shatter in/on/with you horse and to ride his and to shatter in/on/with you chariot and to ride his
22 kwa wewe napondaponda mwanaume na mwanamke, kwa wewe napondaponda mzee na kijana, kwa wewe napondaponda kijana wa kiume na mwanamwali,
and to shatter in/on/with you man and woman and to shatter in/on/with you old and youth and to shatter in/on/with you youth and virgin
23 kwa wewe nampondaponda mchungaji na kundi, kwa wewe nampondaponda mkulima na maksai, kwa wewe nawapondaponda watawala na maafisa.
and to shatter in/on/with you to pasture and flock his and to shatter in/on/with you farmer and pair his and to shatter in/on/with you governor and ruler
24 “Mbele ya macho yako nitamlipiza Babeli na wote waishio Ukaldayo kwa ajili ya makosa yote waliyofanya katika Sayuni,” asema Bwana.
and to complete to/for Babylon and to/for all to dwell Chaldea [obj] all distress: evil their which to make: do in/on/with Zion to/for eye your utterance LORD
25 “Mimi niko kinyume nawe, ee mlima unaoharibu, wewe uangamizaye dunia yote,” asema Bwana. “Nitanyoosha mkono wangu dhidi yako, nikuvingirishe kutoka kwenye kilele cha mwamba, na kukufanya mlima ulioteketezwa kwa moto.
look! I to(wards) you mountain: mount [the] destruction utterance LORD [the] to ruin [obj] all [the] land: country/planet and to stretch [obj] hand my upon you and to roll you from [the] crag and to give: make you to/for mountain: mount fire
26 Hakuna jiwe litakalochukuliwa kutoka kwako kwa ajili ya kufanywa jiwe la pembeni, wala jiwe lolote kwa ajili ya msingi, kwa maana utakuwa ukiwa milele,” asema Bwana.
and not to take: take from you stone to/for corner and stone to/for foundation for devastation forever: enduring to be utterance LORD
27 “Twekeni bendera katika nchi! Pigeni tarumbeta katikati ya mataifa! Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake, iteni falme hizi dhidi yake: Ararati, Mini na Ashkenazi. Wekeni jemadari dhidi yake, pelekeni farasi wengi kama kundi la nzige.
to lift: raise ensign in/on/with land: country/planet to blow trumpet in/on/with nation to consecrate: prepare upon her nation to hear: proclaim upon her kingdom Ararat Minni and Ashkenaz to reckon: overseer upon her official to ascend: attack horse like/as locust rough
28 Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake, wafalme wa Wamedi, watawala wao na maafisa wao wote, pamoja na nchi zote wanazotawala.
to consecrate: prepare upon her nation [obj] king Mede [obj] governor her and [obj] all ruler her and [obj] all land: country/planet dominion his
29 Nchi inatetemeka na kugaagaa, kwa kuwa makusudi ya Bwana dhidi ya Babeli yanasimama: yaani, kuangamiza nchi ya Babeli ili pasiwe na yeyote atakayeishi humo.
and to shake [the] land: country/planet and to twist: writh in pain for to arise: establish upon Babylon plot LORD to/for to set: make [obj] land: country/planet Babylon to/for horror: destroyed from nothing to dwell
30 Mashujaa wa Babeli wameacha kupigana, wamebaki katika ngome zao. Nguvu zao zimekwisha, wamekuwa kama wanawake. Makazi yake yameteketezwa kwa moto, makomeo ya malango yake yamevunjika.
to cease mighty man Babylon to/for to fight to dwell in/on/with stronghold be dry might their to be to/for woman to kindle tabernacle her to break bar her
31 Tarishi mmoja humfuata mwingine, na mjumbe humfuata mjumbe, kumtangazia mfalme wa Babeli kwamba mji wake wote umetekwa,
to run: run to/for to encounter: meet to run: run to run: run and to tell to/for to encounter: meet to tell to/for to tell to/for king Babylon for to capture city his from end
32 Vivuko vya mito vimekamatwa, mabwawa yenye mafunjo yametiwa moto, nao askari wameingiwa na hofu kuu.”
and [the] ford to capture and [obj] [the] pool to burn in/on/with fire and human [the] battle to dismay
33 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria wakati inapokanyagwa; wakati wa kumvuna utakuja upesi.”
for thus to say LORD Hosts God Israel daughter Babylon like/as threshing floor time to tread her still little and to come (in): come time [the] harvest to/for her
34 “Nebukadneza mfalme wa Babeli ametula, ametufanya tuchangayikiwe, ametufanya tuwe gudulia tupu. Kama nyoka ametumeza na kujaza tumbo lake kwa vyakula vyetu vizuri, kisha akatutapika.
(to eat me to confuse me *Q(K)*) Nebuchadnezzar king Babylon (to set me *Q(K)*) article/utensil vain (to swallow up me *Q(K)*) like/as serpent: monster to fill belly his from delicacy my (to wash me *Q(K)*)
35 Jeuri iliyofanyiwa miili yetu na iwe juu ya Babeli,” ndivyo wasemavyo wakaao Sayuni. “Damu yetu na iwe juu ya wale waishio Babeli,” asema Yerusalemu.
violence my and flesh my upon Babylon to say to dwell Zion and blood my to(wards) to dwell Chaldea to say Jerusalem
36 Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo: “Tazama, nitatetea shauri lako na kulipiza kisasi kwa ajili yako; nitaikausha bahari yake na kuzikausha chemchemi zake.
to/for so thus to say LORD look! I to contend [obj] strife your and to avenge [obj] vengeance your and to dry [obj] sea her and to wither [obj] fountain her
37 Babeli utakuwa lundo la magofu na makao ya mbweha, kitu cha kutisha na kudharauliwa, mahali asipoishi mtu.
and to be Babylon to/for heap habitation jackal horror: appalled and hissing from nothing to dwell
38 Watu wake wote wananguruma kama simba wadogo, wanakoroma kama wana simba.
together like/as lion to roar to growl like/as whelp lion
39 Lakini wakati wakiwa wameamshwa, nitawaandalia karamu na kuwafanya walewe, ili wapige kelele kwa kicheko, kisha walale milele na wasiamke,” asema Bwana.
in/on/with to warm they to set: make [obj] feast their and be drunk them because to exult and to sleep sleep forever: enduring and not to awake utterance LORD
40 “Nitawateremsha kama wana-kondoo waendao machinjoni, kama kondoo dume na mbuzi.
to go down them like/as ram to/for to slaughter like/as ram with goat
41 “Tazama jinsi Sheshaki atakamatwa, majivuno ya dunia yote yatakavyonyakuliwa. Babeli atakuwa mwenye hofu kiasi gani kati ya mataifa!
how? to capture Babylon and to capture praise all [the] land: country/planet how? to be to/for horror: appalled Babylon in/on/with nation
42 Bahari itainuka juu ya Babeli; mawimbi yake yenye kunguruma yatamfunika.
to ascend: rise upon Babylon [the] sea in/on/with crowd heap: wave his to cover
43 Miji yake itakuwa ukiwa, kame na jangwa, nchi ambayo hakuna yeyote anayeishi ndani yake, ambayo hakuna mtu anayepita humo.
to be city her to/for horror: appalled land: country/planet dryness and plain land: country/planet not to dwell in/on/with them all man and not to pass in/on/with them son: child man
44 Nitamwadhibu Beli katika Babeli, na kumfanya atapike kile alichokimeza. Mataifa hayatamiminika tena kwake. Nao ukuta wa Babeli utaanguka.
and to reckon: punish upon Bel in/on/with Babylon and to come out: send [obj] swallowing his from lip his and not to flow to(wards) him still nation also wall Babylon to fall: fall
45 “Tokeni ndani yake, enyi watu wangu! Okoeni maisha yenu! Ikimbieni hasira kali ya Bwana.
to come out: come from midst her people my and to escape man: anyone [obj] soul: life his from burning anger face: anger LORD
46 Msikate tamaa wala msiogope tetesi zitakaposikika katika nchi; tetesi moja inasikika mwaka huu, nyingine mwaka unaofuata; tetesi juu ya jeuri katika nchi, na ya mtawala dhidi ya mtawala.
and lest be tender heart your and to fear in/on/with tidings [the] to hear: hear in/on/with land: country/planet and to come (in): come in/on/with year [the] tidings and after him in/on/with year [the] tidings and violence in/on/with land: country/planet and to rule upon to rule
47 Kwa kuwa hakika wakati utawadia nitakapoziadhibu sanamu za Babeli; nchi yake yote itatiwa aibu, na watu wake wote waliouawa wataangukia ndani yake.
to/for so behold day to come (in): come and to reckon: punish upon idol Babylon and all land: country/planet her be ashamed and all slain: killed her to fall: kill in/on/with midst her
48 Ndipo mbingu na dunia na vyote vilivyomo ndani yake vitapiga kelele za shangwe juu ya Babeli, kwa kuwa kutoka kaskazini waharabu watamshambulia,” asema Bwana.
and to sing upon Babylon heaven and land: country/planet and all which in/on/with them for from north to come (in): come to/for her [the] to ruin utterance LORD
49 “Babeli ni lazima aanguke kwa sababu ya kuwaua Waisraeli, kama vile waliouawa duniani kote walivyoanguka kwa sababu ya Babeli.
also Babylon to/for to fall: kill slain: killed Israel also to/for Babylon to fall: kill slain: killed all [the] land: country/planet
50 Wewe uliyepona upanga, ondoka wala usikawie! Mkumbuke Bwana ukiwa katika nchi ya mbali, na utafakari juu ya Yerusalemu.”
survivor from sword to go: went not to stand: stand to remember from distant [obj] LORD and Jerusalem to ascend: rise upon heart your
51 “Tumetahayari, kwa maana tumetukanwa na aibu imefunika nyuso zetu, kwa sababu wageni wameingia mahali patakatifu pa nyumba ya Bwana.”
be ashamed for to hear: hear reproach to cover shame face our for to come (in): come be a stranger upon sanctuary house: temple LORD
52 “Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapoadhibu sanamu zake, na katika nchi yake yote waliojeruhiwa watalia kwa maumivu makali.
to/for so behold day to come (in): come utterance LORD and to reckon: punish upon idol her and in/on/with all land: country/planet her to groan slain: wounded
53 Hata kama Babeli ikifika angani na kuziimarisha ngome zake ndefu, nitatuma waharabu dhidi yake,” asema Bwana.
for to ascend: rise Babylon [the] heaven and for to gather/restrain/fortify height strength her from with me to come (in): come to ruin to/for her utterance LORD
54 “Sauti ya kilio inasikika kutoka Babeli, sauti ya uharibifu mkuu kutoka nchi ya Wakaldayo.
voice outcry from Babylon and breaking great: large from land: country/planet Chaldea
55 Bwana ataiangamiza Babeli, atanyamazisha makelele ya kishindo chake. Mawimbi ya adui yatanguruma kama maji makuu, ngurumo ya sauti zao itavuma.
for to ruin LORD [obj] Babylon and to perish from her voice great: large and to roar heap: wave their like/as water many to give: cry out roar voice their
56 Mharabu atakuja dhidi ya Babeli, mashujaa wake watakamatwa, nazo pinde zao zitavunjwa. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa kisasi, yeye atalipiza kikamilifu.
for to come (in): come upon her upon Babylon to ruin and to capture mighty man her to to be dismayed bow their for God recompense LORD to complete to complete
57 Nitawafanya maafisa wake na wenye busara walewe, watawala wao, maafisa, pamoja na wapiganaji wao; watalala milele na hawataamka,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote.
and be drunk ruler her and wise her governor her and ruler her and mighty man her and to sleep sleep forever: enduring and not to awake utterance [the] king LORD Hosts name his
58 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Ukuta mnene wa Babeli utasawazishwa, na malango yaliyoinuka yatateketezwa kwa moto; mataifa yanajichosha bure, taabu ya mataifa ni nishati tu ya miali ya moto.”
thus to say LORD Hosts wall Babylon [the] broad: wide to strip to strip and gate her [the] high in/on/with fire to kindle and be weary/toil people in/on/with sufficiency vain and people in/on/with sufficiency fire and to faint
59 Huu ndio ujumbe Yeremia aliompa afisa Seraya mwana wa Neria mwana wa Maaseya, alipokwenda Babeli pamoja na Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wake.
[the] word which to command Jeremiah [the] prophet [obj] Seraiah son: child Neriah son: child Mahseiah in/on/with to go: went he with Zedekiah king Judah Babylon in/on/with year [the] fourth to/for to reign him and Seraiah ruler resting
60 Yeremia alikuwa ameandika ndani ya kitabu kuhusu maafa yote yatakayoipata Babeli, yaani yote yaliyokuwa yameandikwa kuhusu Babeli.
and to write Jeremiah [obj] all [the] distress: harm which to come (in): come to(wards) Babylon to(wards) scroll: book one [obj] all [the] word [the] these [the] to write to(wards) Babylon
61 Yeremia akamwambia Seraya, “Utakapofika Babeli, hakikisha kwamba umesoma maneno haya yote kwa sauti kubwa.
and to say Jeremiah to(wards) Seraiah like/as to come (in): come you Babylon and to see: see and to call: read out [obj] all [the] word [the] these
62 Kisha sema, ‘Ee Bwana, umesema utaangamiza mahali hapa ili mtu wala mnyama asiishi ndani yake, napo patakuwa ukiwa milele.’
and to say LORD you(m. s.) to speak: speak to(wards) [the] place [the] this to/for to cut: eliminate him to/for lest to be in/on/with him to dwell to/for from man and till animal for devastation forever: enduring to be
63 Utakapomaliza kusoma hiki kitabu, kifungie jiwe kisha ukitupe ndani ya Mto Frati.
and to be like/as to end: finish you to/for to call: read out [obj] [the] scroll: book [the] this to conspire upon him stone and to throw him to(wards) midst Euphrates
64 Kisha sema, ‘Hivi ndivyo Babeli utakavyozama na usiinuke tena, kwa sababu ya maafa nitakayoleta juu yake. Nao watu wake wataanguka.’” Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.
and to say thus to sink Babylon and not to arise: rise from face: because [the] distress: harm which I to come (in): bring upon her and to faint till here/thus word Jeremiah