< Yeremia 50 >

1 Hili ndilo neno alilosema Bwana kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:
Yahweh gave to [me, ] Jeremiah the prophet, a message about Babylon [city] and the country of Babylonia.
2 “Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa, twekeni bendera na mkahubiri; msiache kitu chochote, bali semeni, ‘Babeli utatekwa; Beli ataaibishwa, Merodaki atajazwa na hofu kuu. Sanamu zake zitaaibishwa na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’
[This is what Yahweh says]: “Proclaim [DOU] [a message] among the nations; do not withhold any of it; raise up a signal flag to announce that Babylon will be captured. [Its chief god] Marduk, [whose other name is] Bel, will be completely disgraced, and all the [other] statues and idols will be shattered.
3 Taifa kutoka kaskazini litamshambulia, na kuifanya nchi yake ukiwa. Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake, watu na wanyama wataikimbia.
[The army of] a nation will come from the north to attack Babylon and destroy the city very thoroughly, [with the result that] no one will live there [again]. Both people and animals will run away.”
4 “Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mungu wao.
“But [I, ] Yahweh, say that in the future, when that is about to happen, the people of Israel and the people of Judah will join together. They will be weeping and wanting [to worship] me, their God.
5 Wataiuliza njia iendayo Sayuni na kuelekeza nyuso zao huko. Watakuja na kuambatana na Bwana katika agano la milele ambalo halitasahaulika.
They will inquire about the road to Jerusalem, [and then] they will start traveling [IDM] toward it. They will say [to each other], ‘We must return to Yahweh [again]!’ They will make an everlasting agreement with me that they will never forget.
6 “Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha na kuwasababisha kuzurura juu ya milima. Walitangatanga juu ya mlima na kilima, na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.
My people have been [like] [MET] lost sheep. Their [leaders/rulers] have caused them [to abandon me] like [MET] shepherds who have allowed their sheep to wander in the hills and mountains. [My people are like] [MET] sheep that do not know the path to return to the sheepfold.
7 Yeyote aliyewakuta aliwala; adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia, kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi, Bwana, aliye tumaini la baba zao.’
All their enemies who found them attacked them. They said, ‘We did not sin [by attacking them], because they sinned against Yahweh; he is the one who provides what they need; he is the one to whom they should have remained faithful; he is the one whom their ancestors confidently expected [to help them].’
8 “Kimbieni kutoka Babeli; ondokeni katika nchi ya Wakaldayo tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.
[But now, I say to the leaders of my people], ‘Flee from Babylon! Leave the land of Babylonia! Be like [SIM] male goats [that go] in front of [the rest of] the flock; [lead my people back to their own land].
9 Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli muungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini. Watashika nafasi zao dhidi yake, naye kutokea kaskazini atatekwa. Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari, ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.
[Do that] because I am going to gather an army of great nations to the north [of Babylon]. They will join together to attack Babylon and will capture it. Their arrows will be like [SIM] skilled warriors that always hit what they aim at.
10 Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara; wote wamtekao nyara watapata za kutosha,” asema Bwana.
Babylonia will be conquered, and those who conquer it will take away everything they want. [That will surely happen because I, ] Yahweh, have said it.’”
11 “Kwa sababu hushangilia na kufurahi, wewe utekaye urithi wangu, kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka, na kulia kama farasi dume,
“You people [of Babylon] who (plundered/stole everything valuable from) my chosen people, now you are very happy [DOU]. You run around joyfully like [SIM] a calf in a meadow, and are happy like [SIM] male horses are happy when they are neighing.
12 mama yako ataaibika mno, yeye aliyekuzaa atatahayari. Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote, atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.
But [soon] your people will be very disgraced [DOU] [as a result of being conquered]. Your country will be the most insignificant nation; it will be a desert, a dry and deserted land.
13 Kwa sababu ya hasira ya Bwana hatakaliwa na mtu, lakini ataachwa ukiwa kabisa. Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
Because [I, ] Yahweh, am angry [with you people of Babylon], I will cause your city to become completely deserted. All who pass by will be horrified and will (gasp/be shocked) because of the destruction there.
14 “Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli, enyi nyote mvutao upinde. Mpigeni! Msibakize mshale wowote, kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya Bwana.
[All you nations that surround Babylon, ] prepare to attack it! Tell your archers to shoot at their enemies; shoot all of your arrows at them [LIT], because [the people/leaders of Babylon have sinned against me, ] Yahweh.
15 Piga kelele dhidi yake kila upande! Anajisalimisha, minara yake inaanguka, kuta zake zimebomoka. Kwa kuwa hiki ni kisasi cha Bwana, mlipizeni kisasi; mtendeeni kama alivyowatendea wengine.
Shout [war-cries] against Babylon from all sides [of the city]. [The soldiers of] Babylon will surrender; the towers and walls will be torn down. It is [I, ] Yahweh, who will be getting revenge [on the people of Babylon], [so help me to] get revenge. Do to [the people of] Babylon what they have done to others!
16 Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli, pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna. Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu kila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja na akimbilie kwenye nchi yake mwenyewe.
Take away from Babylon those who plant [crops] and those who reap the harvests! Because of the swords carried by those who will attack [Babylon], [those people in Babylon who have come from other countries] should all run away, back to their own countries [DOU]!”
17 “Israeli ni kundi lililotawanyika ambalo simba wamelifukuzia mbali. Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru, wa mwisho kuponda mifupa yake alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”
“The Israeli [people] are [like] [MET] sheep that have been scattered by lions. First [the army of] the King of Assyria defeated them. Then [the army of] King Nebuchadnezzar of Babylon smashed them.
18 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
So this is what I, the Commander of the armies of angels, the God whom the Israeli people [worship], say: ‘Now I will punish the King of Babylon and the people of his land, like I punished the King of Assyria.
19 Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe naye atalisha huko Karmeli na Bashani; njaa yake itashibishwa juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.
And I will bring the people of Israel back to their own land where they will eat [the food that grows] in the fields of the Carmel and Bashan [regions], and [the people in] the hilly areas of Ephraim and Gilead will have all they want to eat.
20 Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli, lakini halitakuwepo, kwa ajili ya dhambi za Yuda, lakini haitapatikana hata moja, kwa kuwa nitawasamehe mabaki nitakaowaacha.
At that time, there will not be people in Israel and in Judah who [are still guilty for having] sinned [DOU], because I will forgive the small group of people whom I enable to still be alive.’”
21 “Shambulieni nchi ya Merathaimu na wale waishio huko Pekodi. Wafuatieni, waueni na kuwaangamiza kabisa,” asema Bwana. “Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.
“[So, I, Yahweh, say to the enemies of Babylonia, ]‘Attack [the people who live in] the Merathaim [region] and the people in the Pekod [region of Babylonia]. Pursue them, kill them, and completely get rid of them, as I have commanded you to do.
22 Kelele ya vita iko ndani ya nchi, kelele ya maangamizi makuu!
Shout your battle cries throughout the land; shout [when you are causing] great destruction.
23 Tazama jinsi nyundo ya dunia yote ilivyovunjika na kuharibika! Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa miongoni mwa mataifa!
[The army of Babylon is like] [MET] the most powerful hammer on the earth, but it will be completely shattered. Babylon will be deserted among the [other] nations.’
24 Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli, nawe ukakamatwa kabla haujafahamu; ulipatikana na ukakamatwa kwa sababu ulimpinga Bwana.
You [people of] Babylon, [listen, ] [because] I have set a trap for you; you will be caught [in that trap], because you fought against me.
25 Bwana amefungua ghala lake la silaha na kuzitoa silaha za ghadhabu yake, kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mwenye Nguvu Zote anayo kazi ya kufanya katika nchi ya Wakaldayo.
[It is as though] I have opened the place where I store my weapons, and I have brought out [all] the weapons [to use against the people with whom] I am angry. [I, ] the Commander of the armies of angels, have [a lot of] work to do [to punish] the people of Babylonia.
26 Njooni dhidi yake kutoka mbali. Zifungueni ghala zake za nafaka; mlundikeni kama lundo la nafaka. Mwangamizeni kabisa na msimwachie mabaki yoyote.
[So, you enemies of Babylonia, ] come from distant lands and attack it. Break open the places where they store the grain. Crush the walls of the city and the houses and pile up [the rubble like] [SIM] heaps of grain. Destroy everything; do not leave anything that is not destroyed.
27 Waueni mafahali wake wachanga wote; waacheni washuke machinjoni! Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia, wakati wao wa kuadhibiwa.
Destroy all the [young men who are as strong as] [MET] bulls; take them to where you will slaughter them. It will be terrible for them, because it will be time for them to be punished.
28 Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli wakitangaza katika Sayuni jinsi Bwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
Listen to the people who have fled and escaped from Babylon while they tell in Jerusalem how [I, ] Yahweh, have gotten revenge against those who destroyed my temple [in Jerusalem].
29 “Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli, wote wale wavutao upinde. Pigeni kambi kumzunguka kabisa, asitoroke mtu yeyote. Mlipizeni kwa matendo yake; mtendeeni kama alivyotenda. Kwa kuwa alimdharau Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Summon archers [DOU] to come to attack Babylon; surround the city in order that no one will escape. Do to [the people of] Babylon what they have done to others [DOU], because they have defied [me, ] the Holy One of the Israeli [people].
30 Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku ile,” asema Bwana.
The young men of Babylon will fall in the streets; all their soldiers will be killed in one day.
31 “Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, “kwa kuwa siku yako imewadia, yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.
[I, ] the Commander of the armies of angels, say this: ‘You arrogant/proud people, it is now the time; it is the time [DOU] when I will punish you.
32 Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka, wala hakuna yeyote atakayemuinua; nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”
[Your land is full of] proud people, but you will stumble and fall, and no one will lift you up [again]. I will light a fire in the cities in Babylonia that will burn up everything that is nearby.’
33 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Watu wa Israeli wameonewa, nao watu wa Yuda pia. Wote waliowateka wamewashikilia sana, wanakataa kuwaachia waende.
[I], the Commander of the armies of angels, also say this: ‘The people of Israel and Judah were (oppressed/treated cruelly); those who captured them guarded them carefully and would not allow them to leave [Babylon].
34 Lakini Mkombozi wao ana nguvu; Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake. Atatetea kwa nguvu shauri lao ili alete raha katika nchi yao, lakini ataleta msukosuko kwa wale waishio Babeli.
But I am strong, and I will free them. I am the Commander of the armies of angels; I will defend my people and enable them [to return to] their land where they will have peace, but the people of Babylonia will not have peace.
35 “Upanga dhidi ya Wakaldayo!” asema Bwana, “dhidi ya wale waishio Babeli na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!
[I will send enemy soldiers carrying] swords [PRS] to strike the people of Babylonia; they will strike the officials and wise men and all the [other] people who live in Babylon.
36 Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo! Watakuwa wapumbavu. Upanga dhidi ya mashujaa wake! Watajazwa na hofu kuu
They will strike their false prophets with swords and they will become foolish. They will strike the [strongest] warriors of Babylonia, and they will all be terrified.
37 Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake! Wao watakuwa kama wanawake. Upanga dhidi ya hazina zake! Hizo zitatekwa nyara.
They will strike their horses and chariots and the foreigners who are in the army of Babylonia, and they will [all] become [as weak] as [MET] women. They will seize [MTY] all the valuable things there in Babylon and take them away.
38 Ukame juu ya maji yake! Nayo yatakauka. Kwa kuwa ni nchi ya sanamu, wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu.
[I] cause the streams to become dry. [I will do all those things] because the [entire] land [of Babylonia] is filled with idols, and those [horrible] idols have caused the people [who worship them] to become crazy.
39 “Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo, nao bundi watakaa humo. Kamwe haitakaliwa tena wala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
[Soon only] hyenas and [other] wild creatures will live there; and it will be a place where owls live. People will never live there again; it will be uninhabited forever [DOU].
40 Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
[I will destroy Babylon] like I destroyed Sodom and Gomorrah and the nearby towns; no one will [ever] live there [again] [DOU].
41 “Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini; taifa kubwa na wafalme wengi wanaamshwa kutoka miisho ya dunia.
Look! A [great] army will come from the north. A great nation far away with many kings is preparing [to attack you people of Babylon].
42 Wamejifunga pinde na mikuki; ni wakatili na wasio na huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao; wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Babeli.
Their [army] has bows [and arrows] and spears; they are [very] cruel, and do not act mercifully [to anyone]. [As] they ride along on [their] horses, the sound of the horses’ hooves is like [SIM] the roaring of the ocean [waves]; they are riding in battle formation to attack you, you people of Babylon.
43 Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu, nayo mikono yake imelegea. Uchungu umemshika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
The King of Babylon says, “[I] have heard reports about the enemy [approaching]; [so I am very frightened, with the result that] I am weak. I am [very fearful, and] anguished/worried, like [SIM] a woman who is about to give birth to a baby.”
44 Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule, nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
I, [Yahweh], will come to Babylon [suddenly] like a lion comes out of the jungle and [leaps on the sheep that are eating] the good pastureland. I will quickly chase the people of Babylonia from their land. And [then] I will appoint for them [a leader] whom I will choose; [I will do that] because there is no one [RHQ] like me who can say that what I have done is not right. No ruler can [RHQ] oppose me.
45 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Babeli, kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali. Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
Listen to what I have planned to do to the people of Babylon [city] and the rest of Babylonia: [even] the little children will be dragged away, and I will completely destroy the people [MET] who live there.
46 Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka; kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.
When Babylon is destroyed, the noise will be extremely loud, with the result that the earth will shake, and the wailing of the people will be heard by the [people of other] nations.’”

< Yeremia 50 >