< Yeremia 45 >

1 Hili ndilo nabii Yeremia alilomwambia Baruku mwana wa Neria katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, baada ya Baruku kuandika katika kitabu maneno ambayo yalitoka kinywani mwa Yeremia wakati ule:
The word that Jeremiah the prophet spoke to Baruch, the son of Neriah, when he had written these words in a book, from the mouth of Jeremiah, in the fourth year of Jehoiakim, the son of Josiah, the king of Judah, saying:
2 “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, akuambialo wewe Baruku:
“Thus says the Lord, the God of Israel, to you, Baruch:
3 Ulisema, ‘Ole wangu! Bwana ameongeza huzuni juu ya maumivu yangu, nimechoka kwa kulia kwa uchungu wala sipati pumziko.’”
You have said: ‘Woe to me, a wretched man! For the Lord has added sorrow to my sorrow. I have labored in my groaning, and I have not found rest.’
4 Bwana akasema, “Mwambie hivi: ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Nitakibomoa kile nilichokijenga, na kungʼoa kile nilichokipanda katika nchi yote.
Thus says the Lord: So shall you say to him: Behold, those whom I have built up, I destroy, and those whom I have planted, I uproot, even this entire land.
5 Je, utajitafutia mambo makubwa kwa ajili yako mwenyewe? Usiyatafute hayo. Kwa kuwa nitaleta maangamizi juu ya watu wote, asema Bwana, lakini popote utakapokwenda, nitayaokoa maisha yako.’”
And are you seeking great things for yourself? Do not choose to seek them. For behold, I will lead evil over all that is flesh, says the Lord. But I will give your life to you unto salvation, in every place, wherever you may travel.”

< Yeremia 45 >