< Yeremia 48 >
1 Kuhusu Moabu: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Ole wake Nebo, kwa maana utaharibiwa. Kiriathaimu utaaibishwa na kutekwa; Misgabu itaaibishwa na kuvunjavunjwa.
A Moab. Ainsi parle Yahweh des armées, Dieu d’Israël: Malheur à Nabo, car elle est ravagée; Cariathaïm est couverte de honte, elle est prise; la forteresse est couverte de honte, elle est abattue;
2 Moabu haitasifiwa tena; huko Heshboni watu watafanya shauri baya la anguko lake: ‘Njooni na tuangamize taifa lile.’ Wewe nawe, ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.
elle n’est plus, la gloire de Moab! A Hésebon on médite contre lui le mal: Allons et exterminons-le d’entre les nations! Toi aussi, Madmen, tu seras réduite au silence, l’épée marche derrière toi.
3 Sikiliza kilio kutoka Horonaimu, kilio cha maangamizi makuu na uharibifu.
Des cris partent de Horonaïm; dévastation et grande ruine!
4 Moabu utavunjwa, wadogo wake watapiga kelele.
Moab est brisé; ses petits enfants font entendre des cris.
5 Wanapanda kwenda njia ya kuelekea Luhithi, wakilia kwa uchungu wanapotembea, kwenye njia inayoshuka kwenda Horonaimu, kilio cha uchungu kwa ajili ya uharibifu kinasikika.
Oui! à la montée de Luith il y a des pleurs, on la gravit en pleurant; oui! à la descente de Horonaïm, on entend les cris de détresse.
6 Kimbieni! Okoeni maisha yenu, kuweni kama kichaka jangwani.
Fuyez, sauvez vos vies! Qu’elles soient comme une bruyère dans la lande!
7 Kwa kuwa mmetumainia matendo yenu na mali zenu, ninyi pia mtachukuliwa mateka, naye Kemoshi atakwenda uhamishoni, pamoja na makuhani wake na maafisa wake.
Car, puisque tu as mis ta confiance en tes ouvrages et en tes trésors, toi aussi tu seras conquis; et Chamos ira en exil, avec ses prêtres et ses princes, tous ensemble.
8 Mharabu atakuja dhidi ya kila mji, wala hakuna mji utakaookoka. Bonde litaangamizwa na uwanda utaharibiwa, kwa sababu Bwana amesema.
Le dévastateur viendra contre toutes les villes, et pas une ville n’échappera; la vallées sera ruinée, et le plateau saccagé, comme l’a dit Yahweh.
9 Wekeni chumvi kwa ajili ya Moabu, kwa kuwa ataangamizwa; miji yake itakuwa ukiwa, pasipo kuwa na mtu atakayeishi ndani yake.
Donnez des ailes à Moab, car il faut qu’il s’envole; ses villes seront dévastées, sans qu’il y ait d’habitant.
10 “Alaaniwe yeye afanyaye kazi ya Bwana kwa hila! Alaaniwe yeye auzuiaye upanga wake usimwage damu!
Maudit soit celui qui fait mollement l’œuvre du Seigneur! Maudit celui qui refuse le sang à son épée!
11 “Moabu amestarehe tangu ujana wake, kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake, haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine, hajaenda uhamishoni. Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo, nayo harufu yake haijabadilika.
Moab a été tranquille depuis sa jeunesse; il a reposé sur sa lie; il n’a pas été vidé d’un vase dans un autre, et il n’est pas allé en captivité. Aussi son goût lui est-il resté, et son parfum ne s’est pas altéré.
12 Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapotuma watu wamiminao kutoka kwenye magudulia, nao watamimina; wataacha magudulia yake yakiwa matupu na kuvunja mitungi yake.
C’est pourquoi voici que des jours viennent, — oracle Yahweh, où je lui enverrai des transvaseurs qui le transvaseront; ils videront ses vases, et ils briseront ses cruches.
13 Kisha Moabu atamwonea aibu mungu wao Kemoshi, kama vile nyumba ya Israeli walivyoona aibu walipotegemea mungu wa Betheli.
Et Moab aura honte de Chamos, comme la maison d’Israël a eu honte de Béthel, en qui était sa confiance.
14 “Mwawezaje kusema, ‘Sisi ni mashujaa, watu jasiri katika vita’?
Comment pouvez-vous dire: « Nous sommes des guerriers, des hommes vaillants au combat? »
15 Moabu ataangamizwa na miji yake itavamiwa, vijana wake waume walio bora sana watachinjwa,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
Moab est ravagé, ses villes montent en fumée, l’élite de ses jeunes gens descend pour la boucherie; — oracle du roi, dont le nom est Yahweh des armées.
16 “Kuanguka kwa Moabu kumekaribia, janga kubwa litamjia kwa haraka.
La ruine de Moab approche, son malheur vient en grande hâte.
17 Ombolezeni kwa ajili yake, ninyi nyote mnaomzunguka, ninyi nyote mnaojua sifa zake, semeni, ‘Tazama jinsi ilivyovunjika fimbo ya kifalme yenye nguvu, tazama jinsi ilivyovunjika fimbo iliyotukuka!’
Consolez-le, vous tous, ses voisins, et vous tous qui connaissez son nom, dites: « Comment a été brisé un bâton si fort, un sceptre si magnifique? »
18 “Shuka kutoka fahari yako na uketi katika ardhi iliyokauka, enyi wenyeji wa Binti wa Diboni, kwa maana yeye aangamizaye Moabu atakuja dhidi yako, na kuangamiza miji yako iliyozungushiwa maboma.
Descends de ta gloire et assieds-toi sur la terre aride, habitante, fille de Dibon; car le dévastateur de Moab est monté contre toi, il a renversé tes remparts.
19 Simama kando ya barabara na utazame, wewe unayeishi Aroeri. Muulize mwanaume anayekimbia na mwanamke anayetoroka, waulize, ‘Kumetokea nini?’
Tiens-toi sur le chemin, et observe, habitante d’Aroër; interroge celui qui fuit et celle qui s’échappe; dis: « Qu’est-il arrivé? —
20 Moabu amefedheheshwa, kwa kuwa amevunjavunjwa. Lieni kwa huzuni na kupiga kelele! Tangazeni kando ya Arnoni kwamba Moabu ameangamizwa.
« Moab est confus, car il est renversé. Poussez des gémissements et des cris! Annoncez sur l’Arnon que Moab est ravagé! »
21 Hukumu imefika kwenye uwanda wa juu: katika Holoni, Yahasa na Mefaathi,
Un jugement est venu sur le pays de la plaine, sur Hélon, sur Jasa, sur Méphaath,
22 katika Diboni, Nebo na Beth-Diblathaimu,
sur Dibon, sur Nabo, sur Beth-Deblathaïm,
23 katika Kiriathaimu, Beth-Gamuli na Beth-Meoni,
sur Cariathaïm, sur Beth-Gamul, sur Beth-Maon,
24 katika Keriothi na Bosra; kwa miji yote ya Moabu, iliyoko mbali na karibu.
sur Carioth, sur Bosra et sur toutes les villes du pays de Moab, éloignées et proches.
25 Pembe ya Moabu imekatwa, mkono wake umevunjwa,” asema Bwana.
La corne de Moab est abattue, et son bras est brisé, — oracle de Yahweh.
26 “Mlevye, kwa kuwa amemdharau Bwana. Moabu na agaegae katika matapishi yake, yeye na awe kitu cha dhihaka.
Enivrez-le; car il s’est élevé contre Yahweh! que Moab se vautre dans son vomissement, et qu’il devienne un objet de risée, lui aussi!
27 Je, Israeli hakuwa kitu chako cha kudhihakiwa? Je, alikamatwa miongoni mwa wezi, kiasi cha kutikisa kichwa chako kwa dharau kila mara unapozungumza juu yake?
Israël n’a-t-il pas été pour toi un objet de risée? L’a-t-on surpris avec des voleurs, pour que, chaque fois que tu parlés de lui, tu hoches la tête?
28 Ondokeni kwenye miji yenu, mkaishi katikati ya miamba, enyi mnaoishi Moabu. Kuweni kama huwa ambaye hutengeneza kiota chake kwenye mdomo wa pango.
Abandonnez les villes; demeurez dans les rochers, habitants de Moab, et soyez comme la colombe qui fait son nid au-dessus du précipice béant.
29 “Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kutakabari kwake kwa kiburi na majivuno, kiburi chake na ufidhuli wake, na kujivuna kwa moyo wake.
Nous avons entendu l’orgueil de Moab, le très orgueilleux, sa hauteur, son orgueil, sa fierté, et la fierté de son cœur.
30 Ninaujua ujeuri wake, lakini ni bure,” asema Bwana, “nako kujisifu kwake hakumsaidii chochote.
Moi aussi je connais, — oracle de Yahweh, sa jactance, et ses vains discours, et ses œuvres vaines.
31 Kwa hiyo namlilia Moabu, kwa ajili ya Moabu yote ninalia, ninaomboleza kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
C’est pourquoi je me lamente sur Moab; sur tout Moab je pousse des cris; on gémit sur les gens de Qir-Hérès.
32 Ninalia machozi kwa ajili yenu, kama Yazeri aliavyo, enyi mizabibu ya Sibma. Matawi yako yameenea hadi baharini; yamefika hadi bahari ya Yazeri. Mharabu ameyaangukia matunda yako yaliyoiva na mizabibu yako iliyoiva.
Plus encore que sur Jazer, je pleure sur toi, vigne de Sabama. Tes sarments dépassaient la mer, ils touchaient à la mer de Jazer. Sur ta récolte et sur ta vendange le dévastateur s’est jeté.
33 Shangwe na furaha vimetoweka kutoka bustani na mashamba ya Moabu. Nimekomesha kutiririka kwa divai kutoka mashinikizo; hakuna hata mmoja ayakanyagaye kwa kelele za shangwe. Ingawa kuna kelele, sio kelele za shangwe.
La joie et l’allégresse ont disparu des vergers et de la terre de Moab; j’ai fait tarir le vin des cuves; on ne le foule plus au bruit des hourrahs; le hourrah n’est plus le hourrah.
34 “Sauti ya kilio chao inapanda kutoka Heshboni hadi Eleale na Yahazi, kutoka Soari hadi Horonaimu na Eglath-Shelishiya, kwa kuwa hata maji ya Nimrimu yamekauka.
A cause du cri de Hésébon jusqu’à Eléalé; jusqu’à Jasa, ils font entendre leur cri; de Segor jusqu’à Horonaïm, jusqu’à Eglath-Sélisia; Car même les eaux de Nemrim seront taries.
35 Nitakomesha wale wote katika Moabu watoao sadaka mahali pa juu, na kufukiza uvumba kwa miungu yao,” asema Bwana.
Je veux, en finir avec Moab, — oracle de Yahweh, avec celui qui monte à son haut-lieu et offre de l’encens à son dieu.
36 “Kwa hiyo moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama filimbi; unaomboleza kama filimbi kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi. Utajiri waliojipatia umetoweka.
C’est pourquoi mon cœur au sujet de Moab, gémit comme une flûte, oui, mon cœur au sujet des gens de Qir-Hérès, gémit comme une flûte. C’est pourquoi le gain qu’ils avaient fait est perdu.
37 Kila kichwa kimenyolewa na kila mwenye ndevu zimekatwa; kila mkono umekatwa na kila kiuno kimefunikwa kwa nguo ya gunia.
Car toute tête est rasée, et toute barbe coupée; sur toutes les mains il y a des incisions; et sur les reins des sacs.
38 Juu ya mapaa yote katika Moabu na katika viwanja hakuna kitu chochote isipokuwa maombolezo, kwa kuwa nimemvunja Moabu kama gudulia ambalo hakuna mtu yeyote anayelitaka,” asema Bwana.
Sur tous les toits de Moab et sur ses places, ce ne sont que lamentations; car j’ai brisé Moab comme un vase dont on ne veut plus, — oracle de Yahweh.
39 “Tazama jinsi alivyovunjikavunjika! Jinsi wanavyolia kwa huzuni! Tazama jinsi Moabu anavyogeuka kwa aibu! Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa, kitu cha kutisha kwa wale wote wanaomzunguka.”
Comme il est brisé! Gémissez! Comme Moab a honteusement tourné le dos! Moab est devenu un objet de risée, et d’épouvante pour tous ses voisins.
40 Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama! Tai anashuka chini, akitanda mabawa yake juu ya Moabu.
Car ainsi parle Yahweh: Voici qu’il prend son vol comme l’aigle, il étend ses ailes sur Moab.
41 Miji itatekwa na ngome zake zitatwaliwa. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Moabu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
Carioth est prise, les forteresses sont emportées, et le cœur des guerriers de Moab est, en ce jour, comme le cœur d’une femme en travail.
42 Moabu ataangamizwa kama taifa kwa sababu amemdharau Bwana.
Moab est exterminé du rang des peuples, parce qu’il s’est élevé contre Yahweh.
43 Hofu kuu, shimo na mtego vinawangojea, enyi watu wa Moabu,” asema Bwana.
Epouvante, fosse et filet, sont sur toi, habitant de Moab! — oracle de Yahweh.
44 “Yeyote atakayeikimbia hiyo hofu kuu ataanguka ndani ya shimo, yeyote atakayepanda kutoka shimoni, atanaswa katika mtego, kwa sababu nitaletea Moabu mwaka wa adhabu yake,” asema Bwana.
Celui qui fuit devant l’objet d’épouvante tombera dans la fosse, et celui qui remontera de la fosse sera pris au filet; car je vais faire venir sur lui, sur Moab, l’année de sa visitation, — oracle de Yahweh.
45 “Katika kivuli cha Heshboni, wakimbizi wamesimama pasipo msaada, kwa kuwa moto umezimika huko Heshboni, mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni; unaunguza vipaji vya nyuso za Moabu, mafuvu yao wenye kujivuna kwa kelele.
A l’ombre de Hésébon ils s’arrêtent, les fuyards à bout de forces; mais il est sorti un feu de Hésébon, et une flamme du milieu de Séhon; elle a dévoré les flancs de Moab et le crâne des fils du tumulte.
46 Ole wako, ee Moabu! Watu wa Kemoshi wameangamizwa; wana wako wamepelekwa uhamishoni na binti zako wamechukuliwa mateka.
Malheur à toi, Moab! Il est perdu, le peuple de Chamos; car tes fils sont emmenés en exil, et tes filles en captivité.
47 “Lakini nitarudisha mateka wa Moabu, katika siku zijazo,” asema Bwana. Huu ndio mwisho wa hukumu juu ya Moabu.
Mais je ramènerai les captifs de Moab; à la fin des jours, — oracle de Yahweh. Jusqu’ici le jugement de Moab.