< Yeremia 46 >
1 Hili ni neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu mataifa:
Słowo PANA, które doszło do proroka Jeremiasza przeciw poganom;
2 Kuhusu Misri: Huu ni ujumbe dhidi ya jeshi la Farao Neko mfalme wa Misri, lililoshindwa huko Karkemishi kwenye Mto Frati na Nebukadneza mfalme wa Babeli, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda:
Przeciw Egiptowi, przeciw wojsku faraona Neko, króla Egiptu, które znajdowało się nad rzeką Eufrat pod Karkemisz, a które pobił Nabuchodonozor, król Babilonu, w czwartym roku Joakima, syna Jozjasza, króla Judy:
3 “Wekeni tayari ngao zenu, kubwa na ndogo, mtoke kwa ajili ya vita!
Przygotujcie puklerz i tarczę i ruszajcie do walki.
4 Fungieni farasi lijamu, pandeni farasi! Shikeni nafasi zenu mkiwa mmevaa chapeo! Isugueni mikuki yenu, vaeni dirii vifuani!
Zaprzęgajcie konie i wsiadajcie, jeźdźcy; stańcie w hełmach, ostrzcie włócznie, przywdziejcie pancerze.
5 Je, ninaona nini? Wametiwa hofu, wanarudi nyuma, askari wao wameshindwa. Wanakimbia kwa haraka pasipo kutazama nyuma, tena kuna hofu kuu kila upande,” asema Bwana.
Czemu widzę ich zatrwożonych i cofających się? Ich mocarze są pobici i uciekają w popłochu, nie oglądając się. Strach jest wszędzie, mówi PAN.
6 Walio wepesi na wenye mbio hawawezi kukimbia, wala wenye nguvu hawawezi kutoroka. Kaskazini, kando ya Mto Frati, wanajikwaa na kuanguka.
Prędki nie ucieknie i mocarz nie ujdzie; na północy, nad brzegiem rzeki Eufrat, potkną się i upadną.
7 “Ni nani huyu ajiinuaye kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi?
Kim jest ten, co się podnosi jak rzeka, a jego wody piętrzą się jak rzeki?
8 Misri hujiinua kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi. Husema, ‘Nitainuka na kufunika dunia, nitaiangamiza miji na watu wake.’
Egipt podnosi się jak rzeka, a jego wody piętrzą się jak w rzece i mówi: Podnoszę się, pokryję ziemię, zniszczę miasto i jego mieszkańców.
9 Songeni mbele, enyi farasi! Endesheni kwa ukali, enyi magari ya farasi, Endeleeni mbele, enyi mashujaa: watu wa Kushi na Putu wachukuao ngao, watu wa Ludi wavutao upinde.
Nacierajcie, konie, pędźcie, rydwany; niech się ruszą mocarze: Etiopczycy i Libańczycy noszący tarcze, Ludyjczycy, którzy noszą i napinają łuk.
10 Lakini ile siku ni ya Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, siku ya kulipiza kisasi, kisasi juu ya adui zake. Upanga utakula hata utakapotosheka, hadi utakapozima kiu yake kwa damu. Kwa maana Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatoa dhabihu kwenye nchi ya kaskazini, kando ya Mto Frati.
Ten dzień bowiem należy do Pana BOGA zastępów i jest dniem pomsty, aby się zemścił nad swoimi wrogami. Miecz będzie pożerał i nasyci się, i upije się ich krwią, gdyż Pan Bóg zastępów ma ofiarę w ziemi północnej, nad rzeką Eufrat.
11 “Panda hadi Gileadi ukapate zeri, ee Bikira Binti wa Misri. Lakini umetumia dawa nyingi bila mafanikio; huwezi kupona.
Wstąp do Gileadu i nabierz balsamu, dziewico, córko Egiptu. Ale daremnie używasz wielu lekarstw, bo nie będziesz uleczona.
12 Mataifa yatasikia juu ya aibu yako, kilio chako kitaijaza dunia. Shujaa mmoja atajikwaa juu ya mwingine, nao wataanguka chini pamoja.”
Narody słyszały o twojej hańbie i twój lament napełnił ziemię, gdyż mocarz potknął się o mocarza i obaj razem upadli.
13 Huu ndio ujumbe Bwana aliomwambia nabii Yeremia kuhusu kuja kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ili kuishambulia Misri:
Słowo, które PAN wypowiedział do proroka Jeremiasza, o wyprawie Nabuchodonozora, króla Babilonu, aby uderzyć ziemię Egiptu:
14 “Tangaza hili katika Misri, nawe ulihubiri katika Migdoli, hubiri pia katika Memfisi na Tahpanhesi: ‘Shikeni nafasi zenu na mwe tayari, kwa kuwa upanga unawala wale wanaokuzunguka.’
Oznajmijcie w Egipcie i ogłoście w Migdol; opowiadajcie w Nof i w Tachpanches. Powiedzcie: Stań i przygotuj się, bo miecz pożre to, co jest dokoła ciebie.
15 Kwa nini mashujaa wako wamesombwa na kupelekwa mbali? Hawawezi kusimama, kwa maana Bwana atawasukuma awaangushe chini.
Czemu twoi mocarze zostali powaleni? Nie mogli się ostać, gdyż natarł na nich PAN.
16 Watajikwaa mara kwa mara, wataangukiana wao kwa wao. Watasema, ‘Amka, turudi kwa watu wetu na nchi yetu, mbali na upanga wa mtesi.’
Wielu potknęło się, a padli jeden na drugiego. Mówili: Wstań, wróćmy do naszego ludu i do ziemi ojczystej przed ostrzem niszczycielskiego miecza.
17 Huko watatangaza, ‘Farao mfalme wa Misri ni makelele tu, amekosa wasaa wake.’
Tam zawołali: Faraon, król Egiptu, [to tylko próżny] trzask; [jego] ustalony czas już minął.
18 “Kwa hakika kama niishivyo,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote, “mmoja atakuja ambaye ni kama Tabori miongoni mwa milima, kama Karmeli kando ya bahari.
Jak żyję ja – mówi Król, a jego imię PAN zastępów – jak Tabor wśród gór i jak Karmel nad morzem, [tak] on przyjdzie.
19 Funga mizigo yako kwenda uhamishoni, wewe ukaaye Misri, kwa kuwa Memfisi utaangamizwa na kuwa magofu pasipo mkazi.
Córko, która mieszkasz w Egipcie, przygotuj swoje rzeczy na niewolę, bo Nof będzie pustkowiem i spustoszeniem, bez mieszkańców.
20 “Misri ni mtamba mzuri, lakini kipanga anakuja dhidi yake kutoka kaskazini.
Egipt [jest jak] piękna jałówka, [ale jej] zniszczenie nadchodzi, idzie z północy.
21 Askari wake waliokodiwa katika safu zake wako kama ndama walionenepeshwa. Wao pia watageuka na kukimbia pamoja, hawataweza kuhimili vita, kwa maana siku ya msiba inakuja juu yao, wakati wao wa kuadhibiwa.
Najemnicy pośród niego [są] jak tuczone cielęta, bo oni także odwrócili się i uciekli razem. Nie ostali się, bo przyszedł na nich dzień ich porażki, czas ich nawiedzenia.
22 Misri atatoa sauti kama ya nyoka anayekimbia kadiri adui anavyowasogelea na majeshi, watakuja dhidi yake wakiwa na mashoka, kama watu wakatao miti.
Jego głos jak [głos] węża, bo nadciągną z wojskiem, z siekierami przyjdą przeciw niemu jak rąbiący drzewa.
23 Wataufyeka msitu wake,” asema Bwana, “hata kama umesongamana kiasi gani. Ni wengi kuliko nzige, hawawezi kuhesabika.
Wyrąbią jego las, mówi PAN, choć nie da się [go] policzyć. Są bowiem liczniejsi od szarańczy i niezliczeni.
24 Binti wa Misri ataaibishwa, atatiwa mikononi mwa watu wa kaskazini.”
Zawstydzi się córka Egiptu, będzie wydana w ręce ludu z północy.
25 Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asema: “Nakaribia kuleta adhabu juu ya Amoni mungu wa Thebesi, na juu ya Farao, Misri na miungu yake, na wafalme wake, pamoja na wale wanaomtegemea Farao.
PAN zastępów, Bóg Izraela, mówi: Oto ukarzę cały liczny lud miasta No, także faraona i Egipt, jego bogów i królów, faraona i tych, którzy pokładają w nim ufność.
26 Nitawatia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wao, yaani Nebukadneza mfalme wa Babeli na maafisa wake. Hatimaye, hata hivyo, Misri itakaliwa kama nyakati zilizopita,” asema Bwana.
I wydam ich w ręce tych, którzy czyhają na ich życie, w ręce Nabuchodonozora, króla Babilonu, i w ręce jego sług. Lecz potem będzie zamieszkały jak za dawnych dni, mówi PAN.
27 “Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, usifadhaike, ee Israeli. Hakika nitakuokoa kutoka nchi za mbali, uzao wako kutoka nchi ya uhamisho wao. Yakobo atakuwa tena na amani na salama, wala hakuna hata mmoja atakayewatia hofu.
Ale ty się nie bój, mój sługo, Jakubie, i nie lękaj się, Izraelu. Oto bowiem wybawię cię z daleka i twoje potomstwo z ziemi jego niewoli. Jakub powróci i zazna odpoczynku i pokoju, a nikt go nie zatrwoży.
28 Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, kwa maana mimi niko pamoja nawe,” asema Bwana. “Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambayo miongoni mwake nimekutawanya, sitakuangamiza wewe kabisa. Nitakurudi, lakini kwa haki tu, wala sitakuacha kabisa bila kukuadhibu.”
Nie bój się, Jakubie, mój sługo, mówi PAN, bo ja jestem z tobą. Położę kres wszystkim narodom, do których cię wypędziłem. Tobie jednak nie położę kresu, ale będę cię karał sprawiedliwie; nie zostawię cię całkiem bez kary.