< Yeremia 45 >

1 Hili ndilo nabii Yeremia alilomwambia Baruku mwana wa Neria katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, baada ya Baruku kuandika katika kitabu maneno ambayo yalitoka kinywani mwa Yeremia wakati ule:
The message that Jeremiah the prophet spoke to Baruch the son of Neriah, when he wrote these words in a book at the mouth of Jeremiah, in the fourth year of Jehoiakim the son of Josiah, king of Judah, saying,
2 “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, akuambialo wewe Baruku:
“Yahweh, the God of Israel, says to you, Baruch:
3 Ulisema, ‘Ole wangu! Bwana ameongeza huzuni juu ya maumivu yangu, nimechoka kwa kulia kwa uchungu wala sipati pumziko.’”
‘You said, “Woe is me now! For Yahweh has added sorrow to my pain! I am weary with my groaning, and I find no rest.”’
4 Bwana akasema, “Mwambie hivi: ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Nitakibomoa kile nilichokijenga, na kungʼoa kile nilichokipanda katika nchi yote.
“You shall tell him, Yahweh says: ‘Behold, that which I have built, I will break down, and that which I have planted I will pluck up; and this in the whole land.
5 Je, utajitafutia mambo makubwa kwa ajili yako mwenyewe? Usiyatafute hayo. Kwa kuwa nitaleta maangamizi juu ya watu wote, asema Bwana, lakini popote utakapokwenda, nitayaokoa maisha yako.’”
Do you seek great things for yourself? Don’t seek them; for, behold, I will bring evil on all flesh,’ says Yahweh, ‘but I will let you escape with your life wherever you go.’”

< Yeremia 45 >