< Yeremia 46 >

1 Hili ni neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu mataifa:
which to be word LORD to(wards) Jeremiah [the] prophet upon [the] nation
2 Kuhusu Misri: Huu ni ujumbe dhidi ya jeshi la Farao Neko mfalme wa Misri, lililoshindwa huko Karkemishi kwenye Mto Frati na Nebukadneza mfalme wa Babeli, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda:
to/for Egypt upon strength: soldiers Pharaoh (Neco) (Pharaoh) Neco king Egypt which to be upon river Euphrates in/on/with Carchemish which to smite Nebuchadnezzar king Babylon in/on/with year [the] fourth to/for Jehoiakim son: child Josiah king Judah
3 “Wekeni tayari ngao zenu, kubwa na ndogo, mtoke kwa ajili ya vita!
to arrange shield and shield and to approach: approach to/for battle
4 Fungieni farasi lijamu, pandeni farasi! Shikeni nafasi zenu mkiwa mmevaa chapeo! Isugueni mikuki yenu, vaeni dirii vifuani!
to bind [the] horse and to ascend: copulate [the] horse and to stand in/on/with helmet to polish [the] spear to clothe [the] armor
5 Je, ninaona nini? Wametiwa hofu, wanarudi nyuma, askari wao wameshindwa. Wanakimbia kwa haraka pasipo kutazama nyuma, tena kuna hofu kuu kila upande,” asema Bwana.
why? to see: see they(masc.) shattered to turn back and mighty man their to crush and refuge to flee and not to turn terror from around: side utterance LORD
6 Walio wepesi na wenye mbio hawawezi kukimbia, wala wenye nguvu hawawezi kutoroka. Kaskazini, kando ya Mto Frati, wanajikwaa na kuanguka.
not to flee [the] swift and not to escape [the] mighty man north [to] upon hand: by river Euphrates to stumble and to fall: fall
7 “Ni nani huyu ajiinuaye kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi?
who? this like/as Nile to ascend: rise like/as river to shake water his
8 Misri hujiinua kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi. Husema, ‘Nitainuka na kufunika dunia, nitaiangamiza miji na watu wake.’
Egypt like/as Nile to ascend: rise and like/as river to shake water and to say to ascend: rise to cover land: country/planet to perish city and to dwell in/on/with her
9 Songeni mbele, enyi farasi! Endesheni kwa ukali, enyi magari ya farasi, Endeleeni mbele, enyi mashujaa: watu wa Kushi na Putu wachukuao ngao, watu wa Ludi wavutao upinde.
to ascend: rise [the] horse and to boast: rave madly [the] chariot and to come out: come [the] mighty man Cush and Put to capture shield and Lydian to capture to tread bow
10 Lakini ile siku ni ya Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, siku ya kulipiza kisasi, kisasi juu ya adui zake. Upanga utakula hata utakapotosheka, hadi utakapozima kiu yake kwa damu. Kwa maana Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatoa dhabihu kwenye nchi ya kaskazini, kando ya Mto Frati.
and [the] day [the] he/she/it to/for Lord YHWH/God Hosts day vengeance to/for to avenge from enemy his and to eat sword and to satisfy and to quench from blood their for sacrifice to/for Lord YHWH/God Hosts in/on/with land: country/planet north to(wards) river Euphrates
11 “Panda hadi Gileadi ukapate zeri, ee Bikira Binti wa Misri. Lakini umetumia dawa nyingi bila mafanikio; huwezi kupona.
to ascend: rise Gilead and to take: take balsam virgin daughter Egypt to/for vanity: vain (to multiply *Q(K)*) remedy healing nothing to/for you
12 Mataifa yatasikia juu ya aibu yako, kilio chako kitaijaza dunia. Shujaa mmoja atajikwaa juu ya mwingine, nao wataanguka chini pamoja.”
to hear: hear nation dishonor your and outcry your to fill [the] land: country/planet for mighty man in/on/with mighty man to stumble together to fall: fall two their
13 Huu ndio ujumbe Bwana aliomwambia nabii Yeremia kuhusu kuja kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ili kuishambulia Misri:
[the] word which to speak: speak LORD to(wards) Jeremiah [the] prophet to/for to come (in): come Nebuchadnezzar king Babylon to/for to smite [obj] land: country/planet Egypt
14 “Tangaza hili katika Misri, nawe ulihubiri katika Migdoli, hubiri pia katika Memfisi na Tahpanhesi: ‘Shikeni nafasi zenu na mwe tayari, kwa kuwa upanga unawala wale wanaokuzunguka.’
to tell in/on/with Egypt and to hear: proclaim in/on/with Migdol and to hear: proclaim in/on/with Memphis and in/on/with Tahpanhes to say to stand and to establish: prepare to/for you for to eat sword around you
15 Kwa nini mashujaa wako wamesombwa na kupelekwa mbali? Hawawezi kusimama, kwa maana Bwana atawasukuma awaangushe chini.
why? to prostatrate mighty: strong your not to stand: stand for LORD to thrust him
16 Watajikwaa mara kwa mara, wataangukiana wao kwa wao. Watasema, ‘Amka, turudi kwa watu wetu na nchi yetu, mbali na upanga wa mtesi.’
to multiply to stumble also to fall: fall man: anyone to(wards) neighbor his and to say to arise: rise [emph?] and to return: return to(wards) people our and to(wards) land: country/planet relatives our from face: because sword [the] to oppress
17 Huko watatangaza, ‘Farao mfalme wa Misri ni makelele tu, amekosa wasaa wake.’
to call: call to there Pharaoh king Egypt roar to pass [the] meeting: time appointed
18 “Kwa hakika kama niishivyo,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote, “mmoja atakuja ambaye ni kama Tabori miongoni mwa milima, kama Karmeli kando ya bahari.
alive I utterance [the] king LORD Hosts name his for like/as (Mount) Tabor in/on/with mountain: mount and like/as Carmel in/on/with sea to come (in): come
19 Funga mizigo yako kwenda uhamishoni, wewe ukaaye Misri, kwa kuwa Memfisi utaangamizwa na kuwa magofu pasipo mkazi.
article/utensil captivity to make to/for you to dwell daughter Egypt for Memphis to/for horror: destroyed to be and to kindle from nothing to dwell
20 “Misri ni mtamba mzuri, lakini kipanga anakuja dhidi yake kutoka kaskazini.
heifer pretty pretty Egypt stinging fly from north to come (in): come to come (in): come
21 Askari wake waliokodiwa katika safu zake wako kama ndama walionenepeshwa. Wao pia watageuka na kukimbia pamoja, hawataweza kuhimili vita, kwa maana siku ya msiba inakuja juu yao, wakati wao wa kuadhibiwa.
also hired her in/on/with entrails: among her like/as calf stall for also they(masc.) to turn to flee together not to stand: stand for day calamity their to come (in): come upon them time punishment their
22 Misri atatoa sauti kama ya nyoka anayekimbia kadiri adui anavyowasogelea na majeshi, watakuja dhidi yake wakiwa na mashoka, kama watu wakatao miti.
voice: sound her like/as serpent to go: walk for in/on/with strength: soldiers to go: walk and in/on/with axe to come (in): come to/for her like/as to chop tree
23 Wataufyeka msitu wake,” asema Bwana, “hata kama umesongamana kiasi gani. Ni wengi kuliko nzige, hawawezi kuhesabika.
to cut: cut wood her utterance LORD for not to search for to multiply from locust and nothing to/for them number
24 Binti wa Misri ataaibishwa, atatiwa mikononi mwa watu wa kaskazini.”
be ashamed daughter Egypt to give: give in/on/with hand: power people north
25 Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asema: “Nakaribia kuleta adhabu juu ya Amoni mungu wa Thebesi, na juu ya Farao, Misri na miungu yake, na wafalme wake, pamoja na wale wanaomtegemea Farao.
to say LORD Hosts God Israel look! I to reckon: punish to(wards) Amon from Thebes and upon Pharaoh and upon Egypt and upon God her and upon king her and upon Pharaoh and upon [the] to trust in/on/with him
26 Nitawatia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wao, yaani Nebukadneza mfalme wa Babeli na maafisa wake. Hatimaye, hata hivyo, Misri itakaliwa kama nyakati zilizopita,” asema Bwana.
and to give: give them in/on/with hand: power to seek soul: life their and in/on/with hand: power Nebuchadnezzar king Babylon and in/on/with hand: power servant/slave his and after so to dwell like/as day front: old utterance LORD
27 “Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, usifadhaike, ee Israeli. Hakika nitakuokoa kutoka nchi za mbali, uzao wako kutoka nchi ya uhamisho wao. Yakobo atakuwa tena na amani na salama, wala hakuna hata mmoja atakayewatia hofu.
and you(m. s.) not to fear servant/slave my Jacob and not to to be dismayed Israel for look! I to save you from distant and [obj] seed: children your from land: country/planet captivity their and to return: return Jacob and to quiet and to rest and nothing to tremble
28 Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, kwa maana mimi niko pamoja nawe,” asema Bwana. “Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambayo miongoni mwake nimekutawanya, sitakuangamiza wewe kabisa. Nitakurudi, lakini kwa haki tu, wala sitakuacha kabisa bila kukuadhibu.”
you(m. s.) not to fear servant/slave my Jacob utterance LORD for with you I for to make consumption in/on/with all [the] nation which to banish you there [to] and [obj] you not to make consumption and to discipline you to/for justice and to clear not to clear you

< Yeremia 46 >