< Yeremia 49 >

1 Kuhusu Waamoni: Hili ndilo asemalo Bwana: “Je, Israeli hana wana? Je, hana warithi? Kwa nini basi Moleki amechukua milki ya Gadi? Kwa nini watu wake wanaishi katika miji yake?
Pour les enfants d'Ammon. Ainsi a dit l'Éternel: Israël n'a-t-il point de fils? N'a-t-il point d'héritier? Pourquoi Malcam hérite-t-il de Gad, et son peuple habite-t-il dans ses villes?
2 Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapopiga kelele ya vita dhidi ya Raba mji wa Waamoni; utakuwa kilima cha magofu, navyo vijiji vinavyouzunguka vitateketezwa kwa moto. Kisha Israeli atawafukuza wale waliomfukuza,” asema Bwana.
C'est pourquoi les jours viennent, dit l'Éternel, où je ferai entendre le cri de guerre vers Rabba des enfants d'Ammon; elle deviendra un monceau de ruines, et les villes de son ressort seront consumées par le feu, et Israël possédera ceux qui l'auront possédé, a dit l'Éternel.
3 “Lia kwa huzuni, ee Heshboni, kwa kuwa Ai umeangamizwa! Pigeni kelele, enyi wakazi wa Raba! Vaeni nguo za gunia na kuomboleza, kimbieni hapa na pale ndani ya kuta, kwa kuwa Moleki atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na makuhani na maafisa wake.
Hurle, Hesbon! car Haï est saccagée; filles de Rabba, criez, revêtez-vous de sacs, lamentez-vous, courez çà et là le long des murailles. Car Malcam ira en captivité, avec ses sacrificateurs et ses chefs.
4 Kwa nini unajivunia mabonde yako, kujivunia mabonde yako yaliyozaa sana? Ee binti usiye mwaminifu, unayeutumainia utajiri wako na kusema, ‘Ni nani atakayenishambulia?’
Pourquoi te glorifies-tu de tes vallées? Le sang coulera dans ta vallée, fille infidèle, qui te confies dans tes trésors et dis: Qui viendra contre moi?
5 Nitaleta hofu kuu juu yako kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Kila mmoja wenu ataondolewa, wala hakuna hata mmoja atakayekusanya wakimbizi.
Voici, je vais faire venir de tous tes environs la terreur contre toi, dit le Seigneur, l'Éternel des armées; et vous serez chassés chacun devant soi, et personne ne rassemblera les fugitifs.
6 “Lakini hatimaye, nitarudisha mateka wa Waamoni,” asema Bwana.
Mais, après cela, je ramènerai les captifs des enfants d'Ammon, dit l'Éternel.
7 Kuhusu Edomu: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Je, hakuna tena hekima katika Temani? Je, shauri limewapotea wenye busara? Je, hekima yao imechakaa?
Pour Édom. Ainsi a dit l'Éternel des armées: N'y a-t-il plus de sagesse dans Théman? Le conseil manque-t-il aux hommes entendus? Leur sagesse s'est-elle évanouie?
8 Geuka na ukimbie, jifiche katika mapango marefu kabisa, wewe uishiye Dedani, kwa kuwa nitaleta maafa juu ya Esau wakati nitakapomwadhibu.
Fuyez, tournez le dos, prenez des cavernes pour demeures, habitants de Dédan! car je fais venir sur Ésaü sa calamité, le temps auquel je veux le visiter.
9 Je, kama wachuma zabibu wangekuja kwako, wasingebakiza zabibu chache? Kama wezi wangekujia usiku, je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji?
Si des vendangeurs entraient chez toi, ne laisseraient-ils pas des grappillages? Si c'étaient des voleurs de nuit, ils ne prendraient que ce qui leur suffit.
10 Lakini nitamvua Esau nguo abaki uchi, nitayafunua maficho yake, ili asiweze kujificha. Watoto wake, jamaa na majirani wataangamia, naye hatakuwepo tena.
Mais moi, j'ai dépouillé Ésaü, j'ai découvert ses retraites, il ne peut plus se cacher; sa postérité, ses frères, ses voisins sont dévastés, et il n'est plus.
11 Waache yatima wako; nitayalinda maisha yao. Wajane wako pia wanaweza kunitumaini mimi.”
Laisse tes orphelins; je les ferai vivre; et que tes veuves s'assurent en moi!
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama wale wasiostahili kukinywea kikombe ni lazima wakinywe, kwa nini wewe usiadhibiwe? Hutakwepa kuadhibiwa, ni lazima ukinywe.
Car ainsi a dit l'Éternel: Voici, ceux qui ne devaient pas boire la coupe la boiront, et toi, en serais-tu exempt? Tu n'en seras pas exempt; mais tu la boiras certainement.
13 Ninaapa kwa nafsi yangu,” asema Bwana, “kwamba Bosra utakuwa magofu na kitu cha kutisha, cha aibu na cha kulaania; miji yake yote itakuwa magofu milele.”
Car j'ai juré par moi-même, dit l'Éternel, que Botsra sera réduite en désolation, en opprobre, en désert et en malédiction, et que toutes ses villes deviendront des solitudes éternelles.
14 Nimesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Jikusanyeni ili kuushambulia! Inukeni kwa ajili ya vita!”
Je l'ai entendu de la part de l'Éternel: Un messager est envoyé parmi les nations: “Assemblez-vous, dit-il, et venez contre elle, et levez-vous pour combattre! “
15 “Sasa nitakufanya uwe mdogo miongoni mwa mataifa, aliyedharauliwa miongoni mwa watu.
Car voici, je te rendrai petite entre les nations, et méprisée entre les hommes.
16 Vitisho vyako na kiburi cha moyo wako vimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba, wewe unayedumu katika miinuko ya kilima. Ujapojenga kiota chako juu sana kama cha tai, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
Ta présomption, l'orgueil de ton cœur t'a séduite, toi qui habites le creux des rochers et qui occupes le sommet des collines. Quand tu élèverais ton nid comme l'aigle, je te précipiterai de là, dit l'Éternel.
17 “Edomu atakuwa kitu cha kuogofya; wote wapitao karibu watashangaa na kuzomea kwa sababu ya majeraha yake yote.
Et l'Idumée sera réduite en désolation; tellement que quiconque passera près d'elle en sera étonné, et sifflera à cause de toutes ses plaies.
18 Kama vile Sodoma na Gomora zilivyoangamizwa, pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
Comme dans la destruction de Sodome et de Gomorrhe, et des villes voisines, a dit l'Éternel, il n'y habitera personne et aucun fils d'homme n'y séjournera.
19 “Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Edomu kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
Voici, tel qu'un lion, il monte des bords orgueilleux du Jourdain vers la demeure forte. Car, en un moment, je le ferai courir sur elle, et je donnerai mission contre elle à celui que j'ai choisi. Car qui est semblable à moi? Qui m'assignera? Et quel est le berger qui me résistera?
20 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Edomu, kile alichokusudia dhidi ya wale waishio Temani: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali; yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
C'est pourquoi, écoutez la résolution que l'Éternel a prise contre Édom, et les desseins qu'il a formés contre les habitants de Théman: Certainement on les traînera comme les plus petits du troupeau! Certainement on détruira sur eux leurs demeures!
21 Kwa sauti ya anguko lao, dunia itatetemeka. Kilio chao kitasikika hadi Bahari ya Shamu.
Au bruit de leur chute, la terre tremble, et la voix de leur cri se fait entendre jusqu'à la mer Rouge.
22 Tazama! Tai atapaa juu angani na kuruka chini kwa ghafula, akitandaza mabawa yake juu ya Bosra. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Voici, il monte comme l'aigle, il vole, il étend ses ailes sur Botsra, et en ce jour-là le cœur des héros d'Édom sera comme le cœur d'une femme en travail.
23 Kuhusu Dameski: “Hamathi na Arpadi imetahayarika, kwa kuwa wamesikia habari mbaya. Wamevunjika moyo na wametaabika kama bahari iliyochafuka.
Pour Damas. Hamath et Arpad sont confondues; car elles ont appris de fâcheuses nouvelles; elles défaillent! C'est comme la mer par une tourmente; elle ne peut s'apaiser.
24 Dameski amedhoofika, amegeuka na kukimbia, hofu ya ghafula imemkamata sana; amepatwa na uchungu na maumivu, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Damas n'a plus de force; elle se tourne pour fuir; la peur s'empare d'elle; l'angoisse et les douleurs la saisissent comme celle qui enfante.
25 Kwa nini mji ambao unajulikana haujaachwa, mji ambao ninaupenda?
Comment n'est-elle point abandonnée, la ville fameuse, la cité de ma joie?
26 Hakika, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku hiyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
C'est pourquoi ses jeunes gens tomberont dans ses rues, et tous les hommes de guerre périront en ce jour-là, dit l 'Éternel des armées.
27 “Nitatia moto kuta za Dameski; utaangamiza ngome za Ben-Hadadi.”
Et je mettrai le feu dans les murs de Damas, et il dévorera les palais de Ben-Hadad.
28 Kuhusu Kedari na falme za Hazori, ambazo Nebukadneza mfalme wa Babeli alizishambulia: Hili ndilo asemalo Bwana: “Inuka, ushambulie Kedari na kuwaangamiza watu wa mashariki.
Pour Kédar et les royaumes de Hatsor, que frappa Nébucadnetsar, roi de Babylone. Ainsi a dit l'Éternel: Levez-vous, montez vers Kédar, et détruisez les enfants de l'Orient.
29 Hema zao na makundi yao ya kondoo yatachukuliwa; vibanda vyao vitatwaliwa pamoja na mali zao zote na ngamia zao. Watu watawapigia kelele, ‘Hofu kuu iko kila upande!’
On enlèvera leurs tentes et leurs troupeaux; on s'emparera de leurs tapis, de tous leurs bagages et de leurs chameaux, et on criera: “Frayeur de tous côtés! “
30 “Kimbieni haraka! Kaeni kwenye mapango marefu sana, ninyi mkaao Hazori,” asema Bwana. “Nebukadneza, mfalme wa Babeli amepanga shauri baya dhidi yenu; amebuni hila dhidi yenu.
Fuyez! Éloignez-vous tant que vous pourrez! Prenez dans les creux vos demeures, habitants de Hatsor! dit l'Éternel; car Nébucadnetsar, roi de Babylone, a formé contre vous un dessein, il a pris une résolution contre vous.
31 “Inuka na ulishambulie taifa lililo starehe, linaloishi kwa kujiamini,” asema Bwana, “taifa lisilo na malango wala makomeo; watu wake huishi peke yao.
Levez-vous; montez vers une nation qui est en repos et qui habite en assurance, dit l'Éternel. Ils n'ont ni portes, ni barres; ils habitent seuls.
32 Ngamia wao watakuwa nyara, nayo makundi yao makubwa ya ngʼombe yatatekwa. Wale walio maeneo ya mbali nitawatawanya pande zote, nami nitaleta maafa juu yao kutoka kila upande,” asema Bwana.
Leurs chameaux seront au pillage, et la multitude de leur bétail sera une proie. Je les disperserai à tout vent, ces gens qui se rasent les coins de la barbe, et je ferai venir leur calamité de tous les côtés, dit l'Éternel.
33 “Hazori itakuwa makao ya mbweha, mahali pa ukiwa milele. Hakuna yeyote atakayeishi humo; hakuna mtu atakayekaa ndani yake.”
Et Hatsor deviendra un repaire de chacals et un désert à toujours. Il n'y demeurera personne, et aucun fils d'homme n'y séjournera!
34 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Elamu, mapema katika utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda:
La parole de l'Éternel qui fut adressée à Jérémie, le prophète, touchant Élam, au commencement du règne de Sédécias, roi de Juda, en ces termes:
35 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama, nitavunja upinde wa Elamu, ulio tegemeo la nguvu zao.
Ainsi a dit l'Éternel des armées: Voici, je vais rompre l'arc d'Élam, leur principale force.
36 Nitaleta pepo nne dhidi ya Elamu toka pande nne za mbingu, nitawatawanya katika hizo pande nne, wala hapatakuwa na taifa ambalo watu wa Elamu waliofukuzwa hawatakwenda.
Et je ferai venir contre Élam, les quatre vents, des quatre extrémités des cieux; et je les disperserai par tous ces vents-là, et il n'y aura pas de nation où ne viennent des fugitifs d'Élam.
37 Nitamfadhaisha Elamu mbele ya adui zao, mbele yao wale wanaotafuta uhai wao; nitaleta maafa juu yao, naam, hasira yangu kali,” asema Bwana. “Nitawafuatia kwa upanga mpaka nitakapowamaliza.
Je ferai que les Élamites seront épouvantés devant leurs ennemis et devant ceux qui cherchent leur vie; et j'amènerai sur eux le malheur, l'ardeur de ma colère, dit l'Éternel; et j'enverrai après eux l'épée, jusqu'à ce que je les aie consumés.
38 Nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme wake na maafisa wake,” asema Bwana.
Et je placerai mon trône dans Élam, et j'en détruirai les rois et les chefs, dit l'Éternel.
39 “Lakini nitarudisha mateka wa Elamu katika siku zijazo,” asema Bwana.
Mais il arrivera qu'aux derniers jours je ramènerai les captifs d'Élam, dit l'Éternel.

< Yeremia 49 >