< Yeremia 50 >

1 Hili ndilo neno alilosema Bwana kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:
این است سخنانی که خداوند علیه سرزمین بابِل و مردم آن به ارمیای نبی فرمود:
2 “Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa, twekeni bendera na mkahubiri; msiache kitu chochote, bali semeni, ‘Babeli utatekwa; Beli ataaibishwa, Merodaki atajazwa na hofu kuu. Sanamu zake zitaaibishwa na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’
«به همۀ دنیا اعلام کنید، پرچم را برافرازید و به همه بگویید که بابِل تسخیر خواهد شد! تمثالها و بتهایش شکسته خواهند شد. خدایانش، بِل و مردوک سرافکنده و رسوا خواهند گردید.
3 Taifa kutoka kaskazini litamshambulia, na kuifanya nchi yake ukiwa. Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake, watu na wanyama wataikimbia.
زیرا قومی از سوی شمال بر بابِل هجوم خواهد آورد و آن را ویران خواهد کرد، و دیگر کسی در آن ساکن نخواهد شد بلکه همه، چه انسان و چه حیوان، از آنجا خواهند گریخت.
4 “Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mungu wao.
«در آن زمان، مردم اسرائیل و یهودا، هر دو گریه‌کنان خواهند آمد و خداوند، خدای خود را خواهند طلبید.
5 Wataiuliza njia iendayo Sayuni na kuelekeza nyuso zao huko. Watakuja na kuambatana na Bwana katika agano la milele ambalo halitasahaulika.
آنها راه اورشلیم را جویا خواهند شد تا به آنجا بازگردند. ایشان با تمام قلب به سوی من باز خواهند گشت و با من عهدی ابدی خواهند بست و آن را هرگز نخواهند شکست.
6 “Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha na kuwasababisha kuzurura juu ya milima. Walitangatanga juu ya mlima na kilima, na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.
«قوم من مانند گوسفندان گمشده می‌باشند؛ چوپانانشان ایشان را گمراه کرده و در میان کوهها آواره نموده‌اند. گوسفندان نیز راه خود را گم کرده‌اند و نمی‌دانند چگونه به آغل بازگردند.
7 Yeyote aliyewakuta aliwala; adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia, kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi, Bwana, aliye tumaini la baba zao.’
دشمنانی که به ایشان برمی‌خورند، ایشان را می‌درند و می‌گویند:”ما اجازه داریم که با ایشان این گونه رفتار کنیم، چون بر ضد خداوند، خدای عادل که امید اجدادشان بود، گناه کرده‌اند.“
8 “Kimbieni kutoka Babeli; ondokeni katika nchi ya Wakaldayo tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.
«ولی حال از بابِل فرار کنید! مانند بزهای نر که پیشاپیش گله می‌روند، قوم مرا به خانه هدایت کنید.
9 Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli muungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini. Watashika nafasi zao dhidi yake, naye kutokea kaskazini atatekwa. Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari, ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.
زیرا من لشکر بزرگی از قومهای نیرومند شمال را برخواهم انگیخت تا بر بابِل هجوم آورند و نابودش کنند؛ تیرهای آنها همگی به هدف خواهند خورد و خطا نخواهند رفت!
10 Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara; wote wamtekao nyara watapata za kutosha,” asema Bwana.
بابِل را غارت خواهند کرد و غنیمت فراوان نصیب غارت‌کنندگان خواهد شد. من، خداوند، این را می‌گویم.»
11 “Kwa sababu hushangilia na kufurahi, wewe utekaye urithi wangu, kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka, na kulia kama farasi dume,
«ای مردم بابِل، ای غارت‌کنندگان قوم من، شما شادید و همچون گاوهای پروار در چراگاههای سبز و خرم می‌چرید و مانند اسبهای نر شیهه می‌زنید و سرمستید!
12 mama yako ataaibika mno, yeye aliyekuzaa atatahayari. Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote, atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.
ولی بدانید که شهر پرآوازهٔ شما نیز تحقیر و رسوا خواهد شد. بابِل سرزمینی خواهد شد بی‌اهمیت، با بیابانهای خشک و متروک.
13 Kwa sababu ya hasira ya Bwana hatakaliwa na mtu, lakini ataachwa ukiwa kabisa. Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
در اثر خشم و غضب من، بابِل متروک و به کلی ویران خواهد شد و هر که از آنجا عبور کند، مبهوت و متحیر خواهد گردید.
14 “Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli, enyi nyote mvutao upinde. Mpigeni! Msibakize mshale wowote, kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya Bwana.
«ای قومهای اطراف، برای جنگ با بابِل آماده شوید! ای تیراندازان، همۀ تیرهایتان را به سوی او رها کنید، چون به من گناه ورزیده است.
15 Piga kelele dhidi yake kila upande! Anajisalimisha, minara yake inaanguka, kuta zake zimebomoka. Kwa kuwa hiki ni kisasi cha Bwana, mlipizeni kisasi; mtendeeni kama alivyowatendea wengine.
از هر سو بر او فریاد جنگ برآورید. بنگرید! تسلیم می‌شود! دیوارهای بابِل فرو می‌ریزد! این انتقام من است! همان بلایی را که بر سر دیگران آورد، بر سر او بیاورید.
16 Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli, pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna. Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu kila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja na akimbilie kwenye nchi yake mwenyewe.
نگذارید برزگرها در آنجا تخم بکارند و دروکنندگان درو نمایند؛ همهٔ غریبانی که در آنجا هستند به سرزمین خود فرار کنند، چون شمشیر دشمن امان نخواهد داد.
17 “Israeli ni kundi lililotawanyika ambalo simba wamelifukuzia mbali. Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru, wa mwisho kuponda mifupa yake alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”
«قوم اسرائیل مانند گوسفندانی هستند که مورد حملهٔ شیران قرار گرفته‌اند. اول پادشاه آشور آنها را درید، سپس نِبوکَدنِصَّر، پادشاه بابِل، استخوانهای ایشان را خرد کرد.
18 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
از این رو من، خداوند لشکرهای آسمان، خدای اسرائیل، پادشاه بابِل و سرزمین او را مجازات خواهم کرد، همان‌طور که پادشاه آشور را مجازات نمودم؛
19 Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe naye atalisha huko Karmeli na Bashani; njaa yake itashibishwa juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.
و قوم اسرائیل را به سرزمین خودشان باز خواهم گرداند تا مانند گوسفندان در چراگاههای کرمل و باشان چرا کنند و بار دیگر در کوههای افرایم و جلعاد شادی نمایند.
20 Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli, lakini halitakuwepo, kwa ajili ya dhambi za Yuda, lakini haitapatikana hata moja, kwa kuwa nitawasamehe mabaki nitakaowaacha.
در آن زمان در اسرائیل و یهودا گناهی پیدا نخواهد شد، چون گناه بازماندگانشان را خواهم آمرزید.
21 “Shambulieni nchi ya Merathaimu na wale waishio huko Pekodi. Wafuatieni, waueni na kuwaangamiza kabisa,” asema Bwana. “Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.
«ای مردان جنگی، بر ضد سرزمین مراتایم و اهالی فقود برخیزید! همچنانکه دستور داده‌ام، همه را بکشید و از بین ببرید.
22 Kelele ya vita iko ndani ya nchi, kelele ya maangamizi makuu!
بگذارید فریاد جنگ و نالهٔ نابودی از آن سرزمین برخیزد!
23 Tazama jinsi nyundo ya dunia yote ilivyovunjika na kuharibika! Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa miongoni mwa mataifa!
بابِل، مانند چکشی تمام جهان را خرد کرد، ولی حال، آن چکش، خود شکسته و خرد شده است. بابِل در میان قومها مطرود و منزوی گردیده است!
24 Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli, nawe ukakamatwa kabla haujafahamu; ulipatikana na ukakamatwa kwa sababu ulimpinga Bwana.
ای بابِل، بدون آنکه بدانی، در دامی که برایت گذاشته بودم گرفتار شده‌ای، چون با من دشمنی نمودی!
25 Bwana amefungua ghala lake la silaha na kuzitoa silaha za ghadhabu yake, kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mwenye Nguvu Zote anayo kazi ya kufanya katika nchi ya Wakaldayo.
«خداوند اسلحه‌خانهٔ خود را گشوده و اسلحهٔ خشم و غضب خود را بیرون آورده است. زیرا خداوند لشکرهای آسمان با مردم بابِل کار دارد.
26 Njooni dhidi yake kutoka mbali. Zifungueni ghala zake za nafaka; mlundikeni kama lundo la nafaka. Mwangamizeni kabisa na msimwachie mabaki yoyote.
از سرزمینهای دور دست به جنگ بابِل بیایید! انبارهای غله‌اش را خالی کنید؛ دیوارهایش را فرو ریزید، خانه‌هایش را ویران سازید؛ همه جا را با خاک یکسان کنید؛ چیزی باقی نگذارید!
27 Waueni mafahali wake wachanga wote; waacheni washuke machinjoni! Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia, wakati wao wa kuadhibiwa.
سربازانش را بکشید، همه را از دم تیغ بگذرانید. وای برحال بابِلی‌ها! زمان نابودی‌شان فرا رسیده است!
28 Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli wakitangaza katika Sayuni jinsi Bwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
«ولی قوم من از بابِل جان به در خواهند برد. ایشان به سرزمین خود باز خواهند گشت تا خبر دهند که من چگونه از کسانی که خانه‌ام را خراب کرده‌اند، انتقام گرفته‌ام.
29 “Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli, wote wale wavutao upinde. Pigeni kambi kumzunguka kabisa, asitoroke mtu yeyote. Mlipizeni kwa matendo yake; mtendeeni kama alivyotenda. Kwa kuwa alimdharau Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
«کمانداران و تیراندازان را جمع کنید تا به بابِل بیایند و شهر را محاصره کنند، طوری که هیچ‌کس نتواند بگریزد. همان بلایی را که بابِل بر سر دیگران آورد، بر سرش بیاورید، چون از روی تکبر، به من، خداوند مقدّس اسرائیل بی‌احترامی کرده است.
30 Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku ile,” asema Bwana.
بنابراین جوانان او در کوچه‌ها افتاده، خواهند مرد و همهٔ مردان جنگی‌اش کشته خواهند شد.»
31 “Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, “kwa kuwa siku yako imewadia, yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.
خداوند لشکرهای آسمان می‌فرماید: «ای قوم مغرور، من بر ضد تو هستم، چون روز مکافاتت رسیده است.
32 Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka, wala hakuna yeyote atakayemuinua; nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”
ای سرزمین متکبر، تو لغزیده، فرو خواهی افتاد و هیچ‌کس تو را بر پا نخواهد کرد. من در شهرهای بابِل آتشی خواهم افروخت که همه چیز را در اطراف خود بسوزاند.»
33 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Watu wa Israeli wameonewa, nao watu wa Yuda pia. Wote waliowateka wamewashikilia sana, wanakataa kuwaachia waende.
خداوند لشکرهای آسمان می‌فرماید: «بر مردم اسرائیل و یهودا ظلم شده است. آنانی که ایشان را اسیر کرده‌اند، سخت مراقبشان هستند و نمی‌گذارند رهایی یابند.
34 Lakini Mkombozi wao ana nguvu; Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake. Atatetea kwa nguvu shauri lao ili alete raha katika nchi yao, lakini ataleta msukosuko kwa wale waishio Babeli.
ولی من که نجا‌ت‌دهندۀ ایشان می‌باشم، نیرومندم و نامم خداوند لشکرهای آسمان می‌باشد و از ایشان حمایت نموده، آرامش و آزادی را به ایشان باز خواهم گرداند. اما اهالی بابِل، هرگز روی آرامش را نخواهند دید!»
35 “Upanga dhidi ya Wakaldayo!” asema Bwana, “dhidi ya wale waishio Babeli na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!
خداوند می‌فرماید: «شمشیر هلاکت بر ساکنان بابِل و بر بزرگان و حکیمانش فرو خواهد آمد.
36 Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo! Watakuwa wapumbavu. Upanga dhidi ya mashujaa wake! Watajazwa na hofu kuu
تمام حکیمان دروغینش، احمق خواهند شد! در دل مردان شجاع جنگی‌اش ترس و هراس خواهد افتاد!
37 Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake! Wao watakuwa kama wanawake. Upanga dhidi ya hazina zake! Hizo zitatekwa nyara.
اسبها و ارابه‌هایش در جنگ از بین خواهند رفت و سربازان مزدورش مانند زنان، از ترس ضعف خواهند کرد. خزانه‌هایش نیز همه غارت خواهند شد؛
38 Ukame juu ya maji yake! Nayo yatakauka. Kwa kuwa ni nchi ya sanamu, wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu.
حتی ذخایر آبش نیز از بین خواهند رفت. چون تمام سرزمین از بتها پر است و مردم دیوانه‌وار به آنها عشق می‌ورزند.
39 “Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo, nao bundi watakaa humo. Kamwe haitakaliwa tena wala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
«از این رو بابِل، لانهٔ شترمرغها و شغالها و مسکن حیوانات وحشی خواهد شد. دیگر هرگز انسانی در آن زندگی نخواهد کرد و برای همیشه ویران خواهد ماند.
40 Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
همان‌گونه که شهرهای سدوم و عموره و آبادی‌های اطراف آنها را از بین بردم، بابِل را نیز ویران خواهم ساخت و دیگر کسی در آنجا زندگی نخواهد کرد.» این است فرمودۀ خداوند.
41 “Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini; taifa kubwa na wafalme wengi wanaamshwa kutoka miisho ya dunia.
«بنگرید! سپاهی بزرگ از طرف شمال می‌آید! پادشاهان بسیار از سرزمینهای مختلف برای جنگ مهیا می‌شوند.
42 Wamejifunga pinde na mikuki; ni wakatili na wasio na huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao; wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Babeli.
آنها سلاحهای خود را برداشته‌اند و برای کشتار آماده‌اند. ایشان سنگدلند و به کسی رحم نمی‌کنند! فریاد آنان مانند خروش دریاست. ای بابِل، ایشان سوار بر اسب، به تاخت به جنگ تو می‌آیند.
43 Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu, nayo mikono yake imelegea. Uchungu umemshika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
«وقتی خبر به پادشاه بابِل برسد، دستهایش سست شده، زانوهایش خواهد لرزید و همچون زنی که درد زایمان داشته باشد، به خود خواهد پیچید.
44 Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule, nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
«همان‌گونه که شیری از جنگلهای اردن بیرون می‌آید و ناگهان به گوسفندان در حال چریدن هجوم می‌آورد، من نیز ناگهان بر بابِلی‌ها هجوم آورده، ایشان را از سرزمینشان بیرون خواهم راند. آنگاه شخص مورد نظر خود را تعیین خواهم نمود تا بر ایشان حکومت کند. زیرا کیست که مثل من باشد و کیست که بتواند از من بازخواست کند؟ کدام رهبر است که با من مخالفت نماید؟
45 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Babeli, kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali. Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
بنابراین، ارادهٔ من دربارهٔ بابِل و مردم آن این است که دشمن، آنها و حتی کودکانشان را به زور ببرد، و همه چیزشان را نابود کند.
46 Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka; kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.
از صدای شکست بابِل، زمین خواهد لرزید و قومها فریاد مردم آن را خواهند شنید.»

< Yeremia 50 >