< Yeremia 48 >
1 Kuhusu Moabu: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Ole wake Nebo, kwa maana utaharibiwa. Kiriathaimu utaaibishwa na kutekwa; Misgabu itaaibishwa na kuvunjavunjwa.
Moav'a ilişkin: İsrail'in Tanrısı, Her Şeye Egemen RAB şöyle diyor: “Vay Nevo'nun başına gelenlere! Çünkü viraneye çevrilecek. Kiryatayim utandırılacak, ele geçirilecek. Misgav utandırılacak, kırılıp dökülecek.
2 Moabu haitasifiwa tena; huko Heshboni watu watafanya shauri baya la anguko lake: ‘Njooni na tuangamize taifa lile.’ Wewe nawe, ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.
Moav artık övülmeyecek, Heşbon'da onun yıkımı için düzen kuracak, ‘Haydi, şu Moav ulusuna son verelim’ diyecekler. Ey Madmen, sen de susturulacaksın, Kılıç kovalayacak seni.
3 Sikiliza kilio kutoka Horonaimu, kilio cha maangamizi makuu na uharibifu.
Horonayim'den feryat duyulacak: ‘Kent mahvoldu, büyük yıkıma uğradı!’
4 Moabu utavunjwa, wadogo wake watapiga kelele.
“Moav yıkılacak, Yavrularının ağlayışı duyulacak.
5 Wanapanda kwenda njia ya kuelekea Luhithi, wakilia kwa uchungu wanapotembea, kwenye njia inayoshuka kwenda Horonaimu, kilio cha uchungu kwa ajili ya uharibifu kinasikika.
Ağlaya ağlaya çıkıyorlar Luhit Yokuşu'ndan, Horonayim inişinde Yıkımın neden olduğu acı feryatlar duyuluyor.
6 Kimbieni! Okoeni maisha yenu, kuweni kama kichaka jangwani.
Kaçın, canınızı kurtarın! Çölde yaban eşeği gibi koşun!
7 Kwa kuwa mmetumainia matendo yenu na mali zenu, ninyi pia mtachukuliwa mateka, naye Kemoshi atakwenda uhamishoni, pamoja na makuhani wake na maafisa wake.
“Evet, başarılarına, mal varlığına güvendiğin için Sen de ele geçirileceksin. İlahın Kemoş da kâhinleri ve görevlileriyle birlikte Sürgün edilecek.
8 Mharabu atakuja dhidi ya kila mji, wala hakuna mji utakaookoka. Bonde litaangamizwa na uwanda utaharibiwa, kwa sababu Bwana amesema.
Yok edici her kente uğrayacak, Tek kent kurtulmayacak. Vadi yerle bir olacak, Yayla altüst edilecek” diyor RAB.
9 Wekeni chumvi kwa ajili ya Moabu, kwa kuwa ataangamizwa; miji yake itakuwa ukiwa, pasipo kuwa na mtu atakayeishi ndani yake.
“Moav toprağına tuz dökün, kısırlaşsın, Kentleri öyle viran olacak ki, Kimse yaşamayacak oralarda.
10 “Alaaniwe yeye afanyaye kazi ya Bwana kwa hila! Alaaniwe yeye auzuiaye upanga wake usimwage damu!
Lanet olsun RAB'bin işini savsaklayana! Kılıcını kan dökmekten alıkoyana lanet olsun!
11 “Moabu amestarehe tangu ujana wake, kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake, haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine, hajaenda uhamishoni. Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo, nayo harufu yake haijabadilika.
Moav gençliğinden bu yana güvenlikteydi, Şarap tortusu gibi durgun kaldı, Bir kaptan öbürüne boşaltılmadı, Sürgüne gönderilmedi. O yüzden tadını yitirmedi, kokusu bozulmadı.
12 Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapotuma watu wamiminao kutoka kwenye magudulia, nao watamimina; wataacha magudulia yake yakiwa matupu na kuvunja mitungi yake.
“Ama onu boşaltacak adamları göndereceğim günler geliyor” diyor RAB, “Onu boşaltacaklar. Kaplarını boşaltacak, küplerini paramparça edecekler.
13 Kisha Moabu atamwonea aibu mungu wao Kemoshi, kama vile nyumba ya Israeli walivyoona aibu walipotegemea mungu wa Betheli.
İsrail halkı güvendiği Beytel'den nasıl utandıysa, Moav da Kemoş ilahından öyle utanacak.
14 “Mwawezaje kusema, ‘Sisi ni mashujaa, watu jasiri katika vita’?
“Nasıl, ‘Biz yiğidiz, Savaşa hazır askerleriz’ dersiniz?
15 Moabu ataangamizwa na miji yake itavamiwa, vijana wake waume walio bora sana watachinjwa,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
Moav ve kentlerini yerle bir eden, Saldırıya geçti. En seçkin gençleri kesime gidecek. Adı Her Şeye Egemen RAB olan Kral böyle diyor.
16 “Kuanguka kwa Moabu kumekaribia, janga kubwa litamjia kwa haraka.
Moav'ın yıkımı yakında geliyor, Uğrayacağı felaket hızla yaklaşıyor.
17 Ombolezeni kwa ajili yake, ninyi nyote mnaomzunguka, ninyi nyote mnaojua sifa zake, semeni, ‘Tazama jinsi ilivyovunjika fimbo ya kifalme yenye nguvu, tazama jinsi ilivyovunjika fimbo iliyotukuka!’
Dövünün onun için, Ey çevresinde yaşayan, ününü bilen sizler! ‘Kudret asası, Görkemli değnek nasıl da kırıldı!’ deyin.
18 “Shuka kutoka fahari yako na uketi katika ardhi iliyokauka, enyi wenyeji wa Binti wa Diboni, kwa maana yeye aangamizaye Moabu atakuja dhidi yako, na kuangamiza miji yako iliyozungushiwa maboma.
“Ey Divon Kenti'nde yaşayan halk, Görkeminden in, Kuru toprak üstünde otur. Çünkü Moav'ı yerle bir eden sana da saldıracak, Kalelerini yıkacak.
19 Simama kando ya barabara na utazame, wewe unayeishi Aroeri. Muulize mwanaume anayekimbia na mwanamke anayetoroka, waulize, ‘Kumetokea nini?’
Ey sen, Aroer'de oturan, Yol kenarında dur da gözle! Kaçan adama, kurtulan kadına, ‘Ne oldu?’ diye sor.
20 Moabu amefedheheshwa, kwa kuwa amevunjavunjwa. Lieni kwa huzuni na kupiga kelele! Tangazeni kando ya Arnoni kwamba Moabu ameangamizwa.
Moav utandırıldı, darmadağın oldu. Feryat et, haykır! Moav'ın yıkıldığını Arnon Vadisi'nde duyur.
21 Hukumu imefika kwenye uwanda wa juu: katika Holoni, Yahasa na Mefaathi,
“Yayladaki kentler –Holan, Yahas, Mefaat, Divon, Nevo, Beytdivlatayim, Kiryatayim, Beytgamul, Beytmeon, Keriyot, Bosra, uzak yakın bütün Moav kentleri– yargılanacak.
22 katika Diboni, Nebo na Beth-Diblathaimu,
23 katika Kiriathaimu, Beth-Gamuli na Beth-Meoni,
24 katika Keriothi na Bosra; kwa miji yote ya Moabu, iliyoko mbali na karibu.
25 Pembe ya Moabu imekatwa, mkono wake umevunjwa,” asema Bwana.
Moav'ın boynuzu kesildi, kolu kırıldı” diyor RAB.
26 “Mlevye, kwa kuwa amemdharau Bwana. Moabu na agaegae katika matapishi yake, yeye na awe kitu cha dhihaka.
“Moav'ı sarhoş edin, Çünkü RAB'be büyüklük tasladı. Moav kendi kusmuğunda yuvarlanacak, Alay konusu olacak.
27 Je, Israeli hakuwa kitu chako cha kudhihakiwa? Je, alikamatwa miongoni mwa wezi, kiasi cha kutikisa kichwa chako kwa dharau kila mara unapozungumza juu yake?
İsrail senin için gülünesi bir ulus mu oldu? Hırsızlar arasında mı yakalandı ki, Ondan söz ettikçe baş sallıyorsun?
28 Ondokeni kwenye miji yenu, mkaishi katikati ya miamba, enyi mnaoishi Moabu. Kuweni kama huwa ambaye hutengeneza kiota chake kwenye mdomo wa pango.
“Ey Moav'da yaşayanlar, Kentlerinizi terk edip kayalara sığının. Uçurumun ağzında yuvasını yapan Güvercin gibi olun.
29 “Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kutakabari kwake kwa kiburi na majivuno, kiburi chake na ufidhuli wake, na kujivuna kwa moyo wake.
Moav'ın ne denli gururlanıp büyüklendiğini, Kendini ne denli beğendiğini, Kibirlenip küstahlaştığını, Övünüp kabardığını duyduk.
30 Ninaujua ujeuri wake, lakini ni bure,” asema Bwana, “nako kujisifu kwake hakumsaidii chochote.
Küstahlığını biliyorum” diyor RAB, “Övünmesi boşunadır, yaptıkları da.
31 Kwa hiyo namlilia Moabu, kwa ajili ya Moabu yote ninalia, ninaomboleza kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
Bu yüzden Moav için haykıracak, Bütün Moav için feryat edeceğim. Ağlayacağım Kîr-Hereset halkı için.
32 Ninalia machozi kwa ajili yenu, kama Yazeri aliavyo, enyi mizabibu ya Sibma. Matawi yako yameenea hadi baharini; yamefika hadi bahari ya Yazeri. Mharabu ameyaangukia matunda yako yaliyoiva na mizabibu yako iliyoiva.
Ey Sivma asması, Senin için Yazer halkından çok ağlayacağım. Filizlerin gölü aşıp Yazer'e ulaştı. Yok edici yaz meyvelerini, üzümünü yok etti.
33 Shangwe na furaha vimetoweka kutoka bustani na mashamba ya Moabu. Nimekomesha kutiririka kwa divai kutoka mashinikizo; hakuna hata mmoja ayakanyagaye kwa kelele za shangwe. Ingawa kuna kelele, sio kelele za shangwe.
Moav'ın meyve bahçelerinden, tarlalarından Sevinç ve neşe yok oldu. Üzüm sıkma çukurlarından şarap akışını durdurdum; Kimse sevinç çığlıklarıyla üzüm ezmiyor, Çığlıklar var, ama sevinç çığlıkları değil.
34 “Sauti ya kilio chao inapanda kutoka Heshboni hadi Eleale na Yahazi, kutoka Soari hadi Horonaimu na Eglath-Shelishiya, kwa kuwa hata maji ya Nimrimu yamekauka.
“Heşbon ve Elale'nin haykırışları Yahas'a ulaşıyor. Soar'dan Horonayim'e, Eglat-Şelişiya'ya dek çığlıklar yükseliyor. Çünkü Nimrim suları bile kurudu.
35 Nitakomesha wale wote katika Moabu watoao sadaka mahali pa juu, na kufukiza uvumba kwa miungu yao,” asema Bwana.
Moav'da puta tapılan yerlerde Sunu sunanları, İlahlarına buhur yakanları Yok edeceğim” diyor RAB.
36 “Kwa hiyo moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama filimbi; unaomboleza kama filimbi kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi. Utajiri waliojipatia umetoweka.
“Bu yüzden yüreğim ney gibi İnliyor Moav için; Kîr-Hereset halkı için ney gibi İnliyor yüreğim. Çünkü elde ettikleri zenginlik uçup gitti.
37 Kila kichwa kimenyolewa na kila mwenye ndevu zimekatwa; kila mkono umekatwa na kila kiuno kimefunikwa kwa nguo ya gunia.
“Herkes saçını sakalını kesecek, Elini yaralayacak, Beline çul saracak.
38 Juu ya mapaa yote katika Moabu na katika viwanja hakuna kitu chochote isipokuwa maombolezo, kwa kuwa nimemvunja Moabu kama gudulia ambalo hakuna mtu yeyote anayelitaka,” asema Bwana.
Moav damlarında, meydanlarında Yalnız ağlayış var. Çünkü Moav'ı kimsenin beğenmediği Bir kap gibi kırdım” diyor RAB.
39 “Tazama jinsi alivyovunjikavunjika! Jinsi wanavyolia kwa huzuni! Tazama jinsi Moabu anavyogeuka kwa aibu! Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa, kitu cha kutisha kwa wale wote wanaomzunguka.”
“Nasıl da darmadağın oldu Moav! Nasıl acıyla feryat ediyor! Nasıl da sırtını dönüyor utançtan! Moav çevresindekilere alay konusu, Dehşet verici bir örnek oldu.”
40 Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama! Tai anashuka chini, akitanda mabawa yake juu ya Moabu.
RAB diyor ki, “Bakın! Düşman birden çullanan bir kartal gibi Kanatlarını Moav'ın üzerine açacak.
41 Miji itatekwa na ngome zake zitatwaliwa. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Moabu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Keriyot ele geçirilecek, Kaleler alınacak. O gün Moavlı askerlerin yüreği, Doğum sancısı çeken kadının yüreği gibi olacak.
42 Moabu ataangamizwa kama taifa kwa sababu amemdharau Bwana.
Moav yıkıma uğrayacak, Halk olmaktan çıkacak; Çünkü RAB'be karşı büyüklük tasladı.
43 Hofu kuu, shimo na mtego vinawangojea, enyi watu wa Moabu,” asema Bwana.
Önünde dehşet, çukur ve tuzak var, Ey Moav halkı!” diyor RAB.
44 “Yeyote atakayeikimbia hiyo hofu kuu ataanguka ndani ya shimo, yeyote atakayepanda kutoka shimoni, atanaswa katika mtego, kwa sababu nitaletea Moabu mwaka wa adhabu yake,” asema Bwana.
“Dehşetten kaçan çukura düşecek, Çukurdan çıkan tuzağa yakalanacak; Çünkü Moav'ın üzerine Cezalandırma yılını getireceğim” diyor RAB.
45 “Katika kivuli cha Heshboni, wakimbizi wamesimama pasipo msaada, kwa kuwa moto umezimika huko Heshboni, mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni; unaunguza vipaji vya nyuso za Moabu, mafuvu yao wenye kujivuna kwa kelele.
“Heşbon'un gölgesinde Bitkin düşmüş kaçkınlar. Çünkü Heşbon'dan ateş, Sihon'un ortasından alev çıktı; Moavlılar'ın alınlarını, Kargaşa çıkaranların başlarını yakıp yok etti.
46 Ole wako, ee Moabu! Watu wa Kemoshi wameangamizwa; wana wako wamepelekwa uhamishoni na binti zako wamechukuliwa mateka.
Vay sana, ey Moav! İlah Kemoş'un halkı yok oldu, Oğulların sürgüne gönderildi, Kızların tutsak alındı.
47 “Lakini nitarudisha mateka wa Moabu, katika siku zijazo,” asema Bwana. Huu ndio mwisho wa hukumu juu ya Moabu.
Ama son günlerde Yine eski gönencine kavuşturacağım Moav'ı” diyor RAB. Moav'ın yargısı burada sona eriyor.