< Yeremia 45 >

1 Hili ndilo nabii Yeremia alilomwambia Baruku mwana wa Neria katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, baada ya Baruku kuandika katika kitabu maneno ambayo yalitoka kinywani mwa Yeremia wakati ule:
The word which Jeremiah the prophet spake to Baruch, the son of Neriah, after he had written these words in a book from the mouth of Jeremiah, in the fourth year of Jehoiakim, the son of Josiah, the king of Judah, saying: —
2 “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, akuambialo wewe Baruku:
Thus saith Jehovah, the God of Israel, to thee, O Baruch!
3 Ulisema, ‘Ole wangu! Bwana ameongeza huzuni juu ya maumivu yangu, nimechoka kwa kulia kwa uchungu wala sipati pumziko.’”
Thou sayest, “Woe now to me, for Jehovah hath added grief to my sorrow! I am weary with my sighing, and find no rest.”
4 Bwana akasema, “Mwambie hivi: ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Nitakibomoa kile nilichokijenga, na kungʼoa kile nilichokipanda katika nchi yote.
Thus shalt thou say to him: Thus saith Jehovah: Behold, that which I myself have builded do I break down, and that which I myself have planted do I pluck up, even this whole land;
5 Je, utajitafutia mambo makubwa kwa ajili yako mwenyewe? Usiyatafute hayo. Kwa kuwa nitaleta maangamizi juu ya watu wote, asema Bwana, lakini popote utakapokwenda, nitayaokoa maisha yako.’”
and seekest thou great things for thyself? Seek them not; for behold, I am about to bring evil upon all flesh, saith Jehovah; but thy life will I give thee, as a prey, in all places whither thou shalt go.

< Yeremia 45 >