< Yeremia 49 >

1 Kuhusu Waamoni: Hili ndilo asemalo Bwana: “Je, Israeli hana wana? Je, hana warithi? Kwa nini basi Moleki amechukua milki ya Gadi? Kwa nini watu wake wanaishi katika miji yake?
Of the children of Ammon. Thus saith the LORD: Hath Israel no sons? Hath he no heir? Why then doth Malcam take possession of Gad, and his people dwell in the cities thereof?
2 Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapopiga kelele ya vita dhidi ya Raba mji wa Waamoni; utakuwa kilima cha magofu, navyo vijiji vinavyouzunguka vitateketezwa kwa moto. Kisha Israeli atawafukuza wale waliomfukuza,” asema Bwana.
Therefore, behold, the days come, saith the LORD, that I will cause an alarm of war to be heard against Rabbah of the children of Ammon; and it shall become a desolate mound, and her daughters shall be burned with fire; then shall Israel dispossess them that did dispossess him, saith the LORD.
3 “Lia kwa huzuni, ee Heshboni, kwa kuwa Ai umeangamizwa! Pigeni kelele, enyi wakazi wa Raba! Vaeni nguo za gunia na kuomboleza, kimbieni hapa na pale ndani ya kuta, kwa kuwa Moleki atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na makuhani na maafisa wake.
Wail, O Heshbon, for Ai is undone; cry, ye daughters of Rabbah, gird you with sackcloth; lament, and run to and fro among the folds; for Malcam shall go into captivity, his priests and his princes together.
4 Kwa nini unajivunia mabonde yako, kujivunia mabonde yako yaliyozaa sana? Ee binti usiye mwaminifu, unayeutumainia utajiri wako na kusema, ‘Ni nani atakayenishambulia?’
Wherefore gloriest thou in the valleys, thy flowing valley, O backsliding daughter? that didst trust in thy treasures: 'Who shall come unto me?'
5 Nitaleta hofu kuu juu yako kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Kila mmoja wenu ataondolewa, wala hakuna hata mmoja atakayekusanya wakimbizi.
Behold, I will bring a terror upon thee, saith the Lord GOD of hosts, from all that are round about thee; and ye shall be driven out every man right forth, and there shall be none to gather up him that wandereth.
6 “Lakini hatimaye, nitarudisha mateka wa Waamoni,” asema Bwana.
But afterward I will bring back the captivity of the children of Ammon, saith the LORD.
7 Kuhusu Edomu: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Je, hakuna tena hekima katika Temani? Je, shauri limewapotea wenye busara? Je, hekima yao imechakaa?
Of Edom. Thus saith the LORD of hosts: Is wisdom no more in Teman? Is counsel perished from the prudent? Is their wisdom vanished?
8 Geuka na ukimbie, jifiche katika mapango marefu kabisa, wewe uishiye Dedani, kwa kuwa nitaleta maafa juu ya Esau wakati nitakapomwadhibu.
Flee ye, turn back, dwell deep, O inhabitants of Dedan; For I do bring the calamity of Esau upon him, the time that I shall punish him.
9 Je, kama wachuma zabibu wangekuja kwako, wasingebakiza zabibu chache? Kama wezi wangekujia usiku, je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji?
If grape-gatherers came to thee, would they not leave some gleaning grapes? if thieves by night, would they not destroy till they had enough?
10 Lakini nitamvua Esau nguo abaki uchi, nitayafunua maficho yake, ili asiweze kujificha. Watoto wake, jamaa na majirani wataangamia, naye hatakuwepo tena.
But I have made Esau bare, I have uncovered his secret places, and he shall not be able to hide himself; his seed is spoiled, and his brethren, and his neighbours, and he is not.
11 Waache yatima wako; nitayalinda maisha yao. Wajane wako pia wanaweza kunitumaini mimi.”
Leave thy fatherless children, I will rear them, and let thy widows trust in Me.
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama wale wasiostahili kukinywea kikombe ni lazima wakinywe, kwa nini wewe usiadhibiwe? Hutakwepa kuadhibiwa, ni lazima ukinywe.
For thus saith the LORD: Behold, they to whom it pertained not to drink of the cup shall assuredly drink; and art thou he that shall altogether go unpunished? thou shalt not go unpunished, but thou shalt surely drink.
13 Ninaapa kwa nafsi yangu,” asema Bwana, “kwamba Bosra utakuwa magofu na kitu cha kutisha, cha aibu na cha kulaania; miji yake yote itakuwa magofu milele.”
For I have sworn by Myself, saith the LORD, that Bozrah shall become an astonishment, a reproach, a waste, and a curse; and all the cities thereof shall be perpetual wastes.
14 Nimesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Jikusanyeni ili kuushambulia! Inukeni kwa ajili ya vita!”
I have heard a message from the LORD, and an ambassador is sent among the nations: 'Gather yourselves together, and come against her, and rise up to the battle.'
15 “Sasa nitakufanya uwe mdogo miongoni mwa mataifa, aliyedharauliwa miongoni mwa watu.
For, behold, I make thee small among the nations, and despised among men.
16 Vitisho vyako na kiburi cha moyo wako vimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba, wewe unayedumu katika miinuko ya kilima. Ujapojenga kiota chako juu sana kama cha tai, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
Thy terribleness hath deceived thee, even the pride of thy heart, O thou that dwellest in the clefts of the rock, that holdest the height of the hill; though thou shouldest make thy nest as high as the eagle, I will bring thee down from thence, saith the LORD.
17 “Edomu atakuwa kitu cha kuogofya; wote wapitao karibu watashangaa na kuzomea kwa sababu ya majeraha yake yote.
And Edom shall become an astonishment; every one that passeth by it shall be astonished and shall hiss at all the plagues thereof.
18 Kama vile Sodoma na Gomora zilivyoangamizwa, pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
As in the overthrow of Sodom and Gomorrah and the neighbour cities thereof, saith the LORD, no man shall abide there, neither shall any son of man dwell therein.
19 “Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Edomu kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
Behold, he shall come up like a lion from the thickets of the Jordan against the strong habitation; for I will suddenly make him run away from it, and whoso is chosen, him will I appoint over it; for who is like Me? and who will appoint Me a time? and who is that shepherd that will stand before Me?
20 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Edomu, kile alichokusudia dhidi ya wale waishio Temani: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali; yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
Therefore hear ye the counsel of the LORD, that He hath taken against Edom; and His purposes, that He hath purposed against the inhabitants of Teman: Surely the least of the flock shall drag them away, surely their habitation shall be appalled at them.
21 Kwa sauti ya anguko lao, dunia itatetemeka. Kilio chao kitasikika hadi Bahari ya Shamu.
The earth quaketh at the noise of their fall; there is a cry, the noise whereof is heard in the Red Sea.
22 Tazama! Tai atapaa juu angani na kuruka chini kwa ghafula, akitandaza mabawa yake juu ya Bosra. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Behold, he shall come up and swoop down as the vulture, and spread out his wings against Bozrah; and the heart of the mighty men of Edom at that day shall be as the heart of a woman in her pangs.
23 Kuhusu Dameski: “Hamathi na Arpadi imetahayarika, kwa kuwa wamesikia habari mbaya. Wamevunjika moyo na wametaabika kama bahari iliyochafuka.
Of Damascus. Hamath is ashamed, and Arpad; for they have heard evil tidings, they are melted away; there is trouble in the sea; it cannot be quiet.
24 Dameski amedhoofika, amegeuka na kukimbia, hofu ya ghafula imemkamata sana; amepatwa na uchungu na maumivu, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Damascus is waxed feeble, she turneth herself to flee, and trembling hath seized on her; anguish and pangs have taken hold of her, as of a woman in travail.
25 Kwa nini mji ambao unajulikana haujaachwa, mji ambao ninaupenda?
'How is the city of praise left unrepaired, the city of my joy?'
26 Hakika, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku hiyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Therefore her young men shall fall in her broad places, and all the men of war shall be brought to silence in that day, saith the LORD of hosts.
27 “Nitatia moto kuta za Dameski; utaangamiza ngome za Ben-Hadadi.”
And I will kindle a fire in the wall of Damascus, and it shall devour the palaces of Ben-hadad.
28 Kuhusu Kedari na falme za Hazori, ambazo Nebukadneza mfalme wa Babeli alizishambulia: Hili ndilo asemalo Bwana: “Inuka, ushambulie Kedari na kuwaangamiza watu wa mashariki.
Of Kedar, and of the kingdoms of Hazor, which Nebuchadrezzar king of Babylon smote. Thus saith the LORD: Arise ye, go up against Kedar, and spoil the children of the east.
29 Hema zao na makundi yao ya kondoo yatachukuliwa; vibanda vyao vitatwaliwa pamoja na mali zao zote na ngamia zao. Watu watawapigia kelele, ‘Hofu kuu iko kila upande!’
Their tents and their flocks shall they take, they shall carry away for themselves their curtains, and all their vessels, and their camels; and they shall proclaim against them a terror on every side.
30 “Kimbieni haraka! Kaeni kwenye mapango marefu sana, ninyi mkaao Hazori,” asema Bwana. “Nebukadneza, mfalme wa Babeli amepanga shauri baya dhidi yenu; amebuni hila dhidi yenu.
Flee ye, flit far off, dwell deep, O ye inhabitants of Hazor, saith the LORD; for Nebuchadrezzar king of Babylon hath taken counsel against you, and hath conceived a purpose against you.
31 “Inuka na ulishambulie taifa lililo starehe, linaloishi kwa kujiamini,” asema Bwana, “taifa lisilo na malango wala makomeo; watu wake huishi peke yao.
Arise, get you up against a nation that is at ease, that dwelleth without care, saith the LORD; that have neither gates nor bars, that dwell alone.
32 Ngamia wao watakuwa nyara, nayo makundi yao makubwa ya ngʼombe yatatekwa. Wale walio maeneo ya mbali nitawatawanya pande zote, nami nitaleta maafa juu yao kutoka kila upande,” asema Bwana.
And their camels shall be a booty, and the multitude of their cattle a spoil; and I will scatter unto all winds them that have the corners polled; and I will bring their calamity from every side of them, saith the LORD.
33 “Hazori itakuwa makao ya mbweha, mahali pa ukiwa milele. Hakuna yeyote atakayeishi humo; hakuna mtu atakayekaa ndani yake.”
And Hazor shall be a dwelling-place of jackals, a desolation for ever; no man shall abide there, neither shall any son of man dwell therein.
34 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Elamu, mapema katika utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda:
The word of the LORD that came to Jeremiah the prophet concerning Elam in the beginning of the reign of Zedekiah king of Judah, saying:
35 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama, nitavunja upinde wa Elamu, ulio tegemeo la nguvu zao.
Thus saith the LORD of hosts: Behold, I will break the bow of Elam, the chief of their might.
36 Nitaleta pepo nne dhidi ya Elamu toka pande nne za mbingu, nitawatawanya katika hizo pande nne, wala hapatakuwa na taifa ambalo watu wa Elamu waliofukuzwa hawatakwenda.
And I will bring against Elam the four winds from the four quarters of heaven, and will scatter them toward all those winds; and there shall be no nation whither the dispersed of Elam shall not come.
37 Nitamfadhaisha Elamu mbele ya adui zao, mbele yao wale wanaotafuta uhai wao; nitaleta maafa juu yao, naam, hasira yangu kali,” asema Bwana. “Nitawafuatia kwa upanga mpaka nitakapowamaliza.
And I will cause Elam to be dismayed before their enemies, and before them that seek their life; and I will bring evil upon them, even My fierce anger, saith the LORD; and I will send the sword after them, till I have consumed them;
38 Nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme wake na maafisa wake,” asema Bwana.
And I will set My throne in Elam, and will destroy from thence king and princes, saith the LORD.
39 “Lakini nitarudisha mateka wa Elamu katika siku zijazo,” asema Bwana.
But it shall come to pass in the end of days, that I will bring back the captivity of Elam, saith the LORD.

< Yeremia 49 >