< Yeremia 45 >
1 Hili ndilo nabii Yeremia alilomwambia Baruku mwana wa Neria katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, baada ya Baruku kuandika katika kitabu maneno ambayo yalitoka kinywani mwa Yeremia wakati ule:
[the] word which to speak: speak Jeremiah [the] prophet to(wards) Baruch son: child Neriah in/on/with to write he [obj] [the] word [the] these upon scroll: book from lip Jeremiah in/on/with year [the] fourth to/for Jehoiakim son: child Josiah king Judah to/for to say
2 “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, akuambialo wewe Baruku:
thus to say LORD God Israel upon you Baruch
3 Ulisema, ‘Ole wangu! Bwana ameongeza huzuni juu ya maumivu yangu, nimechoka kwa kulia kwa uchungu wala sipati pumziko.’”
to say woe! please to/for me for to add LORD sorrow upon pain my be weary/toil in/on/with sighing my and resting not to find
4 Bwana akasema, “Mwambie hivi: ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Nitakibomoa kile nilichokijenga, na kungʼoa kile nilichokipanda katika nchi yote.
thus to say to(wards) him thus to say LORD behold which to build I to overthrow and [obj] which to plant I to uproot and [obj] all [the] land: country/planet he/she/it
5 Je, utajitafutia mambo makubwa kwa ajili yako mwenyewe? Usiyatafute hayo. Kwa kuwa nitaleta maangamizi juu ya watu wote, asema Bwana, lakini popote utakapokwenda, nitayaokoa maisha yako.’”
and you(m. s.) to seek to/for you great: large not to seek for look! I to come (in): bring distress: harm upon all flesh utterance LORD and to give: give to/for you [obj] soul: life your to/for spoil upon all [the] place which to go: went there