< Yeremia 47 >
1 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Wafilisti, kabla Farao hajaishambulia Gaza:
Yahweh gave to the prophet Jeremiah a message about the people of Philistia. [The message was given to me] before Gaza [city in Philistia] was captured by [the army of] Egypt.
2 Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama jinsi maji yanavyoinuka huko kaskazini, yatakuwa mafuriko yenye nguvu sana. Yataifurikia nchi na vitu vyote vilivyomo ndani yake, miji na wale waishio ndani yake. Watu watapiga kelele; wote waishio katika nchi wataomboleza
This is what Yahweh said: “[An army] [MET] will be coming from the northeast that will cover the land like a flood. They will destroy the land and everything in it; [they will destroy] people and cities. People will scream; everyone in the land will wail.
3 kwa sauti ya kwato za farasi waendao mbio, kwa sauti ya magari ya adui na mngurumo wa magurudumu yake. Baba hawatageuka kuwasaidia watoto wao, mikono yao italegea.
[They will hear] the sound of the hooves of the [enemy] horses, and [they will hear] the rumble/noise of the wheels [of their enemies’] chariots. Men [will run away; ] they will not stop to help their children; they will be completely weak and helpless [MTY].
4 Kwa maana siku imewadia kuwaangamiza Wafilisti wote na kuwakatilia mbali walionusurika wote ambao wangeweza kusaidia Tiro na Sidoni. Bwana anakaribia kuwaangamiza Wafilisti, mabaki toka pwani za Kaftori.
It will be the time for all the people of Philistia to be destroyed, and the time to prevent the remaining soldiers from helping [the people of] Tyre and Sidon [cities]. [I, ] Yahweh, will get rid of the people of Philistia, those whose ancestors [long ago] came from Crete [island].
5 Gaza atanyoa kichwa chake katika kuomboleza, Ashkeloni atanyamazishwa. Enyi mabaki kwenye tambarare, mtajikatakata wenyewe mpaka lini?
[The people of] Gaza will be humiliated; they will shave off all the hair on their heads [to indicate that they are ashamed]. The [people of] [city] will all be silent [because they will be mourning]. [All you people who live] along the coast [of the Mediterranean Sea] who are still alive, how long [RHQ] will you gash yourselves [because you are mourning]?”
6 “Mnalia, ‘Aa, upanga wa Bwana, utaendelea mpaka lini ndipo upumzike? Rudi ndani ya ala yako; acha na utulie.’
[The people of Philistia say, ] “Yahweh, when [RHQ] will you [tell our enemies to stop killing us with] [PRS] their swords? Tell them to [PRS] put them back into their sheaths and keep them there!”
7 Lakini upanga utatuliaje wakati Bwana ameuamuru, wakati ameuagiza kuishambulia Ashkeloni pamoja na pwani yake?”
But it would not be right [RHQ] for their swords to stay there, because Yahweh has commanded their enemies [to do something more]; Yahweh intends to tell them to attack [all the people living in] Ashkelon and [in other cities] along the coast.