< Yeremia 48 >
1 Kuhusu Moabu: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Ole wake Nebo, kwa maana utaharibiwa. Kiriathaimu utaaibishwa na kutekwa; Misgabu itaaibishwa na kuvunjavunjwa.
Acerca de Moab. El Señor de los ejércitos, el Dios de Israel, ha dicho: Dolor en Nebo, porque ha sido destruida; Quiriataim ha sido avergonzado y ha sido tomado; el lugar fuerte ha sido avergonzado y destruido.
2 Moabu haitasifiwa tena; huko Heshboni watu watafanya shauri baya la anguko lake: ‘Njooni na tuangamize taifa lile.’ Wewe nawe, ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.
La alabanza de Moab ha llegado a su fin; En cuanto a Hesbón, el mal ha sido diseñado contra ella; Ven, pongámosle fin a ella como nación. Mas tu boca será cerrada, O Madmen; La espada te perseguirá.
3 Sikiliza kilio kutoka Horonaimu, kilio cha maangamizi makuu na uharibifu.
Se oye el llanto de Horonaim, ruina y gran destrucción;
4 Moabu utavunjwa, wadogo wake watapiga kelele.
Moab está quebrantado; Su grito ha salido a Zoar.
5 Wanapanda kwenda njia ya kuelekea Luhithi, wakilia kwa uchungu wanapotembea, kwenye njia inayoshuka kwenda Horonaimu, kilio cha uchungu kwa ajili ya uharibifu kinasikika.
Porque por la ladera de Luhit subirán llorando todo el camino; porque en el camino a Horonaim, el grito de destrucción ha llegado a sus oídos.
6 Kimbieni! Okoeni maisha yenu, kuweni kama kichaka jangwani.
Ve en vuelo, escapa de tus vidas y Sean como la zarza en el desierto.
7 Kwa kuwa mmetumainia matendo yenu na mali zenu, ninyi pia mtachukuliwa mateka, naye Kemoshi atakwenda uhamishoni, pamoja na makuhani wake na maafisa wake.
Porque por haber puesto tu fe en tus obras y tus riquezas, tú, incluso tú, serás tomado; y Quemos saldrá como prisionero, sus sacerdotes y sus gobernantes juntos.
8 Mharabu atakuja dhidi ya kila mji, wala hakuna mji utakaookoka. Bonde litaangamizwa na uwanda utaharibiwa, kwa sababu Bwana amesema.
Y el atacante vendrá contra todos los pueblos, ni uno estará a salvo; y el valle será arruinado, y la destrucción llegará a las tierras bajas, como el Señor lo ha dicho.
9 Wekeni chumvi kwa ajili ya Moabu, kwa kuwa ataangamizwa; miji yake itakuwa ukiwa, pasipo kuwa na mtu atakayeishi ndani yake.
Levante un pilar para Moab, porque ella llegará a su fin; y sus pueblos se convertirán en ruinas, sin que nadie viva en ellos.
10 “Alaaniwe yeye afanyaye kazi ya Bwana kwa hila! Alaaniwe yeye auzuiaye upanga wake usimwage damu!
Sea maldito el que hace la obra del Señor con engaño; Que sea maldito el que retiene su espada de sangre.
11 “Moabu amestarehe tangu ujana wake, kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake, haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine, hajaenda uhamishoni. Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo, nayo harufu yake haijabadilika.
Desde sus primeros días, Moab ha estado viviendo en comodidad; como el vino almacenado durante mucho tiempo, no ha sido drenado de un recipiente a otro, nunca se ha ido como prisionero; por lo que su sabor aún está en él, su olor no ha cambiado.
12 Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapotuma watu wamiminao kutoka kwenye magudulia, nao watamimina; wataacha magudulia yake yakiwa matupu na kuvunja mitungi yake.
Ciertamente, los días se acercan, dice el Señor, cuando le enviaré a los hombres que le harán volverse hasta que no haya más vino en sus vasijas, y sus odres vacíos de vino se romperán por completo.
13 Kisha Moabu atamwonea aibu mungu wao Kemoshi, kama vile nyumba ya Israeli walivyoona aibu walipotegemea mungu wa Betheli.
Y se avergonzará Moab a causa de Quemos, como se avergonzó a los hijos de Israel a causa de Betel su esperanza.
14 “Mwawezaje kusema, ‘Sisi ni mashujaa, watu jasiri katika vita’?
¿Cómo pueden decir: Somos hombres de guerra y combatientes fuertes?
15 Moabu ataangamizwa na miji yake itavamiwa, vijana wake waume walio bora sana watachinjwa,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
El que trae destrucción a Moab ha subido contra ella; y sus jóvenes escogidos han bajado al degolladero, dice el Rey, cuyo nombre es el Señor de los ejércitos.
16 “Kuanguka kwa Moabu kumekaribia, janga kubwa litamjia kwa haraka.
La calamidad de Moab está cerca, y su mal viene muy rápido.
17 Ombolezeni kwa ajili yake, ninyi nyote mnaomzunguka, ninyi nyote mnaojua sifa zake, semeni, ‘Tazama jinsi ilivyovunjika fimbo ya kifalme yenye nguvu, tazama jinsi ilivyovunjika fimbo iliyotukuka!’
Todos los que lo rodean, den señales de dolor por él, y todos los que conocen su nombre, digan: ¡Cómo se rompe la vara fuerte, incluso él glorioso bordon!
18 “Shuka kutoka fahari yako na uketi katika ardhi iliyokauka, enyi wenyeji wa Binti wa Diboni, kwa maana yeye aangamizaye Moabu atakuja dhidi yako, na kuangamiza miji yako iliyozungushiwa maboma.
Desciende de tu gloria, pueblo de Dibón, y toma asiento en el lugar reseco; porque él destructor de Moab ha subido contra ti, enviando destrucción a tus fortalezas.
19 Simama kando ya barabara na utazame, wewe unayeishi Aroeri. Muulize mwanaume anayekimbia na mwanamke anayetoroka, waulize, ‘Kumetokea nini?’
Oh hija de Aroer, toma tu puesto por cierto, de guardia; pregúntale quién está huyendo y quién se ha escapado, pregunta, ¿qué se ha hecho?
20 Moabu amefedheheshwa, kwa kuwa amevunjavunjwa. Lieni kwa huzuni na kupiga kelele! Tangazeni kando ya Arnoni kwamba Moabu ameangamizwa.
Moab ha sido avergonzada, está quebrantada; hace fuertes ruidos de dolor, pidiendo ayuda; den la noticia junto al Arnón, que Moab ha sido destruida.
21 Hukumu imefika kwenye uwanda wa juu: katika Holoni, Yahasa na Mefaathi,
Y el castigo ha llegado a las tierras bajas; en Holon, Jahaza, Mefaat,
22 katika Diboni, Nebo na Beth-Diblathaimu,
Dibón, Nebo, Bet-diblataim,
23 katika Kiriathaimu, Beth-Gamuli na Beth-Meoni,
Quiriataim, y en Beth-gamul, y en Bet-meon,
24 katika Keriothi na Bosra; kwa miji yote ya Moabu, iliyoko mbali na karibu.
Queriot, y en Bosra, y en todos los pueblos de la tierra de Moab, lejanos y cercanos.
25 Pembe ya Moabu imekatwa, mkono wake umevunjwa,” asema Bwana.
Se corta el poder de Moab y su poder destruido, dice el Señor.
26 “Mlevye, kwa kuwa amemdharau Bwana. Moabu na agaegae katika matapishi yake, yeye na awe kitu cha dhihaka.
Emborrachenlo, porque su corazón se ha enorgullecido contra el Señor; y Moab se revolcara en su vómito, y todos se burlarán de él.
27 Je, Israeli hakuwa kitu chako cha kudhihakiwa? Je, alikamatwa miongoni mwa wezi, kiasi cha kutikisa kichwa chako kwa dharau kila mara unapozungumza juu yake?
¿No hiciste burla de Israel? fue tomado entre los ladrones? porque cuando estabas hablando de él, estabas hablando con desprecio.
28 Ondokeni kwenye miji yenu, mkaishi katikati ya miamba, enyi mnaoishi Moabu. Kuweni kama huwa ambaye hutengeneza kiota chake kwenye mdomo wa pango.
Oh pueblo de Moab, sal de los pueblos y escápate en la roca; Sé como la paloma de Araba, que la convierte en lugar de vivir detrás de la boca de la caverna.
29 “Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kutakabari kwake kwa kiburi na majivuno, kiburi chake na ufidhuli wake, na kujivuna kwa moyo wake.
Hemos recibido la noticia del orgullo de Moab, de su soberbia; y su gran opinión de sí mismo, de su arrogancia, la altivez de su corazón.
30 Ninaujua ujeuri wake, lakini ni bure,” asema Bwana, “nako kujisifu kwake hakumsaidii chochote.
Tengo conocimiento de su ira, dice el Señor, que no es nada; Sus jactancias no han hecho nada.
31 Kwa hiyo namlilia Moabu, kwa ajili ya Moabu yote ninalia, ninaomboleza kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
Por esta causa daré gritos de dolor por Moab, clamando por todo Moab; Estaré triste por los hombres de Kir-heres.
32 Ninalia machozi kwa ajili yenu, kama Yazeri aliavyo, enyi mizabibu ya Sibma. Matawi yako yameenea hadi baharini; yamefika hadi bahari ya Yazeri. Mharabu ameyaangukia matunda yako yaliyoiva na mizabibu yako iliyoiva.
Mi llanto por ti, oh viña de Sibma, será más que el llanto de Jazer; tus ramas se han extendido sobre el mar, extendiéndose incluso hasta Jazer; la destrucción ha caído sobre tus frutos de verano y tus uvas cortadas.
33 Shangwe na furaha vimetoweka kutoka bustani na mashamba ya Moabu. Nimekomesha kutiririka kwa divai kutoka mashinikizo; hakuna hata mmoja ayakanyagaye kwa kelele za shangwe. Ingawa kuna kelele, sio kelele za shangwe.
Todo el gozo se ha ido; ya no se alegran por el campo fértil y por la tierra de Moab; He hecho que el vino llegue a su fin en los lagares donde los pisan; ya no pisaran las uvas con el sonido de voces alegres.
34 “Sauti ya kilio chao inapanda kutoka Heshboni hadi Eleale na Yahazi, kutoka Soari hadi Horonaimu na Eglath-Shelishiya, kwa kuwa hata maji ya Nimrimu yamekauka.
El clamor de Hesbón llega incluso a Eleale; a Jahaz suena su voz; desde Zoar hasta Horonaim y Eglat-selisiya; porque las aguas de Nimrim se secarán.
35 Nitakomesha wale wote katika Moabu watoao sadaka mahali pa juu, na kufukiza uvumba kwa miungu yao,” asema Bwana.
Y pondré fin a Moab, dice el Señor al que hace ofrendas en el lugar alto y quema incienso a sus dioses.
36 “Kwa hiyo moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama filimbi; unaomboleza kama filimbi kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi. Utajiri waliojipatia umetoweka.
Entonces mi corazón gemirá por Moab como el sonido de las flautas, y mi corazón está sonando como flautas por los hombres de Kir-heres: porque la riqueza que él tiene para sí mismo ha llegado a su fin.
37 Kila kichwa kimenyolewa na kila mwenye ndevu zimekatwa; kila mkono umekatwa na kila kiuno kimefunikwa kwa nguo ya gunia.
Porque en todas partes se corta el vello de la cabeza y el vello de la cara; en cada mano hay heridas y se han vestido de silicio.
38 Juu ya mapaa yote katika Moabu na katika viwanja hakuna kitu chochote isipokuwa maombolezo, kwa kuwa nimemvunja Moabu kama gudulia ambalo hakuna mtu yeyote anayelitaka,” asema Bwana.
En todas las casas de Moab y en sus calles hay llanto por todas partes; porque Moab se ha roto como un vaso en el cual no hay placer, dice el Señor.
39 “Tazama jinsi alivyovunjikavunjika! Jinsi wanavyolia kwa huzuni! Tazama jinsi Moabu anavyogeuka kwa aibu! Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa, kitu cha kutisha kwa wale wote wanaomzunguka.”
Hagan lamentación por Moab ¿Cómo ha sido quebrantado? ¿Cómo se ha vuelto la espalda de Moab avergonzado? así que Moab será una causa de burla y espanto para todos los que lo rodean.
40 Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama! Tai anashuka chini, akitanda mabawa yake juu ya Moabu.
Porque el Señor ha dicho: Mira, vendrá como un águila en vuelo, extendiendo sus alas contra Moab.
41 Miji itatekwa na ngome zake zitatwaliwa. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Moabu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Ha sido tomado Queriot, y las fortalezas han sido ocupadas por los enemigos, y los corazones de los hombres de guerra de Moab en ese día serán como el corazón de una mujer en los dolores de parto.
42 Moabu ataangamizwa kama taifa kwa sababu amemdharau Bwana.
Y Moab llegará a su fin como pueblo, porque él se ha estado levantando contra el Señor.
43 Hofu kuu, shimo na mtego vinawangojea, enyi watu wa Moabu,” asema Bwana.
El temor, la muerte y la red han caído sobre ti, pueblo de Moab, dice el Señor.
44 “Yeyote atakayeikimbia hiyo hofu kuu ataanguka ndani ya shimo, yeyote atakayepanda kutoka shimoni, atanaswa katika mtego, kwa sababu nitaletea Moabu mwaka wa adhabu yake,” asema Bwana.
El que huya del miedo será vencido por la muerte; y el que se libere de la muerte, será capturado en la red: porque haré que venga esto a Moab, el año de su castigo, dice el Señor.
45 “Katika kivuli cha Heshboni, wakimbizi wamesimama pasipo msaada, kwa kuwa moto umezimika huko Heshboni, mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni; unaunguza vipaji vya nyuso za Moabu, mafuvu yao wenye kujivuna kwa kelele.
Los que salieron huyendo del miedo están esperando a la sombra de Hesbón, porque se está quemando Hesbón y una llama de la casa de Sehón, se extiende y quema los montes Moab y la corona de cabeza de esos revoltosos.
46 Ole wako, ee Moabu! Watu wa Kemoshi wameangamizwa; wana wako wamepelekwa uhamishoni na binti zako wamechukuliwa mateka.
¡El dolor es tuyo, oh Moab! La gente de Quemos ha perecido, porque tus hijos y tus hijas han sido llevados prisioneros.
47 “Lakini nitarudisha mateka wa Moabu, katika siku zijazo,” asema Bwana. Huu ndio mwisho wa hukumu juu ya Moabu.
Pero aún así, dejaré que el destino de Moab cambie en los últimos días, dice el Señor.