< Yeremia 49 >

1 Kuhusu Waamoni: Hili ndilo asemalo Bwana: “Je, Israeli hana wana? Je, hana warithi? Kwa nini basi Moleki amechukua milki ya Gadi? Kwa nini watu wake wanaishi katika miji yake?
Quant aux enfants de Hammon, ainsi a dit l'Eternel: Israël n'a-t-il point d'enfants, ou n'a-t-il point d'héritier? pourquoi donc Malcam a-t-il hérité [du pays] de Gad, et pourquoi son peuple demeure-t-il dans les villes [de Gad]?
2 Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapopiga kelele ya vita dhidi ya Raba mji wa Waamoni; utakuwa kilima cha magofu, navyo vijiji vinavyouzunguka vitateketezwa kwa moto. Kisha Israeli atawafukuza wale waliomfukuza,” asema Bwana.
C'est pourquoi voici, les jours viennent, dit l'Eternel, que je ferai ouïr l'alarme dans Rabba des enfants de Hammon, et elle sera réduite en un monceau de ruines, et les villes de son ressort seront brûlées au feu, et Israël possédera ceux qui l'auront possédé, a dit l'Eternel.
3 “Lia kwa huzuni, ee Heshboni, kwa kuwa Ai umeangamizwa! Pigeni kelele, enyi wakazi wa Raba! Vaeni nguo za gunia na kuomboleza, kimbieni hapa na pale ndani ya kuta, kwa kuwa Moleki atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na makuhani na maafisa wake.
Hurle, ô Hesbon! car Haï a été ravagée. Villes du ressort de Rabba, criez; ceignez le sac sur vous, lamentez, courez le long des haies; car Malcam ira en captivité avec ses Sacrificateurs et ses principaux.
4 Kwa nini unajivunia mabonde yako, kujivunia mabonde yako yaliyozaa sana? Ee binti usiye mwaminifu, unayeutumainia utajiri wako na kusema, ‘Ni nani atakayenishambulia?’
Pourquoi te glorifies-tu de tes vallées? ta vallée est écoulée, fille revêche. Elle se confiait en ses trésors, et [disait]: qui viendra contre moi?
5 Nitaleta hofu kuu juu yako kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Kila mmoja wenu ataondolewa, wala hakuna hata mmoja atakayekusanya wakimbizi.
Voici, je m'en vais faire venir de tous tes environs la frayeur sur toi, dit le Seigneur l'Eternel des armées, et vous serez chassés chacun çà et là, et il n'y aura personne qui rassemble les dispersés.
6 “Lakini hatimaye, nitarudisha mateka wa Waamoni,” asema Bwana.
Mais après cela je ferai retourner les captifs des enfants de Hammon, dit l'Etemel.
7 Kuhusu Edomu: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Je, hakuna tena hekima katika Temani? Je, shauri limewapotea wenye busara? Je, hekima yao imechakaa?
Quant à Edom, ainsi a dit l'Eternel des armées: n'est-il pas vrai qu'[il] n'[y a] plus de sagesse dans Téman? le conseil a manqué à ses habitants, leur sagesse s'est évanouie.
8 Geuka na ukimbie, jifiche katika mapango marefu kabisa, wewe uishiye Dedani, kwa kuwa nitaleta maafa juu ya Esau wakati nitakapomwadhibu.
Fuyez, tournez [le dos], vous habitants de Dédan, qui avez fait des creux pour y habiter; car j'ai fait venir sur Esaü sa calamité, le temps auquel je l'ai visité.
9 Je, kama wachuma zabibu wangekuja kwako, wasingebakiza zabibu chache? Kama wezi wangekujia usiku, je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji?
Est-il entré chez toi des vendangeurs? ils ne t'auraient point laissé de grappillage. Sont-ce des larrons de nuit? ils auraient fait du dégât autant qu'il leur aurait suffi.
10 Lakini nitamvua Esau nguo abaki uchi, nitayafunua maficho yake, ili asiweze kujificha. Watoto wake, jamaa na majirani wataangamia, naye hatakuwepo tena.
Mais j'ai fouillé Esaü, j'ai découvert ses lieux secrets, tellement qu'il ne se pourra cacher; sa postérité est ravagée, ses frères aussi, et ses voisins; et ce n'est plus rien.
11 Waache yatima wako; nitayalinda maisha yao. Wajane wako pia wanaweza kunitumaini mimi.”
Laisse tes orphelins, et je leur donnerai de quoi vivre, et que tes veuves s'assurent sur moi.
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama wale wasiostahili kukinywea kikombe ni lazima wakinywe, kwa nini wewe usiadhibiwe? Hutakwepa kuadhibiwa, ni lazima ukinywe.
Car ainsi a dit l'Eternel: voici, ceux qui ne devaient point boire de la coupe, en boiront certainement; et toi en serais-tu exempt en quelque manière? tu n'en seras point exempt; mais tu en boiras certainement.
13 Ninaapa kwa nafsi yangu,” asema Bwana, “kwamba Bosra utakuwa magofu na kitu cha kutisha, cha aibu na cha kulaania; miji yake yote itakuwa magofu milele.”
Car j'ai juré par moi-même, dit l'Eternel, que Botsra sera réduite en désolation, en opprobre, en désert, et en malédiction, et que toutes ses villes seront réduites en déserts perpétuels.
14 Nimesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Jikusanyeni ili kuushambulia! Inukeni kwa ajili ya vita!”
J'ai ouï une publication de par l'Eternel, et il y a un ambassadeur envoyé parmi les nations, [pour leur dire]: assemblez-vous, et venez contre elle, et levez-vous pour combattre.
15 “Sasa nitakufanya uwe mdogo miongoni mwa mataifa, aliyedharauliwa miongoni mwa watu.
Car voici, je t'avais fait petit entre les nations, et contemptible entre les hommes.
16 Vitisho vyako na kiburi cha moyo wako vimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba, wewe unayedumu katika miinuko ya kilima. Ujapojenga kiota chako juu sana kama cha tai, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
Mais ta présomption, [et] la fierté de ton cœur t'ont séduit, toi qui habites dans les creux des rochers, et qui occupes la hauteur des coteaux. Quand tu aurais élevé ton nid comme l'aigle, je t'en ferai descendre, dit l'Eternel.
17 “Edomu atakuwa kitu cha kuogofya; wote wapitao karibu watashangaa na kuzomea kwa sababu ya majeraha yake yote.
Et l'Idumée sera réduite en désolation, tellement que quiconque passera près d'elle en sera étonné, et lui insultera à cause de toutes ses plaies.
18 Kama vile Sodoma na Gomora zilivyoangamizwa, pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
Il n'y demeurera personne, a dit l'Eternel, et aucun fils d'homme n'y séjournera, comme dans la subversion de Sodome et de Gomorrhe, et de leurs lieux circonvoisins.
19 “Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Edomu kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
Voici, il montera comme un lion à cause de l'enflure du Jourdain, vers la demeure du pays rude, et après l'avoir fait reposer je le ferai courir hors de l'Idumée. Et qui [est] d'élite, que je lui donne commission contre elle? car qui est semblable à moi? et qui me déterminera le temps? et qui sera le Pasteur qui tiendra ferme contre moi?
20 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Edomu, kile alichokusudia dhidi ya wale waishio Temani: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali; yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
C'est pourquoi écoutez la résolution que l'Eternel a prise contre Edom, et les desseins qu'il a formés contre les habitants de Téman; si les plus petits du troupeau ne les traînent par terre, et si l'on ne réduit en désolation leurs cabanes sur eux.
21 Kwa sauti ya anguko lao, dunia itatetemeka. Kilio chao kitasikika hadi Bahari ya Shamu.
La terre a été ébranlée du bruit de leur ruine; il y a eu un cri, le son en a été ouï en la mer Rouge.
22 Tazama! Tai atapaa juu angani na kuruka chini kwa ghafula, akitandaza mabawa yake juu ya Bosra. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Voici, il montera comme un aigle, et il volera, et étendra ses ailes sur Botsra; et le cœur des forts d'Edom en ce jour-là sera comme le cœur d'une femme qui est en travail.
23 Kuhusu Dameski: “Hamathi na Arpadi imetahayarika, kwa kuwa wamesikia habari mbaya. Wamevunjika moyo na wametaabika kama bahari iliyochafuka.
Quant à Damas; Hamath et Arpad ont été rendues honteuses, parce qu'elles ont appris des nouvelles très mauvaises, ils sont fondus, il y a une tourmente en la mer, elle ne se peut apaiser.
24 Dameski amedhoofika, amegeuka na kukimbia, hofu ya ghafula imemkamata sana; amepatwa na uchungu na maumivu, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Damas est toute lâche, elle est mise en fuite, la peur l'a surprise, l'angoisse et les douleurs l'ont saisie comme d'une femme qui enfante.
25 Kwa nini mji ambao unajulikana haujaachwa, mji ambao ninaupenda?
Comment n'a été réservée la ville renommée, ma ville de plaisance?
26 Hakika, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku hiyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Car ses gens d'élite tomberont dans ses rues, et on fera perdre la parole à tous ses hommes de guerre en ce jour-là, dit l'Eternel des armées.
27 “Nitatia moto kuta za Dameski; utaangamiza ngome za Ben-Hadadi.”
Et je mettrai le feu à la muraille de Damas, qui dévorera les palais de Ben-hadad.
28 Kuhusu Kedari na falme za Hazori, ambazo Nebukadneza mfalme wa Babeli alizishambulia: Hili ndilo asemalo Bwana: “Inuka, ushambulie Kedari na kuwaangamiza watu wa mashariki.
Quant à Kédar, et aux Royaumes de Hatsor, lesquels Nébucanetsar Roi de Babylone frappera, ainsi a dit l'Eternel: levez-vous, montez vers Kédar, et détruisez les enfants d'Orient.
29 Hema zao na makundi yao ya kondoo yatachukuliwa; vibanda vyao vitatwaliwa pamoja na mali zao zote na ngamia zao. Watu watawapigia kelele, ‘Hofu kuu iko kila upande!’
Ils enlèveront leurs tentes et leurs troupeaux, et prendront pour eux leurs tentes, et tout leur équipage, et leurs chameaux, et on criera: frayeur tout autour.
30 “Kimbieni haraka! Kaeni kwenye mapango marefu sana, ninyi mkaao Hazori,” asema Bwana. “Nebukadneza, mfalme wa Babeli amepanga shauri baya dhidi yenu; amebuni hila dhidi yenu.
Fuyez, écartez-vous tant que vous pourrez, vous habitants de Hatsor, qui avez fait des creux pour y habiter, dit l'Eternel; car Nébucadnetsar Roi de Babylone a formé un dessein contre vous, il a pris une résolution contre vous.
31 “Inuka na ulishambulie taifa lililo starehe, linaloishi kwa kujiamini,” asema Bwana, “taifa lisilo na malango wala makomeo; watu wake huishi peke yao.
Levez-vous, montez vers la nation qui est en repos, qui habite en assurance, dit l'Eternel; qui n'ont ni portes, ni barres, et qui habitent seuls.
32 Ngamia wao watakuwa nyara, nayo makundi yao makubwa ya ngʼombe yatatekwa. Wale walio maeneo ya mbali nitawatawanya pande zote, nami nitaleta maafa juu yao kutoka kila upande,” asema Bwana.
Et leurs chameaux seront au pillage, et la multitude de leur bétail sera en proie; et je les disperserai à tout vent, vers ceux qui se coupent l'extrémité des cheveux, et je ferai venir de tous les côtés leur calamité, dit l'Eternel.
33 “Hazori itakuwa makao ya mbweha, mahali pa ukiwa milele. Hakuna yeyote atakayeishi humo; hakuna mtu atakayekaa ndani yake.”
Et Hatsor deviendra un repaire de dragons, et un désert à toujours; il n'y demeurera personne, et aucun fils d'homme n'y séjournera.
34 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Elamu, mapema katika utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda:
La parole de l'Eternel qui fut [adressée] à Jérémie le Prophète, contre Hélam, au commencement du règne de Sédécias Roi de Juda, en disant:
35 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama, nitavunja upinde wa Elamu, ulio tegemeo la nguvu zao.
Ainsi a dit l'Eternel des armées: voici, je m'en vais rompre l'arc d'Hélam, qui est leur principale force.
36 Nitaleta pepo nne dhidi ya Elamu toka pande nne za mbingu, nitawatawanya katika hizo pande nne, wala hapatakuwa na taifa ambalo watu wa Elamu waliofukuzwa hawatakwenda.
Et je ferai venir contre Hélam les quatre vents, des quatre bouts des cieux; et je les disperserai par tous ces vents-là; et il n'y aura point de nation chez laquelle ne viennent ceux qui seront chassés d'Hélam.
37 Nitamfadhaisha Elamu mbele ya adui zao, mbele yao wale wanaotafuta uhai wao; nitaleta maafa juu yao, naam, hasira yangu kali,” asema Bwana. “Nitawafuatia kwa upanga mpaka nitakapowamaliza.
Et je ferai que ceux d'Hélam seront épouvantés devant leurs ennemis, et devant ceux qui cherchent leur vie; et je ferai venir du mal sur eux, l'ardeur de ma colère, dit l'Eternel; et j'enverrai l'épée après eux, jusqu’à ce que je les aie consumés.
38 Nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme wake na maafisa wake,” asema Bwana.
Et je mettrai mon trône en Hélam, et j'en détruirai les Rois et les principaux, dit l'Eternel.
39 “Lakini nitarudisha mateka wa Elamu katika siku zijazo,” asema Bwana.
Mais il arrivera qu'aux derniers jours je ferai retourner d'Hélam les captifs, dit l'Eternel.

< Yeremia 49 >