< Yeremia 50 >

1 Hili ndilo neno alilosema Bwana kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:
The word that the Lord has spoken about Babylon and about the land of the Chaldeans, by the hand of Jeremiah the prophet.
2 “Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa, twekeni bendera na mkahubiri; msiache kitu chochote, bali semeni, ‘Babeli utatekwa; Beli ataaibishwa, Merodaki atajazwa na hofu kuu. Sanamu zake zitaaibishwa na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’
“Announce it among the Gentiles, and make it known. Lift up a sign. Proclaim it and do not conceal it. Say this: ‘Babylon has been captured. Bel has been confounded. Merodach has been conquered. Their graven things have been confounded. Their idols have not survived.’
3 Taifa kutoka kaskazini litamshambulia, na kuifanya nchi yake ukiwa. Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake, watu na wanyama wataikimbia.
For a nation has ascended against her from the north, which will set her land in desolation. And there will be no one who may live within it, from man even to beast. For they have been removed and have gone away.
4 “Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mungu wao.
In those days and in that time, says the Lord, the sons of Israel will advance, they and the sons of Judah together. Weeping as they walk, they will hurry on, and they will seek the Lord their God.
5 Wataiuliza njia iendayo Sayuni na kuelekeza nyuso zao huko. Watakuja na kuambatana na Bwana katika agano la milele ambalo halitasahaulika.
They will ask the way to Zion; their faces will be set toward this place. They will arrive and will be joined to the Lord by an everlasting covenant, which nothing will wipe away into oblivion.
6 “Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha na kuwasababisha kuzurura juu ya milima. Walitangatanga juu ya mlima na kilima, na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.
My people have become a lost flock. Their shepherds have led them astray and have caused them to wander in the mountains. They have crossed from mountain to hill. They have forgotten their resting place.
7 Yeyote aliyewakuta aliwala; adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia, kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi, Bwana, aliye tumaini la baba zao.’
All whom they have found, they have devoured. And their enemies have said: ‘We have not sinned. For it is they who have sinned against the Lord, the beauty of justice, and against the Lord, the hope of their fathers.’
8 “Kimbieni kutoka Babeli; ondokeni katika nchi ya Wakaldayo tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.
Withdraw from the midst of Babylon, and go forth from the land of the Chaldeans. And be like young goats before the flock.
9 Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli muungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini. Watashika nafasi zao dhidi yake, naye kutokea kaskazini atatekwa. Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari, ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.
For behold, I am raising up, and I will lead against Babylon, a congregation of great nations from the land of the north. And they will be prepared against her, and from there she will be taken. Their arrows, like those of a strong man, a killer, will not return empty.
10 Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara; wote wamtekao nyara watapata za kutosha,” asema Bwana.
And Chaldea will become a prey. All who lay waste to her will be filled, says the Lord.
11 “Kwa sababu hushangilia na kufurahi, wewe utekaye urithi wangu, kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka, na kulia kama farasi dume,
For you exult and you speak great things, plundering my inheritance. For you have spread out like calves upon the grass, and you have bellowed like bulls.
12 mama yako ataaibika mno, yeye aliyekuzaa atatahayari. Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote, atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.
Your mother has been exceedingly shamed, and she who bore you has become equal to the dust. Behold, she will be the last among the nations, a desert, impassable and dry.
13 Kwa sababu ya hasira ya Bwana hatakaliwa na mtu, lakini ataachwa ukiwa kabisa. Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
By the wrath of the Lord, it will not be inhabited. Instead, it will be entirely desolate. Everyone who passes by Babylon will be stupefied and will hiss over all her wounds.
14 “Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli, enyi nyote mvutao upinde. Mpigeni! Msibakize mshale wowote, kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya Bwana.
Prepare yourselves against Babylon, on every side, all you who bend the bow. Make war against her! You should not spare the arrows, for she has sinned against the Lord.
15 Piga kelele dhidi yake kila upande! Anajisalimisha, minara yake inaanguka, kuta zake zimebomoka. Kwa kuwa hiki ni kisasi cha Bwana, mlipizeni kisasi; mtendeeni kama alivyowatendea wengine.
Cry out against her! For where she has put forth a hand, her foundations have fallen, her walls have been destroyed. For it is the vengeance of the Lord. Take vengeance against her! Just as she has done, do so to her.
16 Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli, pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna. Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu kila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja na akimbilie kwenye nchi yake mwenyewe.
Destroy the founder from Babylon, and the one who holds the sickle in the time of harvest. Before the face of the sword of the dove, each one will turn back to his people, and every one will flee to his own land.
17 “Israeli ni kundi lililotawanyika ambalo simba wamelifukuzia mbali. Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru, wa mwisho kuponda mifupa yake alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”
Israel is a scattered flock. The lions have driven him away. First, the king of Assyria devoured him. And last, this Nebuchadnezzar, the king of Babylon, has taken away his bones.
18 Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
Because of this, thus says the Lord of hosts, the God of Israel: Behold, I will visit the king of Babylon and his land, just as I have visited the king of Assyria.
19 Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe naye atalisha huko Karmeli na Bashani; njaa yake itashibishwa juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.
And I will lead back Israel to his habitation. And he will pasture on Carmel and Bashan, and his soul will be satiated at mount Ephraim and Gilead.
20 Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli, lakini halitakuwepo, kwa ajili ya dhambi za Yuda, lakini haitapatikana hata moja, kwa kuwa nitawasamehe mabaki nitakaowaacha.
In those days and at that time, says the Lord, the iniquity of Israel will be sought, and there will be none. And the sin of Judah will be sought, and none will be found. For I will be forgiving to them, whom I will leave behind.
21 “Shambulieni nchi ya Merathaimu na wale waishio huko Pekodi. Wafuatieni, waueni na kuwaangamiza kabisa,” asema Bwana. “Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.
Ascend against the land of the rulers, and visit against its inhabitants! Scatter and destroy whatever has been left behind them, says the Lord, and act according to all that I have instructed you.
22 Kelele ya vita iko ndani ya nchi, kelele ya maangamizi makuu!
A voice of war in the land, and great destruction!
23 Tazama jinsi nyundo ya dunia yote ilivyovunjika na kuharibika! Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa miongoni mwa mataifa!
How has the mallet of the entire earth been broken and crushed? How has Babylon been turned into a desert among the nations?
24 Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli, nawe ukakamatwa kabla haujafahamu; ulipatikana na ukakamatwa kwa sababu ulimpinga Bwana.
I have ensnared you, and you have been captured, O Babylon, and you did not realize it. You have been discovered and seized, because you provoked the Lord.
25 Bwana amefungua ghala lake la silaha na kuzitoa silaha za ghadhabu yake, kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mwenye Nguvu Zote anayo kazi ya kufanya katika nchi ya Wakaldayo.
The Lord has opened his storehouse, and he has brought forth the instruments of his wrath. For there is work for the Lord, the God of hosts, within the land of the Chaldeans.
26 Njooni dhidi yake kutoka mbali. Zifungueni ghala zake za nafaka; mlundikeni kama lundo la nafaka. Mwangamizeni kabisa na msimwachie mabaki yoyote.
Advance against her from the furthest regions! Open, so that those who will trample her may go out! Take stones from the road, and gather them into piles, and destroy her. And let there be nothing left of her.
27 Waueni mafahali wake wachanga wote; waacheni washuke machinjoni! Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia, wakati wao wa kuadhibiwa.
Scatter all her strong ones. Let them descend to the slaughter. Woe to them! For their day has arrived, the time of their visitation.
28 Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli wakitangaza katika Sayuni jinsi Bwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
It is the voice of those who are fleeing and of those who have escaped from the land of Babylon: to announce in Zion the revenge of the Lord our God, the revenge of his Temple.
29 “Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli, wote wale wavutao upinde. Pigeni kambi kumzunguka kabisa, asitoroke mtu yeyote. Mlipizeni kwa matendo yake; mtendeeni kama alivyotenda. Kwa kuwa alimdharau Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Announce it to the many in Babylon, to all who bend the bow. Stand together against her all around, and let no one escape. Repay her according to her work. In accord with all that she has done, do to her. For she has raised herself up against the Lord, against the Holy One of Israel.
30 Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku ile,” asema Bwana.
For this reason, her young men will fall in her streets. And all her men of war will be silenced, in that day, says the Lord.
31 “Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, “kwa kuwa siku yako imewadia, yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.
Behold, I am against you, O proud one, says the Lord, the God of hosts. For your day has arrived, the time of your visitation.
32 Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka, wala hakuna yeyote atakayemuinua; nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”
And the proud one will fall and be ruined. And there will be no one who may lift him up. And I will kindle a fire in his cities, and it will devour everything around him.”
33 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Watu wa Israeli wameonewa, nao watu wa Yuda pia. Wote waliowateka wamewashikilia sana, wanakataa kuwaachia waende.
Thus says the Lord of hosts: “The sons of Israel and the sons of Judah have endured calumny together. All who have seized them are holding them and refusing to release them.
34 Lakini Mkombozi wao ana nguvu; Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake. Atatetea kwa nguvu shauri lao ili alete raha katika nchi yao, lakini ataleta msukosuko kwa wale waishio Babeli.
Their redeemer is strong. The Lord of hosts is his name. He will defend their case in judgment, so that he may terrify the land and disturb the inhabitants of Babylon.
35 “Upanga dhidi ya Wakaldayo!” asema Bwana, “dhidi ya wale waishio Babeli na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!
A sword is for the Chaldeans, says the Lord, and for the inhabitants of Babylon, and for her leaders, and for her wise ones.
36 Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo! Watakuwa wapumbavu. Upanga dhidi ya mashujaa wake! Watajazwa na hofu kuu
A sword is for her diviners, who will be fooled. A sword is for her strong ones, who will be afraid.
37 Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake! Wao watakuwa kama wanawake. Upanga dhidi ya hazina zake! Hizo zitatekwa nyara.
A sword is for their horses, and for their chariots, and for all the common people who are in her midst. And they will be like women. A sword is for her storehouses, and they will be plundered.
38 Ukame juu ya maji yake! Nayo yatakauka. Kwa kuwa ni nchi ya sanamu, wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu.
A drought is over her waters, and they will be dried up. For it is a land of graven images, and they glory in portents.
39 “Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo, nao bundi watakaa humo. Kamwe haitakaliwa tena wala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
Because of this, dragons will live there with the fig fauns, and ostriches will live in it. And it will no longer be inhabited, even in perpetuity, nor will it be raised up, even from generation to generation.
40 Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
Just as the Lord overthrew Sodom and Gomorrah, and their neighboring towns, says the Lord, no man will live there, and a son of man will not tend it.
41 “Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini; taifa kubwa na wafalme wengi wanaamshwa kutoka miisho ya dunia.
Behold, a people arrives from the north, and a great nation. And many kings will rise up from the ends of the earth.
42 Wamejifunga pinde na mikuki; ni wakatili na wasio na huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao; wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Babeli.
They will take up the bow and the shield. They are cruel and merciless. Their voice will sound out, like the sea, and they will ride upon horses, like a man prepared for battle against you, O daughter of Babylon.
43 Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu, nayo mikono yake imelegea. Uchungu umemshika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
The king of Babylon has heard the report about them, and his hands have been weakened. Anguish has overtaken him, like the pains of a woman giving birth.
44 Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule, nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
Behold, he will ascend like a lion from the arrogance of the Jordan to the robust beauty. For I will cause him to rush upon her suddenly. And who will be the elect one, whom I may appoint over her? For who is like me? And who can endure me? And who is that pastor who can withstand my countenance?”
45 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Babeli, kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali. Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
Because of this, listen to the counsel of the Lord, which he has conceived in his mind against Babylon, and to his thoughts, which he has devised against the land of the Chaldeans: “Certainly the little ones of the flocks will pull them down, unless their habitation will have been destroyed with them.
46 Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka; kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.
At the voice of the captivity of Babylon, the earth has been moved, and an outcry has been heard among the nations.”

< Yeremia 50 >