< Yeremia 48 >

1 Kuhusu Moabu: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Ole wake Nebo, kwa maana utaharibiwa. Kiriathaimu utaaibishwa na kutekwa; Misgabu itaaibishwa na kuvunjavunjwa.
Przeciwko Moabowi. Tak mówi Pan zastępów, Bóg Izraelski: Biada miastu Nebo, bo spustoszone będzie; pohańbione i wzięte będzie Karyjataim; zawstydzone będzie miasto na miejscu wysokiem, i bać się będzie.
2 Moabu haitasifiwa tena; huko Heshboni watu watafanya shauri baya la anguko lake: ‘Njooni na tuangamize taifa lile.’ Wewe nawe, ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.
Nie będzie się więcej chlubił Moab z Hesebonu; myślą złe przeciwko niemu, mówiąc: Pójdźcie, a wytraćmy ich z narodu. I ty, Madmenie! wykorzeniony będziesz, miecz pójdzie za tobą.
3 Sikiliza kilio kutoka Horonaimu, kilio cha maangamizi makuu na uharibifu.
Głos krzyku z Choronaim: O spustoszenie i zburzenie wielkie!
4 Moabu utavunjwa, wadogo wake watapiga kelele.
Starty będzie Moab, słyszany będzie krzyk maluczkich jego,
5 Wanapanda kwenda njia ya kuelekea Luhithi, wakilia kwa uchungu wanapotembea, kwenye njia inayoshuka kwenda Horonaimu, kilio cha uchungu kwa ajili ya uharibifu kinasikika.
Przeto, że na drodze Luchytskiej będzie ustawiczny płacz, a którędy zstępują do Choronaim, nieprzyjaciele krzyk zburzenia słyszeć będą,
6 Kimbieni! Okoeni maisha yenu, kuweni kama kichaka jangwani.
Mówiących: Uciekajcie, wybawcie duszę swoję, a stańcie się jako wrzos na puszczy.
7 Kwa kuwa mmetumainia matendo yenu na mali zenu, ninyi pia mtachukuliwa mateka, naye Kemoshi atakwenda uhamishoni, pamoja na makuhani wake na maafisa wake.
Bo dlatego, że masz nadzieję w dostatku twoim, i w skarbach twoich, będziesz też wzięte, i Chamos pójdzie w pojmanie, kapłani jego, także i książęta jego.
8 Mharabu atakuja dhidi ya kila mji, wala hakuna mji utakaookoka. Bonde litaangamizwa na uwanda utaharibiwa, kwa sababu Bwana amesema.
Bo burzyciel przyjdzie na każde miasto, a żadne miasto nie ujdzie; zginie i dolina, i równiny spustoszone będą, jako mówi Pan.
9 Wekeni chumvi kwa ajili ya Moabu, kwa kuwa ataangamizwa; miji yake itakuwa ukiwa, pasipo kuwa na mtu atakayeishi ndani yake.
Dajcie skrzydła Moabowi, niech prędko uleci; bo miasta jego przyjdą w spustoszenie, tak, że nie będzie w nich obywatela.
10 “Alaaniwe yeye afanyaye kazi ya Bwana kwa hila! Alaaniwe yeye auzuiaye upanga wake usimwage damu!
Przeklęty, kto zdradliwie czyni sprawę Pańską; przeklęty także, kto hamuje miecz swój ode krwi.
11 “Moabu amestarehe tangu ujana wake, kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake, haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine, hajaenda uhamishoni. Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo, nayo harufu yake haijabadilika.
Miałci Moab pokój od dzieciństwa swego, i usadził się na drożdżach swoich, ani był przelewany z naczynia w naczynie, to jest, w pojmanie nie chodził, dla czego został w nim smak jego, a woń jego nie zmieniła się.
12 Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapotuma watu wamiminao kutoka kwenye magudulia, nao watamimina; wataacha magudulia yake yakiwa matupu na kuvunja mitungi yake.
Przetoż oto dni idą, mówi Pan, że poślę nań tych, którzy wtargnienia czynią, a pojmają go, i naczynia jego wypróżnią, a łagwie jego potłuką.
13 Kisha Moabu atamwonea aibu mungu wao Kemoshi, kama vile nyumba ya Israeli walivyoona aibu walipotegemea mungu wa Betheli.
I zawstydzony będzie Moab od Chamosa, jako zawstydzony jest dom Izraelski od Betel, nadziei swojej.
14 “Mwawezaje kusema, ‘Sisi ni mashujaa, watu jasiri katika vita’?
Jakoż mówicie: Mocniśmy, a mężowie duży do boju?
15 Moabu ataangamizwa na miji yake itavamiwa, vijana wake waume walio bora sana watachinjwa,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
Zburzony będzie Moab, i z miast swoich wynijdzie, a wyborni młodzieńcy jego pójdą na zabicie, mówi król, Pan zastępów imię jego.
16 “Kuanguka kwa Moabu kumekaribia, janga kubwa litamjia kwa haraka.
Blisko jest zginienie Moabowe, i przyjdzie; a nieszczęście jego prędko się pospieszy.
17 Ombolezeni kwa ajili yake, ninyi nyote mnaomzunguka, ninyi nyote mnaojua sifa zake, semeni, ‘Tazama jinsi ilivyovunjika fimbo ya kifalme yenye nguvu, tazama jinsi ilivyovunjika fimbo iliyotukuka!’
Użalcie się go wszyscy, którzy mieszkacie około niego, i wszyscy, którzy znacie imię jego, mówcie: Jakoż się złamała laska mocy, i kij ozdobny?
18 “Shuka kutoka fahari yako na uketi katika ardhi iliyokauka, enyi wenyeji wa Binti wa Diboni, kwa maana yeye aangamizaye Moabu atakuja dhidi yako, na kuangamiza miji yako iliyozungushiwa maboma.
Zstąp z sławy, a siądź w pragnieniu, obywatelko, córko Dybońska! bo zburzyciel Moabu przyciągnie przeciwko tobie, rozrzuci twierdze twoje.
19 Simama kando ya barabara na utazame, wewe unayeishi Aroeri. Muulize mwanaume anayekimbia na mwanamke anayetoroka, waulize, ‘Kumetokea nini?’
Stań na drodze a przypatrz się pilnie, obywatelko Aroer! pytaj tego, który ucieka, i tej, która uchodzi, mówiąc: Co się dzieje?
20 Moabu amefedheheshwa, kwa kuwa amevunjavunjwa. Lieni kwa huzuni na kupiga kelele! Tangazeni kando ya Arnoni kwamba Moabu ameangamizwa.
Zawstydzony jest Moab, bo jest potarty; narzekajcie a wołajcie, opowiadajcie w Arnon, że pustoszą Moaba.
21 Hukumu imefika kwenye uwanda wa juu: katika Holoni, Yahasa na Mefaathi,
Bo sąd przyszedł na ziemię tej równiny, na Holon, i na Jassa, i na Mefaat,
22 katika Diboni, Nebo na Beth-Diblathaimu,
I na Dybon, i na Nebo, i na Bet Dyblataim,
23 katika Kiriathaimu, Beth-Gamuli na Beth-Meoni,
I na Kiryjataim, i na Betgamul, i Betmehon.
24 katika Keriothi na Bosra; kwa miji yote ya Moabu, iliyoko mbali na karibu.
I na Karyjot, i na Bocrę, i na wszystkie miasta ziemi Moabskiej, dalekie i bliskie.
25 Pembe ya Moabu imekatwa, mkono wake umevunjwa,” asema Bwana.
Odcięty będzie róg Moabski, i ramię jego będzie starte, mówi Pan.
26 “Mlevye, kwa kuwa amemdharau Bwana. Moabu na agaegae katika matapishi yake, yeye na awe kitu cha dhihaka.
Opójcie go, ponieważ się przeciw Panu podniósł; niech się wala Moab w blwocinach swoich, niech będzie i on na pośmiech.
27 Je, Israeli hakuwa kitu chako cha kudhihakiwa? Je, alikamatwa miongoni mwa wezi, kiasi cha kutikisa kichwa chako kwa dharau kila mara unapozungumza juu yake?
Bo azaż w pośmiewisku nie był u ciebie Izrael? Izali go między złodziejami zastano? że, ilekroć mówisz o nim, wyskakujesz.
28 Ondokeni kwenye miji yenu, mkaishi katikati ya miamba, enyi mnaoishi Moabu. Kuweni kama huwa ambaye hutengeneza kiota chake kwenye mdomo wa pango.
Opuszczajcie miasta a mieszkajcie na skale, obywatele Moabscy! a bądźcie jako gołębica, która ściele gniazdo swoje na kraju dziury.
29 “Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kutakabari kwake kwa kiburi na majivuno, kiburi chake na ufidhuli wake, na kujivuna kwa moyo wake.
Słyszeliśmy o pysze Moabowej, że jest bardzo pyszny; o wysokomyślności jego, i o hardości jego, i o nadętości jego, i o wyniosłości serca jego.
30 Ninaujua ujeuri wake, lakini ni bure,” asema Bwana, “nako kujisifu kwake hakumsaidii chochote.
Znamci Ja, mówi Pan, zagniewanie jego; lecz nie ma siły; kłamstwa jego nie dowiodą tego.
31 Kwa hiyo namlilia Moabu, kwa ajili ya Moabu yote ninalia, ninaomboleza kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
Dlatego nad Moabczykami narzekam, a nade wszystkim Moabem wołam, a dla obywateli Kircheres wzdycha serce moje.
32 Ninalia machozi kwa ajili yenu, kama Yazeri aliavyo, enyi mizabibu ya Sibma. Matawi yako yameenea hadi baharini; yamefika hadi bahari ya Yazeri. Mharabu ameyaangukia matunda yako yaliyoiva na mizabibu yako iliyoiva.
Bardziej niż płakano Jazerczyków, płaczę nad tobą, o winna macico Sabama! Latorośli twoje dostaną się za morze, aż do morza Jazer dosięgną; na letnie owoce twoje, i na zbieranie wina twego burzyciel przypadnie.
33 Shangwe na furaha vimetoweka kutoka bustani na mashamba ya Moabu. Nimekomesha kutiririka kwa divai kutoka mashinikizo; hakuna hata mmoja ayakanyagaye kwa kelele za shangwe. Ingawa kuna kelele, sio kelele za shangwe.
I ustanie wesele i radość nad polem urodzajnem w ziemi Moabskiej, a winu z prasy wstręt uczynię; nie będą go tłoczyć z wykrzykaniem, a wykrzykanie nie będzie wykrzykaniem.
34 “Sauti ya kilio chao inapanda kutoka Heshboni hadi Eleale na Yahazi, kutoka Soari hadi Horonaimu na Eglath-Shelishiya, kwa kuwa hata maji ya Nimrimu yamekauka.
Bardziej krzyczeć będą niż Hesebończycy; aż do Eleale, aż do Jazy wydadzą głos swój, od Zoar aż do Choronaim, jako jałowica trzecioletnia; bo też i wody Nimrym zniszczeją.
35 Nitakomesha wale wote katika Moabu watoao sadaka mahali pa juu, na kufukiza uvumba kwa miungu yao,” asema Bwana.
I uczynię, mówi Pan, że ustanie w Moabie ofiarujący na wyżynach, i kadzący bogom swoim.
36 “Kwa hiyo moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama filimbi; unaomboleza kama filimbi kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi. Utajiri waliojipatia umetoweka.
Przetoż serce moje nad Moabem jako piszczałki piszczeć będzie; także nad obywatelami w Kircheres serce moje jako piszczałki piszczeć będzie, i dlatego, że i zboże zgromadzone wniwecz się obróci.
37 Kila kichwa kimenyolewa na kila mwenye ndevu zimekatwa; kila mkono umekatwa na kila kiuno kimefunikwa kwa nguo ya gunia.
Bo na każdej głowie będzie łysina, i każda broda ogolona będzie; na wszystkich rękach będą szramy, a na biodrach wór.
38 Juu ya mapaa yote katika Moabu na katika viwanja hakuna kitu chochote isipokuwa maombolezo, kwa kuwa nimemvunja Moabu kama gudulia ambalo hakuna mtu yeyote anayelitaka,” asema Bwana.
Po wszystkich dachach Moabskich i po ulicach jego, wszędy nic nie będzie, tylko narzekanie; bom skruszył Moaba jako naczynie nieużyteczne, mówi Pan.
39 “Tazama jinsi alivyovunjikavunjika! Jinsi wanavyolia kwa huzuni! Tazama jinsi Moabu anavyogeuka kwa aibu! Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa, kitu cha kutisha kwa wale wote wanaomzunguka.”
Narzekać będą, mówiąc: Jakoć jest starty! Jako tył podał Moab z hańbą! i jest Moab pośmiewiskiem, i postrachem wszystkim, którzy są około niego.
40 Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama! Tai anashuka chini, akitanda mabawa yake juu ya Moabu.
Bo tak mówi Pan: Oto nieprzyjaciel jako orzeł przyleci, a rozciągnie skrzydła swe na Moaba.
41 Miji itatekwa na ngome zake zitatwaliwa. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Moabu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Karyjot wzięte będzie, i zamki wzięte będą, a serce mocarzów Moabskich dnia onego będzie jako serce niewiasty bolejącej.
42 Moabu ataangamizwa kama taifa kwa sababu amemdharau Bwana.
I wygładzony będzie Moab z ludu; bo się przeciwko Panu podnosił.
43 Hofu kuu, shimo na mtego vinawangojea, enyi watu wa Moabu,” asema Bwana.
Strach i dół, i sidło nad tobą, o obywatelu Moabski! mówi Pan.
44 “Yeyote atakayeikimbia hiyo hofu kuu ataanguka ndani ya shimo, yeyote atakayepanda kutoka shimoni, atanaswa katika mtego, kwa sababu nitaletea Moabu mwaka wa adhabu yake,” asema Bwana.
Kto uciecze przed strachem, wpadnie w dół; a kto wynijdzie z dołu, sidłem ułapiony będzie; bo przywiodę nań, to jest na Moaba, rok nawiedzienia jego, mówi Pan.
45 “Katika kivuli cha Heshboni, wakimbizi wamesimama pasipo msaada, kwa kuwa moto umezimika huko Heshboni, mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni; unaunguza vipaji vya nyuso za Moabu, mafuvu yao wenye kujivuna kwa kelele.
W cieniu Hesebon stawali ci, którzy uciekali przed gwałtem; ale ogień wynijdzie z Hesebonu, i płomień z pośrodku Sehonu, i pożre kąt Moabski, i wierzch głowy tych, którzy go burzą.
46 Ole wako, ee Moabu! Watu wa Kemoshi wameangamizwa; wana wako wamepelekwa uhamishoni na binti zako wamechukuliwa mateka.
Biada tobie, Moabie! zaginieć lud Chamosowy; bo synowie twoi zabrani będą w niewolę, i córki twoje do więzienia.
47 “Lakini nitarudisha mateka wa Moabu, katika siku zijazo,” asema Bwana. Huu ndio mwisho wa hukumu juu ya Moabu.
Wszakże zasię przywrócę więźniów Moabskich w ostateczne dni, mówi Pan. Aż dotąd sąd o Moabie.

< Yeremia 48 >