< Yeremia 49 >

1 Kuhusu Waamoni: Hili ndilo asemalo Bwana: “Je, Israeli hana wana? Je, hana warithi? Kwa nini basi Moleki amechukua milki ya Gadi? Kwa nini watu wake wanaishi katika miji yake?
Glede Amóncev tako govori Gospod: »Mar Izrael nima sinov? Mar nima dediča? Zakaj potem njihovi kralji podedujejo Gad in njegovo ljudstvo prebiva v njegovih mestih.
2 Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapopiga kelele ya vita dhidi ya Raba mji wa Waamoni; utakuwa kilima cha magofu, navyo vijiji vinavyouzunguka vitateketezwa kwa moto. Kisha Israeli atawafukuza wale waliomfukuza,” asema Bwana.
Zatorej, glejte, pridejo dnevi, ‹ govori Gospod, ›ko bom povzročil alarm vojne, da se bo slišal v Rabi Amóncev in ta bo zapuščen kup in njene hčere bodo požgane z ognjem. Potem bo Izrael dedič tistim, ki so bili njegovi dediči, ‹ govori Gospod.
3 “Lia kwa huzuni, ee Heshboni, kwa kuwa Ai umeangamizwa! Pigeni kelele, enyi wakazi wa Raba! Vaeni nguo za gunia na kuomboleza, kimbieni hapa na pale ndani ya kuta, kwa kuwa Moleki atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na makuhani na maafisa wake.
Tuli, oh Hešbón, kajti Aj je oplenjen. Jokajte ve Rabine hčere, opašite se z vrečevino; objokujte in tecite sem ter tja pri ograjah; kajti njihov kralj bo šel v ujetništvo skupaj z njegovimi duhovniki in njegovimi princi.
4 Kwa nini unajivunia mabonde yako, kujivunia mabonde yako yaliyozaa sana? Ee binti usiye mwaminifu, unayeutumainia utajiri wako na kusema, ‘Ni nani atakayenishambulia?’
Zakaj se ponašaš z dolinami, tvoji tekoči dolini, oh odpadla hči, ki si zaupala v svoje zaklade, rekoč: ›Kdo bo prišel k meni?‹
5 Nitaleta hofu kuu juu yako kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Kila mmoja wenu ataondolewa, wala hakuna hata mmoja atakayekusanya wakimbizi.
Glej, nadte bom privedel strah, ‹ govori Gospod Bog nad bojevniki, ›od vseh teh, ki bodo okoli tebe. Izgnani boste, vsak človek naravnost naprej in nihče ne bo zbral tistega, ki tava.
6 “Lakini hatimaye, nitarudisha mateka wa Waamoni,” asema Bwana.
Potem bom ponovno privedel ujetništvo Amónovih otrok, ‹ govori Gospod.
7 Kuhusu Edomu: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Je, hakuna tena hekima katika Temani? Je, shauri limewapotea wenye busara? Je, hekima yao imechakaa?
Glede Edóma tako govori Gospod nad bojevniki: › Mar v Temánu ni več modrosti? Je nasvet izginil pred razsodnim? Je njihova modrost izginila?
8 Geuka na ukimbie, jifiche katika mapango marefu kabisa, wewe uishiye Dedani, kwa kuwa nitaleta maafa juu ya Esau wakati nitakapomwadhibu.
Pobegnite, obrnite se nazaj, prebivajte globoko, oh prebivalci Dedána; kajti nadenj bom privedel Ezavovo katastrofo, čas, ko ga bom obiskal.
9 Je, kama wachuma zabibu wangekuja kwako, wasingebakiza zabibu chache? Kama wezi wangekujia usiku, je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji?
Če pridejo k tebi obiralci grozdja, ali ne bodo pustili nekaj paberkovalnih grozdov? Če tatovi ponoči, bodo uničevali, dokler ne bodo imeli dovolj.
10 Lakini nitamvua Esau nguo abaki uchi, nitayafunua maficho yake, ili asiweze kujificha. Watoto wake, jamaa na majirani wataangamia, naye hatakuwepo tena.
Toda jaz sem naredil Ezava razgaljenega, jaz sem odkril njegove skrite kraje in se ne bo mogel skriti. Njegovo seme je oplenjeno in njegovih bratov, njegovih sosedov in njega ni.
11 Waache yatima wako; nitayalinda maisha yao. Wajane wako pia wanaweza kunitumaini mimi.”
Pusti svoje osirotele otroke, jaz jih bom ohranil žive; in tvoje vdove naj zaupajo vame.‹
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama wale wasiostahili kukinywea kikombe ni lazima wakinywe, kwa nini wewe usiadhibiwe? Hutakwepa kuadhibiwa, ni lazima ukinywe.
Kajti tako govori Gospod: ›Glej, tisti, katerih sodba ni bila, da pijejo iz čaše, so zagotovo pijani; in ali si ti tisti, ki naj bi odšel čisto nekaznovan? Ne boš odšel nekaznovan, temveč boš zagotovo pil od tega.
13 Ninaapa kwa nafsi yangu,” asema Bwana, “kwamba Bosra utakuwa magofu na kitu cha kutisha, cha aibu na cha kulaania; miji yake yote itakuwa magofu milele.”
Kajti prisegel sem sam pri sebi, ‹ govori Gospod, ›da bo Bocra postala opustošenje, graja, opustošenost in prekletstvo in vsa njena mesta bodo neprestane opustošenosti.‹«
14 Nimesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Jikusanyeni ili kuushambulia! Inukeni kwa ajili ya vita!”
Slišal sem govorico od Gospoda in predstavnik je poslan k poganom, rekoč: »Zberite se skupaj in pridite zoper njo in se vzdignite k bitki.«
15 “Sasa nitakufanya uwe mdogo miongoni mwa mataifa, aliyedharauliwa miongoni mwa watu.
›Kajti glej, naredil te bom majhnega med pogani in preziranega med ljudmi.
16 Vitisho vyako na kiburi cha moyo wako vimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba, wewe unayedumu katika miinuko ya kilima. Ujapojenga kiota chako juu sana kama cha tai, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
Tvoja strašnost te je zavedla in ponos tvojega srca, oh ti, ki prebivaš v skalnih razpokah, ki držiš višino hriba. Čeprav bi si svoje gnezdo naredil tako visoko kakor orel, te bom od tam privedel dol, ‹ govori Gospod.
17 “Edomu atakuwa kitu cha kuogofya; wote wapitao karibu watashangaa na kuzomea kwa sababu ya majeraha yake yote.
›Tudi Edóm bo opustošenje. Vsak, kdor gre mimo, bo osupel in sikal bo nad vsemi njegovimi nadlogami.
18 Kama vile Sodoma na Gomora zilivyoangamizwa, pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
Kakor v razdejanju Sódome in Gomóre in njunih sosednjih mest, ‹ govori Gospod, ›noben človek ne bo vzdržal tam niti človeški sin ne bo prebival v tem.
19 “Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Edomu kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
Glej, vzpel se bo kakor lev iz naraščanja Jordana zoper prebivališče močnega. Toda naredil bom, da bo nenadoma pobegnil pred njo. In kdo je izbran mož, da bi ga lahko določil nad njo? Kajti kdo je podoben meni? In kdo mi bo določil čas? In kdo je tisti pastir, ki bo stal pred menoj?
20 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Edomu, kile alichokusudia dhidi ya wale waishio Temani: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali; yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
Zato prisluhnite Gospodovemu nasvetu, ki ga je svetoval zoper Edóm; in njegove namene, ki jih je namenil zoper prebivalce Temána: ›Zagotovo jih bo najmanjši iz tropa izvlekel ven. Zagotovo bo naredil njihova prebivališča opustela z njimi [vred].
21 Kwa sauti ya anguko lao, dunia itatetemeka. Kilio chao kitasikika hadi Bahari ya Shamu.
Zemlja je stresena ob hrupu njihovega padca, ob hrupu njihovega krika, ki ga je bilo slišati na Rdečem morju.
22 Tazama! Tai atapaa juu angani na kuruka chini kwa ghafula, akitandaza mabawa yake juu ya Bosra. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Glej, prišel bo gor in letel kakor orel in svoji peruti razširil nad Bocro in na ta dan bo srce mogočnih mož iz Edóma kakor srce ženske v njenih ostrih bolečinah.
23 Kuhusu Dameski: “Hamathi na Arpadi imetahayarika, kwa kuwa wamesikia habari mbaya. Wamevunjika moyo na wametaabika kama bahari iliyochafuka.
Glede Damaska. Hamát je zbegan in Arpád, kajti slišala sta zle novice. Boječa sta. Tam je bridkost na morju; ta ne more biti utišana.
24 Dameski amedhoofika, amegeuka na kukimbia, hofu ya ghafula imemkamata sana; amepatwa na uchungu na maumivu, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Damask je postal slaboten in se obrača, da pobegne in strah se ga je polastil. Tesnoba in bridkosti so ga prevzele kakor žensko v porodnih mukah.
25 Kwa nini mji ambao unajulikana haujaachwa, mji ambao ninaupenda?
Kako mesto hvale ni zapuščeno, mesto moje radosti!
26 Hakika, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku hiyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Zato bodo njegovi mladeniči padli na njegovih ulicah in vsi bojevniki bodo iztrebljeni na ta dan, ‹ govori Gospod nad bojevniki.
27 “Nitatia moto kuta za Dameski; utaangamiza ngome za Ben-Hadadi.”
›Zanetil bom ogenj v zidu Damaska in ta bo použil palače Ben Hadáda.‹
28 Kuhusu Kedari na falme za Hazori, ambazo Nebukadneza mfalme wa Babeli alizishambulia: Hili ndilo asemalo Bwana: “Inuka, ushambulie Kedari na kuwaangamiza watu wa mashariki.
Glede Kedárja in glede Hacórjevih kraljestev, ki jih bo babilonski kralj Nebukadnezar udaril, tako govori Gospod: ›Vstanite, pojdite gor v Kedár in oplenite može vzhoda.
29 Hema zao na makundi yao ya kondoo yatachukuliwa; vibanda vyao vitatwaliwa pamoja na mali zao zote na ngamia zao. Watu watawapigia kelele, ‘Hofu kuu iko kila upande!’
Njihove šotore in njihove trope bodo odvzeli. K sebi bodo vzeli njihove zavese in vse njihove posode in njihove kamele; in vpili jim bodo: ›Strah je na vsaki strani.‹
30 “Kimbieni haraka! Kaeni kwenye mapango marefu sana, ninyi mkaao Hazori,” asema Bwana. “Nebukadneza, mfalme wa Babeli amepanga shauri baya dhidi yenu; amebuni hila dhidi yenu.
Pobegnite, odpravite se daleč proč, prebivajte globoko, oh vi prebivalci Hacórja, ‹ govori Gospod; ›kajti babilonski kralj Nebukadnezar je zoper vas sprejel nasvet in je zoper vas spočel namen.
31 “Inuka na ulishambulie taifa lililo starehe, linaloishi kwa kujiamini,” asema Bwana, “taifa lisilo na malango wala makomeo; watu wake huishi peke yao.
Vstani, spravi se gor k premožnemu narodu, ki prebiva brez skrbi, ‹ govori Gospod, ›ki nima niti velikih vrat niti zapahov, ki prebiva sam.
32 Ngamia wao watakuwa nyara, nayo makundi yao makubwa ya ngʼombe yatatekwa. Wale walio maeneo ya mbali nitawatawanya pande zote, nami nitaleta maafa juu yao kutoka kila upande,” asema Bwana.
In njihove kamele bodo plen in množica njihove živine plen, in razkropil jih bom na vse vetrove, tiste, ki so na skrajnih vogalih; in jaz bom privedel njihovo katastrofo od vseh njihovih strani, ‹ govori Gospod.
33 “Hazori itakuwa makao ya mbweha, mahali pa ukiwa milele. Hakuna yeyote atakayeishi humo; hakuna mtu atakayekaa ndani yake.”
Hacór bo prebivališče za zmaje in opustošenje na veke. Tam ne bo prebival noben človek niti noben človeški sin ne prebiva v njem.‹«
34 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Elamu, mapema katika utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda:
Beseda od Gospoda, ki je prišla preroku Jeremiju zoper Elám v začetku kraljevanja Judovega kralja Sedekíja, rekoč:
35 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama, nitavunja upinde wa Elamu, ulio tegemeo la nguvu zao.
»Tako govori Gospod nad bojevniki: ›Glej, jaz bom zlomil Elámov lok, njihovo glavno moč.
36 Nitaleta pepo nne dhidi ya Elamu toka pande nne za mbingu, nitawatawanya katika hizo pande nne, wala hapatakuwa na taifa ambalo watu wa Elamu waliofukuzwa hawatakwenda.
Nad Elám bom privedel štiri vetrove iz štirih četrtin neba in razkropil jih bom proti vsem tem vetrovom; in tam ne bo nobenega naroda, kamor ne bi prišli pregnanci Eláma.
37 Nitamfadhaisha Elamu mbele ya adui zao, mbele yao wale wanaotafuta uhai wao; nitaleta maafa juu yao, naam, hasira yangu kali,” asema Bwana. “Nitawafuatia kwa upanga mpaka nitakapowamaliza.
Kajti Elámu bom povzročil, da bo zaprepaden pred svojimi sovražniki in pred tistimi, ki jim strežejo po življenju, in nanje bom privedel zlo, celó svojo kruto jezo, ‹ govori Gospod: ›in za njimi bom poslal meč, dokler jih ne bom použil.
38 Nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme wake na maafisa wake,” asema Bwana.
Svoj prestol bom postavil v Elámu in od tam bom uničil kralja in prince, ‹ govori Gospod.
39 “Lakini nitarudisha mateka wa Elamu katika siku zijazo,” asema Bwana.
›Toda to se bo zgodilo v zadnjih dneh, da bom ponovno privedel ujetništvo Eláma, ‹ govori Gospod.«

< Yeremia 49 >