< Yeremia 49 >

1 Kuhusu Waamoni: Hili ndilo asemalo Bwana: “Je, Israeli hana wana? Je, hana warithi? Kwa nini basi Moleki amechukua milki ya Gadi? Kwa nini watu wake wanaishi katika miji yake?
`Go ye to the sones of Amon. The Lord seith these thingis. Whether no sones ben of Israel, ether an eir is not to it? whi therfor weldide Melchon the eritage of Gad, and the puple therof dwellide in the citees of Gad?
2 Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapopiga kelele ya vita dhidi ya Raba mji wa Waamoni; utakuwa kilima cha magofu, navyo vijiji vinavyouzunguka vitateketezwa kwa moto. Kisha Israeli atawafukuza wale waliomfukuza,” asema Bwana.
Lo! daies comen, seith the Lord, and Y schal make the gnaisting of batel herd on Rabath of the sones of Amon; and it schal be distried in to noise, and the vilagis therof schulen be brent with fier, and Israel schal welde hise welderis, seith the Lord.
3 “Lia kwa huzuni, ee Heshboni, kwa kuwa Ai umeangamizwa! Pigeni kelele, enyi wakazi wa Raba! Vaeni nguo za gunia na kuomboleza, kimbieni hapa na pale ndani ya kuta, kwa kuwa Moleki atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na makuhani na maafisa wake.
Yelle ye, Esebon, for Hay is distried; crie, ye douytris of Rabath, girde you with heiris, weile ye, and cumpasse bi heggis; for whi Melchon schal be lad in to passyng ouer, the prestis therof and princes therof togidere.
4 Kwa nini unajivunia mabonde yako, kujivunia mabonde yako yaliyozaa sana? Ee binti usiye mwaminifu, unayeutumainia utajiri wako na kusema, ‘Ni nani atakayenishambulia?’
What hast thou glorie in valeis? Thi valeis fleet awei, thou delicat douyter, that haddist trist in thi tresours, and seidist, Who schal come to me?
5 Nitaleta hofu kuu juu yako kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Kila mmoja wenu ataondolewa, wala hakuna hata mmoja atakayekusanya wakimbizi.
Lo! Y schal bringe in drede on thee, seith the Lord God of oostis, God of Israel, of alle men that ben in thi cumpasse; and ye schulen be scaterid, ech bi hym silf, fro youre siyt, and noon schal be, that gadere hem that fleen.
6 “Lakini hatimaye, nitarudisha mateka wa Waamoni,” asema Bwana.
And after these thingis Y schal make the fleeris and prisoneris of the sones of Amon to turne ayen, seith the Lord.
7 Kuhusu Edomu: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Je, hakuna tena hekima katika Temani? Je, shauri limewapotea wenye busara? Je, hekima yao imechakaa?
To Ydumee the Lord God of oostis seith these thingis. Whether wisdom is no more in Theman? Councel perischide fro sones, the wisdom of hem is maad vnprofitable.
8 Geuka na ukimbie, jifiche katika mapango marefu kabisa, wewe uishiye Dedani, kwa kuwa nitaleta maafa juu ya Esau wakati nitakapomwadhibu.
Fle ye, and turne ye backis; go doun in to a swolowe, ye dwelleris of Dedan, for Y haue brouyt the perdicioun of Esau on hym, the tyme of his visitacioun.
9 Je, kama wachuma zabibu wangekuja kwako, wasingebakiza zabibu chache? Kama wezi wangekujia usiku, je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji?
If gadereris of grapis hadden come on thee, thei schulden haue left a clustre; if theues in the niyt, thei schulden haue rauyschid that that suffiside to hem.
10 Lakini nitamvua Esau nguo abaki uchi, nitayafunua maficho yake, ili asiweze kujificha. Watoto wake, jamaa na majirani wataangamia, naye hatakuwepo tena.
Forsothe Y haue vnhilid Esau, and Y haue schewid the hid thingis of hym, and he mai not mow be hid; his seed is distried, and hise britheren, and hise neiyboris, and it schal not be.
11 Waache yatima wako; nitayalinda maisha yao. Wajane wako pia wanaweza kunitumaini mimi.”
Forsake thi fadirles children, and Y schal make hem to lyue, and thi widewis schulen hope in me.
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama wale wasiostahili kukinywea kikombe ni lazima wakinywe, kwa nini wewe usiadhibiwe? Hutakwepa kuadhibiwa, ni lazima ukinywe.
For the Lord seith these thingis, Lo! thei drynkynge schulen drynke, to whiche was no doom, that thei schulden drynke the cuppe. And `schalt thou be left as innocent? thou schalt not be innocent, but thou drynkynge schalt drynke.
13 Ninaapa kwa nafsi yangu,” asema Bwana, “kwamba Bosra utakuwa magofu na kitu cha kutisha, cha aibu na cha kulaania; miji yake yote itakuwa magofu milele.”
For Y swoor bi my silf, seith the Lord, that Bosra schal be in to wildirnesse, and in to schenschipe, and in to forsakyng, and in to cursyng; and alle the citees therof schulen be in to euerlastynge wildirnessis.
14 Nimesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Jikusanyeni ili kuushambulia! Inukeni kwa ajili ya vita!”
I herde an heryng of the Lord, and Y am sent a messanger to hethene men; be ye gaderid togidere, and come ye ayens it, and rise we togidere in to batel.
15 “Sasa nitakufanya uwe mdogo miongoni mwa mataifa, aliyedharauliwa miongoni mwa watu.
For lo! Y haue youe thee a litil oon among hethene men, despisable among men.
16 Vitisho vyako na kiburi cha moyo wako vimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba, wewe unayedumu katika miinuko ya kilima. Ujapojenga kiota chako juu sana kama cha tai, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
Thi boost, and the pride of thin herte, hath disseyued thee, that dwellist in the caues of stoon, and enforsist to take the hiynesse of a litil hil; whanne thou as an egle hast reisid thi nest, fro thennus Y schal drawe thee doun, seith the Lord.
17 “Edomu atakuwa kitu cha kuogofya; wote wapitao karibu watashangaa na kuzomea kwa sababu ya majeraha yake yote.
And Ydumee schal be forsakun; ech man that schal passe bi it, schal wondre, and schal hisse on alle the woundis therof;
18 Kama vile Sodoma na Gomora zilivyoangamizwa, pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
as Sodom and Gommor is distried, and the niy citees therof, seith the Lord. A man schal not dwelle there, and the sone of man schal not enhabite it.
19 “Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Edomu kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
Lo! as a lioun he schal stie, fro the pride of Jordan to the strong fairnesse; for Y schal make hym renne sudenli to it; and who schal be the chosun man, whom Y schal sette bifore hym? For who is lijk to me, and who schal suffre me? and who is this scheepherde, that schal ayenstonde my cheer?
20 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Edomu, kile alichokusudia dhidi ya wale waishio Temani: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali; yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
Therfor here ye the councel of the Lord, which he took of Edom, and his thouytis, whiche he thouyte of the dwelleris of Theman. If the litle of the floc caste not hem doun, if thei distrien not with hem the dwellyng of hem, ellis no man yyue credence to me.
21 Kwa sauti ya anguko lao, dunia itatetemeka. Kilio chao kitasikika hadi Bahari ya Shamu.
The erthe was mouyd of the vois of fallyng of hem; the cry of vois therof was herd in the reed see.
22 Tazama! Tai atapaa juu angani na kuruka chini kwa ghafula, akitandaza mabawa yake juu ya Bosra. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Lo! as an egle he schal stie, and fle out, and he schal sprede abrood hise wynges on Bosra; and the herte of the strong men of Idumee schal be in that dai, as the herte of a womman trauelynge of child.
23 Kuhusu Dameski: “Hamathi na Arpadi imetahayarika, kwa kuwa wamesikia habari mbaya. Wamevunjika moyo na wametaabika kama bahari iliyochafuka.
To Damask. Emath is schent, and Arphath, for thei herden a ful wickid heryng; thei weren disturblid in the see, for angwisch thei miyten not haue reste.
24 Dameski amedhoofika, amegeuka na kukimbia, hofu ya ghafula imemkamata sana; amepatwa na uchungu na maumivu, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Damask was discoumfortid, it was turned in to fliyt; tremblyng took it, angwischis and sorewis helden it, as a womman trauelynge of child.
25 Kwa nini mji ambao unajulikana haujaachwa, mji ambao ninaupenda?
How forsoken thei a preisable citee, the citee of gladnesse?
26 Hakika, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku hiyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Therfor the yonge men therof schulen falle in the stretis therof, and alle men of batel schulen be stille in that dai, seith the Lord of oostis.
27 “Nitatia moto kuta za Dameski; utaangamiza ngome za Ben-Hadadi.”
And Y schal kyndle fier in the wal of Damask, and it schal deuoure the bildyngis of Benadab.
28 Kuhusu Kedari na falme za Hazori, ambazo Nebukadneza mfalme wa Babeli alizishambulia: Hili ndilo asemalo Bwana: “Inuka, ushambulie Kedari na kuwaangamiza watu wa mashariki.
To Cedar, and to the rewme of Azor, which Nabugodonosor, kyng of Babiloyne, smoot, the Lord seith these thingis. Rise ye, and stie to Cedar, and distrie ye the sones of the eest.
29 Hema zao na makundi yao ya kondoo yatachukuliwa; vibanda vyao vitatwaliwa pamoja na mali zao zote na ngamia zao. Watu watawapigia kelele, ‘Hofu kuu iko kila upande!’
Thei schulen take the tabernaclis of hem, and the flockis of hem; thei schulen take to hem the skynnes of hem, and alle the vessels of hem, and the camels of hem; and thei schulen clepe on hem inward drede in cumpas.
30 “Kimbieni haraka! Kaeni kwenye mapango marefu sana, ninyi mkaao Hazori,” asema Bwana. “Nebukadneza, mfalme wa Babeli amepanga shauri baya dhidi yenu; amebuni hila dhidi yenu.
Fle ye, go ye awei greetli, ye that dwellen in Asor, sitte in swolewis, seith the Lord. For whi Nabugodonosor, kyng of Babiloyne, hath take councel ayens you, and he thouyte thouytis ayens you.
31 “Inuka na ulishambulie taifa lililo starehe, linaloishi kwa kujiamini,” asema Bwana, “taifa lisilo na malango wala makomeo; watu wake huishi peke yao.
Rise ye togidere, and stie ye to a pesible folk, and dwellinge tristili, seith the Lord; not doris nether barris ben to it, thei dwellen aloone.
32 Ngamia wao watakuwa nyara, nayo makundi yao makubwa ya ngʼombe yatatekwa. Wale walio maeneo ya mbali nitawatawanya pande zote, nami nitaleta maafa juu yao kutoka kila upande,” asema Bwana.
And the camels of hem schulen be in to rauyschyng, and the multitude of her beestis in to prey; and Y schal schatere hem in to ech wynd, that ben biclippid on the long heer, and bi ech coost of hem Y schal brynge perischyng on hem, seith the Lord.
33 “Hazori itakuwa makao ya mbweha, mahali pa ukiwa milele. Hakuna yeyote atakayeishi humo; hakuna mtu atakayekaa ndani yake.”
And Asor schal be in to a dwellyng place of dragouns; it schal be forsakun `til in to withouten ende; a man schal not dwelle there, nether the sone of man schal enhabite it.
34 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Elamu, mapema katika utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda:
The word of the Lord that was maad to Jeremye, the profete, ayens Elam, in the bigynnyng of the rewme of Sedechie,
35 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama, nitavunja upinde wa Elamu, ulio tegemeo la nguvu zao.
kyng of Juda, and seide, The Lord of oostis, God of Israel, seith these thingis, Lo! Y schal breke the bowe of Elam, and Y schal take the strengthe of hem.
36 Nitaleta pepo nne dhidi ya Elamu toka pande nne za mbingu, nitawatawanya katika hizo pande nne, wala hapatakuwa na taifa ambalo watu wa Elamu waliofukuzwa hawatakwenda.
And I schal bringe on Elam foure wyndis; fro foure coostis of heuene, and Y schal wyndewe hem in to alle these wyndis, and no folc schal be, to which the fleeris of Elam schulen not come.
37 Nitamfadhaisha Elamu mbele ya adui zao, mbele yao wale wanaotafuta uhai wao; nitaleta maafa juu yao, naam, hasira yangu kali,” asema Bwana. “Nitawafuatia kwa upanga mpaka nitakapowamaliza.
And Y schal make Elam for to drede bifore her enemyes, and in the siyt of men sekynge the lijf of hem; and Y schal brynge on hem yuel, the wraththe of my strong veniaunce, seith the Lord; and Y schal sende after hem a swerd, til Y waste hem.
38 Nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme wake na maafisa wake,” asema Bwana.
And Y schal sette my kyngis seete in Elam, and Y schal leese therof kyngis, and princes, seith the Lord.
39 “Lakini nitarudisha mateka wa Elamu katika siku zijazo,” asema Bwana.
But in the laste daies Y schal make the prisoneris of Elam to turne ayen, seith the Lord.

< Yeremia 49 >