< Yeremia 50 >
1 Hili ndilo neno alilosema Bwana kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:
La parole que l’Éternel dit sur Babylone, sur le pays des Chaldéens, par Jérémie le prophète:
2 “Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa, twekeni bendera na mkahubiri; msiache kitu chochote, bali semeni, ‘Babeli utatekwa; Beli ataaibishwa, Merodaki atajazwa na hofu kuu. Sanamu zake zitaaibishwa na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’
Annoncez parmi les nations, et faites-le entendre, et élevez l’étendard; faites-le entendre, ne le cachez pas; dites: Babylone est prise, Bel est honteux; Merodac est brisé; ses idoles sont honteuses, ses images sont brisées.
3 Taifa kutoka kaskazini litamshambulia, na kuifanya nchi yake ukiwa. Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake, watu na wanyama wataikimbia.
Car une nation est montée du nord contre elle; elle a mis en désolation son pays, et il n’y aura plus là d’habitant: tant les hommes que les bêtes se sont enfuis, ils s’en sont allés.
4 “Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mungu wao.
En ces jours-là et en ce temps-là, dit l’Éternel, les fils d’Israël viendront, eux et les fils de Juda ensemble; ils iront, marchant et pleurant, et ils chercheront l’Éternel leur Dieu.
5 Wataiuliza njia iendayo Sayuni na kuelekeza nyuso zao huko. Watakuja na kuambatana na Bwana katika agano la milele ambalo halitasahaulika.
Ils s’enquerront de Sion; vers elle leur face [sera tournée]: Venez, attachons-nous à l’Éternel par une alliance éternelle qui ne sera pas oubliée.
6 “Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha na kuwasababisha kuzurura juu ya milima. Walitangatanga juu ya mlima na kilima, na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.
Mon peuple est un troupeau perdu; leurs pasteurs les ont fait errer, les égarant sur les montagnes; ils sont allés de montagne en colline, ils ont oublié leur gîte.
7 Yeyote aliyewakuta aliwala; adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia, kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi, Bwana, aliye tumaini la baba zao.’
Tous ceux qui les ont trouvés les ont dévorés; et leurs ennemis disent: Nous ne sommes pas coupables, parce qu’ils ont péché contre l’Éternel, contre la demeure de la justice, contre l’Éternel, l’attente de leurs pères.
8 “Kimbieni kutoka Babeli; ondokeni katika nchi ya Wakaldayo tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.
Fuyez du milieu de Babylone, et sortez du pays des Chaldéens, et soyez comme les boucs [qui vont] devant le troupeau.
9 Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli muungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini. Watashika nafasi zao dhidi yake, naye kutokea kaskazini atatekwa. Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari, ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.
Car voici, du pays du nord je réveillerai et je ferai monter contre Babylone un rassemblement de grandes nations qui se rangeront contre elle: de là elle sera prise. Leurs flèches sont comme celles d’un habile homme fort; pas une ne reviendra à vide.
10 Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara; wote wamtekao nyara watapata za kutosha,” asema Bwana.
Et la Chaldée sera un butin; tous ceux qui la pilleront seront rassasiés, dit l’Éternel;
11 “Kwa sababu hushangilia na kufurahi, wewe utekaye urithi wangu, kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka, na kulia kama farasi dume,
parce que vous vous êtes réjouis, parce que vous vous êtes égayés, vous qui avez pillé mon héritage, parce que vous avez bondi comme une génisse qui foule le blé, et que vous avez henni comme de puissants chevaux.
12 mama yako ataaibika mno, yeye aliyekuzaa atatahayari. Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote, atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.
Votre mère est fort honteuse, celle qui vous enfanta est couverte d’opprobre: voici, [elle est] la dernière des nations, un désert, un pays stérile et une solitude!
13 Kwa sababu ya hasira ya Bwana hatakaliwa na mtu, lakini ataachwa ukiwa kabisa. Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
À cause du courroux de l’Éternel elle ne sera pas habitée, elle sera tout entière une désolation; quiconque passera près de Babylone sera étonné et sifflera à cause de toutes ses plaies.
14 “Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli, enyi nyote mvutao upinde. Mpigeni! Msibakize mshale wowote, kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya Bwana.
Rangez-vous en bataille contre Babylone, tout alentour, vous tous qui bandez l’arc; tirez contre elle, n’épargnez pas les flèches, car elle a péché contre l’Éternel.
15 Piga kelele dhidi yake kila upande! Anajisalimisha, minara yake inaanguka, kuta zake zimebomoka. Kwa kuwa hiki ni kisasi cha Bwana, mlipizeni kisasi; mtendeeni kama alivyowatendea wengine.
Poussez des cris contre elle tout alentour! Elle s’est rendue, ses remparts sont tombés, ses murailles sont renversées, car c’est ici la vengeance de l’Éternel. Vengez-vous sur elle, faites-lui comme elle a fait!
16 Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli, pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna. Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu kila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja na akimbilie kwenye nchi yake mwenyewe.
Retranchez de Babylone celui qui sème, et celui qui tient la faucille au temps de la moisson. À cause de l’épée qui ravage, qu’ils s’en retournent chacun vers son peuple, et qu’ils fuient chacun vers son pays.
17 “Israeli ni kundi lililotawanyika ambalo simba wamelifukuzia mbali. Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru, wa mwisho kuponda mifupa yake alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”
Israël est une brebis chassée çà et là; les lions l’ont pourchassée. Le roi d’Assyrie, le premier, l’a dévorée; et celui-ci, le dernier, Nebucadretsar, roi de Babylone, lui a brisé les os.
18 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
C’est pourquoi, ainsi dit l’Éternel des armées, le Dieu d’Israël: Voici, je visite le roi de Babylone et son pays, comme j’ai visité le roi d’Assyrie;
19 Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe naye atalisha huko Karmeli na Bashani; njaa yake itashibishwa juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.
et je ferai revenir Israël à ses pâturages; et il paîtra sur le Carmel et en Basan, et son âme sera rassasiée dans la montagne d’Éphraïm et en Galaad.
20 Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli, lakini halitakuwepo, kwa ajili ya dhambi za Yuda, lakini haitapatikana hata moja, kwa kuwa nitawasamehe mabaki nitakaowaacha.
En ces jours-là et en ce temps-là, dit l’Éternel, on cherchera l’iniquité d’Israël, et il n’y en aura point, et les péchés de Juda, et ils ne seront pas trouvés; car je pardonnerai à ceux que j’aurai fait demeurer de reste.
21 “Shambulieni nchi ya Merathaimu na wale waishio huko Pekodi. Wafuatieni, waueni na kuwaangamiza kabisa,” asema Bwana. “Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.
Monte contre le pays doublement rebelle, contre lui et contre les habitants destinés à la visitation; dévaste et détruis entièrement derrière eux, dit l’Éternel, et fais selon tout ce que je t’ai commandé.
22 Kelele ya vita iko ndani ya nchi, kelele ya maangamizi makuu!
Le cri de guerre est dans le pays, et une grande ruine.
23 Tazama jinsi nyundo ya dunia yote ilivyovunjika na kuharibika! Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa miongoni mwa mataifa!
Comment est mis en pièces et brisé le marteau de toute la terre! Comment Babylone est-elle réduite en désolation parmi les nations!
24 Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli, nawe ukakamatwa kabla haujafahamu; ulipatikana na ukakamatwa kwa sababu ulimpinga Bwana.
Je t’ai tendu un piège, et aussi tu es prise, Babylone! et tu ne le savais pas; tu as été trouvée, et tu as aussi été saisie, parce que tu as combattu contre l’Éternel.
25 Bwana amefungua ghala lake la silaha na kuzitoa silaha za ghadhabu yake, kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mwenye Nguvu Zote anayo kazi ya kufanya katika nchi ya Wakaldayo.
L’Éternel a ouvert son trésor, et il en a fait sortir les armes de son indignation; car c’est ici l’œuvre du Seigneur, l’Éternel des armées, dans le pays des Chaldéens.
26 Njooni dhidi yake kutoka mbali. Zifungueni ghala zake za nafaka; mlundikeni kama lundo la nafaka. Mwangamizeni kabisa na msimwachie mabaki yoyote.
Venez contre elle de toute part; ouvrez ses granges, entassez-la comme des gerbes et détruisez-la entièrement; qu’elle n’ait rien de reste!
27 Waueni mafahali wake wachanga wote; waacheni washuke machinjoni! Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia, wakati wao wa kuadhibiwa.
Tuez tous ses taureaux; qu’ils descendent à la tuerie. Malheur à eux! car leur jour est venu, le temps de leur visitation.
28 Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli wakitangaza katika Sayuni jinsi Bwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
La voix de ceux qui fuient, qui sont réchappés du pays de Babylone, pour annoncer dans Sion la vengeance de l’Éternel, notre Dieu, la vengeance de son temple!
29 “Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli, wote wale wavutao upinde. Pigeni kambi kumzunguka kabisa, asitoroke mtu yeyote. Mlipizeni kwa matendo yake; mtendeeni kama alivyotenda. Kwa kuwa alimdharau Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Convoquez des archers contre Babylone, tous ceux qui bandent l’arc! Campez contre elle tout alentour, qu’elle n’ait pas de réchappés; rendez-lui selon son œuvre, faites-lui selon tout ce qu’elle a fait; car elle a été fière contre l’Éternel, contre le Saint d’Israël.
30 Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku ile,” asema Bwana.
C’est pourquoi ses jeunes gens tomberont dans ses places et tous ses hommes de guerre seront détruits en ce jour-là, dit l’Éternel.
31 “Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, “kwa kuwa siku yako imewadia, yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.
Voici, [j’en veux] à toi, orgueilleuse, dit le Seigneur, l’Éternel des armées; car ton jour est venu, le temps où je te visite.
32 Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka, wala hakuna yeyote atakayemuinua; nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”
Et l’orgueilleuse a bronché et est tombée, et il n’y a personne qui la relève; et j’allumerai dans ses villes un feu qui dévorera tous ses alentours.
33 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Watu wa Israeli wameonewa, nao watu wa Yuda pia. Wote waliowateka wamewashikilia sana, wanakataa kuwaachia waende.
Ainsi dit l’Éternel des armées: Les fils d’Israël et les fils de Juda ont été ensemble opprimés; et tous ceux qui les emmenèrent captifs les ont retenus, ils ont refusé de les laisser aller.
34 Lakini Mkombozi wao ana nguvu; Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake. Atatetea kwa nguvu shauri lao ili alete raha katika nchi yao, lakini ataleta msukosuko kwa wale waishio Babeli.
Leur rédempteur est fort. Son nom est l’Éternel des armées; il prendra certainement en main leur cause, afin de donner du repos au pays et de troubler les habitants de Babylone.
35 “Upanga dhidi ya Wakaldayo!” asema Bwana, “dhidi ya wale waishio Babeli na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!
L’épée est sur les Chaldéens, dit l’Éternel, et sur les habitants de Babylone, et sur ses princes, et sur ses sages;
36 Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo! Watakuwa wapumbavu. Upanga dhidi ya mashujaa wake! Watajazwa na hofu kuu
l’épée est sur les menteurs, et ils deviendront insensés; l’épée est sur ses hommes forts, et ils seront terrifiés;
37 Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake! Wao watakuwa kama wanawake. Upanga dhidi ya hazina zake! Hizo zitatekwa nyara.
l’épée est sur ses chevaux, et sur ses chars, et sur tout le peuple mélangé qui est au milieu d’elle, et ils seront comme des femmes; l’épée est sur ses trésors, et ils seront pillés;
38 Ukame juu ya maji yake! Nayo yatakauka. Kwa kuwa ni nchi ya sanamu, wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu.
la sécheresse est sur ses eaux, et elles tarissent; car c’est un pays d’images taillées, et ils sont fous de leurs affreuses idoles.
39 “Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo, nao bundi watakaa humo. Kamwe haitakaliwa tena wala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
C’est pourquoi les bêtes du désert, avec des chacals, y habiteront, et il y habitera des autruches; et elle ne sera plus jamais habitée, et on n’y demeurera plus, de génération en génération.
40 Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
Comme dans la subversion que Dieu a faite de Sodome et de Gomorrhe et des villes voisines, dit l’Éternel, personne n’y habitera et aucun fils d’homme n’y séjournera.
41 “Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini; taifa kubwa na wafalme wengi wanaamshwa kutoka miisho ya dunia.
Voici, un peuple vient du nord, et une grande nation et beaucoup de rois se réveillent des extrémités de la terre.
42 Wamejifunga pinde na mikuki; ni wakatili na wasio na huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao; wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Babeli.
Ils saisissent l’arc et le javelot; ils sont cruels, et ils n’ont pas de compassion; leur voix bruit comme la mer, et ils sont montés sur des chevaux, préparés comme un homme pour la guerre, contre toi, fille de Babylone.
43 Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu, nayo mikono yake imelegea. Uchungu umemshika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Le roi de Babylone en a entendu la rumeur, et ses mains sont devenues lâches; la détresse l’a saisi, l’angoisse comme celle d’une femme qui enfante.
44 Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule, nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
Voici, comme un lion il monte de la crue du Jourdain contre la demeure forte; car je les en chasserai précipitamment. Et qui est l’homme choisi, que je préposerai sur elle? Car qui est comme moi, et qui m’assignera le temps, et qui sera le pasteur qui se tiendra devant moi?
45 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Babeli, kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali. Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
C’est pourquoi, écoutez le conseil de l’Éternel, qu’il a formé contre Babylone, et les pensées qu’il a pensées contre le pays des Chaldéens: Si les petits du troupeau ne les entraînent! S’il ne rend désolée pour eux [leur] habitation!…
46 Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka; kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.
Au bruit de la prise de Babylone la terre est ébranlée, et il y a un cri, entendu parmi les nations.