< Yeremia 46 >

1 Hili ni neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu mataifa:
Palabra de Yahvé que vino al profeta Jeremías sobre las naciones.
2 Kuhusu Misri: Huu ni ujumbe dhidi ya jeshi la Farao Neko mfalme wa Misri, lililoshindwa huko Karkemishi kwenye Mto Frati na Nebukadneza mfalme wa Babeli, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda:
De Egipto: sobre el ejército del faraón Necoh, rey de Egipto, que estaba junto al río Éufrates, en Carquemis, que Nabucodonosor, rey de Babilonia, atacó en el cuarto año de Joacim, hijo de Josías, rey de Judá.
3 “Wekeni tayari ngao zenu, kubwa na ndogo, mtoke kwa ajili ya vita!
“Prepara el broquel y el escudo, ¡y acércate a la batalla!
4 Fungieni farasi lijamu, pandeni farasi! Shikeni nafasi zenu mkiwa mmevaa chapeo! Isugueni mikuki yenu, vaeni dirii vifuani!
Enjaezad los caballos y levantaos, jinetes, y se pongan de pie con sus cascos. Pulir las lanzas, poner los abrigos de correo.
5 Je, ninaona nini? Wametiwa hofu, wanarudi nyuma, askari wao wameshindwa. Wanakimbia kwa haraka pasipo kutazama nyuma, tena kuna hofu kuu kila upande,” asema Bwana.
¿Por qué lo he visto? Están consternados y se vuelven hacia atrás. Sus poderosos son derrotados, han huido a toda prisa, y no mires atrás. El terror está en todos los lados”. dice Yahvé.
6 Walio wepesi na wenye mbio hawawezi kukimbia, wala wenye nguvu hawawezi kutoroka. Kaskazini, kando ya Mto Frati, wanajikwaa na kuanguka.
“No dejes que el veloz huya, ni el hombre poderoso escapará. En el norte, junto al río Éufrates han tropezado y han caído.
7 “Ni nani huyu ajiinuaye kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi?
“¿Quién es ese que sube como el Nilo, como los ríos cuyas aguas crecen?
8 Misri hujiinua kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi. Husema, ‘Nitainuka na kufunika dunia, nitaiangamiza miji na watu wake.’
Egipto sube como el Nilo, como los ríos cuyas aguas crecen. Dice: “Me levantaré. Cubriré la tierra. Destruiré las ciudades y sus habitantes’.
9 Songeni mbele, enyi farasi! Endesheni kwa ukali, enyi magari ya farasi, Endeleeni mbele, enyi mashujaa: watu wa Kushi na Putu wachukuao ngao, watu wa Ludi wavutao upinde.
¡Subid, caballos! ¡Fuerza, carros! Que salgan los poderosos: Cush y Put, que manejan el escudo; y el Ludim, que maneja y dobla el arco.
10 Lakini ile siku ni ya Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, siku ya kulipiza kisasi, kisasi juu ya adui zake. Upanga utakula hata utakapotosheka, hadi utakapozima kiu yake kwa damu. Kwa maana Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatoa dhabihu kwenye nchi ya kaskazini, kando ya Mto Frati.
Porque ese día es del Señor, Yahvé de los Ejércitos, un día de venganza, para poder vengarse de sus adversarios. La espada devorará y se saciará, y beberá hasta saciarse de su sangre; porque el Señor, Yahvé de los Ejércitos, tiene un sacrificio en el país del norte, junto al río Éufrates.
11 “Panda hadi Gileadi ukapate zeri, ee Bikira Binti wa Misri. Lakini umetumia dawa nyingi bila mafanikio; huwezi kupona.
Sube a Galaad y toma bálsamo, virgen hija de Egipto. Usas muchas medicinas en vano. No hay curación para ti.
12 Mataifa yatasikia juu ya aibu yako, kilio chako kitaijaza dunia. Shujaa mmoja atajikwaa juu ya mwingine, nao wataanguka chini pamoja.”
Las naciones han oído hablar de tu vergüenza, y la tierra está llena de tu grito; porque el poderoso ha tropezado con el poderoso, caen los dos juntos”.
13 Huu ndio ujumbe Bwana aliomwambia nabii Yeremia kuhusu kuja kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ili kuishambulia Misri:
La palabra que Yahvé habló al profeta Jeremías, de que Nabucodonosor, rey de Babilonia, vendría a golpear la tierra de Egipto:
14 “Tangaza hili katika Misri, nawe ulihubiri katika Migdoli, hubiri pia katika Memfisi na Tahpanhesi: ‘Shikeni nafasi zenu na mwe tayari, kwa kuwa upanga unawala wale wanaokuzunguka.’
“Declara en Egipto, publicar en Migdol, y publicar en Memphis y en Tahpanhes; dicen: “Levántate y prepárate”, porque la espada ha devorado a tu alrededor’.
15 Kwa nini mashujaa wako wamesombwa na kupelekwa mbali? Hawawezi kusimama, kwa maana Bwana atawasukuma awaangushe chini.
¿Por qué son arrastrados tus fuertes? No se pusieron de pie, porque Yahvé los empujó.
16 Watajikwaa mara kwa mara, wataangukiana wao kwa wao. Watasema, ‘Amka, turudi kwa watu wetu na nchi yetu, mbali na upanga wa mtesi.’
Hizo tropezar a muchos. Sí, cayeron uno sobre otro. Dijeron: ‘¡Levántate! Volvamos a nuestro pueblo’, y a la tierra que nos vio nacer, de la espada opresora”.
17 Huko watatangaza, ‘Farao mfalme wa Misri ni makelele tu, amekosa wasaa wake.’
Allí gritaron: “El faraón, rey de Egipto, no es más que un ruido; ha dejado pasar el tiempo previsto”.
18 “Kwa hakika kama niishivyo,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote, “mmoja atakuja ambaye ni kama Tabori miongoni mwa milima, kama Karmeli kando ya bahari.
“Vivo yo”, dice el Rey, cuyo nombre es Yahvé de los Ejércitos, “seguramente como Tabor entre las montañas, y como el Carmelo junto al mar, para que venga.
19 Funga mizigo yako kwenda uhamishoni, wewe ukaaye Misri, kwa kuwa Memfisi utaangamizwa na kuwa magofu pasipo mkazi.
Tú, hija que vives en Egipto, amueblarse para ir al cautiverio; porque Menfis se convertirá en una desolación, y será quemado, sin habitante.
20 “Misri ni mtamba mzuri, lakini kipanga anakuja dhidi yake kutoka kaskazini.
“Egipto es una novilla muy hermosa; pero la destrucción del norte ha llegado. Ha llegado.
21 Askari wake waliokodiwa katika safu zake wako kama ndama walionenepeshwa. Wao pia watageuka na kukimbia pamoja, hawataweza kuhimili vita, kwa maana siku ya msiba inakuja juu yao, wakati wao wa kuadhibiwa.
También sus jornaleros, en medio de ella, son como terneros de corral, ya que ellos también son devueltos. Han huido juntos. No se pusieron de pie, porque les ha llegado el día de su calamidad, el momento de su visita.
22 Misri atatoa sauti kama ya nyoka anayekimbia kadiri adui anavyowasogelea na majeshi, watakuja dhidi yake wakiwa na mashoka, kama watu wakatao miti.
Su sonido será como el de la serpiente, pues marcharán con un ejército, y vienen contra ella con hachas, como cortadores de madera.
23 Wataufyeka msitu wake,” asema Bwana, “hata kama umesongamana kiasi gani. Ni wengi kuliko nzige, hawawezi kuhesabika.
Cortarán su bosque”, dice Yahvé, “aunque no se puede registrar; porque son más que las langostas, y son innumerables.
24 Binti wa Misri ataaibishwa, atatiwa mikononi mwa watu wa kaskazini.”
La hija de Egipto quedará decepcionada; será entregada a la mano de los pueblos del norte”.
25 Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asema: “Nakaribia kuleta adhabu juu ya Amoni mungu wa Thebesi, na juu ya Farao, Misri na miungu yake, na wafalme wake, pamoja na wale wanaomtegemea Farao.
Yahvé de los Ejércitos, el Dios de Israel, dice: “He aquí que yo castigaré a Amón de No, al Faraón y a Egipto, con sus dioses y sus reyes, al Faraón y a los que confían en él.
26 Nitawatia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wao, yaani Nebukadneza mfalme wa Babeli na maafisa wake. Hatimaye, hata hivyo, Misri itakaliwa kama nyakati zilizopita,” asema Bwana.
Los entregaré en manos de los que buscan su vida, en manos de Nabucodonosor, rey de Babilonia, y en manos de sus servidores. Después será habitada, como en los días de antaño”, dice Yahvé.
27 “Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, usifadhaike, ee Israeli. Hakika nitakuokoa kutoka nchi za mbali, uzao wako kutoka nchi ya uhamisho wao. Yakobo atakuwa tena na amani na salama, wala hakuna hata mmoja atakayewatia hofu.
“Pero no tengas miedo, Jacob, mi siervo. No te desanimes, Israel; pues, he aquí que te salvaré desde lejos, y tu descendencia de la tierra de su cautiverio. Jacob volverá, y estará tranquilo y a gusto. Nadie le hará tener miedo.
28 Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, kwa maana mimi niko pamoja nawe,” asema Bwana. “Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambayo miongoni mwake nimekutawanya, sitakuangamiza wewe kabisa. Nitakurudi, lakini kwa haki tu, wala sitakuacha kabisa bila kukuadhibu.”
No temas, siervo mío Jacob, dice Yahvé, “porque yo estoy con vosotros; porque voy a acabar por completo con todas las naciones a las que te he expulsado, pero no haré un final completo de ti, pero te corregiré en la medida, y de ninguna manera te dejará impune”.

< Yeremia 46 >