< Yeremia 44 >
1 Neno hili lilimjia Yeremia kuhusu Wayahudi wote waishio Misri, huko Migdoli, Tahpanhesi na Memfisi, katika nchi ya Pathrosi kusema:
Beseda, ki je prišla Jeremiju glede vseh Judov, ki prebivajo v egiptovski deželi, ki prebivajo v Migdólu, v Tahpanhésu, v Nofu in v deželi Patrós, rekoč:
2 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Mliona maangamizi makubwa niliyoyaleta juu ya Yerusalemu na juu ya miji yote ya Yuda. Leo imeachwa ukiwa na magofu
»Tako govori Gospod nad bojevniki, Izraelov Bog: ›Videli ste vse zlo, ki sem ga privedel nad Jeruzalem in nad vsa Judova mesta, in glejte, ta dan so ta opustošenje in noben človek ne prebiva tam
3 kwa sababu ya uovu waliokuwa wameufanya. Walinikasirisha kwa kufukiza uvumba na kwa kuabudu miungu mingine ambayo kamwe wao, wala ninyi, wala baba zenu hawakuifahamu.
zaradi njihove zlobnosti, ki so jo zagrešili, da me dražijo do jeze v tem, da so odšli zažigat kadilo in da služijo drugim bogovom, ki jih niso poznali niti oni, da, niti vaši očetje.
4 Tena na tena, niliwatuma watumishi wangu manabii ambao walisema, ‘Msifanye jambo hili la kuchukiza ambalo nalichukia!’
Vendar sem vam pošiljal vse svoje služabnike preroke, vzdigujoče zgodaj in jih pošiljal, rekoč: ›O ne storite te gnusne stvari, ki jo sovražim.‹
5 Lakini hawakusikiliza wala hawakujali, hawakugeuka ili kuuacha uovu wao, wala hawakuacha kufukiza uvumba kwa miungu mingine.
Toda niso prisluhnili niti nagnili svojega ušesa, da se odvrnejo od svoje zlobnosti, da ne bi zažigali kadila drugim bogovom.
6 Kwa hiyo hasira yangu kali ilimwagika, ikawaka dhidi ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, na kuifanya ukiwa na magofu kama ilivyo leo.
Zato sta bila moj bes in moja jeza izlita naprej in vžgana v Judovih mestih in na ulicah Jeruzalema; in ta so opustošena in zapuščena kakor ta dan.‹
7 “Basi hili ndilo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Kwa nini kujiletea maafa makubwa kama haya juu yenu kwa kujikatilia mbali kutoka Yuda wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao, hata kujiacha bila mabaki?
Zaradi tega sedaj tako govori Gospod, Bog nad bojevniki, Izraelov Bog: ›Zakaj ste zagrešili to veliko zlo zoper svoje duše, da izmed sebe iztrebite moškega in žensko, otroka in dojenčka, ven iz Juda, da nikogar ne pustite, da preostane.
8 Kwa nini kuichochea hasira yangu kwa kile ambacho mikono yenu imekitengeneza, mkaifukizia uvumba miungu mingine huko Misri, mahali mlipokuja kuishi? Mtajiangamiza wenyewe na kujifanya kitu cha kulaania na shutumu miongoni mwa mataifa yote duniani.
V čem ste me dražili do besa z deli svojih rok, zažigajoč kadilo drugim bogovom v egiptovski deželi, kamor ste odšli, da prebivate, da se lahko sami odrežete in da ste lahko prekletstvo in graja med vsemi narodi zemlje?‹
9 Je, mmesahau uovu uliotendwa na baba zenu, na wafalme na malkia wa Yuda, na uovu uliofanywa na ninyi na wake zenu katika nchi ya Yuda na barabara za Yerusalemu?
Mar ste pozabili zlobnost svojih očetov, zlobnost Judovih kraljev, zlobnost njihovih žena, svojo lastno zlobnost in zlobnost svojih žena, ki so jo zagrešili v Judovi deželi in na ulicah Jeruzalema?
10 Mpaka leo hawajajinyenyekeza au kuonyesha heshima, wala hawajafuata sheria yangu na amri nilizoweka mbele yenu na baba zenu.
Niso se ponižali celó do tega dne, niti se niso bali, niti hodili po moji postavi, niti po mojih zakonih, ki sem jih postavil pred vas in vaše očete.
11 “Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Mimi nimekusudia kuleta maafa juu yenu, na kuiangamiza Yuda yote.
Zato tako govori Gospod nad bojevniki, Izraelov Bog: ›Glejte, svoj obraz bom naravnal zoper vas za zlo in da iztrebim vsega Juda.
12 Nitawaondoa mabaki ya Yuda waliokusudia kwenda Misri kukaa humo. Wote wataangamia huko Misri, wataanguka kwa upanga au kufa kwa njaa. Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana, watakufa kwa upanga au njaa. Watakuwa kitu cha kulaania na cha kutisha, cha laumu na shutumu.
Vzel bom preostanek Juda, ki so svoje obraze naravnali, da gredo v egiptovsko deželo, da začasno prebivajo tam in vsi bodo použiti in padli v egiptovski deželi; torej použiti bodo z mečem in z lakoto. Umrli bodo, od najmanjših celo do največjih, z mečem in z lakoto, in bodo preziranje in osuplost, prekletstvo in graja.
13 Nitawaadhibu wale waishio Misri kwa upanga, njaa na tauni kama nilivyoiadhibu Yerusalemu.
Kajti kaznoval bom tiste, ki prebivajo v egiptovski deželi, kakor sem kaznoval Jeruzalem, z mečem, z lakoto in s kužno boleznijo,
14 Hakuna hata mmoja wa mabaki ya Yuda ambaye amekwenda kuishi Misri atakayeepuka au kunusurika ili kurudi katika nchi ya Yuda, ambayo wanaitamani sana kurudi na kuishi ndani yake, hakuna hata mmoja atakayerudi isipokuwa wakimbizi wachache.”
tako da ne bo nihče izmed Judovega preostanka, ki so odšli v egiptovsko deželo, da začasno prebivajo tam, ušel ali preostal, da bi se vrnil v Judovo deželo, h kateri so imeli željo, da se vrnejo, da prebivajo tam. Kajti nihče se ne bo vrnil, razen tistih, ki bodo pobegnili.‹«
15 Kisha wanaume wote ambao walijua kwamba wake zao walikuwa wakifukiza uvumba kwa miungu mingine, pamoja na wanawake wote waliokuwako, yaani, kusanyiko kubwa na watu wote walioishi nchi ya Misri na Pathrosi, wakamwambia Yeremia,
Potem so vsi možje, ki so vedeli, da so njihove žene zažigale kadilo drugim bogovom in vse ženske, ki so stale poleg, velika množica, celo vse ljudstvo, ki prebiva v egiptovski deželi, v Patrósu, odgovorili Jeremiju, rekoč:
16 “Hatutausikiliza ujumbe uliotuambia katika jina la Bwana!
» Glede na besedo, ki si nam jo govoril v imenu Gospoda, ti ne bomo prisluhnili,
17 Hakika tutafanya kila kitu tulichosema tutakifanya: Tutafukiza uvumba kwa Malkia wa Mbinguni na tutammiminia sadaka zetu za kinywaji kama vile sisi na baba zetu, wafalme wetu na maafisa wetu tulivyofanya katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu. Wakati ule tulikuwa na chakula tele, tulikuwa matajiri wala hatukupata dhara lolote.
temveč bomo zagotovo počeli katerokoli stvar, izhajajočo iz naših lastnih ust, da zažigamo kadilo kraljici neba in da ji izlivamo pitne daritve, kakor smo počeli mi in naši očetje, naši kralji in naši princi v Judovih mestih in na ulicah Jeruzalema, kajti tedaj smo imeli obilico živeža in smo bili dobro in nismo videli zla.
18 Lakini tangu tulipoacha kumfukizia uvumba Malkia wa Mbinguni na kummiminia sadaka za kinywaji, hatupati chochote, na tumekuwa tukiangamizwa kwa upanga na njaa.”
Toda odkar smo prenehali zažigati kadilo kraljici neba in ji izlivati pitne daritve, smo bili v potrebi vseh stvari in smo použiti z mečem in z lakoto.«
19 Wanawake wakaongeza kusema, “Wakati tulipomfukizia uvumba Malkia wa Mbinguni na kummiminia sadaka zetu za kinywaji, je, waume zetu hawakujua kwamba tulikuwa tukitengeneza maandazi kwa mfano wake, na kummiminia yeye sadaka za kinywaji?”
»In ko smo zažigale kadilo kraljici neba in ji izlivale pitne daritve, mar smo ji naredile kolačke, da jo obožujemo in ji izlivale pitne daritve, brez naših moških?«
20 Ndipo Yeremia akawaambia watu wote, wanaume na wanawake waliokuwa wakimjibu,
Potem je Jeremija rekel vsemu ljudstvu, moškim in ženskam in vsemu ljudstvu, ki mu je dalo ta odgovor, rekoč:
21 “Je, Bwana hakukumbuka na kufikiri juu ya uvumba uliofukizwa katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu na ninyi pamoja na baba zenu, wafalme wenu, maafisa wenu na watu wa nchi?
»Kadilo, ki ste ga zažigali po Judovih mestih in po ulicah Jeruzalema, vi in vaši očetje, vaši kralji, vaši princi in ljudstvo dežele, ali se jih ni Gospod spomnil in ali to ni prišlo v njegov um?
22 Bwana alipokuwa hawezi kuendelea kuvumilia matendo yenu maovu na mambo ya machukizo mliyoyafanya, nchi yenu ilikuwa kitu cha kulaania na kuachwa ukiwa pasipo wakazi, kama ilivyo leo.
Tako da Gospod ni mogel več trpeti zaradi zla vaših početij in zaradi ogabnosti, ki ste jih zagrešili; zato je vaša dežela opustošenje, osuplost in prekletstvo, brez prebivalca, kakor na ta dan.
23 Kwa sababu mmefukiza uvumba na kufanya dhambi dhidi ya Bwana, nanyi hamkumtii wala kufuata sheria yake au amri zake au maagizo yake, maafa haya yamekuja juu yenu, kama mnavyoona sasa.”
Ker ste zažigali kadilo in ker ste grešili zoper Gospoda in niste ubogali Gospodovega glasu, niti hodili po njegovi postavi, niti po njegovih zakonih, niti po njegovih pričevanjih, zato se vam je zgodilo to zlo, kakor na ta dan.«
24 Kisha Yeremia akawaambia watu wote, pamoja na wanawake, “Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mlioko Misri.
Poleg tega je Jeremija rekel vsemu ljudstvu in vsem ženskam: »Poslušajte besedo od Gospoda, ves Juda, ki ste v egiptovski deželi:
25 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Ninyi na wake zenu mmeonyesha kwa matendo yenu kile mlichoahidi mliposema, ‘Hakika tutatimiza nadhiri tulizoziweka za kumfukizia uvumba na kummiminia sadaka za kinywaji Malkia wa Mbinguni.’ “Endeleeni basi, fanyeni yale mliyoahidi! Timizeni nadhiri zenu!
›Tako govori Gospod nad bojevniki, Izraelov Bog, rekoč: ›Vi in vaše žene ste tako govorili s svojimi usti in s svojo roko izpolnili, rekoč: ›Zagotovo bomo izvajali svoje zaobljube, ki smo se jih zaobljubili, da zažigamo kadilo kraljici neba in da ji izlivamo pitne daritve.‹ Zagotovo boste dokončali svoje zaobljube in zagotovo boste izvedli svoje zaobljube.
26 Lakini sikieni neno la Bwana, enyi Wayahudi wote mnaoishi Misri: ‘Ninaapa kwa Jina langu lililo kuu,’ asema Bwana, ‘kwamba hakuna hata mmoja atokaye Yuda anayeishi popote Misri ambaye kamwe ataomba tena kwa Jina langu au kuapa, akisema, “Hakika kama Bwana Mwenyezi aishivyo.”
Zato poslušajte besedo od Gospoda, ves Juda, ki prebiva v egiptovski deželi: ›Glejte, prisegel sem pri svojem velikem imenu, ‹ govori Gospod, ›da moje ime ne bo več imenovano v ustih kateregakoli moškega iz Juda in po vsej egiptovski deželi, rekoč: ›Gospod Bog živi.‹
27 Kwa maana ninawaangalia kwa ajili ya madhara, wala sio kwa mema. Wayahudi walioko Misri wataangamia kwa upanga na njaa, hadi wote watakapoangamizwa.
Glej, bedel bom nad njimi za zlo in ne za dobro; in vsi Judovi možje, ki so v egiptovski deželi, bodo použiti z mečem in z lakoto, dokler jih ne bo konec.
28 Wale watakaonusurika upanga na kurudi katika nchi ya Yuda kutoka Misri watakuwa wachache sana. Ndipo mabaki wote wa Yuda waliokuja kuishi Misri watakapojua ni neno la nani litakalosimama, kwamba ni langu au lao.
Vendar se bo malo število, ki pobegne meču, vrnilo iz egiptovske dežele v Judovo deželo in ves preostanek Juda, ki so odšli v egiptovsko deželo, da tam začasno prebiva, bo vedel čigave besede bodo obstale, moje ali njihove.
29 “‘Hii itakuwa ndiyo ishara kwenu kwamba nitawaadhibu mahali hapa, asema Bwana, ili mpate kujua kuwa onyo langu la madhara dhidi yenu hakika litatimizwa.’
To vam bo znamenje, ‹ govori Gospod, ›da vas bom kaznoval na tem kraju, da boste lahko vedeli, da bodo moje besede zagotovo obstale zoper vas v zlo.‹
30 Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitamtia Farao Hofra mfalme wa Misri mikononi mwa adui zake wanaoutafuta uhai wake, kama vile nilivyomtia Sedekia mfalme wa Yuda mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, adui aliyekuwa akiutafuta uhai wake.’”
Tako govori Gospod: ›Glejte, izročil bom faraona Hofrája, egiptovskega kralja, v roko njegovih sovražnikov in v roko tistih, ki strežejo po njegovem življenju, kakor sem Judovega kralja Sedekíja izročil v roko babilonskega kralja Nebukadnezarja, njegovega sovražnika in ki je stregel po njegovem življenju.‹«