< Yeremia 45 >

1 Hili ndilo nabii Yeremia alilomwambia Baruku mwana wa Neria katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, baada ya Baruku kuandika katika kitabu maneno ambayo yalitoka kinywani mwa Yeremia wakati ule:
The word which he spoke Jeremiah the prophet to Baruch [the] son of Neriah when wrote he the words these on a scroll from [the] mouth of Jeremiah in the year fourth of Jehoiakim [the] son of Josiah [the] king of Judah saying.
2 “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, akuambialo wewe Baruku:
Thus he says Yahweh [the] God of Israel to you O Baruch.
3 Ulisema, ‘Ole wangu! Bwana ameongeza huzuni juu ya maumivu yangu, nimechoka kwa kulia kwa uchungu wala sipati pumziko.’”
You said woe! please to me for he has added Yahweh sorrow to pain my I am weary with groaning my and rest not I have found.
4 Bwana akasema, “Mwambie hivi: ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Nitakibomoa kile nilichokijenga, na kungʼoa kile nilichokipanda katika nchi yote.
Thus - you will say to him thus he says Yahweh here! [that] which I have built I [am] about to tear down and [that] which I have planted I [am] about to pluck up and all the land it.
5 Je, utajitafutia mambo makubwa kwa ajili yako mwenyewe? Usiyatafute hayo. Kwa kuwa nitaleta maangamizi juu ya watu wote, asema Bwana, lakini popote utakapokwenda, nitayaokoa maisha yako.’”
And you you are seeking for yourself great [things] may not you seek [them] for here I [am] about to bring calamity on all flesh [the] utterance of Yahweh and I will give to you life your to plunder at all the places where you will go there.

< Yeremia 45 >