< Yeremia 49 >

1 Kuhusu Waamoni: Hili ndilo asemalo Bwana: “Je, Israeli hana wana? Je, hana warithi? Kwa nini basi Moleki amechukua milki ya Gadi? Kwa nini watu wake wanaishi katika miji yake?
Against the children of Ammon. Thus saith the Lord: Hath Israel no sons? or hath he no heir? Why then hath Melchom inherited Gad: and his people dwelt in his cities?
2 Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapopiga kelele ya vita dhidi ya Raba mji wa Waamoni; utakuwa kilima cha magofu, navyo vijiji vinavyouzunguka vitateketezwa kwa moto. Kisha Israeli atawafukuza wale waliomfukuza,” asema Bwana.
Therefore behold the days come, saith the Lord, and I will cause the noise of war to be heard in Rabbath of the children of Ammon, and it shall be destroyed into a heap, and her daughters shall be burnt with fire, and Israel shall possess them that have possessed him, saith the Lord.
3 “Lia kwa huzuni, ee Heshboni, kwa kuwa Ai umeangamizwa! Pigeni kelele, enyi wakazi wa Raba! Vaeni nguo za gunia na kuomboleza, kimbieni hapa na pale ndani ya kuta, kwa kuwa Moleki atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na makuhani na maafisa wake.
Howl, O Hesebon, for Hai is wasted. Cry, ye daughters of Rabbath, gird yourselves with haircloth: mourn and go about by the hedges: for Melchom shall be carried into captivity, his priests, and his princes together.
4 Kwa nini unajivunia mabonde yako, kujivunia mabonde yako yaliyozaa sana? Ee binti usiye mwaminifu, unayeutumainia utajiri wako na kusema, ‘Ni nani atakayenishambulia?’
Why gloriest thou in the valleys? thy valley hath flowed away, O delicate daughter, that hast trusted in thy treasures, and hast said: Who shall come to me?
5 Nitaleta hofu kuu juu yako kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Kila mmoja wenu ataondolewa, wala hakuna hata mmoja atakayekusanya wakimbizi.
Behold I will bring a fear upon thee, saith the Lord God of hosts, from all that are round about thee: and you shall be scattered every one out of one another’s sight, neither shall there be any to gather together them that flee.
6 “Lakini hatimaye, nitarudisha mateka wa Waamoni,” asema Bwana.
And afterwards I will cause the captives of the children of Ammon to return, saith the Lord.
7 Kuhusu Edomu: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Je, hakuna tena hekima katika Temani? Je, shauri limewapotea wenye busara? Je, hekima yao imechakaa?
Against Edom. Thus saith the Lord of hosts: Is wisdom no more in Theman? counsel is perished from her children: their wisdom is become unprofitable.
8 Geuka na ukimbie, jifiche katika mapango marefu kabisa, wewe uishiye Dedani, kwa kuwa nitaleta maafa juu ya Esau wakati nitakapomwadhibu.
Flee and turn your backs, go down into the deep hole, ye inhabitants of Dedan: for I have brought the destruction of Esau upon him, the time of his visitation.
9 Je, kama wachuma zabibu wangekuja kwako, wasingebakiza zabibu chache? Kama wezi wangekujia usiku, je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji?
If grapegatherers had come to thee, would they not have left a bunch? if thieves in the night, they would have taken what was enough for them.
10 Lakini nitamvua Esau nguo abaki uchi, nitayafunua maficho yake, ili asiweze kujificha. Watoto wake, jamaa na majirani wataangamia, naye hatakuwepo tena.
But I have made Esau bare, I have revealed his secrets, and he cannot be hid: his seed is laid waste, and his brethren, and his neighbours, and he shall not be.
11 Waache yatima wako; nitayalinda maisha yao. Wajane wako pia wanaweza kunitumaini mimi.”
Leave thy fatherless children: I will make them live: and thy widows shall hope in me.
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama wale wasiostahili kukinywea kikombe ni lazima wakinywe, kwa nini wewe usiadhibiwe? Hutakwepa kuadhibiwa, ni lazima ukinywe.
For thus saith the Lord: Behold they whose judgment was not to drink of the cup, shall certainly drink: and shalt thou come off as innocent? thou shalt not come off as innocent, but drinking thou shalt drink.
13 Ninaapa kwa nafsi yangu,” asema Bwana, “kwamba Bosra utakuwa magofu na kitu cha kutisha, cha aibu na cha kulaania; miji yake yote itakuwa magofu milele.”
For I have sworn by myself, saith the Lord, that Bosra shall become a desolation, and a reproach, and a desert, and a curse: and all her cities shall be everlasting wastes.
14 Nimesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Jikusanyeni ili kuushambulia! Inukeni kwa ajili ya vita!”
I have heard a rumour from the Lord, and an ambassador is sent to the nations: Gather yourselves together, and come against her, and let us rise up to battle.
15 “Sasa nitakufanya uwe mdogo miongoni mwa mataifa, aliyedharauliwa miongoni mwa watu.
For behold I have made thee a little one among the nations, despicable among men.
16 Vitisho vyako na kiburi cha moyo wako vimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba, wewe unayedumu katika miinuko ya kilima. Ujapojenga kiota chako juu sana kama cha tai, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
Thy arrogancy hath deceived thee, and the pride of thy heart: O thou that dwellest in the clefts of the rock, and endeavourest to lay hold on the height of the hill: but though thou shouldst make thy nest as high as an eagle, I will bring thee down from thence, saith the Lord.
17 “Edomu atakuwa kitu cha kuogofya; wote wapitao karibu watashangaa na kuzomea kwa sababu ya majeraha yake yote.
And Edom shall be desolate: every one that shall pass by it, shall be astonished, and shall hiss at all its plagues.
18 Kama vile Sodoma na Gomora zilivyoangamizwa, pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
As Sodom was overthrown and Gomorrha, and the neighbours thereof, saith the Lord: there shall not a man dwell there, and there shall no son of man inhabit it.
19 “Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Edomu kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
Behold one shall come up as a lion from the swelling of the Jordan, against the strong and beautiful: for I will make him run suddenly upon her: and who shall be the chosen one whom I may appoint over her? for who is like to me? and who shall abide me? and who is that shepherd that can withstand my countenance?
20 Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Edomu, kile alichokusudia dhidi ya wale waishio Temani: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali; yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
Therefore hear ye the counsel of the Lord, which he hath taken concerning Edom: and his thoughts which he hath thought concerning the inhabitants of Theman: surely the little ones of the flock shall cast them down, of a truth they shall destroy them with their habitation.
21 Kwa sauti ya anguko lao, dunia itatetemeka. Kilio chao kitasikika hadi Bahari ya Shamu.
The earth is moved at the noise of their fall: the cry of their voice is heard in the Red Sea.
22 Tazama! Tai atapaa juu angani na kuruka chini kwa ghafula, akitandaza mabawa yake juu ya Bosra. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Behold he shall come up as an eagle, and fly: and he shall spread his wings over Bosra: and in that day the heart of the valiant ones of Edom shall be as the heart of a woman in labour.
23 Kuhusu Dameski: “Hamathi na Arpadi imetahayarika, kwa kuwa wamesikia habari mbaya. Wamevunjika moyo na wametaabika kama bahari iliyochafuka.
Against Damascus. Emath is confounded and Arphad: for they have heard very bad tidings, they are troubled as in the sea: through care they could not rest.
24 Dameski amedhoofika, amegeuka na kukimbia, hofu ya ghafula imemkamata sana; amepatwa na uchungu na maumivu, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Damascus is undone, she is put to flight, trembling hath seized on her: anguish and sorrows have taken her as a woman in labour.
25 Kwa nini mji ambao unajulikana haujaachwa, mji ambao ninaupenda?
How have they forsaken the city of renown, the city of joy!
26 Hakika, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku hiyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Therefore her young men shall fall in her streets: and all the men of war shall be silent in that day, saith the Lord of hosts.
27 “Nitatia moto kuta za Dameski; utaangamiza ngome za Ben-Hadadi.”
And I will kindle a fire in the wall of Damascus, rind it shall devour the strong holds of Benadad.
28 Kuhusu Kedari na falme za Hazori, ambazo Nebukadneza mfalme wa Babeli alizishambulia: Hili ndilo asemalo Bwana: “Inuka, ushambulie Kedari na kuwaangamiza watu wa mashariki.
Against Cedar and against the kingdoms of Asor, which Nabuchodonosor king of Babylon destroyed. Thus saith the Lord: Arise, and go ye up to Cedar, and waste the children of the east.
29 Hema zao na makundi yao ya kondoo yatachukuliwa; vibanda vyao vitatwaliwa pamoja na mali zao zote na ngamia zao. Watu watawapigia kelele, ‘Hofu kuu iko kila upande!’
They shall take their tents, and their flocks: and shall carry off for themselves their curtains, and all their vessels, and their camels: and they shall call fear upon them round about.
30 “Kimbieni haraka! Kaeni kwenye mapango marefu sana, ninyi mkaao Hazori,” asema Bwana. “Nebukadneza, mfalme wa Babeli amepanga shauri baya dhidi yenu; amebuni hila dhidi yenu.
Flee ye, get away speedily, sit in deep holes, you that inhabit Asur, saith the Lord: for Nabuchodonosor king of Babylon hath taken counsel against you, and hath conceived designs against you.
31 “Inuka na ulishambulie taifa lililo starehe, linaloishi kwa kujiamini,” asema Bwana, “taifa lisilo na malango wala makomeo; watu wake huishi peke yao.
Arise, and so up to a nation that is at ease, and that dwelleth securely, saith the Lord: they have neither gates, nor bars: they dwell alone.
32 Ngamia wao watakuwa nyara, nayo makundi yao makubwa ya ngʼombe yatatekwa. Wale walio maeneo ya mbali nitawatawanya pande zote, nami nitaleta maafa juu yao kutoka kila upande,” asema Bwana.
And their camels shall be for a spoil, and the multitude of their cattle for a booty, and I will scatter into every wind them that have their hair cut round, and I will bring destruction upon them from I all their confines, saith the Lord.
33 “Hazori itakuwa makao ya mbweha, mahali pa ukiwa milele. Hakuna yeyote atakayeishi humo; hakuna mtu atakayekaa ndani yake.”
And Asor shall be a habitation for dragons, desolate for ever: no man shall abide there, nor son of man inhabit it.
34 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Elamu, mapema katika utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda:
The word of the Lord that came to Jeremias the prophet against Elam, in the beginning of the reign of Sedecias king of Juda, saying:
35 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama, nitavunja upinde wa Elamu, ulio tegemeo la nguvu zao.
Thus saith the Lord of hosts: Behold I will break the bow of Elam, and their chief strength.
36 Nitaleta pepo nne dhidi ya Elamu toka pande nne za mbingu, nitawatawanya katika hizo pande nne, wala hapatakuwa na taifa ambalo watu wa Elamu waliofukuzwa hawatakwenda.
And I will bring upon Elam the four winds from the fear quarters of heaven: and I will scatter them into all these winds: and there shall be no nation, to which the fugitives of Elam shall not come.
37 Nitamfadhaisha Elamu mbele ya adui zao, mbele yao wale wanaotafuta uhai wao; nitaleta maafa juu yao, naam, hasira yangu kali,” asema Bwana. “Nitawafuatia kwa upanga mpaka nitakapowamaliza.
And I will cause Elam to be afraid before their enemies, and in the sight of them that seek their life: and I will bring evil upon them, my fierce wrath, saith the Lord: and will send the sword after them, till I consume them.
38 Nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme wake na maafisa wake,” asema Bwana.
And I will set my throne in Elam, and destroy kings and princes from thence, saith the Lord.
39 “Lakini nitarudisha mateka wa Elamu katika siku zijazo,” asema Bwana.
But in the latter days I will cause the captives of Elam, to return, saith the Lord.

< Yeremia 49 >