< Yeremia 50 >
1 Hili ndilo neno alilosema Bwana kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:
La parole que Yahvé a prononcée sur Babylone, sur le pays des Chaldéens, par Jérémie, le prophète.
2 “Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa, twekeni bendera na mkahubiri; msiache kitu chochote, bali semeni, ‘Babeli utatekwa; Beli ataaibishwa, Merodaki atajazwa na hofu kuu. Sanamu zake zitaaibishwa na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’
« Déclarez parmi les nations et publiez, et établir une norme; publier, et ne pas dissimuler; disent: « Babylone a été prise, Bel est déçu, Merodach est consterné! Ses images sont déçues. Ses idoles sont consternées.
3 Taifa kutoka kaskazini litamshambulia, na kuifanya nchi yake ukiwa. Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake, watu na wanyama wataikimbia.
Car une nation monte du nord contre elle, qui rendra sa terre désolée, et personne n'y habitera. Ils ont fui. Ils sont partis, l'homme et l'animal.
4 “Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mungu wao.
« En ces jours-là, et en ce temps-là, » dit Yahvé, « les enfants d'Israël viendront, eux et les enfants de Juda ensemble; ils poursuivront leur chemin en pleurant, et chercheront Yahvé leur Dieu.
5 Wataiuliza njia iendayo Sayuni na kuelekeza nyuso zao huko. Watakuja na kuambatana na Bwana katika agano la milele ambalo halitasahaulika.
Ils s'informeront sur Sion, le visage tourné vers elle, en disant: « Venez, joignez-vous à Yahvé par une alliance éternelle ». qui ne sera pas oublié.
6 “Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha na kuwasababisha kuzurura juu ya milima. Walitangatanga juu ya mlima na kilima, na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.
Mon peuple est une brebis égarée. Leurs bergers les ont fait s'égarer. Ils les ont repoussés sur les montagnes. Ils sont passés de montagne en colline. Ils ont oublié leur lieu de repos.
7 Yeyote aliyewakuta aliwala; adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia, kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi, Bwana, aliye tumaini la baba zao.’
Tous ceux qui les ont trouvés les ont dévorés. Leurs adversaires ont dit: « Nous ne sommes pas coupables, parce qu'ils ont péché contre Yahvé, la demeure de la justice, Yahvé, l'espoir de leurs pères.
8 “Kimbieni kutoka Babeli; ondokeni katika nchi ya Wakaldayo tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.
« Fuyez du milieu de Babylone! Sortez du pays des Chaldéens, et être comme les boucs devant les troupeaux.
9 Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli muungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini. Watashika nafasi zao dhidi yake, naye kutokea kaskazini atatekwa. Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari, ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.
Car voici que je vais susciter et fais monter contre Babylone une troupe de grandes nations du pays du nord; et ils se rangent en bataille contre elle. Elle sera prise à partir de là. Leurs flèches seront comme celles d'un homme puissant et expert. Aucun d'entre eux ne reviendra en vain.
10 Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara; wote wamtekao nyara watapata za kutosha,” asema Bwana.
La Chaldée sera une proie. Tous ceux qui s'en prennent à elle seront satisfaits », dit Yahvé.
11 “Kwa sababu hushangilia na kufurahi, wewe utekaye urithi wangu, kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka, na kulia kama farasi dume,
« Parce que vous êtes heureux, parce que vous vous réjouissez, O vous qui pillez mon héritage, car tu es dévergondée comme une génisse qui foule le grain, et hennir comme des chevaux forts,
12 mama yako ataaibika mno, yeye aliyekuzaa atatahayari. Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote, atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.
votre mère sera totalement déçue. Celle qui t'a porté sera confondue. Voici qu'elle sera la plus petite des nations, un désert, une terre aride, et un désert.
13 Kwa sababu ya hasira ya Bwana hatakaliwa na mtu, lakini ataachwa ukiwa kabisa. Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
A cause de la colère de Yahvé, elle ne sera pas habitée, mais elle sera totalement désolée. Tous ceux qui passeront par Babylone seront étonnés, et siffler sur tous ses fléaux.
14 “Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli, enyi nyote mvutao upinde. Mpigeni! Msibakize mshale wowote, kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya Bwana.
Mettez-vous en ordre de bataille contre Babylone tout autour, vous tous qui courbez l'arc; lui tirer dessus. N'épargnez aucune flèche, car elle a péché contre Yahvé.
15 Piga kelele dhidi yake kila upande! Anajisalimisha, minara yake inaanguka, kuta zake zimebomoka. Kwa kuwa hiki ni kisasi cha Bwana, mlipizeni kisasi; mtendeeni kama alivyowatendea wengine.
Criez contre elle tout autour. Elle s'est soumise. Ses remparts sont tombés. Ses murs ont été abattus, car c'est la vengeance de Yahvé. Se venger d'elle. Comme elle l'a fait, faites-lui.
16 Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli, pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna. Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu kila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja na akimbilie kwenye nchi yake mwenyewe.
Coupez le semeur de Babylone, et celui qui manie la faucille au moment de la moisson. Par peur de l'épée oppressante, ils retourneront chacun à leur propre peuple, et ils fuiront chacun dans leur pays.
17 “Israeli ni kundi lililotawanyika ambalo simba wamelifukuzia mbali. Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru, wa mwisho kuponda mifupa yake alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”
« Israël est une brebis traquée. Les lions l'ont chassé. D'abord, le roi d'Assyrie l'a dévoré, et enfin, Nebuchadnezzar, roi de Babylone, a brisé ses os. »
18 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
C'est pourquoi Yahvé des armées, le Dieu d'Israël, dit: « Voici, je vais punir le roi de Babylone et son pays, comme j'ai puni le roi d'Assyrie.
19 Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe naye atalisha huko Karmeli na Bashani; njaa yake itashibishwa juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.
Je ramènerai Israël dans son pâturage, et il se nourrira de Carmel et de Bashan. Son âme sera satisfaite sur les collines d'Ephraïm et en Galaad.
20 Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli, lakini halitakuwepo, kwa ajili ya dhambi za Yuda, lakini haitapatikana hata moja, kwa kuwa nitawasamehe mabaki nitakaowaacha.
En ces jours-là, et en ce temps-là, dit Yahvé, « l'iniquité d'Israël sera recherchée, et il n'y en aura pas, aussi les péchés de Juda, et ils ne seront pas trouvés; car je pardonnerai à ceux que j'ai laissés comme restes.
21 “Shambulieni nchi ya Merathaimu na wale waishio huko Pekodi. Wafuatieni, waueni na kuwaangamiza kabisa,” asema Bwana. “Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.
« Monte contre le pays de Merathaim, même contre elle, et contre les habitants de Pekod. Tuez et détruisez tout après eux, dit Yahvé, « et faites tout ce que je vous ai ordonné.
22 Kelele ya vita iko ndani ya nchi, kelele ya maangamizi makuu!
Un bruit de bataille retentit dans le pays, et de grande destruction.
23 Tazama jinsi nyundo ya dunia yote ilivyovunjika na kuharibika! Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa miongoni mwa mataifa!
Comme le marteau de toute la terre est écarté et brisé! Comme Babylone est devenue une désolation parmi les nations!
24 Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli, nawe ukakamatwa kabla haujafahamu; ulipatikana na ukakamatwa kwa sababu ulimpinga Bwana.
Je vous ai tendu un piège, et vous êtes aussi pris, Babylone, et vous n'étiez pas au courant. Vous êtes trouvé, et aussi pris, parce que vous avez combattu contre Yahvé.
25 Bwana amefungua ghala lake la silaha na kuzitoa silaha za ghadhabu yake, kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mwenye Nguvu Zote anayo kazi ya kufanya katika nchi ya Wakaldayo.
Yahvé a ouvert son arsenal, et a sorti les armes de son indignation; car le Seigneur, Yahvé des Armées, a une œuvre à accomplir dans le pays des Chaldéens.
26 Njooni dhidi yake kutoka mbali. Zifungueni ghala zake za nafaka; mlundikeni kama lundo la nafaka. Mwangamizeni kabisa na msimwachie mabaki yoyote.
Venez contre elle depuis la frontière la plus éloignée. Ouvrez ses entrepôts. Jetez-la en tas. Détruisez-la complètement. Qu'il ne reste rien d'elle.
27 Waueni mafahali wake wachanga wote; waacheni washuke machinjoni! Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia, wakati wao wa kuadhibiwa.
Tuez tous ses taureaux. Laissez-les aller à l'abattoir. Malheur à eux! Car leur jour est venu, le moment de leur visite.
28 Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli wakitangaza katika Sayuni jinsi Bwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
Écoutez ceux qui fuient et s'échappent du pays de Babylone, pour annoncer dans Sion la vengeance de Yahvé notre Dieu, la vengeance de son temple.
29 “Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli, wote wale wavutao upinde. Pigeni kambi kumzunguka kabisa, asitoroke mtu yeyote. Mlipizeni kwa matendo yake; mtendeeni kama alivyotenda. Kwa kuwa alimdharau Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
« Convoquez les archers contre Babylone, tous ceux qui tendent l'arc. Encampement contre elle tout autour. Que rien ne s'échappe. Remboursez-la en fonction de son travail. Selon tout ce qu'elle a fait, faites-lui; car elle s'est enflammée contre Yahvé, contre le Saint d'Israël.
30 Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku ile,” asema Bwana.
C'est pourquoi ses jeunes gens tomberont dans ses rues. Tous ses hommes de guerre seront réduits au silence en ce jour-là, dit Yahvé.
31 “Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, “kwa kuwa siku yako imewadia, yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.
« Voici, j'en veux à toi, orgueilleux, dit le Seigneur, Yahvé des armées; « car ton jour est venu, le moment où je vous rendrai visite.
32 Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka, wala hakuna yeyote atakayemuinua; nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”
L'orgueilleux trébuche et tombe, et personne ne le relèvera. Je vais allumer un feu dans ses villes, et il dévorera tous ceux qui sont autour de lui. »
33 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Watu wa Israeli wameonewa, nao watu wa Yuda pia. Wote waliowateka wamewashikilia sana, wanakataa kuwaachia waende.
Yahvé des armées dit: « Les enfants d'Israël et les enfants de Juda sont opprimés ensemble. Tous ceux qui les ont fait prisonniers les retiennent. Ils refusent de les laisser partir.
34 Lakini Mkombozi wao ana nguvu; Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake. Atatetea kwa nguvu shauri lao ili alete raha katika nchi yao, lakini ataleta msukosuko kwa wale waishio Babeli.
Leur rédempteur est fort. Yahvé des Armées est son nom. Il va plaider leur cause de manière approfondie, pour qu'il donne du repos à la terre, et de troubler les habitants de Babylone.
35 “Upanga dhidi ya Wakaldayo!” asema Bwana, “dhidi ya wale waishio Babeli na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!
« L'épée est sur les Chaldéens, dit Yahvé, « et sur les habitants de Babylone, sur ses princes, et sur ses sages.
36 Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo! Watakuwa wapumbavu. Upanga dhidi ya mashujaa wake! Watajazwa na hofu kuu
L'épée est sur les vantards, et ils deviendront des imbéciles. Une épée est sur ses hommes puissants, et ils seront consternés.
37 Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake! Wao watakuwa kama wanawake. Upanga dhidi ya hazina zake! Hizo zitatekwa nyara.
L'épée est sur leurs chevaux, sur leurs chars, et sur toutes les personnes mixtes qui se trouvent au milieu d'elle; et ils deviendront comme des femmes. Une épée est sur ses trésors, et ils seront volés.
38 Ukame juu ya maji yake! Nayo yatakauka. Kwa kuwa ni nchi ya sanamu, wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu.
La sécheresse est sur ses eaux, et ils seront desséchés; car c'est un pays d'images gravées, et ils sont fous des idoles.
39 “Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo, nao bundi watakaa humo. Kamwe haitakaliwa tena wala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
C'est pourquoi les animaux sauvages du désert avec les loups y habiteront. Les autruches y habiteront. Elle ne sera plus habitée à jamais, Elle ne sera pas non plus vécue de génération en génération.
40 Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
Comme lorsque Dieu a renversé Sodome, Gomorrhe et ses villes voisines, dit Yahvé, « pour que personne n'y habite, aucun fils de l'homme n'y vivra.
41 “Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini; taifa kubwa na wafalme wengi wanaamshwa kutoka miisho ya dunia.
« Voici qu'un peuple vient du nord. Une grande nation et de nombreux rois seront suscités des extrémités de la terre.
42 Wamejifunga pinde na mikuki; ni wakatili na wasio na huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao; wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Babeli.
Ils prennent l'arc et la lance. Ils sont cruels, et n'ont aucune pitié. Leur voix gronde comme la mer. Ils montent à cheval, tout le monde dans le tableau, comme un homme à la bataille, contre toi, fille de Babylone.
43 Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu, nayo mikono yake imelegea. Uchungu umemshika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Le roi de Babylone a entendu parler d'eux, et ses mains deviennent faibles. Anguish s'est emparé de lui, des douleurs comme celles d'une femme en travail.
44 Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule, nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
Voici que l'ennemi surgit comme un lion. des fourrés du Jourdain contre la forte habitation; car je les ferai fuir soudainement. Celui qui sera choisi, Je le nommerai à ce poste, car qui est comme moi? Qui me fixera une heure? Qui est le berger qui peut se tenir devant moi? »
45 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Babeli, kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali. Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
C'est pourquoi, écoutez le conseil de Yahvé qu'il a pris contre Babylone; et ses objectifs qu'il s'est proposé contre le pays des Chaldéens: Ils vont sûrement les traîner loin, même les petits du troupeau. Il fera de leur habitation une désolation.
46 Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka; kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.
La terre tremble au bruit de la prise de Babylone. Le cri est entendu parmi les nations.