< Yeremia 50 >
1 Hili ndilo neno alilosema Bwana kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:
Inilah pesan TUHAN kepadaku tentang kota Babel dan penduduknya,
2 “Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa, twekeni bendera na mkahubiri; msiache kitu chochote, bali semeni, ‘Babeli utatekwa; Beli ataaibishwa, Merodaki atajazwa na hofu kuu. Sanamu zake zitaaibishwa na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’
"Pasanglah tanda dan umumkan kepada bangsa-bangsa bahwa Babel telah jatuh! Jangan rahasiakan hal itu! Merodakh dewanya telah dihancurkan, dan patung-patungnya yang cabul pecah berantakan, serta berhala-berhalanya sangat dihinakan.
3 Taifa kutoka kaskazini litamshambulia, na kuifanya nchi yake ukiwa. Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake, watu na wanyama wataikimbia.
Suatu bangsa dari utara akan datang menyerang Babel dan membuat negeri itu menjadi padang tandus. Manusia dan binatang akan lari, dan tak ada lagi yang mau tinggal di sana."
4 “Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mungu wao.
TUHAN berkata, "Pada waktu itu orang Israel dan Yehuda akan datang bersama-sama dengan menangis, mencari Aku, Allah mereka.
5 Wataiuliza njia iendayo Sayuni na kuelekeza nyuso zao huko. Watakuja na kuambatana na Bwana katika agano la milele ambalo halitasahaulika.
Mereka akan menanyakan jalan ke Sion, lalu berjalan ke jurusan itu. Mereka akan membuat perjanjian abadi dengan Aku, dan akan tetap memegangnya.
6 “Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha na kuwasababisha kuzurura juu ya milima. Walitangatanga juu ya mlima na kilima, na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.
Umat-Ku ibarat domba yang telah dibiarkan tersesat di pegunungan oleh gembala-gembalanya. Mereka mengembara dari satu gunung ke gunung yang lain dan tidak tahu lagi di mana rumah mereka.
7 Yeyote aliyewakuta aliwala; adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia, kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi, Bwana, aliye tumaini la baba zao.’
Mereka diserang dan disiksa oleh semua yang bertemu dengan mereka. Musuh-musuh umat-Ku berkata, 'Apa yang kita lakukan, tidak salah, sebab orang-orang itu telah berdosa kepada TUHAN. Leluhur mereka percaya kepada TUHAN, jadi seharusnya mereka pun tetap setia kepada-Nya.'
8 “Kimbieni kutoka Babeli; ondokeni katika nchi ya Wakaldayo tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.
Hai umat Israel, larilah dari Babel! Kamulah yang mula-mula harus pergi, supaya yang lain menyusul.
9 Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli muungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini. Watashika nafasi zao dhidi yake, naye kutokea kaskazini atatekwa. Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari, ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.
Aku akan mengerahkan sejumlah bangsa yang kuat-kuat dari utara supaya mereka menyerang Babel. Mereka akan mengatur barisan untuk bertempur melawan Babel dan mengalahkannya. Mereka adalah pemanah-pemanah ahli yang panahnya tak pernah meleset.
10 Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara; wote wamtekao nyara watapata za kutosha,” asema Bwana.
Babel akan dirampasi, dan perampasnya akan mengambil segalanya dengan sesuka hati. Aku, TUHAN, telah berbicara."
11 “Kwa sababu hushangilia na kufurahi, wewe utekaye urithi wangu, kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka, na kulia kama farasi dume,
TUHAN berkata, "Hai orang Babel, kamu merampok umat-Ku. Kamu melompat-lompat gembira seperti kuda yang meringkik, dan seperti sapi yang sedang merumput.
12 mama yako ataaibika mno, yeye aliyekuzaa atatahayari. Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote, atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.
Tetapi kamu akan menjadi bangsa yang paling tak berarti di antara segala bangsa. Kotamu sendiri yang besar itu akan dihina dan dipermalukan. Negerimu akan menjadi padang gurun yang tandus dan kering.
13 Kwa sababu ya hasira ya Bwana hatakaliwa na mtu, lakini ataachwa ukiwa kabisa. Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
Karena Aku marah, maka Babel akan menjadi reruntuhan dan tak berpenghuni. Semua yang lewat di situ akan terkejut dan ngeri.
14 “Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli, enyi nyote mvutao upinde. Mpigeni! Msibakize mshale wowote, kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya Bwana.
Hai kamu pemanah-pemanah! Aturlah barisanmu untuk mengepung dan menyerang Babel. Bidikkan semua anak panahmu ke arah Babel, karena ia telah berdosa kepada-Ku.
15 Piga kelele dhidi yake kila upande! Anajisalimisha, minara yake inaanguka, kuta zake zimebomoka. Kwa kuwa hiki ni kisasi cha Bwana, mlipizeni kisasi; mtendeeni kama alivyowatendea wengine.
Teriakkanlah pekik pertempuran di sekeliling kota itu! Sekarang Babel sudah menyerah. Tembok-temboknya telah didobrak dan diruntuhkan. Aku sedang melaksanakan pembalasan terhadap Babel. Sebab itu perlakukanlah mereka seperti mereka memperlakukan orang-orang lain.
16 Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli, pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna. Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu kila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja na akimbilie kwenye nchi yake mwenyewe.
Jangan biarkan orang bercocok tanam atau menuai di negeri itu. Semua orang asing yang tinggal di situ akan pulang ke negerinya, karena mereka takut kepada tentara yang menyerang."
17 “Israeli ni kundi lililotawanyika ambalo simba wamelifukuzia mbali. Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru, wa mwisho kuponda mifupa yake alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”
TUHAN berkata, "Orang Israel seperti kawanan domba yang dikejar dan diceraiberaikan oleh singa. Mula-mula mereka diserang oleh raja Asyur, lalu Nebukadnezar raja Babel menggerogoti tulang-tulang mereka.
18 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
Karena itu, Aku, TUHAN Yang Mahakuasa, Allah Israel, akan menghukum Raja Nebukadnezar dan negerinya sama seperti Kuhukum raja Asyur.
19 Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe naye atalisha huko Karmeli na Bashani; njaa yake itashibishwa juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.
Aku akan mengembalikan orang Israel ke negeri mereka. Mereka akan makan dari hasil tanah Gunung Karmel dan daerah Basan. Mereka akan dikenyangkan oleh hasil tanah daerah Efraim dan Gilead.
20 Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli, lakini halitakuwepo, kwa ajili ya dhambi za Yuda, lakini haitapatikana hata moja, kwa kuwa nitawasamehe mabaki nitakaowaacha.
Pada waktu itu Israel dan Yehuda akan bersih dari dosa, karena Aku akan mengampuni orang-orang yang telah Kuselamatkan. Aku, TUHAN telah berbicara."
21 “Shambulieni nchi ya Merathaimu na wale waishio huko Pekodi. Wafuatieni, waueni na kuwaangamiza kabisa,” asema Bwana. “Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.
TUHAN berkata kepada suatu bangsa dari utara, "Seranglah penduduk Merataim dan Pekod. Bunuh dan binasakan mereka. Laksanakanlah perintah-Ku. Aku, TUHAN telah berbicara."
22 Kelele ya vita iko ndani ya nchi, kelele ya maangamizi makuu!
Bunyi pertempuran bergemuruh di negeri, dan terjadilah kehancuran besar.
23 Tazama jinsi nyundo ya dunia yote ilivyovunjika na kuharibika! Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa miongoni mwa mataifa!
Seluruh dunia dipalu oleh Babel sampai hancur, tapi sekarang palu itu sendiri telah patah! Segala bangsa terkejut mendengar apa yang telah terjadi dengan negeri itu.
24 Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli, nawe ukakamatwa kabla haujafahamu; ulipatikana na ukakamatwa kwa sababu ulimpinga Bwana.
TUHAN berkata, "Babel, engkau melawan Aku, sebab itu kau terjebak di dalam jerat yang Kupasang untukmu, tetapi kau tidak menyadarinya.
25 Bwana amefungua ghala lake la silaha na kuzitoa silaha za ghadhabu yake, kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mwenye Nguvu Zote anayo kazi ya kufanya katika nchi ya Wakaldayo.
Gudang senjata-Ku telah Kubuka, dan dengan marah Kukeluarkan senjata-senjata itu, karena Aku TUHAN Yang Mahatinggi dan Mahakuasa harus melakukan suatu tugas di Babel.
26 Njooni dhidi yake kutoka mbali. Zifungueni ghala zake za nafaka; mlundikeni kama lundo la nafaka. Mwangamizeni kabisa na msimwachie mabaki yoyote.
Seranglah Babel dari segala jurusan, dan dobraklah gudang-gudang gandumnya! Tumpuklah barang-barang rampasan seperti kamu menumpuk gandum! Musnahkan negeri itu! Jangan ada yang disisakan!
27 Waueni mafahali wake wachanga wote; waacheni washuke machinjoni! Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia, wakati wao wa kuadhibiwa.
Bunuhlah semua tentaranya! Tewaskan mereka! Celakalah bangsa Babel! Sudah tiba waktunya mereka dihukum!"
28 Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli wakitangaza katika Sayuni jinsi Bwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
(Orang-orang yang lari ke Yerusalem dari Babel menceritakan bagaimana TUHAN Allah kita membalas perbuatan orang Babel terhadap Rumah TUHAN.)
29 “Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli, wote wale wavutao upinde. Pigeni kambi kumzunguka kabisa, asitoroke mtu yeyote. Mlipizeni kwa matendo yake; mtendeeni kama alivyotenda. Kwa kuwa alimdharau Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
TUHAN berkata, "Suruhlah para pemanah menyerang Babel. Kerahkanlah setiap orang yang pandai memanah. Kepunglah kota itu dan jangan biarkan seorang pun lolos. Balaslah semua perbuatannya dan perlakukanlah dia setimpal dengan kelakuannya, sebab ia telah bertindak kurang ajar terhadap Aku, Yang Mahasuci, Allah Israel.
30 Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku ile,” asema Bwana.
Pada hari itu pemuda-pemudanya akan tewas di jalan-jalan kotanya, dan seluruh tentaranya dihancurkan. Aku, TUHAN, telah berbicara.
31 “Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, “kwa kuwa siku yako imewadia, yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.
Babel, engkau terlalu tinggi hati! Karena itu Aku, TUHAN Yang Mahatinggi, Allah Yang Mahakuasa, melawan engkau. Sudah waktunya engkau Kuhukum.
32 Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka, wala hakuna yeyote atakayemuinua; nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”
Bangsamu yang tinggi hati itu akan tersandung dan jatuh. Tak seorang pun akan menolong engkau untuk bangkit. Kota-kotamu akan Kubakar, dan segala yang di sekitarnya akan dimusnahkan."
33 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Watu wa Israeli wameonewa, nao watu wa Yuda pia. Wote waliowateka wamewashikilia sana, wanakataa kuwaachia waende.
TUHAN Yang Mahakuasa berkata, "Orang Israel dan orang Yehuda tertekan. Semua yang menawan mereka menjaga mereka ketat-ketat dan tak mau melepaskan mereka.
34 Lakini Mkombozi wao ana nguvu; Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake. Atatetea kwa nguvu shauri lao ili alete raha katika nchi yao, lakini ataleta msukosuko kwa wale waishio Babeli.
Tetapi Aku penyelamat mereka itu kuat, nama-Ku TUHAN Yang Mahakuasa. Aku sendirilah yang akan memperjuangkan perkara mereka dan membawa damai ke atas bumi. Tetapi ke atas orang Babel akan Kudatangkan kerusuhan dan ketakutan."
35 “Upanga dhidi ya Wakaldayo!” asema Bwana, “dhidi ya wale waishio Babeli na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!
TUHAN berkata, "Binasalah Babel bersama rakyat dan pejabat pemerintah serta kaum cerdik pandai mereka!
36 Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo! Watakuwa wapumbavu. Upanga dhidi ya mashujaa wake! Watajazwa na hofu kuu
Binasalah nabi-nabi Babel! Mereka pendusta dan dungu. Binasalah tentara Babel yang perkasa! Betapa takutnya mereka!
37 Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake! Wao watakuwa kama wanawake. Upanga dhidi ya hazina zake! Hizo zitatekwa nyara.
Hancurkan kuda dan kereta perangnya! Binasalah prajurit-prajurit sewaannya! Betapa lemahnya mereka! Musnahkan kekayaan Babel! Jarahilah harta bendanya!
38 Ukame juu ya maji yake! Nayo yatakauka. Kwa kuwa ni nchi ya sanamu, wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu.
Keringkanlah segala sungai dan ladangnya! Sebab, Babel penuh dengan berhala-berhala yang mengerikan, yang membuat para pemujanya menjadi gila.
39 “Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo, nao bundi watakaa humo. Kamwe haitakaliwa tena wala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
Karena itu Babel akan menjadi tempat jin-jin dan roh-roh jahat serta burung-burung unta. Untuk selama-lamanya tidak akan ada orang yang mau tinggal lagi di sana.
40 Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
Sebagaimana Aku memusnahkan Sodom dan Gomora bersama desa-desa di sekitarnya, begitu juga Aku akan memusnahkan Babel. Tak seorang pun akan tinggal lagi di sana. Aku, TUHAN, telah berbicara.
41 “Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini; taifa kubwa na wafalme wengi wanaamshwa kutoka miisho ya dunia.
Suatu bangsa yang kuat sedang bergerak dari negeri yang jauh di utara. Mereka datang bersama banyak raja untuk berperang.
42 Wamejifunga pinde na mikuki; ni wakatili na wasio na huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao; wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Babeli.
Mereka bersenjatakan panah dan tombak; mereka bengis dan tak kenal ampun. Seperti bunyi laut bergelora begitulah suara derap kuda mereka yang sedang dipacu untuk maju menyerang Babel.
43 Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu, nayo mikono yake imelegea. Uchungu umemshika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Mendengar berita itu, raja Babel menjadi tak berdaya. Ia dicekam perasaan takut, dan menderita seperti wanita yang mau melahirkan.
44 Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule, nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
Seperti singa muncul dari hutan lebat dekat Sungai Yordan dan mendatangi padang tempat domba merumput, demikianlah Aku, TUHAN, akan datang dan membuat orang Babel lari dari kota mereka dengan tiba-tiba. Lalu Aku akan memilih seorang pemimpin untuk memerintah bangsa itu. Siapakah dapat disamakan dengan Aku? Siapakah berani membuat perkara dengan Aku? Apakah ada pemimpin yang dapat melawan Aku?
45 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Babeli, kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali. Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
Karena itu, dengarkanlah apa yang telah Kurencanakan terhadap kota Babel, dan apa yang hendak Kulakukan terhadap penduduknya. Anak-anak mereka pun akan diseret pergi, dan semua orang akan ketakutan.
46 Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka; kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.
Apabila Babel jatuh, akan terdengar keributan yang begitu hebat sehingga seluruh dunia goncang; teriakan-teriakan penduduknya akan terdengar oleh bangsa-bangsa lain."