< Yeremia 50 >

1 Hili ndilo neno alilosema Bwana kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:
Parole que le Seigneur dit sur Babylone et sur les Chaldéens par l’entremise de Jérémie, le prophète.
2 “Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa, twekeni bendera na mkahubiri; msiache kitu chochote, bali semeni, ‘Babeli utatekwa; Beli ataaibishwa, Merodaki atajazwa na hofu kuu. Sanamu zake zitaaibishwa na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’
Annoncez parmi les nations, et faites-le entendre; levez l’étendard, publiez, ne cachez point, dites: Babylone est prise. Bel est couvert de confusion, Mérodach est vaincu; ses images taillées au ciseau sont couvertes de confusion, leurs idoles sont vaincues.
3 Taifa kutoka kaskazini litamshambulia, na kuifanya nchi yake ukiwa. Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake, watu na wanyama wataikimbia.
Parce qu’une nation est montée contre elle venant de l’aquilon, laquelle réduira sa terre en solitude; et il n’y aura personne qui habitera en elle depuis l’homme jusqu’à la bête; et ils ont été troublés, et ils s’en sont allés.
4 “Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mungu wao.
En ces jours-là, et en ce temps-là, dit le Seigneur, viendront les fils d’Israël et les fils de Juda, et marchant ensemble, et pleurant, ils se hâteront et ils chercheront le Seigneur leur Dieu.
5 Wataiuliza njia iendayo Sayuni na kuelekeza nyuso zao huko. Watakuja na kuambatana na Bwana katika agano la milele ambalo halitasahaulika.
Ils demanderont le chemin de Sion; vers elle se tourneront leurs faces. Ils viendront et s’uniront au Seigneur par une alliance éternelle qui ne sera nullement effacée par l’oubli.
6 “Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha na kuwasababisha kuzurura juu ya milima. Walitangatanga juu ya mlima na kilima, na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.
Mon peuple est devenu un troupeau perdu; leurs pasteurs les ont séduits et les ont fait errer dans les montagnes; ils sont passés d’une montagne en une colline; ils ont oublié le lieu de leur repos.
7 Yeyote aliyewakuta aliwala; adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia, kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi, Bwana, aliye tumaini la baba zao.’
Tous ceux qui les ont trouvés les ont dévorés; et leurs ennemis ont dit: Nous n’avons pas péché; parce qu’ils ont péché contre le Seigneur, la splendeur de la justice, contre le Seigneur, l’attente de leurs pères.
8 “Kimbieni kutoka Babeli; ondokeni katika nchi ya Wakaldayo tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.
Retirez-vous du milieu de Babylone, et sortez de la terre des Chaldéens; soyez comme des béliers devant un troupeau.
9 Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli muungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini. Watashika nafasi zao dhidi yake, naye kutokea kaskazini atatekwa. Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari, ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.
Parce que voilà que moi je suscite et que j’amènerai contre Babylone une assemblée de grandes nations de la terre de l’Aquilon; et elles se prépareront contre elle; et de là elle sera prise; sa flèche, comme celle d’un homme fort qui tue, ne retournera pas vide.
10 Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara; wote wamtekao nyara watapata za kutosha,” asema Bwana.
Et la Chaldée sera en proie: tous ses dévasteurs seront remplis de dépouilles, dit le Seigneur.
11 “Kwa sababu hushangilia na kufurahi, wewe utekaye urithi wangu, kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka, na kulia kama farasi dume,
Parce que vous exultez et dites de grandes choses en pillant mon héritage; parce que vous vous êtes répandus comme des veaux sur l’herbe et que vous avez mugi comme des taureaux.
12 mama yako ataaibika mno, yeye aliyekuzaa atatahayari. Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote, atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.
Votre mère a été couverte de confusion extrêmement, et elle a été égalée à la poussière, celle qui vous a engendrés; voilà qu’elle sera la dernière parmi les nations, déserte, sans chemin frayé, et aride.
13 Kwa sababu ya hasira ya Bwana hatakaliwa na mtu, lakini ataachwa ukiwa kabisa. Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
À cause de la colère du Seigneur, elle ne sera pas habitée, mais elle sera tout entière réduite en une solitude; quiconque passera par Babylone, sera frappé de stupeur et sifflera sur toutes ses plaies.
14 “Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli, enyi nyote mvutao upinde. Mpigeni! Msibakize mshale wowote, kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya Bwana.
Préparez-vous contre Babylone de tous côtes, vous tous qui tendez l’arc; combattez-la, n’épargnez point les flèches, parce que c’est contre le Seigneur qu’elle a péché.
15 Piga kelele dhidi yake kila upande! Anajisalimisha, minara yake inaanguka, kuta zake zimebomoka. Kwa kuwa hiki ni kisasi cha Bwana, mlipizeni kisasi; mtendeeni kama alivyowatendea wengine.
Criez contre elle; partout elle a donné la main; ses fondements sont tombés, ses murs sont détruits, parce que c’est la vengeance du Seigneur, prenez vengeance d’elle; comme elle a fait, faites-lui.
16 Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli, pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna. Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu kila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja na akimbilie kwenye nchi yake mwenyewe.
Exterminez de Babylone le semeur, et celui qui tient la faucille au temps de la moisson; à la force du glaive de la colombe chacun vers son peuple retournera, et les uns après les autres dans leur terre s’enfuiront.
17 “Israeli ni kundi lililotawanyika ambalo simba wamelifukuzia mbali. Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru, wa mwisho kuponda mifupa yake alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”
C’est un troupeau dispersé qu’Israël; des lions l’ont chassé; le premier qui l’a mangé est le roi d’Assur; celui-ci, le dernier, lui a brisé les os, Nabuchodonosor, roi de Babylone.
18 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur des armées, le Dieu d’Israël: Voilà que moi je visiterai le roi de Babylone, et sa terre, comme j’ai visité le roi d’Assur;
19 Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe naye atalisha huko Karmeli na Bashani; njaa yake itashibishwa juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.
Et je ramènerai Israël dans sa demeure, il paîtra sur le Carmel et en Basan, et sur la montagne d’Ephraïm et de Galaad son âme se rassasiera.
20 Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli, lakini halitakuwepo, kwa ajili ya dhambi za Yuda, lakini haitapatikana hata moja, kwa kuwa nitawasamehe mabaki nitakaowaacha.
En ces jours-là, et en ce temps-là, dit le Seigneur, on cherchera l’iniquité d’Israël et elle ne sera pas; le péché de Juda et il ne sera pas trouvé; parce que je serai propice à ceux que j’aurai laissés.
21 “Shambulieni nchi ya Merathaimu na wale waishio huko Pekodi. Wafuatieni, waueni na kuwaangamiza kabisa,” asema Bwana. “Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.
Monte sur la terre des dominateurs, et visite ses habitants; dissipe et tue ce qui est derrière eux, dit le Seigneur; et fais tout selon que je t’ai ordonné.
22 Kelele ya vita iko ndani ya nchi, kelele ya maangamizi makuu!
Voix de guerre sur la terre et grande destruction.
23 Tazama jinsi nyundo ya dunia yote ilivyovunjika na kuharibika! Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa miongoni mwa mataifa!
Comment a-t-il été rompu et brisé, le marteau de toute la terre? Comment Babylone a-t-elle été changée en un désert parmi les nations?
24 Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli, nawe ukakamatwa kabla haujafahamu; ulipatikana na ukakamatwa kwa sababu ulimpinga Bwana.
Je t’ai enlacée, et tu as été prise, Babylone, et tu ne le savais pas; tu as été trouvée et saisie, parce que c’est le Seigneur que tu as provoqué.
25 Bwana amefungua ghala lake la silaha na kuzitoa silaha za ghadhabu yake, kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mwenye Nguvu Zote anayo kazi ya kufanya katika nchi ya Wakaldayo.
Le Seigneur a ouvert son trésor et il en a tiré les instruments de sa colère, parce que le Seigneur, Dieu des armées, en a besoin dans la terre des Chaldéens.
26 Njooni dhidi yake kutoka mbali. Zifungueni ghala zake za nafaka; mlundikeni kama lundo la nafaka. Mwangamizeni kabisa na msimwachie mabaki yoyote.
Venez vers elle des confins les plus éloignés; ouvrez, afin que sortent ceux qui doivent la fouler aux pieds; ôtez de la voie les pierres, et mettez-les en monceaux, et tuez-la et qu’il n’y ait rien de reste.
27 Waueni mafahali wake wachanga wote; waacheni washuke machinjoni! Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia, wakati wao wa kuadhibiwa.
Dissipez tous ses braves, qu’ils descendent à la tuerie; malheur à eux, parce qu’est venu leur jour, le temps de leur visite.
28 Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli wakitangaza katika Sayuni jinsi Bwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
Voix de ceux qui fuient, de ceux qui sont échappés de la terre de Babylone, afin qu’ils annoncent à Sion la vengeance du Seigneur, notre Dieu, la vengeance de son temple.
29 “Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli, wote wale wavutao upinde. Pigeni kambi kumzunguka kabisa, asitoroke mtu yeyote. Mlipizeni kwa matendo yake; mtendeeni kama alivyotenda. Kwa kuwa alimdharau Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Annoncez à tous ceux qui tendent l’arc en si grand nombre de marcher contre Babylone; tenez-vous contre elle tout au autour, et que personne n’échappe; rendez-lui selon son œuvre; selon tout ce qu’elle a fait, faites-lui, parce que c’est contre le Seigneur qu’elle s’est élevée, contre le saint d’Israël.
30 Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku ile,” asema Bwana.
C’est pour cela que ses jeunes hommes tomberont sur ses places et que tous ses hommes de guerre se tairont en ce jour-là, dit le Seigneur.
31 “Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, “kwa kuwa siku yako imewadia, yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.
Voilà que moi-même je viens à toi, superbe, dit le Seigneur, Dieu des armées, parce qu’est venu ton jour, le jour de ta visite.
32 Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka, wala hakuna yeyote atakayemuinua; nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”
Et il tombera, le superbe, et il sera renversé, et il n’y aura personne qui le relèvera; et j’allumerai un feu dans ses villes; et il dévorera tout ce qui est autour de lui.
33 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Watu wa Israeli wameonewa, nao watu wa Yuda pia. Wote waliowateka wamewashikilia sana, wanakataa kuwaachia waende.
Voici ce que dit le Seigneur des armées: Les fils d’Israël et les fils de Juda souffrent ensemble l’oppression: tous ceux qui les ont pris les retiennent, et ne veulent pas les laisser aller.
34 Lakini Mkombozi wao ana nguvu; Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake. Atatetea kwa nguvu shauri lao ili alete raha katika nchi yao, lakini ataleta msukosuko kwa wale waishio Babeli.
Leur rédempteur est fort; son nom est le Seigneur des armées; en jugement il défendra leur cause, afin d’épouvanter la terre et d’agiter les habitants de Babylone.
35 “Upanga dhidi ya Wakaldayo!” asema Bwana, “dhidi ya wale waishio Babeli na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!
Glaive sur les Chaldéens, dit le Seigneur, sur les habitants de Babylone, sur ses princes et ses sages.
36 Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo! Watakuwa wapumbavu. Upanga dhidi ya mashujaa wake! Watajazwa na hofu kuu
Glaive sur ses devins qui seront insensés; glaive sur ses braves qui seront dans l’effroi.
37 Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake! Wao watakuwa kama wanawake. Upanga dhidi ya hazina zake! Hizo zitatekwa nyara.
Glaive sur ses chevaux et sur ses chars, et sur tout le peuple qui est au milieu d’elle; et ils seront comme des femmes; glaive sur ses trésors qui seront pillés.
38 Ukame juu ya maji yake! Nayo yatakauka. Kwa kuwa ni nchi ya sanamu, wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu.
La sécheresse sera sur ses eaux, et elles tariront; parce que c’est la terre des images taillées au ciseau, et ils se glorifient dans des monstres.
39 “Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo, nao bundi watakaa humo. Kamwe haitakaliwa tena wala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
À cause de cela, les dragons y habiteront avec les faunes qui recherchent les figues; et les autruches habiteront en elle; et elle ne sera plus habitée à jamais, elle ne sera pas reconstruite dans la suite des générations.
40 Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
Ainsi que le Seigneur a renversé Sodome et Gomorrhe, et ses voisines, dit le Seigneur; un homme n’y habitera pas, et le fils d’un homme n’y séjournera pas.
41 “Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini; taifa kubwa na wafalme wengi wanaamshwa kutoka miisho ya dunia.
Voilà qu’un peuple vient de l’Aquilon, et une grande nation, et un grand nombre de rois s’élèveront des confins de la terre.
42 Wamejifunga pinde na mikuki; ni wakatili na wasio na huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao; wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Babeli.
Ils saisiront l’arc et le bouclier; ils sont cruels et impitoyables; leur voix comme la mer retentira; et sur leurs chevaux ils monteront comme un homme prêt au combat contre toi, fille de Babylone.
43 Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu, nayo mikono yake imelegea. Uchungu umemshika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Le roi de Babylone a appris la nouvelle de leur dessein, et ses mains ont défailli; l’angoisse l’a saisi, et la douleur, comme une femme en travail.
44 Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule, nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
Voilà que comme un lion il montera de l’orgueil du Jourdain vers une beauté puissante; parce que soudain je le ferai courir vers elle; et quel est l’élu que je préposerai sur elle? car qui est semblable à moi? qui tiendra contre moi? et quel est le pasteur qui résistera à mon visage?
45 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Babeli, kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali. Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
À cause de cela, écoutez le dessein que le Seigneur a conçu en son esprit contre Babylone, et les pensées qu’il a méditées contre la terre des Chaldéens; il a dit: Je jure si les petits troupeaux, ne les enlèveront pas; et si leur habitation ne sera pas détruite avec eux.
46 Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka; kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.
À la voix de la captivité de Babylone, la terre a été agitée, et une clameur parmi les nations a été entendue.

< Yeremia 50 >