< Yeremia 49 >

1 Kuhusu Waamoni: Hili ndilo asemalo Bwana: “Je, Israeli hana wana? Je, hana warithi? Kwa nini basi Moleki amechukua milki ya Gadi? Kwa nini watu wake wanaishi katika miji yake?
Concerning the sons of Ammon: “Thus said YHWH: Has Israel no sons? Has he no heir? Why has Malcam possessed Gad, And his people have dwelt in its cities?
2 Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapopiga kelele ya vita dhidi ya Raba mji wa Waamoni; utakuwa kilima cha magofu, navyo vijiji vinavyouzunguka vitateketezwa kwa moto. Kisha Israeli atawafukuza wale waliomfukuza,” asema Bwana.
Therefore, behold, days are coming, A declaration of YHWH, And I have sounded a shout of battle in Rabbah of the sons of Ammon, And it has been for a heap—a desolation, And her daughters are burned with fire, And Israel has succeeded its heirs, said YHWH.
3 “Lia kwa huzuni, ee Heshboni, kwa kuwa Ai umeangamizwa! Pigeni kelele, enyi wakazi wa Raba! Vaeni nguo za gunia na kuomboleza, kimbieni hapa na pale ndani ya kuta, kwa kuwa Moleki atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na makuhani na maafisa wake.
Howl, Heshbon, for Ai is spoiled, Cry, daughters of Rabbah, gird on sackcloth, Lament, and go to and fro by the hedges, For Malcam goes into captivity, His priests and his princes together.
4 Kwa nini unajivunia mabonde yako, kujivunia mabonde yako yaliyozaa sana? Ee binti usiye mwaminifu, unayeutumainia utajiri wako na kusema, ‘Ni nani atakayenishambulia?’
Why do you boast yourself in valleys? Your valley is flowing, O backsliding daughter, Who is trusting in her treasures: Who comes to me?
5 Nitaleta hofu kuu juu yako kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Kila mmoja wenu ataondolewa, wala hakuna hata mmoja atakayekusanya wakimbizi.
Behold, I am bringing fear in on you, A declaration of Lord YHWH of Hosts, From all around you, And you have each been driven out before it, And there is no gatherer of the wandering.
6 “Lakini hatimaye, nitarudisha mateka wa Waamoni,” asema Bwana.
And after this I return the captivity of the sons of Ammon, A declaration of YHWH.”
7 Kuhusu Edomu: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Je, hakuna tena hekima katika Temani? Je, shauri limewapotea wenye busara? Je, hekima yao imechakaa?
Concerning Edom: “Thus said YHWH of Hosts: Is wisdom no longer in Teman? Has counsel perished from the intelligent? Has their wisdom vanished?
8 Geuka na ukimbie, jifiche katika mapango marefu kabisa, wewe uishiye Dedani, kwa kuwa nitaleta maafa juu ya Esau wakati nitakapomwadhibu.
Flee, turn, go deep to dwell, you inhabitants of Dedan, For I brought the calamity of Esau on him, The time I inspected him.
9 Je, kama wachuma zabibu wangekuja kwako, wasingebakiza zabibu chache? Kama wezi wangekujia usiku, je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji?
If gatherers have come to you, They do not leave gleanings, If thieves in the night, They have destroyed their sufficiency!
10 Lakini nitamvua Esau nguo abaki uchi, nitayafunua maficho yake, ili asiweze kujificha. Watoto wake, jamaa na majirani wataangamia, naye hatakuwepo tena.
For I have made Esau bare, I have uncovered his secret places, And he is not able to be hidden, Spoiled [is] his seed, and his brothers, And his neighbors, and he is not.
11 Waache yatima wako; nitayalinda maisha yao. Wajane wako pia wanaweza kunitumaini mimi.”
Leave your orphans—I keep alive, And your widows—trust on Me,
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama wale wasiostahili kukinywea kikombe ni lazima wakinywe, kwa nini wewe usiadhibiwe? Hutakwepa kuadhibiwa, ni lazima ukinywe.
For thus said YHWH: They whose judgment is not to drink of the cup, Do certainly drink, And you [are] he that is entirely acquitted! You are not acquitted, for you certainly drink.
13 Ninaapa kwa nafsi yangu,” asema Bwana, “kwamba Bosra utakuwa magofu na kitu cha kutisha, cha aibu na cha kulaania; miji yake yote itakuwa magofu milele.”
For I have sworn by Myself, A declaration of YHWH, That for a desolation, for a reproach, For a dry place, and for a reviling—is Bozrah, And all her cities are for continuous ruins.
14 Nimesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Jikusanyeni ili kuushambulia! Inukeni kwa ajili ya vita!”
I have heard a report from YHWH, And an ambassador is sent among nations, Gather yourselves and come in against her, And rise for battle.
15 “Sasa nitakufanya uwe mdogo miongoni mwa mataifa, aliyedharauliwa miongoni mwa watu.
For behold, I have made you little among nations, Despised among men.
16 Vitisho vyako na kiburi cha moyo wako vimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba, wewe unayedumu katika miinuko ya kilima. Ujapojenga kiota chako juu sana kama cha tai, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
Your terribleness has lifted you up, The pride of your heart, O dweller in clefts of the rock, Holding the high place of the height, For you make your nest high as an eagle, From there I bring you down, A declaration of YHWH.
17 “Edomu atakuwa kitu cha kuogofya; wote wapitao karibu watashangaa na kuzomea kwa sababu ya majeraha yake yote.
And Edom has been for a desolation, Everyone passing by her is astonished, And hisses because of all her plagues.
18 Kama vile Sodoma na Gomora zilivyoangamizwa, pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
As the overthrow of Sodom and Gomorrah, And its neighbors, said YHWH, No one dwells there, Nor does a son of man sojourn in her.
19 “Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Edomu kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
Behold, he comes up as a lion, Because of the rising of the Jordan, To the enduring habitation, But I cause to rest, I cause him to run from off her, And who is chosen? I lay a charge concerning her, For who is like Me? And who convenes Me? And who [is] this shepherd who stands before Me?
20 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Edomu, kile alichokusudia dhidi ya wale waishio Temani: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali; yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
Therefore, hear the counsel of YHWH, That He has counseled concerning Edom, And His plans that He has devised Concerning the inhabitants of Teman: Do little ones of the flock not drag them out, Does He not make their habitation desolate?
21 Kwa sauti ya anguko lao, dunia itatetemeka. Kilio chao kitasikika hadi Bahari ya Shamu.
The earth has shaken from the noise of their fall, The cry—its voice is heard at the Sea of Suph.
22 Tazama! Tai atapaa juu angani na kuruka chini kwa ghafula, akitandaza mabawa yake juu ya Bosra. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Behold, He comes up as an eagle, and flies, And He spreads His wings over Bozrah, And the heart of the mighty of Edom has been in that day, As the heart of a travailing woman.”
23 Kuhusu Dameski: “Hamathi na Arpadi imetahayarika, kwa kuwa wamesikia habari mbaya. Wamevunjika moyo na wametaabika kama bahari iliyochafuka.
Concerning Damascus: “Hamath and Arpad have been ashamed, For they have heard an evil report, They have been melted, sorrow [is] in the sea, It is not able to be quiet.
24 Dameski amedhoofika, amegeuka na kukimbia, hofu ya ghafula imemkamata sana; amepatwa na uchungu na maumivu, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Damascus has been feeble, She turned to flee, and fear strengthened her, Distress and pangs have seized her, as a travailing woman.
25 Kwa nini mji ambao unajulikana haujaachwa, mji ambao ninaupenda?
How it is not left—the city of praise, The city of My joy!
26 Hakika, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku hiyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Therefore her young men fall in her broad places, And all the men of war are cut off in that day, A declaration of YHWH of Hosts.
27 “Nitatia moto kuta za Dameski; utaangamiza ngome za Ben-Hadadi.”
And I have kindled a fire against the wall of Damascus, And it consumed palaces of Ben-Hadad!”
28 Kuhusu Kedari na falme za Hazori, ambazo Nebukadneza mfalme wa Babeli alizishambulia: Hili ndilo asemalo Bwana: “Inuka, ushambulie Kedari na kuwaangamiza watu wa mashariki.
Concerning Kedar, and concerning the kingdoms of Hazor that Nebuchadnezzar king of Babylon has struck: “Thus said YHWH: Arise, go up to Kedar, And spoil the sons of the east.
29 Hema zao na makundi yao ya kondoo yatachukuliwa; vibanda vyao vitatwaliwa pamoja na mali zao zote na ngamia zao. Watu watawapigia kelele, ‘Hofu kuu iko kila upande!’
They take their tents and their flock, Their curtains, and all their vessels, And they carry away their camels for themselves, And they called concerning them, Fear [is] all around.
30 “Kimbieni haraka! Kaeni kwenye mapango marefu sana, ninyi mkaao Hazori,” asema Bwana. “Nebukadneza, mfalme wa Babeli amepanga shauri baya dhidi yenu; amebuni hila dhidi yenu.
Flee, bemoan mightily, go deep to dwell, You inhabitants of Hazor—a declaration of YHWH, For Nebuchadnezzar king of Babylon has given counsel against you, Indeed, he devises a scheme against them.
31 “Inuka na ulishambulie taifa lililo starehe, linaloishi kwa kujiamini,” asema Bwana, “taifa lisilo na malango wala makomeo; watu wake huishi peke yao.
Rise, go up to a nation at rest, Dwelling confidently, a declaration of YHWH, It has no double gates nor bar, They dwell alone.
32 Ngamia wao watakuwa nyara, nayo makundi yao makubwa ya ngʼombe yatatekwa. Wale walio maeneo ya mbali nitawatawanya pande zote, nami nitaleta maafa juu yao kutoka kila upande,” asema Bwana.
And their camels have been for a prey, And the multitude of their livestock for a spoil, And I have scattered them to every wind, Who cut off the corner [of the beard], And from all its passages I bring in their calamity, A declaration of YHWH.
33 “Hazori itakuwa makao ya mbweha, mahali pa ukiwa milele. Hakuna yeyote atakayeishi humo; hakuna mtu atakayekaa ndani yake.”
And Hazor has been for a habitation of dragons, A desolation for all time, No one dwells there, nor does a son of man sojourn in it!”
34 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Elamu, mapema katika utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda:
That which has been the word of YHWH to Jeremiah the prophet concerning Elam, in the beginning of the reign of Zedekiah king of Judah, saying,
35 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama, nitavunja upinde wa Elamu, ulio tegemeo la nguvu zao.
“Thus said YHWH of Hosts: Behold, I am breaking the bow of Elam, The beginning of their might.
36 Nitaleta pepo nne dhidi ya Elamu toka pande nne za mbingu, nitawatawanya katika hizo pande nne, wala hapatakuwa na taifa ambalo watu wa Elamu waliofukuzwa hawatakwenda.
And I have brought four winds to Elam, From the four ends of the heavens, And have scattered them to all these winds, And there is no nation to where outcasts of Elam do not come in.
37 Nitamfadhaisha Elamu mbele ya adui zao, mbele yao wale wanaotafuta uhai wao; nitaleta maafa juu yao, naam, hasira yangu kali,” asema Bwana. “Nitawafuatia kwa upanga mpaka nitakapowamaliza.
And I have frightened Elam before their enemies, And before those seeking their life, And I have brought calamity on them, The heat of My anger, A declaration of YHWH, And I have sent the sword after them, Until I have consumed them;
38 Nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme wake na maafisa wake,” asema Bwana.
And I have set My throne in Elam, And I have destroyed king and princes from there, A declaration of YHWH.
39 “Lakini nitarudisha mateka wa Elamu katika siku zijazo,” asema Bwana.
And it has come to pass, in the latter end of the days, I return the captivity of Elam, A declaration of YHWH!”

< Yeremia 49 >