< Yeremia 46 >

1 Hili ni neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu mataifa:
Herrens Ord, som kom til Profeten Jeremias, imod Hedningerne.
2 Kuhusu Misri: Huu ni ujumbe dhidi ya jeshi la Farao Neko mfalme wa Misri, lililoshindwa huko Karkemishi kwenye Mto Frati na Nebukadneza mfalme wa Babeli, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda:
Imod Ægypten, imod Farao-Neko, Kongen af Ægyptens Hær, som stod ved Floden Eufrat fra Karkemis, og som Nebukadnezar, Kongen af Babel, slog i Judas Konge Jojakims, Josias's Søns fjerde Aar:
3 “Wekeni tayari ngao zenu, kubwa na ndogo, mtoke kwa ajili ya vita!
Bereder smaa Skjolde og store Skjolde, og kommer frem til Striden.
4 Fungieni farasi lijamu, pandeni farasi! Shikeni nafasi zenu mkiwa mmevaa chapeo! Isugueni mikuki yenu, vaeni dirii vifuani!
Spænder Hestene for og stiger op paa Hestene, og stiller eder frem med Hjelme paa; polerer Spydene, ifører eder Panserne!
5 Je, ninaona nini? Wametiwa hofu, wanarudi nyuma, askari wao wameshindwa. Wanakimbia kwa haraka pasipo kutazama nyuma, tena kuna hofu kuu kila upande,” asema Bwana.
Hvorfor ser jeg dem forfærdede og vigende tilbage, og at deres vældige knuses og ilsomt fly uden at se tilbage? Rædsel trindt omkring, siger Herren.
6 Walio wepesi na wenye mbio hawawezi kukimbia, wala wenye nguvu hawawezi kutoroka. Kaskazini, kando ya Mto Frati, wanajikwaa na kuanguka.
Den lette skal ikke undfly, og den vældige ikke undkomme; imod Nord, ved Bredden af Floden Eufrat, snuble de og falde.
7 “Ni nani huyu ajiinuaye kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi?
Hvo er denne, der stiger op som Nilen, hvis Vande bølge som Floderne?
8 Misri hujiinua kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi. Husema, ‘Nitainuka na kufunika dunia, nitaiangamiza miji na watu wake.’
Ægypten stiger op som Nilen, og Vandene bølge som Floderne; og det sagde: Jeg vil stige op, bedække Landet, ødelægge Stæder og dem, som bo deri.
9 Songeni mbele, enyi farasi! Endesheni kwa ukali, enyi magari ya farasi, Endeleeni mbele, enyi mashujaa: watu wa Kushi na Putu wachukuao ngao, watu wa Ludi wavutao upinde.
Drager op, I Heste! og raser, I Vogne! og lader de vældige drage ud: Morland og Put, udrustede med Skjold, og Ludierne, de i øvede Bueskytter.
10 Lakini ile siku ni ya Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, siku ya kulipiza kisasi, kisasi juu ya adui zake. Upanga utakula hata utakapotosheka, hadi utakapozima kiu yake kwa damu. Kwa maana Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatoa dhabihu kwenye nchi ya kaskazini, kando ya Mto Frati.
Og denne Dag er Herrens, den Herre Zebaoths Hævns Dag, da han vil hævne sig paa sine Modstandere, og Sværdet skal fortære dem, og blive mæt og vædet af deres Blod; thi Herren, den Herre Zebaoth har Slagtoffer i Nordenland ved Floden Eufrat.
11 “Panda hadi Gileadi ukapate zeri, ee Bikira Binti wa Misri. Lakini umetumia dawa nyingi bila mafanikio; huwezi kupona.
Drag op til Gilead og hent Balsam, du Jomfru, Ægyptens Datter! forgæves bruger du megen Lægedom; der er ingen Helbredelse for dig.
12 Mataifa yatasikia juu ya aibu yako, kilio chako kitaijaza dunia. Shujaa mmoja atajikwaa juu ya mwingine, nao wataanguka chini pamoja.”
Folkefærd hørte din Skam, og dit Klagemaal fyldte Landet; thi den vældige snublede over den vældige, de faldt begge tilsammen.
13 Huu ndio ujumbe Bwana aliomwambia nabii Yeremia kuhusu kuja kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ili kuishambulia Misri:
Det Ord, som Herren talte til Profeten Jeremias, om at Nebukadnezar, Kongen af Babel, skulde komme at slaa Ægyptens Land:
14 “Tangaza hili katika Misri, nawe ulihubiri katika Migdoli, hubiri pia katika Memfisi na Tahpanhesi: ‘Shikeni nafasi zenu na mwe tayari, kwa kuwa upanga unawala wale wanaokuzunguka.’
Kundgører det i Ægypten, og lader det høres i Migdol, og lader det høres i Nof og i Thakpankes; siger: Stil dig frem, lav dig til, thi Sværdet har fortæret, hvad der er trindt omkring dig.
15 Kwa nini mashujaa wako wamesombwa na kupelekwa mbali? Hawawezi kusimama, kwa maana Bwana atawasukuma awaangushe chini.
Hvorfor ere dine mægtige slagne ned? de holdt ikke Stand, thi Herren stødte dem ned.
16 Watajikwaa mara kwa mara, wataangukiana wao kwa wao. Watasema, ‘Amka, turudi kwa watu wetu na nchi yetu, mbali na upanga wa mtesi.’
Han bragte mange til at snuble; den ene faldt endog over den anden, og de sagde: Staar op og lader os vende tilbage til vort Folk og til vort Fædreland, for Ødelæggelsens Sværd.
17 Huko watatangaza, ‘Farao mfalme wa Misri ni makelele tu, amekosa wasaa wake.’
Der raabte de: Farao, Kongen af Ægypten, er et Bulder; han lod den bestemte Tid gaa forbi.
18 “Kwa hakika kama niishivyo,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote, “mmoja atakuja ambaye ni kama Tabori miongoni mwa milima, kama Karmeli kando ya bahari.
Saa sandt jeg lever, siger Kongen, hvis Navn er Herre Zebaoth: Som Tabor iblandt Bjergene og som Karmel ved Havet, skal han komme.
19 Funga mizigo yako kwenda uhamishoni, wewe ukaaye Misri, kwa kuwa Memfisi utaangamizwa na kuwa magofu pasipo mkazi.
Skaf dig Rejsetøj, du Indbyggerske, Ægyptens Datter I thi Nof skal blive øde og opbrændes, saa at ingen skal bo deri.
20 “Misri ni mtamba mzuri, lakini kipanga anakuja dhidi yake kutoka kaskazini.
Ægypten er en saare dejlig Kvie; Fordærvelse fra Norden kommer, den kommer.
21 Askari wake waliokodiwa katika safu zake wako kama ndama walionenepeshwa. Wao pia watageuka na kukimbia pamoja, hawataweza kuhimili vita, kwa maana siku ya msiba inakuja juu yao, wakati wao wa kuadhibiwa.
Ogsaa dets Lejesvende i dets Midte, der ere som fedede Kalve, ogsaa disse vende om, de fly til Hobe, de holde ikke Stand; thi deres Fordærvelses Dag kommer over dem, deres Hjemsøgelses Tid.
22 Misri atatoa sauti kama ya nyoka anayekimbia kadiri adui anavyowasogelea na majeshi, watakuja dhidi yake wakiwa na mashoka, kama watu wakatao miti.
Dets Lyd er som Slangens, der bevæger sig frem; thi med en Hær rykke de frem, og med Økser anfalde de det som de, der ville omhugge Træer.
23 Wataufyeka msitu wake,” asema Bwana, “hata kama umesongamana kiasi gani. Ni wengi kuliko nzige, hawawezi kuhesabika.
De skulle udrydde dets Skov, siger Herren, thi den er uigennemtrængelig; thi de ere flere end Græshopper, og der er ikke Tal paa dem.
24 Binti wa Misri ataaibishwa, atatiwa mikononi mwa watu wa kaskazini.”
Ægyptens Datter er beskæmmet, hun er given i Nordens Folks Haand.
25 Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asema: “Nakaribia kuleta adhabu juu ya Amoni mungu wa Thebesi, na juu ya Farao, Misri na miungu yake, na wafalme wake, pamoja na wale wanaomtegemea Farao.
Den Herre Zebaoth, Israels Gud, siger: Se, jeg hjemsøger Amon fra No og Farao og Ægypten, og dets Guder og dets Konger, ja Farao og dem, som forlade sig paa ham.
26 Nitawatia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wao, yaani Nebukadneza mfalme wa Babeli na maafisa wake. Hatimaye, hata hivyo, Misri itakaliwa kama nyakati zilizopita,” asema Bwana.
Og jeg vil give dem i deres Haand, som søge efter deres Liv, i Nebukadnezar, Kongen af Babels, Haand, og i hans Tjeners Haand; og derefter skal det holde sig roligt, ligesom i gamle Dage, siger Herren.
27 “Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, usifadhaike, ee Israeli. Hakika nitakuokoa kutoka nchi za mbali, uzao wako kutoka nchi ya uhamisho wao. Yakobo atakuwa tena na amani na salama, wala hakuna hata mmoja atakayewatia hofu.
Men du, frygt du ej, min Tjener Jakob, og forfærdes ikke, Israel; thi se, jeg frelser dig fra et langt bortliggende Land og din Sæd fra deres Fangenskabs Land; og Jakob skal komme tilbage og bo stille og roligt, og ingen skal forfærde ham.
28 Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, kwa maana mimi niko pamoja nawe,” asema Bwana. “Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambayo miongoni mwake nimekutawanya, sitakuangamiza wewe kabisa. Nitakurudi, lakini kwa haki tu, wala sitakuacha kabisa bila kukuadhibu.”
Frygt du ej, min Tjener Jakob! siger Herren, thi jeg er med dig; thi jeg vil lade det tage en Ende med alle de Folk, til hvilke jeg havde fordrevet dig; men med dig vil jeg ikke lade det tage Ende, men tugte dig med Maade og ikke lade dig slippe aldeles fri.

< Yeremia 46 >